Kwa wahenga tu: Kwanini watu wengi wenye roho nzuri huwa na maisha magumu au ya kawaida tu?

Zuri au baya utakalowafanyia watu litakurudia kwa namna ambayo huwezi kutegemea.

Mwisho wa siku (alama utakayoacha kwa jamii) watu hawatakukumbuka kwa uzuri wa sura yako au umbo lako bali watakukumbuka kwa moyo wako na roho yako nzuri.

Tabia yako nzuri na matendo yako mazuri yataendelea kukufuata kokote uendapo katika dunia hii.
 
Sawa mkuu ila swali langu ni kwa nn hao watu wenye roho nzuri na kujitolea huwa wengi wao wanamaisha magumu au ya kawaida tena wengine wanafirisika kwa kusaidia?Je wanavyotoa huwa hawapati baraka za kubadilisha maisha yao?
 
Hahaha!
 
Usifuate dini inayofundisha kile isichokiishi.

Niambie kanisa au msikiti gani unaojitoa kwa sehemu kubwa kuwasaidia waumini wake kifedha? Wengi wanataka mtoe nyie ila wao ni wagumu sana kuwapa wahitaji.

Mimi mimeshaamua nitakupa kile unachonipa. Ukinipa maombi nitashukuru na kukuombea pia.
Ukinipa mali na fedha nitajitahidi fadhira yangu pia ionekane kwa njia hiyo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mitihani tu ya maisha ndg

Kila mmoja hupitia katika maisha haya ili kukufunza jinsi ya kuishi na kumtegemea Mungu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Sawa mkuu ila swali langu ni kwa nn hao watu wenye roho nzuri na kujitolea huwa wengi wao wanamaisha magumu au ya kawaida tena wengine wanafirisika kwa kusaidia?Je wanavyotoa huwa hawapati baraka za kubadilisha maisha yao?
Tafsiri ya maisha mazuri ipo tofauti kwa mtu na mtu, mwengine mpaka awe na pesa, mtoto, gari, shamba na nyumba (pesa kiasi gani?, watoto wangapi?, magari mangapi au gari la aina gani? shamba heka ngapi? nyumba ngapi au nyumba iwe sehemu gani au nyumba yenye ukubwa gani? majibu yatatofautiana kwa sababu binadamu hatufanani kama vidole vya mkono.

Mwengine tafsiri yake ya maisha mazuri ni kuishi maisha yenye upendo, utulivu, amani, afya na utajiri wake ni maisha yanayompendeza Mungu pamoja na kusaidia watu.

Unaweza kuyaona maisha yake ni ya kawaida kulinganisha na maisha ya mtu mwengine. Lakini watu wanaishi kutokana na malengo waliyojiwekea na maisha ambayo wameamua kuishi.

Binadamu tunategemeana, huwezi kuishi bila binadamu wenzako. Wewe unamsaidia huyu na yeye anaweza akakusaidia wewe kama malipo au atamsaidia mwengine mbele ya safari yake
 
Ni kweli dunia ina mitihani mengi. Kuna nyakati bila kushikwa mkono maisha yanakua machungu sana.

Tujitahidi kufanya kazi ili tupate chetu bila kulazimika kuwapigia watu magoti kwani manyanyaso ya kuomba uumiza sana.

Ila tukikwama , usiche kutoka na kupaza sauti kwa ndg na rafiki kuomba msaada. Mungu utumia watu kujibu mahitaji yetu.

Kumbuka ukiona mtu hajakusaidia usimulaumu, usipokufa yuko aliyeandaliwa kukutoa kwenye janga hilo. Subira na uvumilivu ni nguvu amabayo kila mja anapaswa kuwa nayo.

Kwa upande mwingine, kujenga tabia ya kusaidia ni njema sana kwani unaweza usitambue ila ni moja ya huduma kubwa sana kupunguza maumivu ya maisha


Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umenena vyema ndg

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Umenena vyema ndg

Sent using Jamii Forums mobile app
Lakini ndugu hata dini inatushauri tuwekeze kwa Mungu kupitia sadaka na matendo mema.Sikumbuki ni injili ipi ila kuna mstari YeNsu anasema palipo hazina yako ndipo roho yako itakua tena tuweke akiba zetu kwa Mungu ambapo nondo na wezi hawafiki?Sasa kwa nn unasema kumsaidia mtu sio kuwekeza?waswahili wanasema wema hauozi maana yake nn?Natoa wito wale mliosaidiwa mnawajibu wa kimaadili kuwakumbuka waliowasaidia
 
Kwenye dini kuna mawili kwa watu wenye taswira ya watoaji wa sampuli uliyotolea mfano.
-Awe na subira Mungu hadanganyi kwenye ahadi zake.
-Arekebishe usaidiaji wake.
•Kuna wengine ni rahisi kusaidia lakini anasaidia kwa masimango
•Asisaidie kwa majivuno kuwa ona mimi ndiye msaidiaji.
•Asisaidie kwa kutaraji aonekane mwema kwa watu.
•Asisaidie mkono wa pili ujue.

Afanye hivyo, ataona mabadiliko.

Mambo ya pesa na mali kuongezeka yana mengi. Kila mtu na siri yake.
 
Mwenye roho mbaya anafanya lolote ili afanikiwe, mcha Mungu hathubutu
 
Unaposaidia lengo ni kuondoa kizingiti kinachomzuia mtu kufikia sehemu fulani, ni kumuwezesha pasipo kutaraji malipo.

Ukiwekeza ni kuwa unataraji ulichokiwekeza kikuletee faida zaidi. Hii ni biashara tayari.

Ulichoambiwa ukifanye hapo juu ni kuwekeza kwa Mungu. Ni kufanya biashara na yeye mwenyewe Mungu. Biashara yenyewe ni kufanya wema. Maadamu yeye ndiye muwekezaji mkuu faida utaipata kutoka kwake.

Wewe usihangaike na bidhaa (binadamu) ulipowekeza pesa zako. Hangaika na uliyoingia naye ubia. Faida utaipata kutoka kwake yeye maadamu ndiye aliyekuambia iwe hivyo wekeza kwake.

Ukihangaika na bidhaa (binadamu) itakushughulisha hii bidhaa ina mengi! Utajawa na ghadhabu, chuki na unaweza ukawa na kisasi.

Lakini biashara ni mapatano. Ni muhimu kuyaelewa na yule unayeingia naye ubia ili ufaidike naye.
 
Kula kongole. Nimekupenda bureeeeeh. Chukua kinywaji nakuja kulipia.
Kutaka kupendwa na kila mtu ni njia ya kupoteza.
Angalia dereva yule yule taxi ya muhindi akikosa hesabu anakopa apeleke. Kama bosi mswahili basi anakwenda na maneno kibao. Agressiveness ina nafasi muhimu sana kwenye baadhi ya biashara. Ila wale wakucheka cheka wabaki reception na customer services.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…