Kwa waislamu wenzangu, naombeni mnisaidie hukumu ya kusema uongo

Kwa waislamu wenzangu, naombeni mnisaidie hukumu ya kusema uongo

Idrissou02

JF-Expert Member
Joined
Jul 31, 2018
Posts
354
Reaction score
656
Naam uzi huu naulenga kwa waislamu wenzangu. Je kwa anaefahamu, ipi ni hukumu ya kusema uongo, mtu afanye nini kujitakasa na dhambi iyo baada ya kua ameshaitenda na hawezi badilisha matokeo ya uongo huo?
 
Asalaam Aleykhum warah'matullah wabarakatuh

Dhambi ya kusema uongo ni sawa na dhambi zingine Sheikh, hukumu yake siku ya Qiyama, mwombe Allah Qiyama kisifike wakati hujatubia dhambi hiyo

Allah anajua zaidi.

Wabillah Tawfiq,
 
Asalaam Aleykhum warah'matullah wabarakatuh

Dhambi ya kusema uongo ni sawa na dhambi zingine Sheikh, hukumu yake siku ya Qiyama, mwombe Allah Qiyama kisifike wakati hujatubia dhambi hiyo

Allah anajua zaidi.

Wabillah Tawfiq,
Asalaam aleykhum warah'matulah wabarakatuh.

Dhambi zote sio sawa. Huwezi kulinganisha dhambi ya kumfhulumu yatima au mjane asiyejua chochote na kudanganya.

Wabilah Tawfik
 
Asalaam aleykhum warah'matulah wabarakatuh.

Dhambi zote sio sawa. Huwezi kulinganisha dhambi ya kumfhulumu yatima au mjane asiyejua chochote na kudanganya.

Wabilah Tawfik
Unapimaje ukubwa au udogo wa dhambi ewe Mwanadamu?
 
Assalam alaykum warahamatullahi wabarakatu
Tubu,toba ya kweli Allah atakusamehe.Shirki ndio haina msamaha.
 
Shekhe, Uongo unaruhusiwa ktk Uislamu ikiwa tu unalenga kumtetea Mwislamu mwenzako au ktk jambo lenye maslahi na Uislamu.Nenda kasome Kitabu Cha Ukweli Mwaminifu juzuu ya nne.Kwa hiyo Ndugu yangu Wewe piga uongo tu no problem.
 
Uongo katika mzungumzo ni sifa mojawapo ya alama ya unafiki, hivyo inabidi tung’ang’ane ili tuondoe sifa hiyo katika maisha yetu. Allaah Aliyetukuka Amehimiza sana sifa hiyo pale Aliposema: “Enyi mlioamini! Mcheni Allaah na kuweni pamoja na wakweli” (9: 119). Hii ni sifa ambayo inamwingizaa sahibu wake Peponi: “…na wanaume wasemao kweli na wanawake wasemao kweli…Allaah Amewaandalia msamaha na ujira mkubwa” (33: 35).

Hadithi hizi mbili muhimu toka kwa mjumbe wa mwenyezi mungu

1.Mtume (Swalla Allaahu ‘alayhi wa aalihi wa sallam) amesema:
“Bila shaka, ukweli ni wema, na wema unampeleka (mtu) Peponi. Hakika uongo ni uovu, na uovu unampeleka (mtu) motoni”

2.Amesema tena:
“chungeni sana kuhusu ukweli na ikhlasi, kwani ukweli na ikhlasi inaongoza kwenye wema, na wema unaongoza Peponi”
 
Kuhusu kujitakasa ilibidi useme uongo wa namna gani umesema..

Taratibu za toba ni zile zile siku zote
1) - Kuiacha dhambi hapo hapo.
2) - Kujuta juu ya uliyoyafanya
3) - Kuazimia kutorudia tena (dhambi)
4) - Kurudisha haki za watu uliowadhulumu, na kutafuta njia ya kujiweka mbali na hayo.

Mwenyezi Mungu ni mwingi wa kusamehe, anapenda watu wanaotubia.. Hivyo ni jambo la kheri..

Kama sikosei, "mtume(s..a.w) anasema miongoni mwa watu bora basi ni wenye kuomba msamaha kwa mola wao"
 
Back
Top Bottom