Kwa wale ambao hamna maelewano mazuri na wazazi wenu

Kwa wale ambao hamna maelewano mazuri na wazazi wenu

Ila naomba maelekezo unaishije nae kijanja...Mimi nashindwa kabisa kujizuia najikuta sitaki kabisa mawasiliano yoyote na yeye...ebu nifundishe unavyo ishi na mzazi wako
Mimi huwa nawasiliana nae kunapotokea ulazima kabisa wa kufanya hivyo. Pia nina msimamo kwamba nitakusadia ninavyoweza ila sitaki shinikizo wala ushawishi. Kama ni YES ni YES na kama ni NO ni NO. Mwanzoni ilikuwa utata ila baadae wakaelewa kwasababu pia huwa ikiwa YES huwa sipindishi natimiza. Unajua shida kubwa sana kwa wengi wetu ni ukorofi wa wazazi uliokutana na hali duni (umaskini)... wazazi wengi wana hasira sana kwamba hawasaidiwi na watoto wao huku wakijisahaulisha kuwa kila mwanaume/mwanamke ataachana na wazazi wake na kuambatana na mkewe/mumewe.
 
Mimi huwa nawasiliana nae kunapotokea ulazima kabisa wa kufanya hivyo. Pia nina msimamo kwamba nitakusadia ninavyoweza ila sitaki shinikizo wala ushawishi. Kama ni YES ni YES na kama ni NO ni NO. Mwanzoni ilikuwa utata ila baadae wakaelewa kwasababu pia huwa ikiwa YES huwa sipindishi natimiza. Unajua shida kubwa sana kwa wengi wetu ni ukorofi wa wazazi uliokutana na hali duni (umaskini)... wazazi wengi wana hasira sana kwamba hawasaidiwi na watoto wao huku wakijisahaulisha kuwa kila mwanaume/mwanamke ataachana na wazazi wake na kuambatana na mkewe/mumewe.
Mimi mzazi wangu Bado ni mtumishi...juzi TU hapo amepandishwa tena cheo japo muda wa kustaafu kwake umekaribia...ila kiukweli Mimi Bado najitafuta kimaisha sijawahi kumlilia shida akanisaidia Hadi Huwa najiuliza pengine sio mzazi wangu...nilipo gundua kuwa Hana msaada na Mimi...niliamua kufocus na maisha yangu japo Bado sijayapatia ila ni kitambo sana sijamlilia shida...last time nilikuwa Nina shida ya laki 3 mfukoni nilikuwa na kama 220k nikamwambia mzee Nina shida ila Bado kama elfu 80 hivi....alicho nijibu kilinitoa machozi harafu ilikuwa ni shida muhimu sana maana wife alilazwa hivyo ilikuwa ni bill ya hospital...baba alikataa katakata kunisaidia...nikaamua kuachana nae...hivi sasa Nina mawazo ya kuhama nchi Mimi na watoto wangu...ili niepukane na huyu mzee kwani Najua TU baada ya yeye kustaafu atataabika TU...Hilo lipo wazi wastaafu Huwa wanaponda raha miaka mitatu TU...
 
Kama umelelewa vizuri huwezi elewa vile watu wanapitia. Nimesoma visa vingi hapa nikamshukuru Mungu kwamba sikuwahi pitia waliyoyapitia. Familia yetu haina ugomvi hata chembe tunaishi peace sana.
Pole kwa wate wanaopitia changamoto na wazazi wao.
Hongera sana, Lucky you
 
Again hapo hauongelei mfumo dume. Kuwa muelewa. Mfumo dume ni mfumo unaomtambua kama baba kiongozi wa familia na mama msaidizi wake.

It means wote wanashirikiana. So kama mwanaume analeta ubabe hiyo sio structure ya mfumo dume bali hilo ni tatizo binafsi la muhusika.
Kusaidiana bado haifukii dhana ya mfumo dume. Mwanaume hataki kutumia anachokipata na familia, anataka mke aendelee kumnyenyekea aombe kila shillingi inapelekea watoto kutokusomeshwa shule kwa amani maana ada hazilipwi, so mke anapoamua kupambana ili aje asomeshe wanae mwenyewe mwanaume anaibus sasa kwamba yeye ni mwanaume ila mwanamke anataka kumpanda kichwani. Anashindwa kusema kwamba kwanini atafte kazi nzuri inanishushia uanaume wangu. Wewe kama hayajakukuta usikatae nnachokusimulia. Kama hukielewi
Bora ukatulia maana wanaume mnateteanaga ila wake zenu wanakufa na vitanzi vya kila aina
 
Nakuelewa sana mtu wangu. Hiki unachopitia ni kitu ambacho kuna watu wengi wanapitia halafu wanaamini ndio maisha so kuvumilia na kukubali upuuzi ndio namna ya kuishi. HII SI SAHIHI KABISA.

Mimi pia napitia the same story. Mimi mtoto wa pili kutoka mwisho. Tupo wa 5. Mzee wangu alikuwa mpambanaji sana kutoka mtoto wa mfugaji yaani wale watoto wa kuchunga ng'ombe na kutoroka kuja mjini kujipambania na kujiendeleza kwa elimu hadi akawa mhandisi wa mitambo na kufanya kazi wizara ya ujenzi chini ya magufuri kabla hajawa hata mbunge.

Mzee kapambana na kutafuta mali nyumba 3, biashara za maduka ya spare, trekta 2, mashamba matatu mbeya, mawilli morogoro, land Rover 110, land Rover 109, Isuzu tipper, na garage yenye vifaa vingi tu vya kisasa vya gereji. Hivi ni baadhi ya vitu vichache mzee aliacha. Na kulikuwa na salio Bank pia.

Picha linaanza mshua kafariki ghafla kwa shinikizo la damu. Tukabakia na bi mkubwa kama msimamizi na mshika mirathi. Watoto watano, wakwanza amemaliza form 6 kwa mbinde balaa mzee alikuwa kila siku anampa risala atulie asome yeye michezo, wapili nae mzee kuvuta alikuwa yupo kidato cha n'ne akasema yeye shule hataki, tusome sisi wadogo tu, watatu alikuwa form one, wanne ni mimi nikiwa darasa la 5, na wa mwisho akiwa vidudu ndio anataka kuanza la kwanza.

Sasa kutokea hapo ikawa bi mkubwa kwa kushauriana na sista wa kwanza ni kuuza kitu kimoja baada ya kingine bila consultation ya watu wenye ujuzi. Mfano waliuza gari Isuzu tipper kwa bei ya hasara ya 1 million kwa kupigwa sound na madalali. Then upotevu uliendelea kwa mali zingine ambazo ziliuzwa kwa bei za hasara. Me nikiwa mdogo na sina nguvu za kushauri au kukataa.

Haya yaliendelea kwa muda mrefu na mali nyingi zilitoweka katika mazingira ya uzembe sana. Na wahusika ni bi mkubwa, sista mtoto wa kwanza na bro mtoto wa pili, huyu watatu alikuwa mkoani alipokuwa akisoma boarding. Mimi na mdogo wangu tulikuwa nyumbani.

Mimi nilimaliza primary na kufaulu shule ya Serikali. Kipindi hicho ada kwa mwaka ni elfu 20. Lakini nilikuja kuilipa hiyo pesa mwenyewe nikiwa nakwenda chuo maana nilitakiwa kupeleka cheti na sio results slip. So nilikwenda kulipa ada ya miaka yote minne kwasababu sikuwahi kulipiwa ada na bi mkubwa. Kwakifupi pesa ambazo zilitolewa serikalini kwaajiri ya kusomesha watoto, maza alizigawanya kwa kuwapa wakubwa ambao hawakuwa shule, yule wa boarding alipewa account yake yote ambapo aliacha shule na kuanza kufanya upuuzi wa kujifanya mjasiliamali wa maswala ya miziki na kupromote wasanii akaishiwa kudhurumiwa pesa na mwenzake aliyekuwa mjanja wa mjini so akakosa shule na biashara chali.

Huku nyumbani pesa zangu mimi ambayo ilikuwa ni around 3 milion sikupata hata mia maana account ilikuwa ni ya kusimamiwa sikuwa nimetimiza miaka 18 kwa wakati huo. so bi mkubwa ndie alikuwa na access ya account yangu na ya mdogo wangu wa mwisho. Pesa zetu zilitumika bila sisi kujua na ziliisha haraka sana ndio maana nilipofaulu kwenda sekondari hakukuwa hata na 100 ya kunisapoti.

Huu uharibifu ulifanyika ndani ya muda mfupi na waliofanya ni bi mkubwa, sista mtoto wa kwanza, na bro mtoto wa pili. Bro alisema anataka kupambana akapewa tractor akaenda kulitelekeza huko hadi leo hii haijulikani kuwa aliuza au alifanyaje hiyo ni siri yake, sista kwa kushirikiana na boyfriend wake wa kipindi hicho waliuza mashamba na pesa kidogo wakamtumia maza nyingine sista akala bata na jamaa na kumhonga.

Maisha yakifika kipindi yakawa magumu maana ufujaji ulimaliza pesa zote zilizokuwapo kwenye akiba na asset ambazo zilikuwa za kuuzika kirahisi kama magari, trekta, mashamba, na mzigo kwenye maduka ya spea, waliviuza kwa bei za hasara chini ya bei ya soko so ni kama walivigawa bure na vingine kama tractor vilipotea bila taarifa.

Sasa ilifika kipindi naenda shule kwa shida napewa 200 ndio pocket money. Aisee nikikumbuka nashikwa hasira sana.

Fast forward leo, nilipita kwa shida sana ila MUNGU sio Jr makamba nikafika chuo na kumaliza salama kwa msada wa marafiki, na baadhi ya ndugu ambao walinisaidia kwa lawama sana kwa kuwa mzee alikuwa na mali walihisi mimi ni wale watoto wa kusema uongo jambo ambalo lilinifanya nikiwa na shida kufa na tai shingoni sikuwa tayari kumwambia ndugu bora nimuombe mtu baki au marafiki na familia zao wataweza nipa sapoti bila kuhoji.

Baada ya kumaliza elimu ilikuwa kama zari nilipata ajira ndani ya miezi mitatu tu. Kwa namna nilikuwa nachukia kuwa karibu na ile familia nilikopa hela kidogo nikaondoka nyumbani miezi minne tu baada ya mwezi wa kwanza kuanza kazi. Bi mkubwa alilalamika sana na kunitamkia kuwa naondoka kwasababu nimepata kazi badala ya kukaa na kuwasaidia mahitaji pale ndani.

Nilishajaribu kuweka mambo sawa kwa kulazimisha nyumba zile nyumba mbili kati ya tatu zipangishwe ili kodi isaidie maana nyumba walikuwa wakiishi ndugu so nilizungumza nao kiuungwana wakakubali kupisha. So kodi nikawa nashika mimi nampelekea bi mkubwa mahitaji yake ya ndani kama chakula na kadhalika.

Yule sista ambaye nae anaishi mkoani na jamaa mluga luga tu na bro nae asiyejisoma anaishi kwa mwanamke wake aliezaa nae, wakawa na mawasiliano maana bi mkubwa alikuwa na tabia za umbea za kuwaambia kila ninachofanya. Sasa sijui ni wivu wakaanza kusagia kunguni kuwa kwann nashika pesa za kodi nimuachie mama ashike mwenyewe, yule mtoto wa tatu alikuwa amepotelea mikoani huko maana aliacha shule asijue anafanya nini na maisha yake akarudi home kwa bi mkubwa na kuishi pale na akiwa anajifanya ni mtu wa kusali kumbe unafiki tu maana ndie alikuwa mchochezi.

Kuna siku bila taarifa bi mkubwa ananipigia simu kuwa yupo kwa wapangaji wamegoma kumpa kodi niwaambie kuwa yeye ndie mwenye nyumba na kuanzia sasa atakuwa anapokea yeye, aisee nilimind sana. Nikamuuliza kwann umeenda kwa wapangaji, akaanza kujibu kwa ukali kuwa nisimpande kichwani. Nikaona isiwe shida, ya nini kupata laana ya bure. Nikawaambia wapangaji wote kuwa huyo ni bi mkubwa watoe shaka.

Tokea siku ile nikaachana na maswala ya familia nikapiga kimya. Yule mtoto wa tatu na huyu mdogo wangu wa kike wakageuka masnitch namba moja wakiungana na wale wakubwa wawili kuwa wapinzani kwangu.

Kimsingi nikaamua kujitenga na familia kwasababu katika kitu sipendi ni kuishi na watu ambao hawaeleweki na wana mambo ya ajabu na upuuzi mwingi.

Haiwezekani watu kwa uzembe wenu mharibu na kufuja mali za familia halafu zinabakia chache anatokea moja wa wanafamilia anataka kuzisimamia vizuri mnamletea ligi kwa hoja za kipumbavu na za wivu wivu na mafigisu ya kifala. Mimi nikasema kama mtaniona. Huu ni mwaka wa tano naandika sijaenda tena na bi mkubwa ameshaniulizia sana. Naongea nae tu kwenye simu kumsalimia kawaida akianza kuniuliza nipo wapi au nafanya nini ntasitisha mazungumzo hapo hapo nikate simu na huwa siulizii chochote hapo nyumbani. Nikitaka kutoa sapoti nampigia mpwa wangu namuelekeza nilipo nampa kama vifurushi na pesa kidogo namtumia bi mkubwa napiga kimya.

Kuna familia nadhani tunakuwa tumezaliwa kimakosa. Sasa kulazimisha kublend nazo unaweza kufa kwa pressure. Mimi kama wewe nimeamua kukaa nao mbali na ninaona namna ninavyokwenda vizuri kwasasa maisha yangu yana utulivu na sina msongo wa mawazo
Huwa namuelewa sana mtu akizungumza kama wewe hivi.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Hongera kwa ujasiri
 
Sidhani kama core point ya mada yangu ilikua mzazi kumtegemea mtoto
Hii inafanana na story ya maisha yangu. Mama yangu alikuwa hanipendi tangu nikiwa mtoto. Na hadi nilijua na marehemu bibi yangu ambaye alinipenda sana kuna kipindi aliwahi sema sijui kwanini mama yako hakupendi na mimi wala siwezi sema chochote hii kauli inatembea sana masikioni mwangu kila wakati.

Wakati nakua mama aliwapenda na hata sasa anawapenda sana wadogo zangu kuliko mie, anawashirikisha zaidi wao kuliko mie. Na hata kuna kipindi aliugua sana karibu kufa akagawa mali kwa wadogo zangu wote kasoro mie. Mama yangu yeye ukiona anakuwa karibu na wewe kipindi hicho kuna kitu anataka kwako akishakamilisha anakutakana. Imekuwa hivyo kwenye life langu. Nimekuwa nikijishusha lakini wapi. Ananiombea mabaya wakati wote, sema huwa nasema Mungu siyo mzungu, anapima kila jambo. Right laana zingekuwa rahisi basi ningekuwa Nisha kufa muda mrefu. Nimejitajidi sana kuwa beba wadogo zangu nawasomesha lakini hata Sipati reward. Anawatumia wadogo zangu hao hao kunihujumu.

Kwa kweli imefika mahali nimeamua kunyamaza coz naona naumia bure mahali ambapo sipendwi. Si kwamba huduma sita peleka nitaendelea kutuma huduma kama kawaida. Lakini kuwa karibu kabisa kwa kweli hapana. Nimeamua hata nyumbani kwa sasa sitakanyaga.

Mama ni mtu anataka kukuendesha, right ningekuwa namsikiliza ndoa yangu ingekuwa Isha kufa. Wadogo zangu ambao wanamsikiliza kila kitu ndoa zao zipo very unstable. Mimi sikutaka kumsikiliza kila kitu. Haya maisha nilichojifunza tujifunze sana kujitegemea jenga misingi mizuri ya familia yako. Wapende watoto wako, wape rewards jenga uchumi wako. Anayekupenda mpende asiye kupenda achana naye.

Mama anataka akupangie uishi na nani na usiishi na nani sasa haya maisha hayaendi hivyo.

Sent from my Infinix X672 using JamiiForums mobile app
 
Hii inafanana na story ya maisha yangu. Mama yangu alikuwa hanipendi tangu nikiwa mtoto. Na hadi nilijua na marehemu bibi yangu ambaye alinipenda sana kuna kipindi aliwahi sema sijui kwanini mama yako hakupendi na mimi wala siwezi sema chochote hii kauli inatembea sana masikioni mwangu kila wakati.

Wakati nakua mama aliwapenda na hata sasa anawapenda sana wadogo zangu kuliko mie, anawashirikisha zaidi wao kuliko mie. Na hata kuna kipindi aliugua sana karibu kufa akagawa mali kwa wadogo zangu wote kasoro mie. Mama yangu yeye ukiona anakuwa karibu na wewe kipindi hicho kuna kitu anataka kwako akishakamilisha anakutakana. Imekuwa hivyo kwenye life langu. Nimekuwa nikijishusha lakini wapi. Ananiombea mabaya wakati wote, sema huwa nasema Mungu siyo mzungu, anapima kila jambo. Right laana zingekuwa rahisi basi ningekuwa Nisha kufa muda mrefu. Nimejitajidi sana kuwa beba wadogo zangu nawasomesha lakini hata Sipati reward. Anawatumia wadogo zangu hao hao kunihujumu.

Kwa kweli imefika mahali nimeamua kunyamaza coz naona naumia bure mahali ambapo sipendwi. Si kwamba huduma sita peleka nitaendelea kutuma huduma kama kawaida. Lakini kuwa karibu kabisa kwa kweli hapana. Nimeamua hata nyumbani kwa sasa sitakanyaga.

Mama ni mtu anataka kukuendesha, right ningekuwa namsikiliza ndoa yangu ingekuwa Isha kufa. Wadogo zangu ambao wanamsikiliza kila kitu ndoa zao zipo very unstable. Mimi sikutaka kumsikiliza kila kitu. Haya maisha nilichojifunza tujifunze sana kujitegemea jenga misingi mizuri ya familia yako. Wapende watoto wako, wape rewards jenga uchumi wako. Anayekupenda mpende asiye kupenda achana naye.

Mama anataka akupangie uishi na nani na usiishi na nani sasa haya maisha hayaendi hivyo.

Sent from my Infinix X672 using JamiiForums mobile app
Duuu mzeee mbona huyu unamzungumzia bi mkubwa wangu kabisa.
 
It's Official. We won't be on the same page, never ever.
 
Hii inafanana na story ya maisha yangu. Mama yangu alikuwa hanipendi tangu nikiwa mtoto. Na hadi nilijua na marehemu bibi yangu ambaye alinipenda sana kuna kipindi aliwahi sema sijui kwanini mama yako hakupendi na mimi wala siwezi sema chochote hii kauli inatembea sana masikioni mwangu kila wakati.

Wakati nakua mama aliwapenda na hata sasa anawapenda sana wadogo zangu kuliko mie, anawashirikisha zaidi wao kuliko mie. Na hata kuna kipindi aliugua sana karibu kufa akagawa mali kwa wadogo zangu wote kasoro mie. Mama yangu yeye ukiona anakuwa karibu na wewe kipindi hicho kuna kitu anataka kwako akishakamilisha anakutakana. Imekuwa hivyo kwenye life langu. Nimekuwa nikijishusha lakini wapi. Ananiombea mabaya wakati wote, sema huwa nasema Mungu siyo mzungu, anapima kila jambo. Right laana zingekuwa rahisi basi ningekuwa Nisha kufa muda mrefu. Nimejitajidi sana kuwa beba wadogo zangu nawasomesha lakini hata Sipati reward. Anawatumia wadogo zangu hao hao kunihujumu.

Kwa kweli imefika mahali nimeamua kunyamaza coz naona naumia bure mahali ambapo sipendwi. Si kwamba huduma sita peleka nitaendelea kutuma huduma kama kawaida. Lakini kuwa karibu kabisa kwa kweli hapana. Nimeamua hata nyumbani kwa sasa sitakanyaga.

Mama ni mtu anataka kukuendesha, right ningekuwa namsikiliza ndoa yangu ingekuwa Isha kufa. Wadogo zangu ambao wanamsikiliza kila kitu ndoa zao zipo very unstable. Mimi sikutaka kumsikiliza kila kitu. Haya maisha nilichojifunza tujifunze sana kujitegemea jenga misingi mizuri ya familia yako. Wapende watoto wako, wape rewards jenga uchumi wako. Anayekupenda mpende asiye kupenda achana naye.

Mama anataka akupangie uishi na nani na usiishi na nani sasa haya maisha hayaendi hivyo.

Sent from my Infinix X672 using JamiiForums mobile app

Aiseeee [emoji119][emoji119][emoji119]
 
Kuna makosa mengine mtu hawezi kumsamehe mzazi mfano mzuri ni rafiki ndugu yangu mmoja ambaye baba yake ni mganga wa Jadi huko Shinyanga, huyu mzee alikuwa na wivu wa wazi kwa mtoto wake na mara zote alipinga jamaa kwenda shuleni na hata tupo advance level mzee wake alikuwa hampi sapport yoyote mpaka tuna maliza tunaingia chuoni mzee hana mawasiliano na jamaa wala hatumi pesa.

Sisi ndiyo tunamsaidia hapa na pale jamaa alipomaliza chuo na kupata kazi mzee akaanza maneno kuwa jamaa hasaidii familia kwanza kamtelekeza baba yake kisa amesoma anadharau. Mimi nikamshauri omba msamaha kwani mzazi hakosei ( hizi ni fikra zangu wakati huo saivi nimebadilika).

Kikawekwa kikao jamaa akaomba msamaha mambo mengine yanaendelea. Alivyotaka kuoa ikawa shida mzee hamtaki mwanamke wa jamaa ila tuli force tukamaliza vizuri.

Baada ya ndoa mzee akaleta maneno kuwa mwali akae pale nyumbani ili wachunguze kumbe yule mzee ana nia mbaya na mke wa jamaa. Kwa kutumia dawa zake za kiganga alifarakanisha uhusiano kati ya jamaa (mtoto wake) na mkewe.

Baadaye ikaja kugundulika huyu mzee anamahusiano na mke wa mtoto wake baada ya mke kushika mimba jamaa akaikataa. Sasa wewe hapo unaweza kusamehe uchawi wa hivo? Mimi sio mnafki hapa nilimshauri mwamba akate mawasiliano.

Mfano Mimi sijawahi kuungwa mkono kitu na baba yangu wala mama yangu. Ila waliwapenda sana mpaka sasa wanawapenda dada na kaka yangu na wadogo zangu ila mimi nikawa kama black sheep sihirikishwi kwa chochote lakini sasa hivi nishajua ile familia ni karmic relationship. Hakuna picha hata moja nimepiga nipo na wazazi wangu au nimepiga na baba au mama hakuna wala hawajawahi kuniweka status.

Ila sina ubaya nao japo siongei nao kila mtu na maisha yake na sasa nina familia nimeoa lakini sikuwa shirikisha kitu wala sikutaka mchango wao. Na wala hawana taarifa za life yangu kuwa nina watoto lakini hawajawahi kuwaona.

Huu ni mwaka wa saba sijawahi kukanyaga nyumbani kwetu lakini sio kama kwa ubaya cz nina amani kila mtu sijamkosea kitu. Kama shida walianza wao na uhusiano ni kama daraja kama hukunipenda na kuweka uhusiano mzuri na mimi utotoni usidhani ukubwani nita kupa time wala nafasi Never.
Tuko pamoja mimi nina 3miaka hadi ifike 5 ndio niende nifike jioni niondoke asubuhi

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Bahati mbaya siwezi share nini shida. Ila ndio hivyo itakavyobakia. Mawasiliano yatabakia kumpa shikamoo tu
Dah...! I feel what you are through. What if ukisikia kafariki? Utaumia mno au utaona normal tu? Unaonekana humpendi sana baba/mama yako. Dah!
 
Back
Top Bottom