Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Unajiamini uchukuliwe nami kweli?I'm here take me beib
Sawa,we tuliaKwani wewe uko na shida gani hadi nikuogope
🤣🤣🤭 UnadanganyaNina miaka 3 sijaambiwa nakupenda🙈
Ujue nilijua hili tatizo labda la kutokuelewana na mzee ni la kwangu pekee yangu.. form four nzima nimetumia uniform za washikaji,,, namaliza shule ,, matokeo hayakuwa poa sana mzazi anakwambia toka nyumbani kwangu kwani wewe sio mwanangu nenda kamuulize mama yako baba yako ni nani…..Hili ni tatizo kwa sisi wazazi wa kiume, hata mm nimepitia hili Kuna kipindi nilikosa viatu na shati la shule kuchanika halafu mzee akawa anapiga misele tu Hana time na mm.
Waafrika tumekua malimbukeni wa dini, mbona wazungu hawana maadili kabisa kwa issue za wazazi wao ila wanazidi kupaa ila sisi tunaojifanya tunajua sana maadili ndio umasikini wa kutisha!!Mzee mbona kama unaandika kinyume chake,yaani baraka zitoke kwa watoto ziende kwa wazazi??hata mzazi akosee vipi mtoto anawajibika kwa mzazi wake kulinda hadhi yauungu aliyopewa na mwenyezi Mungu.ndio maana imeandikwa waheshimu baba namama yako siku zako zipate kuongezeka,nasio mzazi aheshimu watoto wake.sipingi kua kuna wazazi vimeo sana,ila mambo haya nadhani yanamiongozo flani ya kuepusha mkanganyiko ktk jamiii ndio maana hata kama mzazi hakumtunza vyema mwanae wakti wautototoni mzazi huyo anaweza asipate laana,lkn mtoto kutokumtunza mzazi wake ktk uzee wake laana inamuhusu.
Jamani!Kumbe kusema vile ulikua unanidanganya😢
Huyo bibi na shangazi ni wapare?Sasa kinachoongelewa hapa sio kuwachukia kuwachukia hawa wanaofanya maamuzi ya kuharibia wengine bali namna ya kuwakalia mbali ili uwepo wao usiendelee kukiathiri. Maana kuna tabia the more unakaa karibu na wahusika the more zinakuathiri na kukupa depression.
So sometimes kukaa mbali na kuwasiliana nao kwa huo umbali ni namna nzuri ya kuishi nao.
Sio mzazi wako ni mkorofi unamleta karibu na kulazimisha kuishi nae karibu na watoto wako yaani wajukuu zake matokeo anawafundisha tabia za hovyo.
Nitakupa mfano.
Kwenye ukoo wa mzee wangu, mama yake alikuwa na dada zake wawili. Yaani kulikuwa na mabibi watatu. Huyu bibi mkubwa ndio focus yetu leo.
Huyu bibi mimi sikuwahi kukaa nae ila story zake nazijua. Nimemuona kama mara tano tu katika maisha yangu tena ya utotoni baada ya hapo ni hadi anafariki sikuwahi muona tena.
Sasa kwenye story zake, yeye alipata watoto wawili moja wa kiume mwingine wa kike, wa kiume akawa padre hadi umauti wake. Wa kike alikuwa tu mfanyakazi wa serikalini.
So kuna kaka yao upande wa baba yaani babu yangu alikuwa ni dereva wa malori, alipokuwa anapiga mishe zake akileta mazaga akawa anampatia huyu bibi mkubwa awapatie na wenzake, yeye akawa anabania anaweka kando.
Sasa akawa anasomesha watoto wake ndio huyu mkubwa akawa padre halafu yule aliyefuata akawa mtumishi wa serikalini.
So huyu padre akawa aliondoka akiwa kijana mdogo sana kwenda kanisani so alimuacha mama yake na mdogo wake wa kike.
So baada ya kuwa padre akawa analeta zawadi na pesa za kusidia wanandugu na maagizo kabisa. Yule bibi akawa zile zawadi hafikishi kwa wahusika anachuna nazo. akamsomesha huyu wakike hadi akawa mtumishi na yeye akawa na watoto wa kiume wawili. So akawa anatumia misaada ya yule padre kuhudumia tena na wajukuu bila kusaidia walengwa wa misaada waliotumiwa na mtoa msaada na zawadi.
Tabia nyingine aliyokuwa nayo ni anaweza leo akapika labda nyama nzuri ya mchuzi, anakwenda kuiweka ndani uvunguni anafunga chumba, halafu ukifika muda wa msosi anachukua mboga ya jana au juzi labda Maharage ndio analeta pale chungu chake ili mle na hapo unaweza kuta yamechacha ila sababu ya njaa watu wanajikaza wanakula. Ile nyama ni hadi hayo maharage yaishe, so kesho au keshokutwa ndipo utaiona hiyo nyama na uombe iwe haijachacha sasa.
Hizi tabia akaja kuzirithi mwanawe wa kike sasa huyu ambaye ni shangazi yetu. Anauwezo wa kupika chakula cha watu kula kushiba ila huwa hataki kuona watu wanafurahia chakula, anapika chakula kidogo watu wanakula hawajashiba vizuri wanaenda kulala na matumbo hayajashiba. Anakwambia anaenda kwa bajeti.
Anatengeneza mikate ile ya skonzi halafu anaipigia hesabu yaani anahesabu ya wiki nzima kwamba kila mtu atakula skonzi mfano mbili mbili so anahesabu watu watano mara mbili jibu lake mara saba.
Sasa ole wako upatwe na njaa iliwe skonzi hata moja. Siku akijua zimepungua mtasemwa nyumba nzima na atatafuta wa kumsukumia kesi ili ale skonzi pungufu.
Sijawahi kumuelewa yule shangazi hadi leo swaga zake.
Mwisho wa siku maisha eventually kila mtu anakuwa na mji wake so utasumbua watu ila watajitegemea na kuwa na maisha yao hayo masharti hayatawapata tena.
Sasa hapa ni mfano wa jinsi tabia mbovu zinaweza safiri kwa mzazi kwenda kwa mtoto kwenda kwa mjukuu.
So its better kujitenga mapema ili matabia ya hovyo yasisambae.
Dah pole Sana mkuuWaafrika tumekua malimbukeni wa dini, mbona wazungu hawana maadili kabisa kwa issue za wazazi wao ila wanazidi kupaa ila sisi tunaojifanya tunajua sana maadili ndio umasikini wa kutisha!!
Biblia mbona imesema kuwa wazazi wasichokoze watoto Bali wawalee katika maadili meaning wakifeli Hilo jukumu obviously laana haiwezi kuwa reliable maana Kila kitu kina Haki na wajibu.
Mfano mzazi wangu alikua hafurahii mafanikio yangu yaani hata nikiwa chuo nikifaulu hawezi nipongeza. Nakumbuka nimepata ajira ya kwanza akanuna hata simu hapokei!! Nakumbuka hata siku naenda interview alininyima nauli na hakupokea simu sema ni vile tu bahati nasibu nikafanyiwa interview kwa simu!!. Na kabla sijapata kazi nlikua nmejiajiri Bado akawa ananikashifu kuwa siwezi fika kokote, nikaanza kuingiza pesa akaanza nifokea kuwa niache hiyo kazi hata kama inanipa Hela ila sio ya mtu mwenye degree!! Hahahah kazi Nako nikapata akanizimia simu!!
Kuna wakati huwa sielewi shida ni nini Hawa wazazi alafu Kuna mpuuzi anasema eti sijui utalaaniwa??
Hapo sijaongelea mama mzazi kabisa ambaye alikua hataki hata nilipiwe ada. Mimi sijawahi mwambia mtu Nina mama Wala kumpost sijui nani kama mama maana nikikumbuka niliyopitia huwa sihesabu kama nina mama. Tukiwa wadogo alikua yupo radhi tulale njaa Ila yeye ashibe!!
So kama Mungu ni mwenye haki kweli sidhani atapokea laana za watu wenye Roho za Giza kama hizo.
Waafrika tumekua malimbukeni wa dini, mbona wazungu hawana maadili kabisa kwa issue za wazazi wao ila wanazidi kupaa ila sisi tunaojifanya tunajua sana maadili ndio umasikini wa kutisha!!
Biblia mbona imesema kuwa wazazi wasichokoze watoto Bali wawalee katika maadili meaning wakifeli Hilo jukumu obviously laana haiwezi kuwa reliable maana Kila kitu kina Haki na wajibu.
Mfano mzazi wangu alikua hafurahii mafanikio yangu yaani hata nikiwa chuo nikifaulu hawezi nipongeza. Nakumbuka nimepata ajira ya kwanza akanuna hata simu hapokei!! Nakumbuka hata siku naenda interview alininyima nauli na hakupokea simu sema ni vile tu bahati nasibu nikafanyiwa interview kwa simu!!. Na kabla sijapata kazi nlikua nmejiajiri Bado akawa ananikashifu kuwa siwezi fika kokote, nikaanza kuingiza pesa akaanza nifokea kuwa niache hiyo kazi hata kama inanipa Hela ila sio ya mtu mwenye degree!! Hahahah kazi Nako nikapata akanizimia simu!!
Kuna wakati huwa sielewi shida ni nini Hawa wazazi alafu Kuna mpuuzi anasema eti sijui utalaaniwa??
Hapo sijaongelea mama mzazi kabisa ambaye alikua hataki hata nilipiwe ada. Mimi sijawahi mwambia mtu Nina mama Wala kumpost sijui nani kama mama maana nikikumbuka niliyopitia huwa sihesabu kama nina mama. Tukiwa wadogo alikua yupo radhi tulale njaa Ila yeye ashibe!!
So kama Mungu ni mwenye haki kweli sidhani atapokea laana za watu wenye Roho za Giza kama hizo.
Ukiacha yote aliyowahi kunifanyia ikiwa ni pamoja na haki ya kumjua baba lkn hii kauli ( NATAKA KUAGIZA GARI LINGINE KWA SASA HVYO SIWEZI KUKUTUMIA MATUMIZI HUKO CHUONI )ndio ilinfanya nione ilikua bahati mbaya sana yeye kunizaa ingawaje hata upendo wa kinafki nimeushindwa.
Yan una mzazi si fukara lkn unaishi maisha ya kuomba omba yeye yupo busy kuhangaika kulinda ndoa yake and worse yeye ni mama, boalra angekua baba huenda ningempa excuse kalishwa limbwa na mke wake sasa mama nae kapewa limbwata na mume wake aisee wazazi ni mtihan mkubwa
ITS SEVEN YEARS NOW NAONA VEMA KUKAA MBALI NAYE, YANI MZAZI ANAKUCHUKIA MPAKA HUELEWI ULIKOSEA NINi
Duh wazazi wengine mizunguo kweli[emoji848]Nakuelewa sana mtu wangu. Hiki unachopitia ni kitu ambacho kuna watu wengi wanapitia halafu wanaamini ndio maisha so kuvumilia na kukubali upuuzi ndio namna ya kuishi. HII SI SAHIHI KABISA.
Mimi pia napitia the same story. Mimi mtoto wa pili kutoka mwisho. Tupo wa 5. Mzee wangu alikuwa mpambanaji sana kutoka mtoto wa mfugaji yaani wale watoto wa kuchunga ng'ombe na kutoroka kuja mjini kujipambania na kujiendeleza kwa elimu hadi akawa mhandisi wa mitambo na kufanya kazi wizara ya ujenzi chini ya magufuri kabla hajawa hata mbunge.
Mzee kapambana na kutafuta mali nyumba 3, biashara za maduka ya spare, trekta 2, mashamba matatu mbeya, mawilli morogoro, land Rover 110, land Rover 109, Isuzu tipper, na garage yenye vifaa vingi tu vya kisasa vya gereji. Hivi ni baadhi ya vitu vichache mzee aliacha. Na kulikuwa na salio Bank pia.
Picha linaanza mshua kafariki ghafla kwa shinikizo la damu. Tukabakia na bi mkubwa kama msimamizi na mshika mirathi. Watoto watano, wakwanza amemaliza form 6 kwa mbinde balaa mzee alikuwa kila siku anampa risala atulie asome yeye michezo, wapili nae mzee kuvuta alikuwa yupo kidato cha n'ne akasema yeye shule hataki, tusome sisi wadogo tu, watatu alikuwa form one, wanne ni mimi nikiwa darasa la 5, na wa mwisho akiwa vidudu ndio anataka kuanza la kwanza.
Sasa kutokea hapo ikawa bi mkubwa kwa kushauriana na sista wa kwanza ni kuuza kitu kimoja baada ya kingine bila consultation ya watu wenye ujuzi. Mfano waliuza gari Isuzu tipper kwa bei ya hasara ya 1 million kwa kupigwa sound na madalali. Then upotevu uliendelea kwa mali zingine ambazo ziliuzwa kwa bei za hasara. Me nikiwa mdogo na sina nguvu za kushauri au kukataa.
Haya yaliendelea kwa muda mrefu na mali nyingi zilitoweka katika mazingira ya uzembe sana. Na wahusika ni bi mkubwa, sista mtoto wa kwanza na bro mtoto wa pili, huyu watatu alikuwa mkoani alipokuwa akisoma boarding. Mimi na mdogo wangu tulikuwa nyumbani.
Mimi nilimaliza primary na kufaulu shule ya Serikali. Kipindi hicho ada kwa mwaka ni elfu 20. Lakini nilikuja kuilipa hiyo pesa mwenyewe nikiwa nakwenda chuo maana nilitakiwa kupeleka cheti na sio results slip. So nilikwenda kulipa ada ya miaka yote minne kwasababu sikuwahi kulipiwa ada na bi mkubwa. Kwakifupi pesa ambazo zilitolewa serikalini kwaajiri ya kusomesha watoto, maza alizigawanya kwa kuwapa wakubwa ambao hawakuwa shule, yule wa boarding alipewa account yake yote ambapo aliacha shule na kuanza kufanya upuuzi wa kujifanya mjasiliamali wa maswala ya miziki na kupromote wasanii akaishiwa kudhurumiwa pesa na mwenzake aliyekuwa mjanja wa mjini so akakosa shule na biashara chali.
Huku nyumbani pesa zangu mimi ambayo ilikuwa ni around 3 milion sikupata hata mia maana account ilikuwa ni ya kusimamiwa sikuwa nimetimiza miaka 18 kwa wakati huo. so bi mkubwa ndie alikuwa na access ya account yangu na ya mdogo wangu wa mwisho. Pesa zetu zilitumika bila sisi kujua na ziliisha haraka sana ndio maana nilipofaulu kwenda sekondari hakukuwa hata na 100 ya kunisapoti.
Huu uharibifu ulifanyika ndani ya muda mfupi na waliofanya ni bi mkubwa, sista mtoto wa kwanza, na bro mtoto wa pili. Bro alisema anataka kupambana akapewa tractor akaenda kulitelekeza huko hadi leo hii haijulikani kuwa aliuza au alifanyaje hiyo ni siri yake, sista kwa kushirikiana na boyfriend wake wa kipindi hicho waliuza mashamba na pesa kidogo wakamtumia maza nyingine sista akala bata na jamaa na kumhonga.
Maisha yakifika kipindi yakawa magumu maana ufujaji ulimaliza pesa zote zilizokuwapo kwenye akiba na asset ambazo zilikuwa za kuuzika kirahisi kama magari, trekta, mashamba, na mzigo kwenye maduka ya spea, waliviuza kwa bei za hasara chini ya bei ya soko so ni kama walivigawa bure na vingine kama tractor vilipotea bila taarifa.
Sasa ilifika kipindi naenda shule kwa shida napewa 200 ndio pocket money. Aisee nikikumbuka nashikwa hasira sana.
Fast forward leo, nilipita kwa shida sana ila MUNGU sio Jr makamba nikafika chuo na kumaliza salama kwa msada wa marafiki, na baadhi ya ndugu ambao walinisaidia kwa lawama sana kwa kuwa mzee alikuwa na mali walihisi mimi ni wale watoto wa kusema uongo jambo ambalo lilinifanya nikiwa na shida kufa na tai shingoni sikuwa tayari kumwambia ndugu bora nimuombe mtu baki au marafiki na familia zao wataweza nipa sapoti bila kuhoji.
Baada ya kumaliza elimu ilikuwa kama zari nilipata ajira ndani ya miezi mitatu tu. Kwa namna nilikuwa nachukia kuwa karibu na ile familia nilikopa hela kidogo nikaondoka nyumbani miezi minne tu baada ya mwezi wa kwanza kuanza kazi. Bi mkubwa alilalamika sana na kunitamkia kuwa naondoka kwasababu nimepata kazi badala ya kukaa na kuwasaidia mahitaji pale ndani.
Nilishajaribu kuweka mambo sawa kwa kulazimisha nyumba zile nyumba mbili kati ya tatu zipangishwe ili kodi isaidie maana nyumba walikuwa wakiishi ndugu so nilizungumza nao kiuungwana wakakubali kupisha. So kodi nikawa nashika mimi nampelekea bi mkubwa mahitaji yake ya ndani kama chakula na kadhalika.
Yule sista ambaye nae anaishi mkoani na jamaa mluga luga tu na bro nae asiyejisoma anaishi kwa mwanamke wake aliezaa nae, wakawa na mawasiliano maana bi mkubwa alikuwa na tabia za umbea za kuwaambia kila ninachofanya. Sasa sijui ni wivu wakaanza kusagia kunguni kuwa kwann nashika pesa za kodi nimuachie mama ashike mwenyewe, yule mtoto wa tatu alikuwa amepotelea mikoani huko maana aliacha shule asijue anafanya nini na maisha yake akarudi home kwa bi mkubwa na kuishi pale na akiwa anajifanya ni mtu wa kusali kumbe unafiki tu maana ndie alikuwa mchochezi.
Kuna siku bila taarifa bi mkubwa ananipigia simu kuwa yupo kwa wapangaji wamegoma kumpa kodi niwaambie kuwa yeye ndie mwenye nyumba na kuanzia sasa atakuwa anapokea yeye, aisee nilimind sana. Nikamuuliza kwann umeenda kwa wapangaji, akaanza kujibu kwa ukali kuwa nisimpande kichwani. Nikaona isiwe shida, ya nini kupata laana ya bure. Nikawaambia wapangaji wote kuwa huyo ni bi mkubwa watoe shaka.
Tokea siku ile nikaachana na maswala ya familia nikapiga kimya. Yule mtoto wa tatu na huyu mdogo wangu wa kike wakageuka masnitch namba moja wakiungana na wale wakubwa wawili kuwa wapinzani kwangu.
Kimsingi nikaamua kujitenga na familia kwasababu katika kitu sipendi ni kuishi na watu ambao hawaeleweki na wana mambo ya ajabu na upuuzi mwingi.
Haiwezekani watu kwa uzembe wenu mharibu na kufuja mali za familia halafu zinabakia chache anatokea moja wa wanafamilia anataka kuzisimamia vizuri mnamletea ligi kwa hoja za kipumbavu na za wivu wivu na mafigisu ya kifala. Mimi nikasema kama mtaniona. Huu ni mwaka wa tano naandika sijaenda tena na bi mkubwa ameshaniulizia sana. Naongea nae tu kwenye simu kumsalimia kawaida akianza kuniuliza nipo wapi au nafanya nini ntasitisha mazungumzo hapo hapo nikate simu na huwa siulizii chochote hapo nyumbani. Nikitaka kutoa sapoti nampigia mpwa wangu namuelekeza nilipo nampa kama vifurushi na pesa kidogo namtumia bi mkubwa napiga kimya.
Kuna familia nadhani tunakuwa tumezaliwa kimakosa. Sasa kulazimisha kublend nazo unaweza kufa kwa pressure. Mimi kama wewe nimeamua kukaa nao mbali na ninaona namna ninavyokwenda vizuri kwasasa maisha yangu yana utulivu na sina msongo wa mawazo
Huwa namuelewa sana mtu akizungumza kama wewe hivi.
Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
HahahahaDawa ya moto moto.
Ujinga na upumbavu wa kukumbatia nge vimewaua wengi sana.
Mzazi mshenzi kaa naye mbali.
Mimi father simpendi.
Kati ya watoto wake 3 ambao tulimaliza la saba siku moja Mimi pekee aliniombea nifeli na cha ajabu ni Mimi pekee nikatoboa tena shule ya vipaji maalumu.
Amezaa huko kwingine?Ukiacha yote aliyowahi kunifanyia ikiwa ni pamoja na haki ya kumjua baba lkn hii kauli ( NATAKA KUAGIZA GARI LINGINE KWA SASA HVYO SIWEZI KUKUTUMIA MATUMIZI HUKO CHUONI )ndio ilinfanya nione ilikua bahati mbaya sana yeye kunizaa ingawaje hata upendo wa kinafki nimeushindwa.
Yan una mzazi si fukara lkn unaishi maisha ya kuomba omba yeye yupo busy kuhangaika kulinda ndoa yake and worse yeye ni mama, boalra angekua baba huenda ningempa excuse kalishwa limbwa na mke wake sasa mama nae kapewa limbwata na mume wake aisee wazazi ni mtihan mkubwa
ITS SEVEN YEARS NOW NAONA VEMA KUKAA MBALI NAYE, YANI MZAZI ANAKUCHUKIA MPAKA HUELEWI ULIKOSEA NINi
Lete hiyo mifano mkuuHii ni kawaida kwa mabinti kuchukiwa na mama zao. Wala usijali sana. Ukitaka nikupe mifano 5 kutoka wanachama wa JF ambao mama zao wa kuwazaa wanawachukia bila sababu, nitakupa
Je yeye babaako anakumiss?Kuna mda watoto hatuna time na wazazi sio kwa sababu walitutesa ila kuna vitu walivipuuza na ss tukajikuta hatuoni umuhimu wao.
Mm sikulelewa na baba mzazi wala mama mzazi(alifariki nikiwa mdogo) nilikulia kwa mazao mkubwa (huyu ndio kama mama vile) ila ku a vitu watoto wake (sio wote) walikuwa wananifanyia kama kaubaguzi flan hv na vipigo visivyo na sababu za msingi na sikuwahi muona akivikemea had ikafikia sehem nikajikuta na mm najitambua kuwa ayo yote ni kwa sababu pale sio nyumbani toka hapo mm sinaga time nao wao wala yeye nikiwa mbali naweza maliza ata miezi 3 sijampigia na alijisikia vibaya.
Kwa mzee napo nimeanza kuishi nae nilipo maliza form 4 najikuta huwa hakuna ile bond ya baba na mtoto kabsa (kwangu mm ) Yan kuna mda nikiwa mbali najilazmisha tu japo kumtumia sms ata mara moja kwa mwezi asijejiona yupo pekee ake ila sijawahi kukaa et nikammis