Kwa wale ambao hamna maelewano mazuri na wazazi wenu

Kwa wale ambao hamna maelewano mazuri na wazazi wenu

Mtu mjinga kuwa mzazi si kigezo cha ujinga wake kuisha Akilini na kupewa heshima..

Kuna wazazi ni wajinga sana..

Baraka na laana kutoka kwa mzazi ni Hofu zilizojengeka kwamba wanaweza kukubariki au kukulaani kitu ambacho Sikweli.

Laana na baraka ni imani na mitazamo ya kufikirika imagination just an illusion.
 
Sasa kinachoongelewa hapa sio kuwachukia kuwachukia hawa wanaofanya maamuzi ya kuharibia wengine bali namna ya kuwakalia mbali ili uwepo wao usiendelee kukiathiri. Maana kuna tabia the more unakaa karibu na wahusika the more zinakuathiri na kukupa depression.

So sometimes kukaa mbali na kuwasiliana nao kwa huo umbali ni namna nzuri ya kuishi nao.

Sio mzazi wako ni mkorofi unamleta karibu na kulazimisha kuishi nae karibu na watoto wako yaani wajukuu zake matokeo anawafundisha tabia za hovyo.

Nitakupa mfano.

Kwenye ukoo wa mzee wangu, mama yake alikuwa na dada zake wawili. Yaani kulikuwa na mabibi watatu. Huyu bibi mkubwa ndio focus yetu leo.

Huyu bibi mimi sikuwahi kukaa nae ila story zake nazijua. Nimemuona kama mara tano tu katika maisha yangu tena ya utotoni baada ya hapo ni hadi anafariki sikuwahi muona tena.

Sasa kwenye story zake, yeye alipata watoto wawili moja wa kiume mwingine wa kike, wa kiume akawa padre hadi umauti wake. Wa kike alikuwa tu mfanyakazi wa serikalini.

So kuna kaka yao upande wa baba yaani babu yangu alikuwa ni dereva wa malori, alipokuwa anapiga mishe zake akileta mazaga akawa anampatia huyu bibi mkubwa awapatie na wenzake, yeye akawa anabania anaweka kando.

Sasa akawa anasomesha watoto wake ndio huyu mkubwa akawa padre halafu yule aliyefuata akawa mtumishi wa serikalini.

So huyu padre akawa aliondoka akiwa kijana mdogo sana kwenda kanisani so alimuacha mama yake na mdogo wake wa kike.

So baada ya kuwa padre akawa analeta zawadi na pesa za kusidia wanandugu na maagizo kabisa. Yule bibi akawa zile zawadi hafikishi kwa wahusika anachuna nazo. akamsomesha huyu wakike hadi akawa mtumishi na yeye akawa na watoto wa kiume wawili. So akawa anatumia misaada ya yule padre kuhudumia tena na wajukuu bila kusaidia walengwa wa misaada waliotumiwa na mtoa msaada na zawadi.

Tabia nyingine aliyokuwa nayo ni anaweza leo akapika labda nyama nzuri ya mchuzi, anakwenda kuiweka ndani uvunguni anafunga chumba, halafu ukifika muda wa msosi anachukua mboga ya jana au juzi labda Maharage ndio analeta pale chungu chake ili mle na hapo unaweza kuta yamechacha ila sababu ya njaa watu wanajikaza wanakula. Ile nyama ni hadi hayo maharage yaishe, so kesho au keshokutwa ndipo utaiona hiyo nyama na uombe iwe haijachacha sasa.

Hizi tabia akaja kuzirithi mwanawe wa kike sasa huyu ambaye ni shangazi yetu. Anauwezo wa kupika chakula cha watu kula kushiba ila huwa hataki kuona watu wanafurahia chakula, anapika chakula kidogo watu wanakula hawajashiba vizuri wanaenda kulala na matumbo hayajashiba. Anakwambia anaenda kwa bajeti.

Anatengeneza mikate ile ya skonzi halafu anaipigia hesabu yaani anahesabu ya wiki nzima kwamba kila mtu atakula skonzi mfano mbili mbili so anahesabu watu watano mara mbili jibu lake mara saba.

Sasa ole wako upatwe na njaa iliwe skonzi hata moja. Siku akijua zimepungua mtasemwa nyumba nzima na atatafuta wa kumsukumia kesi ili ale skonzi pungufu.

Sijawahi kumuelewa yule shangazi hadi leo swaga zake.

Mwisho wa siku maisha eventually kila mtu anakuwa na mji wake so utasumbua watu ila watajitegemea na kuwa na maisha yao hayo masharti hayatawapata tena.

Sasa hapa ni mfano wa jinsi tabia mbovu zinaweza safiri kwa mzazi kwenda kwa mtoto kwenda kwa mjukuu.

So its better kujitenga mapema ili matabia ya hovyo yasisambae.
 
Mwambie aache

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Niliwai kumkalisha chini nikamwambia ,baada ya kumwambia ukweli tangu siku hiyo mimi na yeye tumekuwa kama chui na paka anasema kwamba mimi nimemdharau, sijamuheshimu wakat nilikua namwambia ukwel tuu kwamba asifanye vitendo vya hovyo anaitia aibu familia
 
Niliwai kumkalisha chini nikamwambia ,baada ya kumwambia ukweli tangu siku hiyo mimi na yeye tumekuwa kama chui na paka anasema kwamba mimi nimemdharau, sijamuheshimu wakat nilikua namwambia ukwel tuu kwamba asifanye vitendo vya hovyo anaitia aibu familia
Wazazi ndo walivyo ukiwashauri wanasema umewadharau, wakitaka ufanye watakacho ukakataa wanasema umewadharau

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Wazazi ndo walivyo ukiwashauri wanasema umewadharau, wakitaka ufanye watakacho ukakataa wanasema umewadharau

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
Kuna wazazi ni wajinga pia.

Mtu anataka kutumia uzazi kama kigezo cha kupewa heshima kumbe na yeye ni mjinga tu .

Mzazi anaye jielewa hapangii mtoto maisha yeye akisha timiza wajibu wako wa malezi ana kuacha uka fight sasa kivyako vyako
 
Kuna wazazi ni wajinga pia.

Mtu anataka kutumia uzazi kama kigezo cha kupewa heshima kumbe na yeye ni mjinga tu .

Mzazi anaye jielewa hapangii mtoto maisha yeye akisha timiza wajibu wako wa malezi ana kuacha uka fight sasa kivyako vyako
Kuna wazazi wanazingua sana, ngoja mi nikae kimya tu

Sent from my M2006C3LG using JamiiForums mobile app
 
Sina shida na mzazi wala ndugu.. ila nina changamoto ya kuwa mvivu kuwapigia simu.

Kuna mama wakubwa wakianza kunisemea kwa mdogo wao ambaye ndio mama sasa, mama anakuja ananisema. Nikijitahidi ni hiyo week niliyosemwa, kisha narudi kuwa vile vile.

Sijui hata natokaje kwenye hicho kisanga.
We ni mimi aisee!
 
WAKUU VIPI HII KITU ISHA WAKUTA ?? LITOTO LIMOJA LA FAMILIA LINAFITINISHA(mostly hapa likiwa vyema kifedha). MZAZI(BABA*MAMA) Hapa tayari wote ni wastaafu tena hawajiwezi kifedha DHIDI YA MTOTO MWINGINE(mostly still young and high school or university times . ILI HUYU mWINGUNE ASHIKISHWE MINYORORO YA UNAFIKI ?
 
Hapo shida inawezekana ni utamaduni ambao wazazi wako wameutengeneza wa kutowaweka karibu na ndugu zenu ikiwamo kutowashirikisha katika shughuli mbali mbali za kifamilia. Hii itakuja kuwaathiri ninyi watoto wao hamtakuwa karibu hata kidogo.

Unajua mnaweza ona wachagga kama wachawi vile wanakwenda kila mwezi wa kumi na mbili kwa gharama kubwa ila lengo ni kuweka ukaribu wa watoto watambuane na ndugu zao, wahimize upendo kati yao, kujaliana na kuheshimiana na kusaidia popote wanapokuwa mbali.

Pia inasaidia hata kutazamana tabia sio mtu anakuwa na matukio ya kipuuzi puuzi kama wizi, magendo sijui uhalifu gani kila wiki yupo polisi, au dada zetu kuzaa hovyo na wanaume wasioeleweka mwishowe wanashindwa kumudu gharama za maisha wanaanza kusumbua ndugu kwann sasa wasikukimbie na kukuona kero.

Ukaribu ni muhimu sana ila unaharibiwa na wazazi kutokuwa na utamaduni wa kusema fulani haya jiandae weekend hii tunakwenda kwa baba mkubwa au kwa mama mdogo kutembea. Au tunakwenda kuwatembelea akina binamu.

Watoto wakikuzwa na hizi tabia utaona wanakuwa pamoja na wanakuwa karibu sana.
Umesema kweli kabisa yani.hujakosea kabisa. Home sisi pia ivyo hivyo yani japokua sie pia wachagga.
Sometimes yani unaona ni bonge la task kumpigia aunt,mjomba au cousins. Unapanga na maneno kabisa ya kuongea,convo inakua awkward flani ivi then unaishia na"nilikua nakusalimia tuu"
Yani no story kabisa...
 
Binadamu wajifunze kutafakari na kujiassess kama kweli wanaweza kuwa wazazi. Kazi kuhamasishana kuzaa wakati uwezo wa kuwa wazazi bora hamna!

Mamdo hayo ndiyo exactly yalikuwa mawazo yangu wakati nasoma hivi visa vya humu. Huwa tunahimizana kweli kuzaa watoto; tunaamini tunakuwa "fulfilled" tukishakuwa na watoto na Ile "mtoto raha jamani". Mtu akisema hataki kuzaa mtoto tunamshangaa na kumuona hamnazo; lakini kumbe that's the most "selfless" decision. Je hawa watoto wanaona maisha yao yapo fulfilled kwa sababu ya sisi wazazi wao au ndiyo tunaishia
kuwa -traumatize tu? Kulea ni kujitoa sadaka kwelikweli otherwise utajikuta unazalisha kizazi chenye majeraha na uchungu mwingi
 
Mamdo hayo ndiyo exactly yalikuwa mawazo yangu wakati nasoma hivi visa vya humu. Huwa tunahimizana kweli kuzaa watoto; tunaamini tunakuwa "fulfilled" tukishakuwa na watoto na Ile "mtoto raha jamani". Mtu akisema hataki kuzaa mtoto tunamshangaa na kumuona hamnazo; lakini kumbe that's the most "selfless" decision. Je hawa watoto wanaona maisha yao yapo fulfilled kwa sababu ya sisi wazazi wao au ndiyo tunaishia
kuwa -traumatize tu? Kulea ni kujitoa sadaka kwelikweli otherwise utajikuta unazalisha kizazi chenye majeraha na uchungu mwingi
Always napenda kukusoma, umeiweka vizuri zaidi mamdogo.

Mi nilisoma michango nikawa very worried, nikawa sina la ziada zaidi ya kuwaombea wapone. Unajua kuumizwa duniani ni kawaida, ila kuumizwa na watu wako wa karibu au waliokuleta duniani...... inaogopesha sana!

Btw, you are missed maa.
 
Always napenda kukusoma, umeiweka vizuri zaidi mamdogo.

Mi nilisoma michango nikawa very worried, nikawa sina la ziada zaidi ya kuwaombea wapone. Unajua kuumizwa duniani ni kawaida, ila kuumizwa na watu wako ni waliokuleta duniani...... inaogopesha sana!

Btw, you are missed maa.
Ukiumizwa na mtu kama mzazi au dada, kaka, shangazi, mamdogo, mamkubwa, mjomba, binadamu etc watu ambao walitakiwa kukulinda na kukupa faraja huwa inakuja na traumatizing effect maana hawa ni watu wapo katika life yako na ni sehemu ya familia yako.

So no matter how unawakwepa wanakuwa around you can't escape them the only option ni kukaa nao mbali sana tena sana na kuua mawasiliano ili uokoe nafsi yako isiendelee kuteketea.
 
Kuna makosa mengine mtu hawezi kumsamehe mzazi mfano mzuri ni rafiki ndugu yangu mmoja ambaye baba yake ni mganga wa Jadi huko Shinyanga, huyu mzee alikuwa na wivu wa wazi kwa mtoto wake na mara zote alipinga jamaa kwenda shuleni na hata tupo advance level mzee wake alikuwa hampi sapport yoyote mpaka tuna maliza tunaingia chuoni mzee hana mawasiliano na jamaa wala hatumi pesa.

Sisi ndiyo tunamsaidia hapa na pale jamaa alipomaliza chuo na kupata kazi mzee akaanza maneno kuwa jamaa hasaidii familia kwanza kamtelekeza baba yake kisa amesoma anadharau. Mimi nikamshauri omba msamaha kwani mzazi hakosei ( hizi ni fikra zangu wakati huo saivi nimebadilika).

Kikawekwa kikao jamaa akaomba msamaha mambo mengine yanaendelea. Alivyotaka kuoa ikawa shida mzee hamtaki mwanamke wa jamaa ila tuli force tukamaliza vizuri.

Baada ya ndoa mzee akaleta maneno kuwa mwali akae pale nyumbani ili wachunguze kumbe yule mzee ana nia mbaya na mke wa jamaa. Kwa kutumia dawa zake za kiganga alifarakanisha uhusiano kati ya jamaa (mtoto wake) na mkewe.

Baadaye ikaja kugundulika huyu mzee anamahusiano na mke wa mtoto wake baada ya mke kushika mimba jamaa akaikataa. Sasa wewe hapo unaweza kusamehe uchawi wa hivo? Mimi sio mnafki hapa nilimshauri mwamba akate mawasiliano.

Mfano Mimi sijawahi kuungwa mkono kitu na baba yangu wala mama yangu. Ila waliwapenda sana mpaka sasa wanawapenda dada na kaka yangu na wadogo zangu ila mimi nikawa kama black sheep sihirikishwi kwa chochote lakini sasa hivi nishajua ile familia ni karmic relationship. Hakuna picha hata moja nimepiga nipo na wazazi wangu au nimepiga na baba au mama hakuna wala hawajawahi kuniweka status.

Ila sina ubaya nao japo siongei nao kila mtu na maisha yake na sasa nina familia nimeoa lakini sikuwa shirikisha kitu wala sikutaka mchango wao. Na wala hawana taarifa za life yangu kuwa nina watoto lakini hawajawahi kuwaona.

Huu ni mwaka wa saba sijawahi kukanyaga nyumbani kwetu lakini sio kama kwa ubaya cz nina amani kila mtu sijamkosea kitu. Kama shida walianza wao na uhusiano ni kama daraja kama hukunipenda na kuweka uhusiano mzuri na mimi utotoni usidhani ukubwani nita kupa time wala nafasi Never.
Heee .. niko hapa namwangalia mwanangu naomba Mungu aniepushie hayo yote nisije kukwaza wanangu
 
Niwaambieni tu ukweli ndugu zangu.
Kinachowacost wazazi wengi ambao hata humu mmo na nawashangaa mnachangia mada utasema familia zenu mnaziendesha sawa. Kinawacost MFUME DUME!!!!
Mna ujinga mwingi sana kichwani. Huwa mnaamini wewe kama baba huwezi kukosea, yaani we uwe kilaza darasani miaka yote uje upelekeshe familia nzima uzeeni kweli? Kubali kushauriwa kubali kukosolewa. Kubali kusaidiwa na watoto au mkeo.

Huwa nasoma sana comment zenu mna mawazo ya kiduanzi sana na ndo matokeo yake watoto wenu nao watakuja kuandika nyuzi kama hizi mbeleni. Jitu linainua sharubu linachangia mada unajiuliza huyu huwa anamzalisha mkewe kabisa na anajiita Baba?

Badilikeni. Watoto wanatakiwa kulelewa kwa kueleweshwa, sio ubabe. Na unayomfanyia mzazi mwenzako nayo yanawaathiri. Unadhani kama unamnyanyasa mkeo, mtoto wako atakupenda? Acheni ujinga badilikeni lasivyo watoto wataendelea kuwachukia milele nawatawatelekeza hivyo hivyo
 
Wapo wazazi ambo Ni barakankwa watoto wao, lakn pia wapo wengine ambao wanajihusisha na nguvu za Giza Ni balaaaa kwa familia. Mungu atupe mwisho mwema...
Umeongea safi sana Ila sio wazazi tu hata ndugu kuna ndugu ni nongwa asikwambie mtu, sasa mama hapo yaweza ikawa jamaa akimwambia na yeye anaenda kueleza kwa ndugu mwingine sasa huyo ndugu ndio hataki jamaa atoboe kwa hio anampiga pin, jamaa ilibidi amuulize mama info zake anavujisha kwa nani mwingine?

Ndugu baadhi sio yaan ndugu fitna ndugu baadhi ni nongwa hawapendi utoboe kuzidi wao mama yaweza ikawa hakua na kosa maana hakuna mzazi asiependa mwanae afanikiwe especially wamama wanapenda sana watoto wao waliowazaa watoboe wawe wanawakumbuka hata kwa sukari na chumvi tu au kipande cha nguru doti ya khanga au kitenge,

Kuna wamama nilikua napita sehemu wanasimuliana kuna mama alizaa watoto mfululizo watu wakawa wanamsemea anazaa km panya, sasa wale watoto wamekua wamesoma wamepata kazi wametoboa sasa hivi mama anakula mafao ya uzeeni maana watoto wanamhudumia nikawa nawasikia wanashauriana nao wazae ili nao wanufaike km yule mama anavyonufaika kutoka kwa watoto wake

I will be back again sijamaliza..
 
Niwaambieni tu ukweli ndugu zangu.
Kinachowacost wazazi wengi ambao hata humu mmo na nawashangaa mnachangia mada utasema familia zenu mnaziendesha sawa. Kinawacost MFUME DUME!!!!
Mna ujinga mwingi sana kichwani. Huwa mnaamini wewe kama baba huwezi kukosea, yaani we uwe kilaza darasani miaka yote uje upelekeshe familia nzima uzeeni kweli? Kubali kushauriwa kubali kukosolewa. Kubali kusaidiwa na watoto au mkeo.

Huwa nasoma sana comment zenu mna mawazo ya kiduanzi sana na ndo matokeo yake watoto wenu nao watakuja kuandika nyuzi kama hizi mbeleni. Jitu linainua sharubu linachangia mada unajiuliza huyu huwa anamzalisha mkewe kabisa na anajiita Baba?

Badilikeni. Watoto wanatakiwa kulelewa kwa kueleweshwa, sio ubabe. Na unayomfanyia mzazi mwenzako nayo yanawaathiri. Unadhani kama unamnyanyasa mkeo, mtoto wako atakupenda? Acheni ujinga badilikeni lasivyo watoto wataendelea kuwachukia milele nawatawatelekeza hivyo hivyo
Huo sio mfumo dume. Mfumo dume ni kitu cha tofauti sana ukilinganisha na hicho umesema hapo. Hapo umeongelea shida ya mtu binafsi.

So na hawa wamama wanaobakia kulea watoto wao wa kike hovyo wanakuwa na tabia za hovyo mfano akina kajala, akina Monalisa, akina shilole tuite mfumo jike?

Nadhani unatakiwa kufahamu askari anapokuwa mhalifu haifai kusema jeshi la polisi linatengeneza wahalifu wanaovaa uniform za askari ila tunasema askari polisi amekwenda kinyume na utaratibu wa kazi yake na matakwa ya weledi wake.

Sasa inapotokea Mwanaume anashida kwenye mfumo wake wa kuendesha na kuongoza familia yake hatusemi mfumo dume, bali tunamsema huyo muhusika pekee yake kama mtu baki na utaratibu wake.

Mara nyingi mwanaume akiendesha familia vema mnaanza kusema nyuma ya mwanaume mwenye mafanikio kuna mwanamke (kupenda sifa nzuri na kukwepa lawama) ila pale anapokuwa amekwenda vibaya basi mnasema mfumo dume ni shida. Mfumo dume haukuwahi na hautakuja kuwa shida.
 
Huo sio mfumo dume. Mfumo dume ni kitu cha tofauti sana ukilinganisha na hicho umesema hapo. Hapo umeongelea shida ya mtu binafsi.

So na hawa wamama wanaobakia kulea watoto wao wa kike hovyo wanakuwa na tabia za hovyo mfano akina kajala, akina Monalisa, akina shilole tuite mfumo jike?

Nadhani unatakiwa kufahamu askari anapokuwa mhalifu haifai kusema jeshi la polisi linatengeneza wahalifu wanaovaa uniform za askari ila tunasema askari polisi amekwenda kinyume na utaratibu wa kazi yake na matakwa ya weledi wake.

Sasa inapotokea Mwanaume anashida kwenye mfumo wake wa kuendesha na kuongoza familia yake hatusemi mfumo dume, bali tunamsema huyo muhusika pekee yake kama mtu baki na utaratibu wake.

Mara nyingi mwanaume akiendesha familia vema mnaanza kusema nyuma ya mwanaume mwenye mafanikio kuna mwanamke (kupenda sifa nzuri na kukwepa lawama) ila pale anapokuwa amekwenda vibaya basi mnasema mfumo dume ni shida. Mfumo dume haukuwahi na hautakuja kuwa shida.
Ukitaka nichambue yote nnayotaka kusema ntamaliza kitabu cha page 800. Kwanza nimeongelea kitu ambacho nna experience nacho.

Sijawahi kulelewa na single mom so ukinitajia kajala na monalisa siwezi kuelezea changamoto zao.

Changamoto nlizoziona mimi zimetokana na mfumo dume. Narudia tena! Mfumo dumeeee!!!! Janaume linajiamulia tu kufanya vitu halitaki ushauri wala nini end of the day familia nzima Inakuja kuingia matatizoni na kulipa mateso ambayo mwanaume huyo ameyasababisha.

Majanga ni mengi na kila mtu ana ya kwake. Kwa waliopitia ya wazazi wa kike nao waseme.
 
Back
Top Bottom