Kwa wale ambao hamna maelewano mazuri na wazazi wenu

Kwa wale ambao hamna maelewano mazuri na wazazi wenu

Kupitia uzi huu nimejifunza mambo mengi Sana nilidhan mm pekee ndyo napitia magumu ya familia yangu kumbe tupo wengi Sana

Kikubwa tuchukulie changamoto hizo tulizopitia kurekebisha familia zetu (watotowetu) tiwatendee mema tuwasikilize na tuwashaur vyema


Binafsi mzaz wangu wa kiume alinipa kila kitu kadir ya uwezo wake lakn kitu kimoja pekee udikteta Tena kwangu tuu kutonisikiliza Wala kinishirikisha kwa Jambo lolote badala yake wanasikilizwa watoto wengne na wanakaa nakupanga mambo ya familia mm naambiwa tu

Jambo hili lilinipa msongo wa mawazo Sana ukizingatia mm nilikuwa mtoto mkubwa kat ya wote lakn n mtoto wa nje ya ndoa na nilijipeleka tu kwa baba yangu baada ya shida kuwa nyingi huko nilokokuwa nakaa (kwa Bibi) ujio wangu pale unaonekana uliharibu kanuni na taratibu zao lakn nifanye nn n mm shida zilinikimbiza wakat mzaz wangu anakila kitu alikuwa engineer wa tanroads mkoa X

Hali ya kutengwa kimaamuzi iliendelea had nilipofika chuo pesa za matumizi had nimpigie mdogo wangu ndyo itumwe ukimpigia mzee hapokei simu na akipiga atanilaumu kwanini nilimpigia mda wa kazi ukipiga jion atakuambia yupo na marafk zake nisimsumbue

Amekuja kustaafu mm nipo chuo mwaka wa 4 namalizia akawagawia wanae wote Kia's Cha pesa Kama 5M kwa kila mtu mm sikupata hata shilingi na hii nilikuja kuambiwa na mdogo wangu alikuja kufunga mzgo wa biashara akaniambia wewe pesa yako utafanyia Nini ? Ndipo nikajua kumbe wamepewa pesa

Lakn MUNGU n mwema maisha Sasa yanasonga Nina familia yangu najitahid kuilea kwa upendo ili nisije kosea Kama mm nilivyoona nakosewa

Kwa Sasa mzazi wangu anailaumu simshirikishi katika maamuz ya mambo yangu najitenga Sana na familia sipigi simu mara kwa Mara

Sent using Jamii Forums mobile app
Pole sana broo,huu uzi unasikitisha sana.
 
Unajua wazazi hawajui kuwa pia matendo yao kwa watoto ndio hupelekea baraka za kuishi muda mrefu, kuwa na hekima na afya.

Hebu jiulize kwann wazazi wetu wa kiume yaani Baba pamoja na kujitoa sana kwaajiri ya familia ila muda wao wa kuishi ni mdogo na hata wakiwa wazee watoto huwatenga.

Ni matendo yao na ukaribu wao na watoto ndio chanzo. Mtoto akiwa na furaha na amani na mzazi kila siku moyo huwa unamuenda mbio kama hajaongea na mzazi na pia humuombea mzazi huruma na uzima kwa MUNGU ili aishi muda mrefu na kuwa na afya.

Mtoto au watoto wanapokuwa na connection nzuri na mzazi na kutokuwa na fikra au mawazo ya kudhurumiwa au kuonewa na wazazi hii hali hujenga bondi nzito sana na yenye nguvu na kusaidia mzazi kuwa na baraka za kuishi muda mrefu.

Ndio maana mama zetu wameishi miaka mingi sababu ndani ya mioyo yetu tumewapa hadhi ya utakatifu kutoka na kujitoa kwao kwetu.

But hawa wamama wa miaka hii sijui MUNGU ndie atajua. Maana matendo yao yanaonesha wazi yatafuta baraka zote za uzeeni.
Mzee mbona kama unaandika kinyume chake,yaani baraka zitoke kwa watoto ziende kwa wazazi??hata mzazi akosee vipi mtoto anawajibika kwa mzazi wake kulinda hadhi yauungu aliyopewa na mwenyezi Mungu.ndio maana imeandikwa waheshimu baba namama yako siku zako zipate kuongezeka,nasio mzazi aheshimu watoto wake.sipingi kua kuna wazazi vimeo sana,ila mambo haya nadhani yanamiongozo flani ya kuepusha mkanganyiko ktk jamiii ndio maana hata kama mzazi hakumtunza vyema mwanae wakti wautototoni mzazi huyo anaweza asipate laana,lkn mtoto kutokumtunza mzazi wake ktk uzee wake laana inamuhusu.
 
30 min mnaongea nini, yani mm nikiongea nae mda ukiwa mrefu ni sek 46 na mara nying ni sekunde 23, ujambo sijambo shikamoo, nawajulia hali shukran tumemaliza[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
Daahhh???!!sec23???!!jitahidi uweke mazingira mazuri nababayako kwa ajili yafaida yako ww mwenyewe na nafsi yako.
 
Daahhh???!!sec23???!!jitahidi uweke mazingira mazuri nababayako kwa ajili yafaida yako ww mwenyewe na nafsi yako.
Wazee wachache sana wanaongea muda mrefu kwenye simu na hapo napo ukute ni baba na mtoto wa kike au baba na mtoto wa kiume ambae ana HELA wanashauriana juu ya mambo ya biashara au vitu flani vya maisha.. Ila wengi ni salamu na blaa blaa chache dakika 1 huwa haiishi may b kama kuna mambo ya kifamilia hayajakaa sawa pia mnayaongelea.
 
Kupitia uzi huu nimejifunza mambo mengi Sana nilidhan mm pekee ndyo napitia magumu ya familia yangu kumbe tupo wengi Sana

Kikubwa tuchukulie changamoto hizo tulizopitia kurekebisha familia zetu (watotowetu) tiwatendee mema tuwasikilize na tuwashaur vyema


Binafsi mzaz wangu wa kiume alinipa kila kitu kadir ya uwezo wake lakn kitu kimoja pekee udikteta Tena kwangu tuu kutonisikiliza Wala kinishirikisha kwa Jambo lolote badala yake wanasikilizwa watoto wengne na wanakaa nakupanga mambo ya familia mm naambiwa tu

Jambo hili lilinipa msongo wa mawazo Sana ukizingatia mm nilikuwa mtoto mkubwa kat ya wote lakn n mtoto wa nje ya ndoa na nilijipeleka tu kwa baba yangu baada ya shida kuwa nyingi huko nilokokuwa nakaa (kwa Bibi) ujio wangu pale unaonekana uliharibu kanuni na taratibu zao lakn nifanye nn n mm shida zilinikimbiza wakat mzaz wangu anakila kitu alikuwa engineer wa tanroads mkoa X

Hali ya kutengwa kimaamuzi iliendelea had nilipofika chuo pesa za matumizi had nimpigie mdogo wangu ndyo itumwe ukimpigia mzee hapokei simu na akipiga atanilaumu kwanini nilimpigia mda wa kazi ukipiga jion atakuambia yupo na marafk zake nisimsumbue

Amekuja kustaafu mm nipo chuo mwaka wa 4 namalizia akawagawia wanae wote Kia's Cha pesa Kama 5M kwa kila mtu mm sikupata hata shilingi na hii nilikuja kuambiwa na mdogo wangu alikuja kufunga mzgo wa biashara akaniambia wewe pesa yako utafanyia Nini ? Ndipo nikajua kumbe wamepewa pesa

Lakn MUNGU n mwema maisha Sasa yanasonga Nina familia yangu najitahid kuilea kwa upendo ili nisije kosea Kama mm nilivyoona nakosewa

Kwa Sasa mzazi wangu anailaumu simshirikishi katika maamuz ya mambo yangu najitenga Sana na familia sipigi simu mara kwa Mara

Sent using Jamii Forums mobile app
I hope mna mahusiano mazuri na wadogo zako mpaka saahii,maana ulivoandika looks like they're not a problem. Ni mzee wenu tuu ndo kukosa busara ya kuwalea kwa usawa.
I hope you have them.pole sana.
 
Nakuelewa sana mtu wangu. Hiki unachopitia ni kitu ambacho kuna watu wengi wanapitia halafu wanaamini ndio maisha so kuvumilia na kukubali upuuzi ndio namna ya kuishi. HII SI SAHIHI KABISA.

Mimi pia napitia the same story. Mimi mtoto wa pili kutoka mwisho. Tupo wa 5. Mzee wangu alikuwa mpambanaji sana kutoka mtoto wa mfugaji yaani wale watoto wa kuchunga ng'ombe na kutoroka kuja mjini kujipambania na kujiendeleza kwa elimu hadi akawa mhandisi wa mitambo na kufanya kazi wizara ya ujenzi chini ya magufuri kabla hajawa hata mbunge.

Mzee kapambana na kutafuta mali nyumba 3, biashara za maduka ya spare, trekta 2, mashamba matatu mbeya, mawilli morogoro, land Rover 110, land Rover 109, Isuzu tipper, na garage yenye vifaa vingi tu vya kisasa vya gereji. Hivi ni baadhi ya vitu vichache mzee aliacha. Na kulikuwa na salio Bank pia.

Picha linaanza mshua kafariki ghafla kwa shinikizo la damu. Tukabakia na bi mkubwa kama msimamizi na mshika mirathi. Watoto watano, wakwanza amemaliza form 6 kwa mbinde balaa mzee alikuwa kila siku anampa risala atulie asome yeye michezo, wapili nae mzee kuvuta alikuwa yupo kidato cha n'ne akasema yeye shule hataki, tusome sisi wadogo tu, watatu alikuwa form one, wanne ni mimi nikiwa darasa la 5, na wa mwisho akiwa vidudu ndio anataka kuanza la kwanza.

Sasa kutokea hapo ikawa bi mkubwa kwa kushauriana na sista wa kwanza ni kuuza kitu kimoja baada ya kingine bila consultation ya watu wenye ujuzi. Mfano waliuza gari Isuzu tipper kwa bei ya hasara ya 1 million kwa kupigwa sound na madalali. Then upotevu uliendelea kwa mali zingine ambazo ziliuzwa kwa bei za hasara. Me nikiwa mdogo na sina nguvu za kushauri au kukataa.

Haya yaliendelea kwa muda mrefu na mali nyingi zilitoweka katika mazingira ya uzembe sana. Na wahusika ni bi mkubwa, sista mtoto wa kwanza na bro mtoto wa pili, huyu watatu alikuwa mkoani alipokuwa akisoma boarding. Mimi na mdogo wangu tulikuwa nyumbani.

Mimi nilimaliza primary na kufaulu shule ya Serikali. Kipindi hicho ada kwa mwaka ni elfu 20. Lakini nilikuja kuilipa hiyo pesa mwenyewe nikiwa nakwenda chuo maana nilitakiwa kupeleka cheti na sio results slip. So nilikwenda kulipa ada ya miaka yote minne kwasababu sikuwahi kulipiwa ada na bi mkubwa. Kwakifupi pesa ambazo zilitolewa serikalini kwaajiri ya kusomesha watoto, maza alizigawanya kwa kuwapa wakubwa ambao hawakuwa shule, yule wa boarding alipewa account yake yote ambapo aliacha shule na kuanza kufanya upuuzi wa kujifanya mjasiliamali wa maswala ya miziki na kupromote wasanii akaishiwa kudhurumiwa pesa na mwenzake aliyekuwa mjanja wa mjini so akakosa shule na biashara chali.

Huku nyumbani pesa zangu mimi ambayo ilikuwa ni around 3 milion sikupata hata mia maana account ilikuwa ni ya kusimamiwa sikuwa nimetimiza miaka 18 kwa wakati huo. so bi mkubwa ndie alikuwa na access ya account yangu na ya mdogo wangu wa mwisho. Pesa zetu zilitumika bila sisi kujua na ziliisha haraka sana ndio maana nilipofaulu kwenda sekondari hakukuwa hata na 100 ya kunisapoti.

Huu uharibifu ulifanyika ndani ya muda mfupi na waliofanya ni bi mkubwa, sista mtoto wa kwanza, na bro mtoto wa pili. Bro alisema anataka kupambana akapewa tractor akaenda kulitelekeza huko hadi leo hii haijulikani kuwa aliuza au alifanyaje hiyo ni siri yake, sista kwa kushirikiana na boyfriend wake wa kipindi hicho waliuza mashamba na pesa kidogo wakamtumia maza nyingine sista akala bata na jamaa na kumhonga.

Maisha yakifika kipindi yakawa magumu maana ufujaji ulimaliza pesa zote zilizokuwapo kwenye akiba na asset ambazo zilikuwa za kuuzika kirahisi kama magari, trekta, mashamba, na mzigo kwenye maduka ya spea, waliviuza kwa bei za hasara chini ya bei ya soko so ni kama walivigawa bure na vingine kama tractor vilipotea bila taarifa.

Sasa ilifika kipindi naenda shule kwa shida napewa 200 ndio pocket money. Aisee nikikumbuka nashikwa hasira sana.

Fast forward leo, nilipita kwa shida sana ila MUNGU sio Jr makamba nikafika chuo na kumaliza salama kwa msada wa marafiki, na baadhi ya ndugu ambao walinisaidia kwa lawama sana kwa kuwa mzee alikuwa na mali walihisi mimi ni wale watoto wa kusema uongo jambo ambalo lilinifanya nikiwa na shida kufa na tai shingoni sikuwa tayari kumwambia ndugu bora nimuombe mtu baki au marafiki na familia zao wataweza nipa sapoti bila kuhoji.

Baada ya kumaliza elimu ilikuwa kama zari nilipata ajira ndani ya miezi mitatu tu. Kwa namna nilikuwa nachukia kuwa karibu na ile familia nilikopa hela kidogo nikaondoka nyumbani miezi minne tu baada ya mwezi wa kwanza kuanza kazi. Bi mkubwa alilalamika sana na kunitamkia kuwa naondoka kwasababu nimepata kazi badala ya kukaa na kuwasaidia mahitaji pale ndani.

Nilishajaribu kuweka mambo sawa kwa kulazimisha nyumba zile nyumba mbili kati ya tatu zipangishwe ili kodi isaidie maana nyumba walikuwa wakiishi ndugu so nilizungumza nao kiuungwana wakakubali kupisha. So kodi nikawa nashika mimi nampelekea bi mkubwa mahitaji yake ya ndani kama chakula na kadhalika.

Yule sista ambaye nae anaishi mkoani na jamaa mluga luga tu na bro nae asiyejisoma anaishi kwa mwanamke wake aliezaa nae, wakawa na mawasiliano maana bi mkubwa alikuwa na tabia za umbea za kuwaambia kila ninachofanya. Sasa sijui ni wivu wakaanza kusagia kunguni kuwa kwann nashika pesa za kodi nimuachie mama ashike mwenyewe, yule mtoto wa tatu alikuwa amepotelea mikoani huko maana aliacha shule asijue anafanya nini na maisha yake akarudi home kwa bi mkubwa na kuishi pale na akiwa anajifanya ni mtu wa kusali kumbe unafiki tu maana ndie alikuwa mchochezi.

Kuna siku bila taarifa bi mkubwa ananipigia simu kuwa yupo kwa wapangaji wamegoma kumpa kodi niwaambie kuwa yeye ndie mwenye nyumba na kuanzia sasa atakuwa anapokea yeye, aisee nilimind sana. Nikamuuliza kwann umeenda kwa wapangaji, akaanza kujibu kwa ukali kuwa nisimpande kichwani. Nikaona isiwe shida, ya nini kupata laana ya bure. Nikawaambia wapangaji wote kuwa huyo ni bi mkubwa watoe shaka.

Tokea siku ile nikaachana na maswala ya familia nikapiga kimya. Yule mtoto wa tatu na huyu mdogo wangu wa kike wakageuka masnitch namba moja wakiungana na wale wakubwa wawili kuwa wapinzani kwangu.

Kimsingi nikaamua kujitenga na familia kwasababu katika kitu sipendi ni kuishi na watu ambao hawaeleweki na wana mambo ya ajabu na upuuzi mwingi.

Haiwezekani watu kwa uzembe wenu mharibu na kufuja mali za familia halafu zinabakia chache anatokea moja wa wanafamilia anataka kuzisimamia vizuri mnamletea ligi kwa hoja za kipumbavu na za wivu wivu na mafigisu ya kifala. Mimi nikasema kama mtaniona. Huu ni mwaka wa tano naandika sijaenda tena na bi mkubwa ameshaniulizia sana. Naongea nae tu kwenye simu kumsalimia kawaida akianza kuniuliza nipo wapi au nafanya nini ntasitisha mazungumzo hapo hapo nikate simu na huwa siulizii chochote hapo nyumbani. Nikitaka kutoa sapoti nampigia mpwa wangu namuelekeza nilipo nampa kama vifurushi na pesa kidogo namtumia bi mkubwa napiga kimya.

Kuna familia nadhani tunakuwa tumezaliwa kimakosa. Sasa kulazimisha kublend nazo unaweza kufa kwa pressure. Mimi kama wewe nimeamua kukaa nao mbali na ninaona namna ninavyokwenda vizuri kwasasa maisha yangu yana utulivu na sina msongo wa mawazo
Huwa namuelewa sana mtu akizungumza kama wewe hivi.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Pole Sana mkuu, naomba niku pm
 
Natambua sana mkuu jinsi wazazi wetu walivyo changamoto ndio maana nimeandika mada hii
Inauma mno

Hivi nama akiwa changamoto si ndio inauma zazid??
How did you cope with???
Siko karibu nae so sijui mengi kuhusu yeye. Mkuu,kuna baadhi ya hali unajikuta tu automatically uko hivo.
Hii hali imepelekea mpaka huwa natafuta kitu cha msingi sana katika maisha yangu ila sikioni,hapa namaanisha kitu ambacho hata ukikipoteza wenyewe wanadai utaumia kihisia.
Kwa kifupi nimeharibika sana psychologically,na nishakomaa katika hali hiyo ya uharibifu.
 
Sina shida na mzazi wala ndugu.. ila nina changamoto ya kuwa mvivu kuwapigia simu.

Kuna mama wakubwa wakianza kunisemea kwa mdogo wao ambaye ndio mama sasa, mama anakuja ananisema. Nikijitahidi ni hiyo week niliyosemwa, kisha narudi kuwa vile vile.

Sijui hata natokaje kwenye hicho kisanga.
Hapo shida inawezekana ni utamaduni ambao wazazi wako wameutengeneza wa kutowaweka karibu na ndugu zenu ikiwamo kutowashirikisha katika shughuli mbali mbali za kifamilia. Hii itakuja kuwaathiri ninyi watoto wao hamtakuwa karibu hata kidogo.

Unajua mnaweza ona wachagga kama wachawi vile wanakwenda kila mwezi wa kumi na mbili kwa gharama kubwa ila lengo ni kuweka ukaribu wa watoto watambuane na ndugu zao, wahimize upendo kati yao, kujaliana na kuheshimiana na kusaidia popote wanapokuwa mbali.

Pia inasaidia hata kutazamana tabia sio mtu anakuwa na matukio ya kipuuzi puuzi kama wizi, magendo sijui uhalifu gani kila wiki yupo polisi, au dada zetu kuzaa hovyo na wanaume wasioeleweka mwishowe wanashindwa kumudu gharama za maisha wanaanza kusumbua ndugu kwann sasa wasikukimbie na kukuona kero.

Ukaribu ni muhimu sana ila unaharibiwa na wazazi kutokuwa na utamaduni wa kusema fulani haya jiandae weekend hii tunakwenda kwa baba mkubwa au kwa mama mdogo kutembea. Au tunakwenda kuwatembelea akina binamu.

Watoto wakikuzwa na hizi tabia utaona wanakuwa pamoja na wanakuwa karibu sana.
 
Kumbe tupo wengi!!!!!

Ngoja niishie hapa
Funguka tupe hata kidogo majanga yako, uzuri unaposhare story yako unawafanya na wengine kupata faraja na kupunguza depression maana watajua kumbe hawapo pekee yao katika kupitia misukosuko ya kifamilia na mwisho wa siku tunapeana hata mbinu za kusurvive hizi hali.

Imagine kuna mtu anajiuliza mimi hii familia yangu siwezi kuitenga sasa naishi nayo vipi ila anakuja hapa anaona story ya namna watu kadhaa ambao familia zao zimewaletea mazengwe na mbinu wametumia kukabiriana nazo na kuwaweka kando ili wasiwaletee upuuzi wao. Na cha zaidi utapata namna za kuishi kwa kujitegemea bila muingiliana na wanafamilia wasiojitambua bila kujihisi unahatia yoyote tofauti na jamii wanavyosisitiza kuwa damu ni nzito kuliko maji.

Kimsingi kushare kunakusaidia wewe na wale wanaokuzunguka kuwa salama. Lakini muhimu zaidi kunakuondolea hatari ya kupatwa na msongo wa mawazo yaani kuwa depressed bila sababu za msingi.

Toa shaka sababu hakuna mtu ambaye anaweza kukujua au kukufuatilia personal life yako nje ya hapa kwasababu umetoa story yako. So toa shaka kuwa free. Kuwa kama mtu anayekojoa kwenye bahari wakati yupo ndani ya maji, au mtu ambaye amebanwa na shuzi halafu kasimama katikati ya uwanja wa mpira na hakuna mtu yoyote uwanja mzima namna atakuwa huru kuliachia hilo shuzi.

Au kama mtu anayekojoa kichakani huko porini raha yake na uhuru wake katika kujiachia. Ni raha sana. Wewe toa shaka.
 
Tanzania ina watu wengi ambao kila mtu anakua kwenye mfumo tofauti na mwingine, wewe kama umekua kwenye familia bora yenye upendo basi ni vyema sana ila sio huu utoto unao andika hapa ni aibu mno. Grow up man
Kuna watu kwasababu yeye anakula anashiba, wazazi wake wapo hai wote, na wanawasaliana vizuri na ana ushirikiano mzuri na ndugu zake wa familia yake aliyokulia na wanasaidiana vema basi anaamini dunia yote watu wote wanapitia the same life style yaani hakuna changamoto kwa wengine na kwamba hawa wanaoleta story hapa na confessions zao basi wengi wao haya maisha wamejitakia na pengine wanachangamoto zao binafsi ila hakunaga familia inaweza kuwa tatizo kwa mojawapo wa mtoto.


Kwa kifupi kuna watu hawana exposure. Wanaishi in an eggshell so hawajui nini kipo nje ya maisha yao yenye comfort.

So huyu ni wa kumsamehe na kumuombea aje kujionea kwa watu wakaribu ili ajifunze na sio kuja hapa kukanusha experience za wahanga wa hizi changamoto ambao wamezipitia. TOXIC AND NARCISSISTIC FAMILIES ARE REAL.
 
Tusisahau kuwa wazazi nao ni wanadamu. Wanapokosa hekima au busara katika malezi ya watoto wanatakiwa kunyooshwa na sio kuogopwa au kukaliwa kimya.

Mimi mzazi akileta habari za tofauti ninamwambia. Akiniletea vifungu vya Bible ninamletea sheria na maadili ya malezi bora.

Hii mifumo ya kuwafanya wazazi kutokuwa accountable na makosa yao ni mifumo mibaya sana ambayo inafanya dunia kuwa na watoto wa hovyo sana.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Hakika kabisa. Lowama siku zote zinapelekwa Kwa watoto. Piga picha baba aliyetelekeza Mtoto ambaye hajitambui na hajui lolote Na hawezi jambo lolote.. anahitaji msaada. Mtoto anakua Hadi anafika mkubwa baba Hana habari naye. Siku akifanikiwa Baba anajitokeza anahitaji asaidiwe. Hili hapana aisee

Hata kwenye biblia tunaona wazazi karibia wote tunawaona wanatunza na kujali watoto wao. Manabii na mitume. Hata wafalme walikua wanaandaa watoto wao.

Sasa hii unayoitetea hapa Haina maana. Kuna wazazi hawana sofa za kuitwa baba na mama kutokana na matendo Yao Kwa watoto.



Sent from my TECNO KG6 using JamiiForums mobile app
 
Nakuelewa sana mtu wangu. Hiki unachopitia ni kitu ambacho kuna watu wengi wanapitia halafu wanaamini ndio maisha so kuvumilia na kukubali upuuzi ndio namna ya kuishi. HII SI SAHIHI KABISA.

Mimi pia napitia the same story. Mimi mtoto wa pili kutoka mwisho. Tupo wa 5. Mzee wangu alikuwa mpambanaji sana kutoka mtoto wa mfugaji yaani wale watoto wa kuchunga ng'ombe na kutoroka kuja mjini kujipambania na kujiendeleza kwa elimu hadi akawa mhandisi wa mitambo na kufanya kazi wizara ya ujenzi chini ya magufuri kabla hajawa hata mbunge.

Mzee kapambana na kutafuta mali nyumba 3, biashara za maduka ya spare, trekta 2, mashamba matatu mbeya, mawilli morogoro, land Rover 110, land Rover 109, Isuzu tipper, na garage yenye vifaa vingi tu vya kisasa vya gereji. Hivi ni baadhi ya vitu vichache mzee aliacha. Na kulikuwa na salio Bank pia.

Picha linaanza mshua kafariki ghafla kwa shinikizo la damu. Tukabakia na bi mkubwa kama msimamizi na mshika mirathi. Watoto watano, wakwanza amemaliza form 6 kwa mbinde balaa mzee alikuwa kila siku anampa risala atulie asome yeye michezo, wapili nae mzee kuvuta alikuwa yupo kidato cha n'ne akasema yeye shule hataki, tusome sisi wadogo tu, watatu alikuwa form one, wanne ni mimi nikiwa darasa la 5, na wa mwisho akiwa vidudu ndio anataka kuanza la kwanza.

Sasa kutokea hapo ikawa bi mkubwa kwa kushauriana na sista wa kwanza ni kuuza kitu kimoja baada ya kingine bila consultation ya watu wenye ujuzi. Mfano waliuza gari Isuzu tipper kwa bei ya hasara ya 1 million kwa kupigwa sound na madalali. Then upotevu uliendelea kwa mali zingine ambazo ziliuzwa kwa bei za hasara. Me nikiwa mdogo na sina nguvu za kushauri au kukataa.

Haya yaliendelea kwa muda mrefu na mali nyingi zilitoweka katika mazingira ya uzembe sana. Na wahusika ni bi mkubwa, sista mtoto wa kwanza na bro mtoto wa pili, huyu watatu alikuwa mkoani alipokuwa akisoma boarding. Mimi na mdogo wangu tulikuwa nyumbani.

Mimi nilimaliza primary na kufaulu shule ya Serikali. Kipindi hicho ada kwa mwaka ni elfu 20. Lakini nilikuja kuilipa hiyo pesa mwenyewe nikiwa nakwenda chuo maana nilitakiwa kupeleka cheti na sio results slip. So nilikwenda kulipa ada ya miaka yote minne kwasababu sikuwahi kulipiwa ada na bi mkubwa. Kwakifupi pesa ambazo zilitolewa serikalini kwaajiri ya kusomesha watoto, maza alizigawanya kwa kuwapa wakubwa ambao hawakuwa shule, yule wa boarding alipewa account yake yote ambapo aliacha shule na kuanza kufanya upuuzi wa kujifanya mjasiliamali wa maswala ya miziki na kupromote wasanii akaishiwa kudhurumiwa pesa na mwenzake aliyekuwa mjanja wa mjini so akakosa shule na biashara chali.

Huku nyumbani pesa zangu mimi ambayo ilikuwa ni around 3 milion sikupata hata mia maana account ilikuwa ni ya kusimamiwa sikuwa nimetimiza miaka 18 kwa wakati huo. so bi mkubwa ndie alikuwa na access ya account yangu na ya mdogo wangu wa mwisho. Pesa zetu zilitumika bila sisi kujua na ziliisha haraka sana ndio maana nilipofaulu kwenda sekondari hakukuwa hata na 100 ya kunisapoti.

Huu uharibifu ulifanyika ndani ya muda mfupi na waliofanya ni bi mkubwa, sista mtoto wa kwanza, na bro mtoto wa pili. Bro alisema anataka kupambana akapewa tractor akaenda kulitelekeza huko hadi leo hii haijulikani kuwa aliuza au alifanyaje hiyo ni siri yake, sista kwa kushirikiana na boyfriend wake wa kipindi hicho waliuza mashamba na pesa kidogo wakamtumia maza nyingine sista akala bata na jamaa na kumhonga.

Maisha yakifika kipindi yakawa magumu maana ufujaji ulimaliza pesa zote zilizokuwapo kwenye akiba na asset ambazo zilikuwa za kuuzika kirahisi kama magari, trekta, mashamba, na mzigo kwenye maduka ya spea, waliviuza kwa bei za hasara chini ya bei ya soko so ni kama walivigawa bure na vingine kama tractor vilipotea bila taarifa.

Sasa ilifika kipindi naenda shule kwa shida napewa 200 ndio pocket money. Aisee nikikumbuka nashikwa hasira sana.

Fast forward leo, nilipita kwa shida sana ila MUNGU sio Jr makamba nikafika chuo na kumaliza salama kwa msada wa marafiki, na baadhi ya ndugu ambao walinisaidia kwa lawama sana kwa kuwa mzee alikuwa na mali walihisi mimi ni wale watoto wa kusema uongo jambo ambalo lilinifanya nikiwa na shida kufa na tai shingoni sikuwa tayari kumwambia ndugu bora nimuombe mtu baki au marafiki na familia zao wataweza nipa sapoti bila kuhoji.

Baada ya kumaliza elimu ilikuwa kama zari nilipata ajira ndani ya miezi mitatu tu. Kwa namna nilikuwa nachukia kuwa karibu na ile familia nilikopa hela kidogo nikaondoka nyumbani miezi minne tu baada ya mwezi wa kwanza kuanza kazi. Bi mkubwa alilalamika sana na kunitamkia kuwa naondoka kwasababu nimepata kazi badala ya kukaa na kuwasaidia mahitaji pale ndani.

Nilishajaribu kuweka mambo sawa kwa kulazimisha nyumba zile nyumba mbili kati ya tatu zipangishwe ili kodi isaidie maana nyumba walikuwa wakiishi ndugu so nilizungumza nao kiuungwana wakakubali kupisha. So kodi nikawa nashika mimi nampelekea bi mkubwa mahitaji yake ya ndani kama chakula na kadhalika.

Yule sista ambaye nae anaishi mkoani na jamaa mluga luga tu na bro nae asiyejisoma anaishi kwa mwanamke wake aliezaa nae, wakawa na mawasiliano maana bi mkubwa alikuwa na tabia za umbea za kuwaambia kila ninachofanya. Sasa sijui ni wivu wakaanza kusagia kunguni kuwa kwann nashika pesa za kodi nimuachie mama ashike mwenyewe, yule mtoto wa tatu alikuwa amepotelea mikoani huko maana aliacha shule asijue anafanya nini na maisha yake akarudi home kwa bi mkubwa na kuishi pale na akiwa anajifanya ni mtu wa kusali kumbe unafiki tu maana ndie alikuwa mchochezi.

Kuna siku bila taarifa bi mkubwa ananipigia simu kuwa yupo kwa wapangaji wamegoma kumpa kodi niwaambie kuwa yeye ndie mwenye nyumba na kuanzia sasa atakuwa anapokea yeye, aisee nilimind sana. Nikamuuliza kwann umeenda kwa wapangaji, akaanza kujibu kwa ukali kuwa nisimpande kichwani. Nikaona isiwe shida, ya nini kupata laana ya bure. Nikawaambia wapangaji wote kuwa huyo ni bi mkubwa watoe shaka.

Tokea siku ile nikaachana na maswala ya familia nikapiga kimya. Yule mtoto wa tatu na huyu mdogo wangu wa kike wakageuka masnitch namba moja wakiungana na wale wakubwa wawili kuwa wapinzani kwangu.

Kimsingi nikaamua kujitenga na familia kwasababu katika kitu sipendi ni kuishi na watu ambao hawaeleweki na wana mambo ya ajabu na upuuzi mwingi.

Haiwezekani watu kwa uzembe wenu mharibu na kufuja mali za familia halafu zinabakia chache anatokea moja wa wanafamilia anataka kuzisimamia vizuri mnamletea ligi kwa hoja za kipumbavu na za wivu wivu na mafigisu ya kifala. Mimi nikasema kama mtaniona. Huu ni mwaka wa tano naandika sijaenda tena na bi mkubwa ameshaniulizia sana. Naongea nae tu kwenye simu kumsalimia kawaida akianza kuniuliza nipo wapi au nafanya nini ntasitisha mazungumzo hapo hapo nikate simu na huwa siulizii chochote hapo nyumbani. Nikitaka kutoa sapoti nampigia mpwa wangu namuelekeza nilipo nampa kama vifurushi na pesa kidogo namtumia bi mkubwa napiga kimya.

Kuna familia nadhani tunakuwa tumezaliwa kimakosa. Sasa kulazimisha kublend nazo unaweza kufa kwa pressure. Mimi kama wewe nimeamua kukaa nao mbali na ninaona namna ninavyokwenda vizuri kwasasa maisha yangu yana utulivu na sina msongo wa mawazo
Huwa namuelewa sana mtu akizungumza kama wewe hivi.

Sent from my JKM-LX1 using JamiiForums mobile app
Mali imeleta shida, imagine bila mali kungekuwa na matokeo mabaya kimahusiano kama uliyonayo sasa.
 
Back
Top Bottom