Kwa wale ambao hamna maelewano mazuri na wazazi wenu

Kwa wale ambao hamna maelewano mazuri na wazazi wenu

uhusiano ni kama daraja kama hukunipenda na kuweka uhusiano mzuri na mimi utotoni usidhani ukubwani nita kupa time wala nafasi Never
Hapa ndo kwenye tatizo mkuu, bond mbovu kati yangu na mazaa inatutesa sasa hivi.
Nahisi anaumia lakini na mimi nakosa la kufanya coz sijaishi nae mda mrefu, sijamzoea sana.
 
Me Mzee wangu kavurugwa na mama wa kàmbo ili anione Mimi kinyesi,,,, inafika muda Mzee unampigia Simu hapokei kwa kuhofia nitamlilia shida haya Mzee wangu uliikuta missed call basi nitafute uniulize kunani kijana wangu mbona ulinipigia Simu mida Fulani,Hana kabisa time kisingizio ubuzy wa kazi kweli Mzee wangu,,, au akipokea hata haniulizi mwanangu unaendeleaje na majukumu,,,, Mzee anafahamu fika kuwa maisha yangu yameharibiwa na walimwengu hivyo msaada wake nauhitaji lakini Hana time na Mimi. Anyway namuacha apande mazao yake kikamilifu kwani atakachokuja kuvuna Mungu ndiye anajua.
Dahh! Pole sana ndugu yangu... bin-Adam sisi... mhhhh! Kesho kwa mungu kutakuwa na mengi sana hadharani 😔😔😔
 
Kwakweli nimejitahidi kurudisha mahusiano na baba yangu ila nimeshindwa..japo kosa ni lake mwenyewe. Ila mwenyewe hataki tena anapokea simu tu kwakua namba yangu hajaisevu.

Najitahidi kumsamehe nashindwa kabisa. Maana anayofanya sio kwangu tu hadi kwa ndugu wengine...kiufupi hataki uzao wake wote.
Mzee hakutaka majukumu... alitaka zake kula mtungi na kugonga tu! 😅👍🏾
 
Watz wengi wanamatatizo ya Afya ya Akili

Yaani Mimi Akili yangu bado hipo vizuri siwezi kumchukia Mtu awe au ndugu maana njaa na umasikini na Matatizo ya Afya Akili vikiungana lazima muwachukie watu. Eti Mtu anamchukia Mzazi au Mzazi anamchukia mtoto what a kid?
Ata kushindwa kuchukia unapochukizwa au kuendelea kujikomba kwa watu wasio kuthamin ni tatizo la akili pia
 
Maisha ni mitihani. Kuna wazazi ni mitihani na kuikabili unahitaji uvumilivu wa Hali ya juu. kama hakuna mahusiano mazuri Kati yako na mzazi , wewe maintain your distance. Akiwa na shida msaidie pale unaweza. Ila kamwe usijihusishe na maisha yake kwa ukaribu. Akipiga simu anasema ana shida, mrushie salio. Mengine mwaachie mwenyewe.
 
Ukiacha yote aliyowahi kunifanyia ikiwa ni pamoja na haki ya kumjua baba lkn hii kauli ( NATAKA KUAGIZA GARI LINGINE KWA SASA HVYO SIWEZI KUKUTUMIA MATUMIZI HUKO CHUONI )ndio ilinfanya nione ilikua bahati mbaya sana yeye kunizaa ingawaje hata upendo wa kinafki nimeushindwa. Yan una mzazi si fukara lkn unaishi maisha ya kuomba omba yeye yupo busy kuhangaika kulinda ndoa yake and worse yeye ni mama, boalra angekua baba huenda ningempa excuse kalishwa limbwa na mke wake sasa mama nae kapewa limbwata na mume wake aisee wazazi ni mtihan mkubwa
ITS SEVEN YEARS NOW NAONA VEMA KUKAA MBALI NAYE
YANI MZAZI ANAKUCHUKIA MPAKA HUELEWI ULIKOSEA NINi
Aiseee, pole sana inaumiza mno.!
 
Haya mambo ya familia sometimes acha vitu viflow kama vilivyo yani hata kama unaona sio sawa hasa MAMBO YA HELA yani utagombana na wazazi mpaka ndugu. Kuhusu upendo kwa watoto hilo lipo kila familia hamuwezi kupendwa sawa pia kuna mambo yanafanyika unaona kabisa kuna upendeleo ila kama unapambana unapata riziki yako haviwezi kukupa tabu kabisaa unaishi maisha yako.. Mengine kubali kukosolewa kama kijana kweli unaweza jisahau hata kuwapigia wazazi simu hasa mama zetu wanapenda sana kupigiwa simu hata kama mara moja kwa week na sisi watoto tokana na majukumu tunajisahau kabisa so akilalamika mwambie tu ntakupigia mama sio kwamba nafanya makusudi. Kama mzazi alikuwa na uwezo wa kukusaidia akakutelekeza na kukukaushia aisee KARMA imtafune japo kwa muda flani mpaka ajute na umwambie kabisa ukweli kama atakasirika asuse shauri yake kama anajielewa ataomba radhi MSAMEHE msonge mbele.

USIKUBALI PAST YAKO IKUTESE NA KUKUFUNGA KUISHI MAISHA YA KUUMIZA WENGINE KISA WEW ULITENDEWA.
 
Kupitia uzi huu nimejifunza mambo mengi Sana nilidhan mm pekee ndyo napitia magumu ya familia yangu kumbe tupo wengi Sana

Kikubwa tuchukulie changamoto hizo tulizopitia kurekebisha familia zetu (watotowetu) tiwatendee mema tuwasikilize na tuwashaur vyema


Binafsi mzaz wangu wa kiume alinipa kila kitu kadir ya uwezo wake lakn kitu kimoja pekee udikteta Tena kwangu tuu kutonisikiliza Wala kinishirikisha kwa Jambo lolote badala yake wanasikilizwa watoto wengne na wanakaa nakupanga mambo ya familia mm naambiwa tu

Jambo hili lilinipa msongo wa mawazo Sana ukizingatia mm nilikuwa mtoto mkubwa kat ya wote lakn n mtoto wa nje ya ndoa na nilijipeleka tu kwa baba yangu baada ya shida kuwa nyingi huko nilokokuwa nakaa (kwa Bibi) ujio wangu pale unaonekana uliharibu kanuni na taratibu zao lakn nifanye nn n mm shida zilinikimbiza wakat mzaz wangu anakila kitu alikuwa engineer wa tanroads mkoa X

Hali ya kutengwa kimaamuzi iliendelea had nilipofika chuo pesa za matumizi had nimpigie mdogo wangu ndyo itumwe ukimpigia mzee hapokei simu na akipiga atanilaumu kwanini nilimpigia mda wa kazi ukipiga jion atakuambia yupo na marafk zake nisimsumbue

Amekuja kustaafu mm nipo chuo mwaka wa 4 namalizia akawagawia wanae wote Kia's Cha pesa Kama 5M kwa kila mtu mm sikupata hata shilingi na hii nilikuja kuambiwa na mdogo wangu alikuja kufunga mzgo wa biashara akaniambia wewe pesa yako utafanyia Nini ? Ndipo nikajua kumbe wamepewa pesa

Lakn MUNGU n mwema maisha Sasa yanasonga Nina familia yangu najitahid kuilea kwa upendo ili nisije kosea Kama mm nilivyoona nakosewa

Kwa Sasa mzazi wangu anailaumu simshirikishi katika maamuz ya mambo yangu najitenga Sana na familia sipigi simu mara kwa Mara

Sent using Jamii Forums mobile app
Mkuu wakati mwingine siyo akili zao,,,tusiwalaumu sana,,,aliyelishwa Limbwata hajijui kama karogwa
 
Mimi mpaka kufikia umri huu sijawahi kushuhudia wala kuona upendo wa dhati kutoka kwa mtu yeyote. Kwanza sijalelewa kabisa na mzazi yeyote yule. Nilibahatika kuishi na mlezi kidogo tu nae nikaona ananiongezea mapicha picha tu katika maisha yangu nikatemana nae.

Ninae mzazi mmoja, wenyewe mnamuita "Mama", ila kuhusu huyu Mama naomba niishie hapa hapa.
 
Mkuu hongera kwa bandiko bora sana,ila tambua kwamba kuna wazazi ni changamoto sana yani. Sitaki kusema sana ila tambua hivyo,mpaka likukute ndipo utajua ni nini namaanisha.
Natambua sana mkuu jinsi wazazi wetu walivyo changamoto ndio maana nimeandika mada hii
Inauma mno
Mimi mpaka kufikia umri huu sijawahi kushuhudia wala kuona upendo wa dhati kutoka kwa mtu yeyote. Kwanza sijalelewa kabisa na mzazi yeyote yule. Nilibahatika kuishi na mlezi kidogo tu nae nikaona ananiongezea mapicha picha tu katika maisha yangu nikatemana nae.

Ninae mzazi mmoja, wenyewe mnamuita "Mama", ila kuhusu huyu Mama naomba niishie hapa hapa.
Hivi nama akiwa changamoto si ndio inauma zazid??
How did you cope with???
 
Back
Top Bottom