Kwa wale Mabanker na wakereketwa, tukutane hapa tuambiambiane ya kwetu...

Ukitaka kuwa successful banker unatakiwa uwe unahamahama,Ukiwa na experience na mabenki kuanzia manne au matano maisha yatakuwa mazuri.Usikae benki moja zaidi ya miaka miwili you will never grow na mawazo yako yatakuwa finyu sana
Ukiwa nje unatamani ufanye kazi benki...ila yule mfanyakazi wa benki anapambana kila siku atoke pale aende sehemu nyingine.....bank wanafaidi wale walio kwenye top positions
 
Ukiwa nje unatamani ufanye kazi benki...ila yule mfanyakazi wa benki anapambana kila siku atoke pale aende sehemu nyingine.....bank wanafaidi wale walio kwenye top positions
Top position wanafaidi, posho za mafuta ,na mazagazaga kibao ,per Dm kubwa nk .....ila nnje ya hapo,chini huku streee.....mwingine anaaanza tama life na ukwasi walionao wateja .
Na uwepo Wa bank Nyingi (washindani)umeleta maisha ya kuishi kwa target za kufa mtu
 
Mkuu zile camera inshort sio rahisi kufanya uchunguzi , access ni ngumu , ni process na mpaka issue ifike kwenda camera room imekuwa ngumu , pia hara cashier akipata short mil 1 kuiona kwenye camera ni issue. Unaweza kaa 5 hrs huoni imekuaje kuwaje ,pia baadhi ya wateja NAO SOMETIMES NI WEzi NA WAONGO ,anaweza kumsakizia cashier kumbe anazo mfukoni zingine au ukimzidishia harudi ,imetoka na kwenye camera Mara Nyingi issue .
Maoni tu
 
True ! Not that easy
 
Mkuu technology gani hiyo ya 5 hours kuangalia movement za teller thru Cctv, hiyo ni issue ya dakika 5 Manager amepata complain anafungua pc yake anaangalia transaction hiyo yenye short imefanyika saa ngapi anatrace teller cubic number anatrace video 5 or 10 minutes before the transaction zinaangaliwa movements zote za teller kama aliangusha noti chini ili aje aiokote baadaye inaonekana.
Kuna teller mmoja alikuwa anakula michongo na majambazi kama mtu anakuja kuchukua pesa nyingi anawa text akitoka mteja anatoka na watu ambao wanaenda kumuumiza mbele. Hiyo trend ikawa reported kwa kuwa kulikuwa na mteja kila akihudumiwa na huyo cashier akitoka nje anaona kuna aina fulani ya kufuatiliwa akaripoti huo wasiwasi wake. Management ika trace ktk camera big withdrawals anazoprocess yule teller wakaona kabisa anachukua simu anawatext wazee wa kazi. Siku nyingine akaja jamaa anawithdraw pesa nyingi teller kabla kuprocess akachukua simu, ile anamaliza tu kuwatext jamaa zake police wakamkamata wakamtia pingu wakachukua simu wakaona madudu yoote. Jamaa ananyea debe mwaka wa 3 sasa
Miaka hii ukitaka kuwa mwizi inabidi uwe na akili sana
 
Kuwa banker sio professional ni job hata mtu wa economics,commerce,account,computer science anaweza fanya hio kazi ..........professional ni Kama law,medicine,engineering........
 
Professional bankers wapo kwa bongo wanakuwa qualified baada ya kusomea CPB na kufaulu exams (CERTIFIED PUBLIC BANKER).
Kuwa banker sio professional ni job hata mtu wa economics,commerce,account,computer science anaweza fanya hio kazi ..........professional ni Kama law,medicine,engineering........
 
Certified Professional Banker,sorry
Pamoja mkuu,lakini kwa nini banks zinarihusiwa kuajili watu wasio profession kufanya hio kazi?.......huwezi kuta muhasibu anatibu ama,daktari ni wakili.......ama mwalimu anajenga jengo(contractor).
 
Nyie bankers walala hoi sikilizeni.

Mtu akija kudeposit kuanzia 5mil ujue ashaweka pembeni sio chini ya lak 8 kwa ajili ya mambo madogo madogo

Sasa ukimuambia kuna pungufu ya elf 50 anakupa tu na kukuona choko kama ni mwanamke atachukua namba zako ukalipe hiyo kwenye AC za Babylon Excutive Lodge.

Mbona kuna bankers na maafisa mikopo kibao Bank kubwa wapo real sana anakuambia bro leo sio njema tunalindana na siku inaenda njema kwa kua anajua deposit inasoma ngapi.

Kukwapua hivyo visent hakuna maana jenga urafiki wa maana utakula vingi zaidi
 
Majukumu ya benki ni mapana kidogo na benki ni institution hata ukienda muhimbili Hospital kunawahasibu mpaka social workers.Vile vile hata benki kuna wahasibu,watu wa I.T na kadhalika hata mtu aliyesoma sociology /social work anaweza kufanya kazi benki upande wa marketing na sales maana inainvolve kukutana na watu.Ukitoa upande wa social work na I.T mfanyakazi wa benki lazima awe na knowledge ya accounts au finance.Kama unafani tofauti zaidi ya hizo tatu na uko benki upande wa operations au credit ujue hr kakubeba
Pamoja mkuu,lakini kwa nini banks zinarihusiwa kuajili watu wasio profession kufanya hio kazi?.......huwezi kuta muhasibu anatibu ama,daktari ni wakili.......ama mwalimu anajenga jengo(contractor).
 
Mtu wa I.T kuwa benki teller,mtu wa marketing kuwa manager,............mtu wa economics kuwa afisa mikopo............mtu wa account kufanya marketing ni kawaida kwa benki nyingi za kibongo......Hadi mtu wa agroeconimcs unamkuta.........hutokuja kuta muhasibu anafanya round hospitali kamwe.
 
Mtu wa I.T kuwa benki Teller ni hatari sana
 
Ni kweli mkuuu, Ku track fraud ni rahisi lakini sio Ku track short ndogo ndogo na uwizi Wa elfu 10 ,20,50 aise ........kama ni hivyo kungekuwa hakuna short ...ila kuna short had mil 3 mtu anaata na haionekani .....jua tu banking systems na procedures zina complication Nyingi ..,............ Jaribu chombeza staff .......zaidi let's finish here ....
 
Bank hawachagui mtu ,unaanza chini wanakutrain ...... Kuna fani mtu anafundishika na bank kuna IT Wa kufa mtu ,ila sio branch in large........
 
Hivi ni nani anayegundua suspicious transactions??
 
Eee bana Mabanker mpo? Aisee usawa wetu umekaa vibaya sana.

Naomba tushee mawazo,vikwazo na experiences mbali mbali zilizopo ofisini kwetu na field.

Kama kwangu wateja wetu wanafilisika sana, yani mtu kapewa loan ya 300m, rejesho la pili hoi!
Michezo hiyo, 300M rejesho la pili linakata kivipi?
 
Nadhani huijui banking industry boss. kwa taarifa tu some of the best treasurers kwenye mabank hapo ya hapo azikiwe na ohio ni watu wenye IT background.
 
Naongelea upande wa tellers sio general naushahidi mtu alikuwa anafanya kazi Teller aliyesomea I.T walivyokuja auditors wakapendekeza atolewe mle kwa sababu ya profession yake ni rahisi kucheza na systems
Nadhani huijui banking industry boss. kwa taarifa tu some of the best treasurers kwenye mabank hapo ya hapo azikiwe na ohio ni watu wenye IT background.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…