Kwa wale tuliowahi kwenda kwa waganga wa kienyeji, tukutane hapa

Kwa wale tuliowahi kwenda kwa waganga wa kienyeji, tukutane hapa

Mimi binafsi nimekulia kwenye familia ya dini. Na toka nipo mdogo , nilishawahi kukiri, hata itokee nini kwenye haya maisha, Siwezi kumuacha Bwana Yesu , Kwani yeye Ndio kila kitu kwangu , hakuna kinachomshinda.

Na siku zote nikiona mtu akizungumzia masuala ya kwenda kwa mganga Sijui nilikua namuonaje, yani nilikua nawaona waswahili, hawajenda shule na nilikua Naona wanapoteza muda kufanya huo upuuzi. Inshort nikikuona una mambo ya kishirikina nakutenga na kukukwepa kama ukoma.

Ila Maisha yana siri nzito sana, Na hapa duniani binadamu tumeumbiwa mitihani mizito sana, Mitihani ambayo unafikia hatua kabisa unakiri kwa nafsi yako Mungu hayupo, na kama yupo basi sio kwa ajili yako, Yupo kwa ajili ya watu wengine.

Nakumbuka nilipata changamoto za maisha, nilijitahidi kuomba na kufunga kutokana na dini yangu , kwa kweli nilisimama imara sana na Dini yangu , nilimwabudu Mungu katika roho na kweli. Kama nilivyosema, binadamu tumeumbiwa changamoto kubwa sana hapa duniani, kuna matatizo mengine yanakupelekea kufanya mambo ambayo toka uzaliwe hujawahi kufikiria kuwa utakuja kufanya. Nikatubu kwa Mungu na kuvunja laana zote za ukoo zinazonitesa, pia bado ikagonga mwamba .

Nilikata tamaa sana , niliomba na kulia kwa Mungu anisaidie lakini Mungu hakunisikia. Nikajiuliza Mungu kuna watu hawakujui wewe, hawana muda na nyumba za Ibada, na maisha yao wamejaa furaha tele, wanaishi maisha ya anasa, mambo yao yanawaendea vizuri, wanafanya uchafu wote hapa duniani, Mimi nimeamua kukukimbilia Wewe bado unaniaibisha, mpaka inafikia hatua watu wanakutukana Mungu wako yuko wapi ? unajifanya mlokole kila siku kanisani na mambo yako hayaeleweki.

Kwa kweli kama binadamu, ilifikia stage nikasema NIMECHOKA, Ndipo ikanibidi nitafute njia mbadala ya kuweza kutatua changamoto zangu Sugu iliyonisumbua kwa mda mrefu. Nakumbuka usiku nilioamua kuwa ngoja niende kwa mganga, nililia sana , Kwani nilikua sitaki kabisa kufanya hivyo, nililia kama mtoto mdogo. Ila nilivyomaliza kulia, uchungu wote ukaisha na sikujutia chochote kuhusu maisha yangu mapya niliyoamua kuyachagua.

Tofauti na watu wengine ambao huangaika huku na kule kutafuta waganga, Mimi naweza kusema nilipata bahati, Kwani nilipata rafiki ambayo alikua anafanya sana hayo mambo , so alikua anajua waganga wengi sana kuanzia kigoma, pemba, Mbeya , Tanga na sehem nyingine nyingi.

Sijui niseme ni shetani alikua ameniingia, wakati naenda kwa mganga kwa mara ya kwanza, moyo wangu ulijawa na furaha sana, na nilikua nimeshaamini kuwa ntaenda kufanikiwa Tatizo langu . Yani moyo ulikua mwepesi na kujisemea pengine huku Ndipo nilipotakiwa kwenda miaka yote hiyo, Sijui kwa nini nilikua napoteza mda kwenda kanisani.

Basi safari yangu ya kwenda kwa waganga ikaanzia hapo, na niseme tu , mambo yangu kweli yalibadilika, na kwenda kwa waganga ndo ikawa kama fashion kwangu. Na niweze kusema tu toka nimeanza kujihusisha na ushirikina ni miaka mitatu sasa , na hakuna hata siku ambayo nimewahi kujuta wala kutamani nilipotoka.

Je na wewe ilikuaje mara yako ya kwanza kwenda kwa waganga? Nini kilikusukuma?View attachment 1431306View attachment 1431307View attachment 1431308




Sent from my iPhone using JamiiForums
Zamani ulikuwa genius sasa umekengeuka na kwenda kutafuta hekima kwa hao vinyago hapo. Naomba Yesu Kristo akurudishe kwenye hekima na maarifa yake kwani hakuna linaloshindikana kwa Yesu Kristo. Safari yako ya kurudi kwa Yesu inaanza sasa.
 
Siku nikienda nitaleta mrejesho ila kitakachonipeleka moja ni kufanya utafiti kwamba je,hivi ni kweli hizo tunguli zina effect kwenye maisha..?
Na la pili nadhani itakuwa mapenzi😅
Kama sio hilo basi nawania kiti Cha ikulu full stop😅
 
Waganga anakupa solution fasta...ila maombi sometimes watu wanavunja au wanapiga vitu wasivyojua vimetegewa wapi..wachawi Wana formula...Sasa we unaoomba kitu ambacho hujui kilitegwa vipi..ilo Ni tatizo...pia walokole wengi Hawajui jinsi ya kuita malaika wa kuwasaidia..hawajui majina ya MUNGU yenye nguvu ambayo ukitaja lazima kitu kiwe..ila wachawi wanajua kukusanya roho..pepo na jinni na kuyatuma watakavyo.......Sasa bora niende zangu kwa mganga aniambie fasta na kusolve tatizo bila kupoteza muda
 
Mimi sina imani na waganga Ila ilitokea kasumba flani ilinibidi niende sio MTU wa dini deep yaani nafika taja shida zangu akachukua na maelezo alikuwa ni shekhe flani anatumia ubani na tuvitu twa harufu marashi pia akaanza kuniganga Mimi nam enjoy naona anachora matairi ya gari kwenye liungo lake duh since naingia nilikuwa sina imani kabisa kufupisha alinigonga hela akataka nirudi sijui awasiliane na jini gani nirudi after two day na pesa iliyonona kidogo majibu yake ya awali kwenye tatizo langu hayakuwa na muelekeo sikurudi na paka Leo wengi makanjanja.
Tubaki njia kuu Mungu yupo tummwamini na kumuomba
 
warumi umeshawai kupewa masharti magumu na mganga hadi yakakuogopesha endapo utayashindwa
 
Back
Top Bottom