Huyu ni mmojawapo wa Mastar Holwood simjuwi kwa jina
Sikonge Mkuu Viatu hivyo hapo kwetu watu hawawezi kuvinunuwa vinavaliwa na Ma-Star wa Hollwood mötu masikini hawezi eti atowe Shillingi laki 3 na elfu 50 anunuwe Kiatu cha Timberland wakati kwake anakula ugali kama huyu bibie
FaizaFoxy hana pesa ya kununuwa kiatu kam hicho wakati anashindia kula ugali na kauzu.:A S wink:
Ugali na kauzu my favorite, naona una ilmu finyu sana, kuna chakula gani ambacho ni tofauti kati ya masikini na tajiri? fikiri.
Unaenda restaurant unauziwa wali uliopikwa na mchele ule ule anaokula masikini kwa bei mbaya. Lakini kwa ujinga wako unaona umekula cha maana zaidi.
Hapa unafata jina na nani kapigwa picha (kalipwa) kutangaza hivyo viatu, lakini laiti ungalijuwa mastaa wanavyovaa usingekuja na upuuzi wako hapa wa kusifia viatu vya kufanyia kazi za sulubu wewe ukaona ndio vya maana. Ni ujuha wa hali ya juu, na nna uhakika kuna majuha wenzako humu wanaokuunga mkono.
Isitoshe, kwa umwanjo-mwanjo wako umeona kiatu cha dollar 200 ndiyo ghali sana, amma kweli wewe ni mwanjo-mwanjo. Unajuwa viatu wewe? ngoja tukupe darsa la viatu:
Nna uhakika hujawahi kuyasikia wala kuyaona haya majina, hivi ndivyo viatu ghali, si hivyo viatu vya blue collar:
Miu Miu, Stuart Weitzman, Brian Atwood, Walter Steiger, Christian Loboutin, Jimmy Choo, Manolo Blahnik, Louis Vuitton.
Hayo ndio majina ya viatu unayoweza kusema ghali, Louis Vuitton vya bei ya chini ni around $10,000/= Ukija kwa Jimmy Choo unaongelea kwa uchache uwe na $ 3,500/=
Unajuwa viatu wewe? uvijulie wapi mwanjo mwanjo wa Bagamoyo wewe, nakwambia wewe ni kama kipofu uliyeona punda huko Uturuki, hujijui hujitambui. Weka kiatu cha Manolo Blahnik, ambacho kwa kukujuza tu, nimeshakifuma kwa muuza mtumba Tanzzania kwa TZS 15,000/= na hicho ukiingia dukani nnakuhakikishia ni mshahara wako huko Uturuki wa miaka mitatu au mitano , kwanza duka linavyouzwa hivyo huingii.
Ushasikia viatu vya Jason Arashaben wewe? pair moja ya hicho kiatu ni bajet ya kwenu Bagamoyo ya miaka miwili.
Mwanjomwanjo wahed.