Kwa wale waliopunguzwa kazini (USAID na wengine)

Kwa wale waliopunguzwa kazini (USAID na wengine)

Ulitakiwa uelezee kwamba na hao unaowashauri wasile wanga usiku, pia mchana wasile home..!!

Umeona ulivyokurupuka na hesabu zako 😹
Kumbe wewe mchana hauli na usiku huli lazima huo unga ukae hata mwaka si hautumiki..!!

🤣🤣😂 Familia wasile eti,
Mchana nnakula kwenye mihangaiko yangu, hata kama nikiwa nnakula hiyo budget inatosha na hata kama haitoshi unaongeza mfuko mwingine ni elfu 8 tu,
Na pia huo ni mfano tu wa manunuzi ya mwezi,
Lazima uwe na pakuanzia,
Mfano kama ulinunua mchele debe na halikutosha inabidi mwisho wa mwezi uongeze kiwango,
 
Kusitishwa kwa shirika la USAID na serikali ya Donald Trump kkutagusa maisha ya familia nyingi sana,
Sasa kama wewe ni mwathirika usipanick relax, wewe si wa kwanza kukutwa na hali kama hiyo,
Nimejaribu kukuwekea baadhi hatua za kuchukua ili upite salama

1. FIRST THING FIRST

Ulikuwa unachangia NSSF right?

Sawa hapa ndo pakuanzia, chukua documents zako mapema na uziwasilishe kwenye ofisi za NSSF ili uanze kulipwa haraka,
Ukikamilisha kujaza form yao ndani ya ya siku 30 utaanza kulipwa 33% ya mshahara wako kwa mwezi na utalipwa kwa muda wa miezi 6,
kwa hiyo kama ulikuwa unalipwa mil 1, utalipwa laki 330,000 kwa mwezi,
Unaweza kuiona ndogo ila ni pesa inayoweza kukuweka mjini.

Jitahidi kama una familia hii pesa itatue changamoto za muhimu tu.

Katika kufanya maamuzi ya matumizi nnashauri zingatia vitu vya lazima

a. Matumizi muhimu, mfano kununua nguo mpya ni muhimu ila si lazima
b. Matumizi Lazima mfano kula ni lazima

2. EVERY CENT COUNTS

Kumbuka kuwa mshahara uliokuwa unaingia kila mwezi haupo tena, hivyo ni lazima upitie upya matumizi yako, hasa matumizi makubwa na madogo ya kila siku.
Iko hivi,

a) kodi unalipa sh ngapi? Je inaweza kupungua, jibu ni ndio kama unalipa laki 3 tabata, kwa nn usihamie majohe, kinyerezi, mpiji au Kisemvule kwa nusu ya hiyo kodi,
Kumbuka ulikuwa unakaa karibu kwa sababu ya majukumu, usisubiri kesho anza sasa

b)Matumizi madogo madogo ya kila siku
Mara nyingi hizi huwa zinaonekana ni pesa ndogo zikitolewa kila siku, imagine kila siku unatoa shilingi elfu 10,000 kila siku kwa mwezi sio chini ya laki 3

Okay twende sawa, binafsi hiyo level nilishavuka,

Huwa nnafanya manunuzi ya jumla,
mchele nunua debe 35,000
Sembe nunua kiroba 8,000
Maharage sado 12,000
Dagaa 20,000
Nyama ya 30,000
Samaki 30,000
Mafuta 27,000
Gesi 55,000

Viungo unafanya shopping mara moja kwa wiki unatunza kwenye fridge, inategemeana na idadi ya familia uliyonayo ila kwa haraka haraka baadhi ya vitu hapo vinavuka mwezi na zaidi, mfano gesi matumizi mazuri ni kuanzia miezi miwili

Ni lazima uzingatie na situation yako, huwezi kuendelea kuishi kama awali wakati maisha yamebadilika.

Mpaka hatua hii unapaswa kuwa umejituliza kwenye ile 33%, yaani hakikisha matumizi yako ya mwezi hayazidi ile hela unayoipata,
Sikia watu wanakula mboga za majani kila siku na hawafi, watu wanashindia Maharage mchana na jioni na wanadunda tu,

Laki moja inaweza kutosha familia ya watu 4 vizuri kabisa, kupanga ni kuchagua, don't stress yourself chai asubuhi haina umuhimu wowote, kwanza ni luxury😋

Je unatafuta kazi au unajiajiri?
Ndio nnajua utatafuta kazi nyingine, umetolewa kwenye ajira na ulikuwa hujajipanga it's okay,
Cha kuzingatia wakati unatafuta ajira tafuta ujuzi utakaokuwezesha kuishi mtaani, yaani vi elfu 10,000 au zaidi visikupige chenga.

Please usije jichanganya kuingia kwenye betting, au forex, crypto currency it will be your funeral, usijidanganye hizo mbanga zinahitaji kichwa kisiwe na stress ya aina yoyote.

Tafuta shughuli itakayokufanya uwe busy,
Mfano unaweza kujifunza marketing, tafuta bizaa inayouzika, nenda kwa mfanyabiasha ongea nae ufanye kazi kwa commission, hakuna biashara kwa sasa isiyohitaji mtu wa marketing, haipo,

Ongea na mkurugenzi, mwambie sitaki unilipe mshahara utanipa asilimia % ngapi kwenye kila mauzo.

Mwisho nikutakie kila la kheri, Mungu kufanyie wepesi kwenye upite salama.
Naona mmeanza kufundishana maisha.. sasa hivi kula kwa mrija hakupo tena hadi litimie lile neno mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe..
 
Umejileta vizuri, kwa kukusaidia Mbeya hakuna mchele wa 35000. To yeye nkamu eti Mbeya mchele debe shingapi?

Hapo unataka kujichanganya sasa, mimi nnaagiza kamsamba sio kyela kwenu wanyachu, debe la mpunga 8000, una swali?
 
Naona mmeanza kufundishana maisha.. sasa hivi kula kwa mrija hakupo tena hadi litimie lile neno mtaji wa masikini ni nguvu zake mwenyewe..

Umeona eeh, ujitafute kwanza, ukijipata kanunue mchele wa pakiti korie
 
🤣🤣😂 Familia wasile eti,
Mchana nnakula kwenye mihangaiko yangu, hata kama nikiwa nnakula hiyo budget inatosha na hata kama haitoshi unaongeza mfuko mwingine ni elfu 8 tu,
Na pia huo ni mfano tu wa manunuzi ya mwezi,
Lazima uwe na pakuanzia,
Mfano kama ulinunua mchele debe na halikutosha inabidi mwisho wa mwezi uongeze kiwango,
Hapo sawa km mfano na kuna kuongeza mwingine..!!
 
USAID na taasisi zingine za USA, hawachangii NSSF ya bongo, Makati yanawekwa USA huko huko, kazi ikiisha unapewa mpunga wako wote! Hakuna cha kulipwa kidogokidogo!
Naona umekomenti kwa ujasiri na kwasauti kubwa sana kijana....😜
Sasa kwa taarifa yako, mashirika yapo yalio kua yanachangia hadi 20% of the gross salaries za watumishi wake...🤨
 
Hapo unataka kujichanganya sasa, mimi nnaagiza kamsamba sio kyela kwenu wanyachu, debe la mpunga 8000, una swali?
😹😹😹 kamsamba ipi? Wewe huko napajua na hiyo bei haipo.!!
Tufanye sawa debe 8000 kukoboa na kusafirisha shingapi na kwenye debe unapata kiasi gani?
 
😹😹😹 kamsamba ipi? Wewe huko napajua na hiyo bei haipo.!!
Tufanye sawa debe 8000 kukoboa na kusafirisha shingapi na kwenye debe unapata kiasi gani?

Kamsamba ni moja tu, kupitia mlowo, itaka, mwanjelwa

Kwa haraka hara debe mbili za mpunga unapata debe la mchele (zingatia neno kwa haraka ila ni chini ya debe 2), mimi debe moja elfu 5 limenifia hapa, ila huwa nnaagiza zaidi ya debe 1
 
Mkuu kwanini usinichukue na mimi mdogo wako nikusaidie kuwachambisha hao wazee wa huko mtoni ili tupunguze ugumu wa maisha mtaani.😐
Nae muongo dola elf 80 hajawahipo kuiona aseme kwa saa ni dola 20 x 12 mara ela ya madafu bt huwezi kupata dola elf 80 kwa saa ww www using open
Mkuu kwanini usinichukue na mimi mdogo wako nikusaidie kuwachambisha hao wazee wa huko mtoni ili tupunguze ugumu wa maisha mtaani.
 
Mkuu kwanini usinichukue na mimi mdogo wako nikusaidie kuwachambisha hao wazee wa huko mtoni ili tupunguze ugumu wa maisha mtaani.😐

Una hoja usikilizwe
 
Mbona hiyo ni balaa sasa
Mwanzoni pesa zilikuwa zinawekwa bongo, shida inakuja pale unapostaafu, njoo kesho zikawa nyingi, America akaona huu ni upuuzi, watu wanairumikie kwa much mrefu, wastaafu harafu wazungushwe kuhusu mihela Yao, ! Akajitoa faster
 
Kwanza unapo sema 33% unamaanisha ni aina gani ya mafao..??
 
Mwanzoni pesa zilikuwa zinawekwa bongo, shida inakuja pale unapostaafu, njoo kesho zikawa nyingi, America akaona huu ni upuuzi, watu wanairumikie kwa much mrefu, wastaafu harafu wazungushwe kuhusu mihela Yao, ! Akajitoa faster

Sheria ya Tz inakataa, wafanyakazi wote wanapaswa kuchangia hapa hapa
 
Back
Top Bottom