Kwa wale waliosoma Seminari za Katoliki

Waliopenda mchakamchaka wa roboti. Walofurahia burudani ya makusaro kwenye divinity. Walioipenda divinity ya fr. Minja. Karibuni mfunguke. Mliokuwa mkiyakubali mahubiri ya fr. Mtei mikono juu.

roboti aliendaga marekani mana yule padre alikuwa kama jini aiseee cku moja jamaa angu alikuwa pande za majuu anaongea na phone c ndo mzimu roboti akaibuka mzazi kilichofuata najua mwenyewe...fr.makusaro nae alikuwa noumer mkuu alinipatia B ya divinity...yani wakati huo ukiingia st.james unajua kabisa una division 1 ya points 3 hadi 6...
 
kwani mkuu we unaishi maisha gani bada ya kutoka coz u sound lyk ur totaly livin a different life from the one u had at the seminary...

sitaki kukumbuka hukoo sijui tu ni maisha fulani hivi ya kitumwa zaidi..
 
NAAMINI nimekuPM, sijui kama umeona text. St. James ilikuwa poa sana. Sitasahau zama za kwenda masaera. Tunaletewa wali, ikifika katikati ya shamba watu wanaanza kupima stout inatokea wapi! Masifu asubuhi na rozari jioni..,
 
NAAMINI nimekuPM, sijui kama umeona text. St. James ilikuwa poa sana. Sitasahau zama za kwenda masaera. Tunaletewa wali, ikifika katikati ya shamba watu wanaanza kupima stout inatokea wapi! Masifu asubuhi na rozari jioni..,

mkuu mbona cjaipata hiyo message...
 
St. James' Seminary nakumbuka tulikuwa na upinzani wa jadi na Maua seminary.....
Siku moja wakaja kwenye match pale "uarabuni" tikawapiga 4 na wakaanzisha fujo...sie tukafungua stoo ya slesha naamini siku hiyo wanaMaua wengi walifika kwao kwa miguu maana walitawanyika sana.
Tulipoenda kwao waliogopa kufanya fujo ila nao wakatuiga 4. Enzi hizo kikosi kina watu kama Aron Mwaituka, Mdee, Peter Imani (golie), Aristariki Mwenyeheri a.k.a Beki..huyu wengi walikuwa hawamjui jina hata baadhi ya walimu walimuita BEKI. Jamaa alikuwa na bifu na viatu uwanjani na siku aliyovaa viatu muda mrefu uwanjani ni dakika 7 kwenye match kule Chanjale sem. Tatizo lilikuwa kwenye kumpita. Pia kulikuwa na wachezaji kama vile Sadiki Mwamlima ( aliwaui kuichezea Tukuyu stars kabla ya kuja SAJASE) , Mponzi, Aristablas Macha....na mimi mwenyewe.
Namkumbuka Father Landelin Makiluli alipokuja akiwa Frater...alikuwa anadokoa makwenzi hasa..
Fr Maramba.... Fr Mavumilio....Fr Ruwaichi a.ka. KP... Fr Kenyange....sister Anna (nadhani walienda kuanzisha Anwarite Girls)...Sister Edith...Sister Epimark.... mzee Gabriel....Fr Negro....Fr Kajetan Kazi (huyu sijui kama zilikuwa zinamtosha) Fr Nderumaki....Fr A. Makusaro ( nilibahatika kumuona mwaka jana ile TZC yake bado anayo)
Nilikuwa mtaalamu wa kula VENJA na nilikuwa na MIGODI kadhaa ya MBUNENE na ndizi kule pg project.
Sitasahau siku Ruwaichi alipovizia mgodini na kutukamata mbaya zaidi nikisema " tufanye fasta KP asitukamate" hakuwa na makuu zaidi ya kunitaka nimuambie tu maana ya KP...akili ilifanya kazi ya ziada nikamuambia maana yake ni Kenyan Police....akauliza kwa nini tunamuita vile? Nikaanza kummwagia sifa na kumuambia " hivi Fr ulishaenda jeshi....tunakuita Kenya Polisi maana uko sharp kama wao...ona hata hapa ulivyotukamata kama kuku" alivyopenda kusifiwa akatuambia malizeni kula mkaendelee na kazi.
Next time aliponikamata na miwa mie na group yangu hakutuelewa bali alitufunga mashati na kutuzungusha shule nzima tumebeba miwa yetu huku tunaimba " sisi ni wezi" . Hakika hadi leo sithubutu kuiba chochote.
Nakumbuka pia siku niliyododge kazi kwa saa 1 tu wakati Fr Negro akiwa anasimamia kazi.. wakati huo nilikuwa nafanya kule Phyisics Lab. Negro alinitafuta na nilipopatikana jioni alifanya calculations za muda wa watu wote niliopoteza na ikatakiwa niwalipe...mwisho wa hesabu ikaonekana ninatakiwa kufanya kazi saa 8 kwa siku kwa muda wa siku 36.... kwa sasa huwa ninapata zawadi za mfanyakazi bora ofisini.
Siwezi kusahau tukio la kufariki kwa mwenzetu Gilbert Riziki a.k.a Njuka (R.I.P) wakati tunatoka shambani Masaera. Huyu jamaa wakati huo alikuwa i/c wangu kule Box room na kwa mbwa.
Nakumbuka ratiba ilivyokuwa tight hadi watu walikuwa wakilala na uniform.
Nakumbuka ujanja wa kusaka "VIWAVI" kule Mandaka na wakati mwingine kuvuka mto hadi St. Magreth.
Hakika nikisahau wema wa St. James mkono wangu wa kuume na unyauke.

Baadae nilikuja kwenda Usa Seminary (FREEDOM SQUARE) kwa A-level.
 
Nimeipenda hiyo naration nimesoma hapo enzi za fafu akiwa mwalimu wa kazi. Ukichaguliwa kuwa waziri wa afya moja kwa moja unakuwa incharge wa GWC. Kipindi hicho pia jamaa alikuwa mwl wa litaji, du ukisinzia masifu unaenda kukaa na mapadri kule nyuma. Wakati wa misa unaenda kukaa mbele na f.1.
 

dahh..mkuu nimeipenda hiyo narration mana aha ha ha edith na anna sisters,makusaro na nderumaki
 
Sister Edith alikuwa mwl hesabu wa aina yake.

Hakika... hata sister Anna alikuwa binadamu wa kipekee. Nakumbuka kuna siku alilia kisa kuna jamaa aliua siafu mbele yake..
Kuna siku walifanya sikukuu pale kwao tukazamia na "WAZEE" fulani. Kuna kiwavi alikuwa anafanya kazi kwao. Ishu ni kwamba chakula kilikuwa na pilipili za kutosha na mapapai yalikuwa mabichi na yanawasha hasa!
 
Ni Rector.....Sio Lector....

Kwa Kiswahili anaitwa Gombera....

Mlikuwa mnawakata mikia 'wafollow' eeeh!....

Vp kuhusu 'kuchinja mbuzi'......Teh teh.....

Duh mzee umeua hiyo code kuchinja mbuzi, any way R.I.P mr. Kimomori, maadam Balbina, and Deacon Simwela
 
Makusaro alikuwa gombera wa kipekee pia. Misimamo yako juu ya kuwavumilia wanafunzi nyakati za misukosuko ya kinidhamu ya wanafunzi na pia kwa maswala ya ada haipimiki. Ukidodge rector's conference enzi za Makusaro ulikuwa unajinyima burudani. Truely yule padri alikuwa mtu wa watu.
 
Mie shujaa wangu ni Fr Aloysius Makusaro. Asanteni sana.



Makusaro kweli alikuwa na kipaji cha uongozi...
Nakumbuka wakati anakuja na kupokea kiti toka kwa Kajetan Kazi aliniteua niwe namtembeza maeneo na kumtambulisha kwa watu...
Kuna wakati kesi zangu zilizidi kwa mapadre ila nilikuwa mtaalamu wa kupangua hoja vilivyo...Makusaro na ubishi wake wote hakuwahi kunipata na hatia. Basi siku moja Jumatatu saa mbili wakawa wanafukuzwa watu kwa kosa ambalo nilishiriki ila hakuna ushahidi Makusaro akatangaza wazi kuwa " mkimkamata Isaac msimlete kwangu simuwezi,nsssssh nsssh simuwezi! Mkimleta kwangu mimi ni hukumu tu!"
Kuanzia siku hiyo nilikuwa ninawindwa kuliko kinana anavyowinda tembo.....bahati mbaya ni kuwa ushahidi haukupatikana ......hata nipigwe picha kwenye tukio nilikuwa na uwezo wa kuelezea namna nilivyopigwa picha kwa kulazimishwa...
Pia Makusaro alikuwa anathamini sana wanafunzi na hata kipindi fulani tulipofanya mgomo alilazimishwa kutufukuza maring leader ila akagoma na kusema kama kuna mwalimu hataki kufundisha basi amwambie akaripoti kwa askofu apewe mtu mwingine....ilitokea mgogoro kati yetu na walimu na walimu na Rector ila yaliisha baada ya yeye kuwaelewesha kuwa kazi ya walezi ni kubadili vyijana hivyo kuwafukuza haina maana bali kukwepa majukumu.... Tulibahatika kubaki seminari ila tukapewa adhabu kali sana kama darasa.
 
Hiyo imenifurahisha sana, natamani ningekuwepo sajase enzi hizo. Dah it was funny hiyo ilikuwa mwaka gani?
 
Hiyo imenifurahisha sana, natamani ningekuwepo sajase enzi hizo. Dah it was funny hiyo ilikuwa mwaka gani?
Alikuja mwaka 2000 ila matukio ninayoelezea ni kati ya 2001 & 2002
 

ha ha ha mkuu mimi nilichoka ila wewe ulipitiliza yani ulikuwa zaidi ya mtata binafsi nilianzisha vuguvugu la kubadili chakula ingawa ilibaki kidogo niondoke lakini ndo vile ukiweza kupangua hoja zao...kuna ripoti niliandikiwa vibaya toka kwa paroko yani hiyo ngoma nilikuwa najua nasepa ila mwisho wa cku niliwashinda kwa hoja nikamaliza na nikatoka na summa
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…