Natamani sana hizo,ndio zilikuwa zangu. Home kwangu nimetenga room kabisa. Ilikuwa kila asubuhi,saa moja na nusu namalizia hapo. Naanza na kuruka kamba na kichura hiyo dk 30 nakata. Nakuja push up zile za two nakoz tu,mkupuo wa 30,30 mara 5. Nakuja unashika mikono kwa nyuma kwenye kama mwamba wa kitanda,yaani unaukigeukia huo mwamba unashuka chini na kupanda. Mikono tu na visigino ndio vinakuwa vimeubeba mwili. Hayo mazoezi nimeanza nayo miaka 20 iliyopita. Sasa kilichokuwa kinanitokea kila nikikomaa mayo sana ilikuwa napata bawasiri, yaani kama vidude vinatokea sehemu ya haja kubwa,kama tuvidole tudogo hivi. Wakati wa haja,nikimaliza ile mishipa ya ndani inauma. Ikawa hiyo inakuja na kupotea nikawa naendelea na mazoezi huku nikitafuta tiba. Nimehangaika sana na tiba. Hivi ninavyoongea nimeacha mazoezi kabisa,kwa sababu sasa nikifanya tu kidogo napata maumivu makali balaa. Bado nahangaikia tiba,tiba ni adimu sana. Inaniuma sana nikikumbuka mazoezi,natamani mno
Sent using
Jamii Forums mobile app