Kwa wale wapenda mbwa tuchukue tahadhari

Kwa wale wapenda mbwa tuchukue tahadhari

Ni kweli na ujumbe mzuri

Nilikuwa namiliki mbwa na alitokea kunizoea sana kushinda mtu mwingine yeyote Sasa mihangaiko ikapelekea niwe naye mbali na watu nilimuacha/wanaomuangalia kwa ukaribu ni watoto (14-17yrs) changamoto moja wapo muda wa chakula,kumfungia asubuhi na kumfungulia ndipo kazi ilipo,wanatoa taarifa mbwa ni mkali hata kwao chakula wanamuwekea mbali ndipo wanamfungulia na watu wote muda huo wahakikishe wako ndani maana kawatembezea meno sana,muda wa kumfunga/kumfungulia Hadi wamvizie or kumdanganya na chakula waweke bandani akiingia ndipo wamfungie,kesi kila siku wageni kung'atwa
Kama ningempa mafunzo na ukaribu baadhi ya watu nilikuwa naishi nao asingeleta matatizo mengi maana mwenyewe ndiye niluyekuwa namfunga na kumfungua na hakuna atakayetoka asubuhi kama sijamfunga na akifanikiwa kutoka nje ya uzio siku hiyo kesi tu kwa wapita
njia
Ilipelekea nitoe maamuzi ya kumuua(R.I.P Sargent)
Alikuwa ni mbwa wa aina gani? Pole mkuu..siku ikitokea nikapoteza mbwa wangu kwa namna yoyote ile nitasikitika sana, wamekuwa kama sehemu ya familia.
 
Kwani harufu ya tajiri wao hawaijui kama hawa makoko yetu ukiwa hata mita 300 tu kashakutambua.

Hyo mnayomiliki nyie sio mimbwa, ni minyama ya porini sema binadamu mmeilazimisha kuifuga na matokeo yake ndio inawatafuna wamiliki,inakumbuka asili yao.

Kwa hiyo hao walinzi pua zao hazina uwezo wa kutambua harufu ya bosi wake.Yaani hata panya wa SUA wanawashinda kweli?
 
 
Ni kweli lakini sidhani mtu kawaida kama ingekuwa rahisi kumtrain/kukaua naye labda ningemrudisha nilipomchukua angali mdogo
Ila waliniuzia mbegu ya ajabu wale field force 😅 nilikuwa najua German shepherd ila sijui ilichanganywa na mbegu gani Ile mbwa miguu ya mbele kama anabeba chuma
Itakua hybrid ya fisi mkuu
 
Alikuwa ni mbwa wa aina gani? Pole mkuu..siku ikitokea nikapoteza mbwa wangu kwa namna yoyote ile nitasikitika sana, wamekuwa kama sehemu ya familia.
Nilipoenda kununua wale police waliniambia german shepherd na hata kwenye card,form ya ununuaji ilikuwa imeeleza hivyo na kwakuwa awali alikuwa mdogo alikuwa na muonekano unaoendana ila kadri nilivyokaa naye na kukua,hakuwa mrefu yaan ilikuwa mbegu fupi alaf kajazia sijui sababu ya chakula nilichokuwa Nampatia,mzito.

Mbwa alikuwa mkorofi,kuua mbwa wenzake ni kazi rahisi sana kwake ila nilitokea kumpenda hivyo hivyo
 
Nilipoenda kununua wale police waliniambia german shepherd na hata kwenye card,form ya ununuaji ilikuwa imeeleza hivyo na kwakuwa awali alikuwa mdogo alikuwa na muonekano unaoendana ila kadri nilivyokaa naye na kukua,hakuwa mrefu yaan ilikuwa mbegu fupi alaf kajazia sijui sababu ya chakula nilichokuwa Nampatia,mzito.

Mbwa alikuwa mkorofi,kuua mbwa wenzake ni kazi rahisi sana kwake ila nilitokea kumpenda hivyo hivyo
Itakuwa alichanganywa na mbegu nyingine. Mara nyingi Germany shepherd ni rahisi kuishi nao na wanafundishika. Wapo friendly pia ingawa ni wakali kwa wageni
 
Itakuwa alichanganywa na mbegu nyingine. Mara nyingi Germany shepherd ni rahisi kuishi nao na wanafundishika. Wapo friendly pia ingawa ni wakali kwa wageni
Yea huenda maana kikosi Cha mbwa ni wataalamu na wao huenda walijichanganya kwenye kuuza

Tukio la mwisho napewa taarifa kavunja banda baada ya kusikia Kuna ugeni katembeza meno Hadi kamuacha mama wa jirani uchi.
 
Mbwa wakali kwaajili ya matajiri pambaneni
Mi nauliza nimpeleke wapi paka wangu akafungwe kizazi asizae naona katakuwa kamalaya haka
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji2][emoji1787]
 
Yea huenda maana kikosi Cha mbwa ni wataalamu na wao huenda walijichanganya kwenye kuuza

Tukio la mwisho napewa taarifa kavunja banda baada ya kusikia Kuna ugeni katembeza meno Hadi kamuacha mama wa jirani uchi.
Duh
 
Ni kweli na ujumbe mzuri

Nilikuwa namiliki mbwa na alitokea kunizoea sana kushinda mtu mwingine yeyote Sasa mihangaiko ikapelekea niwe naye mbali na watu nilimuacha/wanaomuangalia kwa ukaribu ni watoto (14-17yrs) changamoto moja wapo muda wa chakula,kumfungia asubuhi na kumfungulia ndipo kazi ilipo,wanatoa taarifa mbwa ni mkali hata kwao chakula wanamuwekea mbali ndipo wanamfungulia na watu wote muda huo wahakikishe wako ndani maana kawatembezea meno sana,muda wa kumfunga/kumfungulia Hadi wamvizie or kumdanganya na chakula waweke bandani akiingia ndipo wamfungie,kesi kila siku wageni kung'atwa
Kama ningempa mafunzo na ukaribu baadhi ya watu nilikuwa naishi nao asingeleta matatizo mengi maana mwenyewe ndiye niluyekuwa namfunga na kumfungua na hakuna atakayetoka asubuhi kama sijamfunga na akifanikiwa kutoka nje ya uzio siku hiyo kesi tu kwa wapita
njia
Ilipelekea nitoe maamuzi ya kumuua(R.I.P Sargent)
Dah rest easy sargent but bro Zulu man ulizingua sana kwani hukujua utarudi kwako ?
 
Dah rest easy sargent but bro Zulu man ulizingua sana kwani hukujua utarudi kwako ?
Tatizo muda mrefu niko mbali na makazi hivyo kuondoa matatizo zaidi nikaona niruhusu tu lifanyike jambo walilokuwa wananishauri

Ilifika kipindi Hadi mmiliki wa duka la mifugo mbwa/mifugo alimjeruhi vibaya nikawa nakosa msaada wa chanjo ya minyoo n.k siunajua tena mjini doctors wa mifugo wachache na wengine wamiliki wa haya maduka

Ukiona simu nyingi hapo unahisi tayari mbwa kafanya yake ujiandae kwa faini na matibabu
 
Baada ya shambulio la kutoka kwa mbwa wake,mzee wetu marehemu Ngombale Mwilu hakurudi tena mpaka kifo chake.............hakika mbwa ni km risasi iliyo kwenye chemba
 
Nikiwa mdg wa miaka 10+++ nilikuwa mfugaji wa mbwa Tena wakali Sana nakumbuka ilikuwa ikifika saa nne za usku hkn mtu barabarani atakatiza dogi wale walikuwa wakali mno

Bas Kuna mzee mmoja alvyoona ananyanyasika kupita njiani alfajir ya saa kumi na moja akaona awaue kwa kununua nyama Kisha na kuingiza sindano nyingi kwenye nyama mbwa alovyo rushiwa kula ikawa mwisho wake alikufa kifo Cha matezo had leo nakumbuka Hali hyo aliuliwa kinyama sana

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom