Kwa waliokojoa kitandani tu!!

Nakumbuka kuliachi nilipolazwa Hosp nikiwa mzee. Sikumbuki niliacha kuliachia lini? Utotoni sikuwam nikiliachia na watoto wangu awachii kabisa
 
Umenikumbusha mbali sana mkuu
kuna jamaa yeye haja kubwa ilimbana sana sema sasa alikuwa anaogopa kwenda chooni(choo kipo nje)
Akayabana sana mwishowe usingizi ukampitia akaanza kuota
Ameamka kisha yupo chooni anajisaidia huku anasikia rahaa gafla anasikia umotomoto kuja kushtuka tayariii kashayajaza
 
Mkuu si useme tu ni wewe??? Maana hebu tuambie ulijuaje kama alikuwa anasikia raha?? Ulijuaje kama alikuwa anasikia umotomoto??... Ulijuaje kama usingizi ulimpitia akaanza kuota kuwa yuko chooni anajisaidia???
 
sema ni wewe . ulikuwepo nae ndotoni?
 
mbona sisi tumekubali tulikojoa bna? ila tuseme kweli ule mkojo wa ndotoni mtamu bna.tatizo lake unashtuka baada ya kumaliza mkojo wooote
Afadhali ukojoe karibia kunakucha... Ole wako uuachie mida ya saa sita hivi... unalala kwa mawazo na shida tupu!
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23]
Kweli we noma, kwahiyo dogo alikuwa anachapwa kwa kosa lako!!
 
Mi nlikua nakereka kipindi hiko nnamchumba wangu kaja home kununua maandazi basi maza alikua ananiharakisha nitoe godoro mbele ya manzi nlikua standard 4
 
Mm nilikuwaga nikikojoa nachelewa kuamka afu nikiamka nimenuna hakuna wa kuniuliza

Sasa kizaazaa kikaja kuna mtoto wa rafiki yake na mzee alikua anakuja kuishi kwetu likizo fupi wakifunga shule sasa nikaambiwa atakuwa analala chumbani kwangu

Mama akamwambia Dada wawatu mm nikikojozi sugu nimeshindikana mtaa mzima awe ananiamsha usiku kukojoa

Sasa nilikuwa darasa LA tatu wazee ila nilikuwa naona aibu balaa

Kweli yule Dada akawa ananiamsha mpaka nikajikuta nimezoea nikiota usiku nataka kujoa mpaka nishituke

Namshukuru sana Dada yule alinisaidia nikaacha ukikojozi mungu amzidishie huko aliko na familia yake

Mpaka Leo cjawahi kutana nae mzee aliniambia alishakuwa mama tena wa watoto 3


.......
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…