Kwa waliomaliza form 4, kama una roho ndogo usiende kusoma special schools (shule za vipaji maalumu)

Kwa waliomaliza form 4, kama una roho ndogo usiende kusoma special schools (shule za vipaji maalumu)

Nilienda nimechelewa nikakuta hao mabongoland wamesharipoti wameshamaliza topic zote

Nikataniwa niandike electronic configuration Mimi akili yangu nikawa natumia zile za o level 2:8:8 walicheka balaa mambo ya orbitals ,Wala vi theory vya aufbau , Pauling exclusion sijui kama zipo

Majamaa yakawa yanadhusha ma theory ya electro chemistry na ma reaction ya delocalization za benzene na Ortho and para kwenye organic nilitaka kulala mbele nimwbie mshua anipeleke shule za arts
 
Hizi shule(mzumbe,pugu,kisimiri,ilboru,kibaha and the likes) japokua siku izi nyingi zimepoteza sifa zake aisee kama una moyo mwepesi usiende huko unaweza kupata depression au pressure ukashindwa kusoma

Miaka Hio mwisho wa miaka ya 2000 niliripoti Moja ya shule tajwa hapo combination ya pcm... Kipindi hicho special school wamejaa watoto wa dar kutoka (kibaha, Azania, pugu) aisee Hawa madogo wana sifa kishenzi.... Mtu anakuja kuripoti form 5 ameshamaliza topic zote za form 5 anakaribia kumaliza za form 6

Sasa si matozi tulivyomaliza form 4 vitabu tukatupa Kule mpaka siku ya kuripoti hujawahi kupiga pindi lolote... Unakutana na vitoto vimesoma sijui mchikichini huko aisee wamefuta topic zote, aisee nilipata presha sana mpaka kuzoea ile Hali.... Nakuta madogo wanapiga integration kama hawana akili, ukikaa bwenini wanaulizana kwa nguvu reaction za organic. Chemistry huko....

Dah yaani mwezi wa kwanza form 5 watu wanasolve necta review nikasema hapa nimeyatimba... Aisee ile presha ya ku catch up nilipata shida Sana sio Siri... Ukiwa na roho nyepesi unaweza kukata tamaa Moja kwa Moja

Kuna dogo tumeingia form 5 alikua anaitwa T.O (Tanzania one) alitukimbiza wote form 4 aisee huyu Jamaa mpaka Leo hua namuogopa. Hua namwambia hata hii kazi ya u engineer unayofanya unastahili kua somewhere else una potential kubwa sana, picha linaanza tumeingia form 5 hapo.... Sasa form 6 walikua wanafanya fitness tests (hii anatokea mwanafunzi mmoja au wawili wanatunga mtihani alafu wengine wanafanya japo sio lazima)

Ujinga wa hii mitihani wanafunzi wanajua kukomoana yaani maswali yote unakuta ya kibabe... Kuzungusha 0 huku ni kawaida tu ndo maana wengi walikua hawataki huu ujinga, dogo bana tunafika form 5 kaskia form 6 wanafanya fitness test ya physics dogo akazamia akapiga Pepa... Matokeo yanatoka form 6 karibu wote wamefeli dogo kawakimbiza.... Wote wanaulizana hili jina nani mbona hatumjui... Kuja kuulizia wakaja kugundua ni dogo wa form 5 aisee jamaa walimind kinoma akapigwa marufuku kabisa kusogeza pua kwenye fitness tests za form 6

Huyu dogo tulipofika form 6 sidhani kama aliwahi kukaa akasoma, jamaa alikua anakaa zake class watu wamepanga foleni na maswali Yao yaliowashinda dogo anapiga yote tu hajali kama ni ya physics, chemistry, pure au bam ye anasolve tu. Alikuja kua Tanzania one tena form 6 jamaa walimtangaza hesabu paper 1 na 2 zote alipiga 100%.

Huku kama una roho ndogo sio pa kwenda mi nusura panishinde nilitaka nirudishe mpira kwa kipa(kuhamia private)
mimi wakati naripoti 4m five nilikutana na the same issue but ki ukweli maisha haya ni kuomba sana wakati unapambana .Unaweza kuwa best darasani but ukaja kupata kazi ya kawaida sana
 
Nimesoma special school ila niwe mkweli kule kuna upuuzi sana. Sio waalimu sio wanafunzi.

Special school za sasa ndio chanzo cha kukosa wataalam wabobevu, watu wapo smart sawa lkn wanatumia uwezo wao kufanya mambo ambayo hayana tija yyt ile kwa future yao na jamii zao. Ni kama ulivosema huyo engineer, na kibaya TZ hawathamini wasomi. Nchi kama India wanathamini sana wasomi wao, na competition iliopo huko ni kama hiihii ya special schools zetu ingawa wao wamewekeza zaidi kwenye mambo muhimu. Tz msomi hauna thamani, huku tunathamini wafanyabiashara tu

Mimi niliwaachia kabisa shule yao, niliamua kuacha shule ila sio kuacha elimu, nikatengeneza syllabus yangu kutokana na ninachotaka kuwa. Now nafanya kazi na watu kutoka nchi kibao, I own companies and I'm creating more.... Sasa ningeendelea kumisuse potential yangu kipuuzi now ningekua nimeajiriwa na kimshahara cha labda 1.5m bado hujaweka makato humo.

Kwa madogo wanaojielewa, Highschool za Tanzania ni upotevu wa muda.
Útakuta mtu amemeza Lambert na Abbott zote.
 
Inanikumbusha enzi zetu Singida tuliomba tufanye mock na ma form six Sema walitubania.
Nakumbuka ticha wa chemistry alikua akiingia darasani anajitetea kabisaa eti hatufundishani bali tunadiskass! Dadeki. Watu tulimeza topic zote za five kwa mkandawire. Ile elimu nyoko niulize saivi nna mbishe gani.
 
Hizi shule(mzumbe,pugu,kisimiri,ilboru,kibaha and the likes) japokua siku izi nyingi zimepoteza sifa zake aisee kama una moyo mwepesi usiende huko unaweza kupata depression au pressure ukashindwa kusoma

Miaka Hio mwisho wa miaka ya 2000 niliripoti Moja ya shule tajwa hapo combination ya pcm... Kipindi hicho special school wamejaa watoto wa dar kutoka (kibaha, Azania, pugu) aisee Hawa madogo wana sifa kishenzi.... Mtu anakuja kuripoti form 5 ameshamaliza topic zote za form 5 anakaribia kumaliza za form 6

Sasa si matozi tulivyomaliza form 4 vitabu tukatupa Kule mpaka siku ya kuripoti hujawahi kupiga pindi lolote... Unakutana na vitoto vimesoma sijui mchikichini huko aisee wamefuta topic zote, aisee nilipata presha sana mpaka kuzoea ile Hali.... Nakuta madogo wanapiga integration kama hawana akili, ukikaa bwenini wanaulizana kwa nguvu reaction za organic. Chemistry huko....

Dah yaani mwezi wa kwanza form 5 watu wanasolve necta review nikasema hapa nimeyatimba... Aisee ile presha ya ku catch up nilipata shida Sana sio Siri... Ukiwa na roho nyepesi unaweza kukata tamaa Moja kwa Moja

Kuna dogo tumeingia form 5 alikua anaitwa T.O (Tanzania one) alitukimbiza wote form 4 aisee huyu Jamaa mpaka Leo hua namuogopa. Hua namwambia hata hii kazi ya u engineer unayofanya unastahili kua somewhere else una potential kubwa sana, picha linaanza tumeingia form 5 hapo.... Sasa form 6 walikua wanafanya fitness tests (hii anatokea mwanafunzi mmoja au wawili wanatunga mtihani alafu wengine wanafanya japo sio lazima)

Ujinga wa hii mitihani wanafunzi wanajua kukomoana yaani maswali yote unakuta ya kibabe... Kuzungusha 0 huku ni kawaida tu ndo maana wengi walikua hawataki huu ujinga, dogo bana tunafika form 5 kaskia form 6 wanafanya fitness test ya physics dogo akazamia akapiga Pepa... Matokeo yanatoka form 6 karibu wote wamefeli dogo kawakimbiza.... Wote wanaulizana hili jina nani mbona hatumjui... Kuja kuulizia wakaja kugundua ni dogo wa form 5 aisee jamaa walimind kinoma akapigwa marufuku kabisa kusogeza pua kwenye fitness tests za form 6

Huyu dogo tulipofika form 6 sidhani kama aliwahi kukaa akasoma, jamaa alikua anakaa zake class watu wamepanga foleni na maswali Yao yaliowashinda dogo anapiga yote tu hajali kama ni ya physics, chemistry, pure au bam ye anasolve tu. Alikuja kua Tanzania one tena form 6 jamaa walimtangaza hesabu paper 1 na 2 zote alipiga 100%.

Huku kama una roho ndogo sio pa kwenda mi nusura panishinde nilitaka nirudishe mpira kwa kipa(kuhamia private)
Mtanzania pekee aliyekuwa T.O O-level na Advanced level ni Martin Chegere,Akaenda mlimani akawa best student,masters akaongoza,PhD Sweeden pia akaongoza!
now yuko Udm anapiga madogo pindi.
 
Mtanzania pekee aliyekuwa T.O O-level na Advanced level ni Martin Chegere,Akaenda mlimani akawa best student,masters akaongoza,PhD Sweeden pia akaongoza!
now yuko Udm anapiga madogo pindi.
Nikajua atakuwa Harvard, oxford, Cambridge anafundisha au kaajiriwa TESLA , google na makampuni makubwa ila kaishia UDSM ,duu basi hatari sana

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
 
Mtanzania pekee aliyekuwa T.O O-level na Advanced level ni Martin Chegere,Akaenda mlimani akawa best student,masters akaongoza,PhD Sweeden pia akaongoza!
now yuko Udm anapiga madogo pindi.
Huyu niliyesoma nae alikua T.0 o level na advance pia... Yaani alivyokuja advance akawa anaitwa T.O nadhani Kuna watu hata jina lake walikua hawalijui

Mwaka wetu top 10 jamaa ndo aliongoza huku hao Tisa wote waliobaki wakiwa mademu tupu, kipindi hicho kifungilo na Marian girls weka mbali na watoto
 
Haha jamaa umenikumbusha jina mmenye..... Vipi ulipita hapo nikupe 1,2,3 za hapo?

Ndio lakini sio miaka uliyotaja, nyuma kidogo...

Afu usikariri, si mwaka wetu Kuna watu wawili walipata div 4... Sio kwamba special school Kila mtu anatoboa chief

Waliokuwa wanapata ufaulu hafifu ni wale waliokuwa...
1. Waoga kama wewe

2. Mabitozi na wapenda starehe

3. Wasukuma na Wakurya ambao kuja kwao shule za mjini kuliwafanya wajihusishe na shughuli za kuwaingizia kipato (kukusanya ada), mfano hapo umenyeni kulikuwa na jamaa mpiga picha maarufu alikuwa hadi na baiskeli, anakula deal za kupiga picha shule kibao kuanzia Ngateu, Kiding'a, Enaboishu hadi Akeri huko, mwingine alikuwa anapiga deal za kusaga nafaka kwa wamenye kwenye mashine ya shule n.k...
 
Nikajua atakuwa Harvard, oxford, Cambridge etc ,ila Kwa kumbukumbu nilizonazo Martin chegere O'level alipata Div one ya point 10 na hakuwa T.O na alimaliza mwaka 2003 au 2004 o'level

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Elimu ya bongo konyo sana, jamaa alikua T.0 hata scholarship hakupata Kila siku tukawa nae tunapigwa vumbi tu kwenye vimbweta vya coet
 
Elimu ya bongo konyo sana, jamaa alikua T.0 hata scholarship hakupata Kila siku tukawa nae tunapigwa vumbi tu kwenye vimbweta vya coet
Hehehehehe ,embu piga hesabu top ten wote kuanzia 2000 Hadi Leo 2024 anza kuwafanyia analysis walipo sasa Yani utakuja kuchoka wengine wanamiliki stationary mjini na kupambana na usafiri wa mwendokasi

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
 
Ndio lakini sio miaka uliyotaja, nyuma kidogo...



Waliokuwa wanapata ufaulu hafifu ni wale waliokuwa...
1. Waoga kama wewe

2. Mabitozi na wapenda starehe

3. Wasukuma na Wakurya ambao kuja kwao shule za mjini kuliwafanya wajihusishe na shughuli za kuwaingizia kipato (kukusanya ada), mfano hapo umenyeni kulikuwa na jamaa mpiga picha maarufu alikuwa hadi na baiskeli, anakula deal za kupiga picha shule kibao kuanzia Ngateu, Kiding'a, Enaboishu hadi Akeri huko, mwingine alikuwa anapiga deal za kusaga nafaka kwa wamenye kwenye mashine ya shule n.k...
Basi umenyeni hapo ndo nimepiga, weekend kwenda mjini ilikua ruksa tulikua tunasikia raha kweli kuvaa vile vi t shirt vya shule... Mi mwenyewe nilikua hustler nimefanya sana deals nyingi shule, ila kunywa Yale maji ya mtoni pale ni kitu kilinishinda... Jioni ikifika Kuna mademu tulikua tunawapigisha tizi kwenye kile kimlima Cha kupanda pitch hukosi hata buku 2 ya kusogeza siku😃😃

Sijawahi kusoma kwa usongo kuanzia o level nilikua nasoma kiasi na relax kabisa
 
Siku Moja nilienda kibaha kujisomea maana nilikua na mshikaji pale, aisee saa 5 naenda kulala watu wananishangaa, nikasema hii elimu siyo mateso,

Watu walikuwa wanalala saa 3 usiku, michezo wanacheza vizuri na wana single digit...

Ili ufaulu unapaswa uelewe ulichosoma, usikisahau na uweze kujua namna ya kukitumia unapopata swali...

Kwa muda gani mtu asome? Kila mtu ana uwezo tofauti wa kusoma na kuelewa...
 
Umenikumbusha kijana mmoja anaitwa Rajabu ndegeulaya.

Tuna report advance Azania yeye alipitisha tangazo la kuwa anafundisha tuition Kwa WANACHUKUA PHYSICS, CHEMISTRY NA PURE MATHEMATICS.

WATU walizani ni form six kumbe ni form five alishamaliza topic zote mpaka za six basi ikabidi tuendelee kupiga mapindi kwa Ndegeulaya.
Mbuzi hizo unakuta zimerudia shule mara kadhaa, tulisoma na watu wa mvi na wengine wana ndevu mpaka kwenye matundu ya pua na masikio
 
Nina washkaji zangu wakali wa mathematics mwaka huo waliondoka na C ,hata ndegeulaya alipiga C ,ule mtihani wa mwaka 2013 ulikuwa wa laana aisee , Tanzania nzima A za advance mathematics zilikuwa 12

Sent from my Infinix X652C using JamiiForums mobile app
Ile pepa ya 2013 ilikuwa balaa... Nimemaliza pugu pcm.... Nakumbuka, ile pepa natoka tu kwa mtihani wa adv math 1... Kichwa kinuma balaaa😂😂
 
Back
Top Bottom