Kwa wanaoamini hakuna Mungu, njooni hapa

Kwa wanaoamini hakuna Mungu, njooni hapa

Dhana ya kuwa Mungu yupo ni wazi maana yupo aliyetuzidi maarifa akatuweka huku duniani Mungu huyo aligundulillka zamani sana kwa watu jamii ya wayahudi,nchini israel ziko shuhuda ukienda nchini humo zikiinyesha shuhuda kwamba yupo Mjanja kuliko sisi ambaye ndiye alituumba,isitoshe alishuka mwamba mmoja toka huko ikulu alipo akazaliwa na mwanamke bikira ,huyu mwamba alifanya meng ya kutisha na inaaminika alikufa akafufuka,haya mambo kama hujafika Israeli hutoamin
Mbona wakina Kisai FaizaFoxy wanasema hajazaliwa, kufa wala kufufuka??
 
Unaweza kuthibitisha?
Unajua mkuu hata kuku haamini kwamba lile banda ni wewe umetengeneza ,yeye anajua ni nature tuu limekuwepo ,japokua anakuona ila hawezi kukukaribia hadi umtupie kitu,hata sisi na huyu aliyetuzidi akili huwa tunamwona kwenye maisha yetu ila hatumfuati hadi tuwe na shida pata shida utajua kuna Mungu au la
 
Unajua mkuu hata kuku haamini kwamba lile banda ni wewe umetengeneza ,yeye anajua ni nature tuu limekuwepo ,japokua anakuona ila hawezi kukukaribia hadi umtupie kitu,hata sisi na huyu aliyetuzidi akili huwa tunamwona kwenye maisha yetu ila hatumfuati hadi tuwe na shida pata shida utajua kuna Mungu au la
Vipi kuhusu swala, pundamilia, Kanga, fisi, chatu, mamba, ngiri, Simba n.k huko porini? Wao wanajua nini??
 
Kwanza kitendo Cha wewe kuandika ya kwamba uandike kitabu kisha useme wewe ndio umeumba, inaonyesha una akili ndogo na hufikirii vitu katika uhalisia au hujui nini unachokiaegemea.
Ad hominem logical fallacy.
Hii hua inatokea pale mtu anaposhindwa kuhimili mjadala kisha anaamua kuku-attack personally.

Usirudie hilo kosa, unapunguza credit, usiruhusu jazba kwenye mijadala.

Kama wewe unauwezo wa kufikiri katika uhalisia, Thibitisha kwa kutumia uhalisia kama Mungu yupo.
Ufunuo kwanza unasema hivi :


35. Au wao wameumbwa pasipo kutokana na kitu chochote, au ni wao ndio waumbaji?

36. Au wao wameziumba mbingu na ardhi? Bali hawana na yakini.

37. Au wanazo khazina za Mola wako Mlezi au wao ndio wenye madaraka?

38. Au wanazo ngazi za kusikilizia? Basi huyo msikilizaji wao na alete hoja ilio wazi! [at-Tur : 35 - 38]

Hapa ufunuo ulikuwa unawajibu wale ambao walikuwa wanaukana na kukana juu ya uwepo wake. Kwanza kabisa unatakiwa ujue ya kuwa nyinyi sio wa kwanza katika kumkana Mungu na Wala hamtokuja kuwa walau na hoja za kuonyesha kutokuwepo kwake. Sababu Kuna ishara nyingi kuanzia kwenye miwili wako, mazingira na viumbe vingine juu ya uwepo wake.
Mkuu nimesoma hapo, Huyo Mungu asijitetee "excusses" lazima apingwe, atapingwa na ataendelea kupingwa sababu hawezi kujithibitisha kama yupo.

Kwanza hata wewe huna hoja ya kumthibitisha kama yupo.
Tafakari kwanza juu ya ufunuo huo na kile kilichoandikwa humo, kisha uje uoanushe na uonyeshe kinyume chake.
Sijaona alipojielezea kwamba yeye ametoka wapi?

Kama ye mwenyewe hawezi kujithibitisha, wewe utawezaje kumthibitisha?

Kama huwezi kumthibitisha kama yupo then hizo ni hadithi za "Alfu lela ulela" .

Kama hizo sio hadithi za kale, Thibitisha yupo, na yuko wapi na alitokea wapi?

Kisai
 
Wakristo wote motoni na waislam wote motoni, hii ni Kwa mujibu wa miungu Yao kwny biblia na Quran walivoandika , yesu ndio njia ya mbingun huwezi kwenda Kwa baba bila yeye pia uislam ndio dini ya haki ya mwenyez mungu. Sawa bhn mtajua wnyw na ma Imani yenu
 
Imani inakuaje ukweli au uhakika?

Uwe unajibu kwanza maswali ninayo kuuliza kisha uulize ili mjadala ulete maana. Unapo uliza swali kabla ya kujibu maswali unaharibu mjadala mzee.

Jibu kwanza maswali niliyo kuuliza kisha uulize maswali yako.

Tuendelee.
 
Ad hominem logical fallacy.
Hii hua inatokea pale mtu anaposhindwa kuhimili mjadala kisha anaamua kuku-attack personally.

Usirudie hilo kosa, unapunguza credit, usiruhusu jazba kwenye mijadala.

Kama wewe unauwezo wa kufikiri katika uhalisia, Thibitisha kwa kutumia uhalisia kama Mungu yupo.

Angalizo kidogo unapotumia misingi ya logic kama msegemeo yako katika mjadala huu ni udhaifu pia, kadhia ya Ad hominem logical fallacy inaingia humo. Hapo hujashambuliwa bali umeambiwa ukweli na kuonyeshwa udhaifu wako, kwenu nyinyi logical kama fani huwa haiwapeleki katika ukweli au kuujua ukweli. Hili kosa usilirudie wewe tena,jikite katika kuutafuta ukweli na uangalie nini kimeandikwa.

Ithibati zangu zote nilizo zitoa ni uhalisia, labda kama hujui uhalisia ni nini ? Unaweza kuonyesha wapi sijatumia uhalisia ?
Mkuu nimesoma hapo, Huyo Mungu asijitetee "excusses" lazima apingwe, atapingwa na ataendelea kupingwa sababu hawezi kujithibitisha kama yupo.

Kwanza hata wewe huna hoja ya kumthibitisha kama yupo.

Nafurahi kwanza kwa wewe kusoma kilicho andikwa. Kingine ambacho huwa mnatupa kazi tunapojadiliana na nyinyi ni kutokujua kwenu maana za maneno. Hakuna sehemu ambayo Allah anajitetea hapo, kasome tena maana ya kujitetea.

Hapo anawazindua watu na kuonyesha sababu miongoni mwa sababu ambazo zinawafanya watu wapinge mambo, miongoni mwa sababu ni ujeuri tu muda ambao wahusika hawana hoja, katika sababu nyingine zinazo fanya watu wapinge ni ujinga yaani kutokujua kama mnavyo fanya nyinyi.

Ili niwe sina hoja ni wewe sasa kukosoa hiki ninacho kiandika na utuandike kilicho sahihi.
Sijaona alipojielezea kwamba yeye ametoka wapi?

Kama ye mwenyewe hawezi kujithibitisha, wewe utawezaje kumthibitisha?

Kama huwezi kumthibitisha kama yupo then hizo ni hadithi za "Alfu lela ulela" .

Kama hizo sio hadithi za kale, Thibitisha yupo, na yuko wapi na alitokea wapi?

@Kisai

Anajieleza vipi ametoka wapi wakati yupo na haja tanguliwa na kutokuwepo yaani wakati. Kusema wapi alipotoka ni udhaifu na kuonyesha yeye si mkamilifu wakati amepwekeka na hiyo sifa.

Yeye amejithibitisha tayari katika kila kitu, hapa ndipo pale tunaangalia sababu zenu za nyinyi kumpinga na tuna washangaa. inakuwaje kwa uwazi ambao Mola ameuweka juu ya uwepo wake nyinyi namuuoni, hapa ndipo pale tunakuja kuhitimisha ya kuwa ni ugonjwa wa akili, ujinga, ulimbukeni, utoto na kutokufikiria mambo katika uhalisia wake.

Kwanza sijashindwa kumthibitisha na hili ni jambo dogo sana, bali tumemthibitisha kila tunapoingia katika hii mijadala.

Kulinganisha ya ufunuo na hadithi za kale huu ni utoto mwingine sababu hivi havifanani kuanzia machimbuko yake na uhalisia. Huku sasa ni kukosa hoja na hili sharti dhaifu sana.

Mola wetu alishatueleza ya kuwa yeye yuko wapi, Allah yuko juu ya Arshi yake amestawi na Arshi ni katika kiumbe kikubwa cha Allah ambacho amekiumba kuzidi viumbe vyote, Arshi iko juu ya mbingu ya saba. Ama ametoka wapi hili swali la uongo sababu haliingii kwake hilo.
 
Kwa wanaoamini hakuna mungu, ukiwachunguza kwa makini hawa watu ndiyo ujifanya wao ni majiniazi, kumbe ni wapumbavu wa mwisho katika hii dunia, na hoja yao kubwa ni kwamba kila kitu ni nature hoja hii haina mashiko hata kidogo na ni hoja ya kipuuzi ambayo utolewa na watu ambao kwa kawaida wameshindwa kuamini katika imani zao kwa uthabiti maybe wamechunguza kuwa katika imani zao ambazo wamekuwa na kulelewa umo aziko sawa sawa na azijawapa majibu yakutosha kiasi cha wao kuamini

Kuna wengine majeuri tu na kwakweli katika hii dunia watu hao awawezi kukosekana wanajua na kuona lakini nyoyo zao zimekufa na wauwaji ni wenyewe na matendo yao.

Na rudi katika hii hoja ya kusema kila kitu kipo sababu ni nature, huyu huyu anaesema hivi anaamini kwamba simu anatengeneza mzungu internet mzungu,

ila jinsi mungu alivyoumba kila kitu kwa ustadi wa hali ya juu wanasema ni nature, ushuuzi!
Ulitakiwa mtoa post utoe hoja nzito kuthibitisha uwepo wa mungu, lakini mtoa post amekuja na mihemko bila hoja.
 
Uwe unajibu kwanza maswali ninayo kuuliza kisha uulize ili mjadala ulete maana. Unapo uliza swali kabla ya kujibu maswali unaharibu mjadala mzee.

Jibu kwanza maswali niliyo kuuliza kisha uulize maswali yako.

Tuendelee.
Swali gani Umemuuliza Nimsaidie Mwanangu Huyu?
 
Kitu kikiwa na jina ni ishara ya kwanza KIPO.Tena kama kina jina la tofauti kwa kila nchi, kila kabila na kila kitongoji
Hoja dhaifu sana hiyo ya kuthibitisha uwepo wa mungu.......Mbona binadamu wanafanya maovu halafu wanamsingizia shetani hasiyekuwepo?
 
Angalizo kidogo unapotumia misingi ya logic kama msegemeo yako katika mjadala huu ni udhaifu pia, kadhia ya Ad hominem logical fallacy inaingia humo. Hapo hujashambuliwa bali umeambiwa ukweli na kuonyeshwa udhaifu wako, kwenu nyinyi logical kama fani huwa haiwapeleki katika ukweli au kuujua ukweli. Hili kosa usilirudie wewe tena,jikite katika kuutafuta ukweli na uangalie nini kimeandikwa.

Ithibati zangu zote nilizo zitoa ni uhalisia, labda kama hujui uhalisia ni nini ? Unaweza kuonyesha wapi sijatumia uhalisia ?


Nafurahi kwanza kwa wewe kusoma kilicho andikwa. Kingine ambacho huwa mnatupa kazi tunapojadiliana na nyinyi ni kutokujua kwenu maana za maneno. Hakuna sehemu ambayo Allah anajitetea hapo, kasome tena maana ya kujitetea.

Hapo anawazindua watu na kuonyesha sababu miongoni mwa sababu ambazo zinawafanya watu wapinge mambo, miongoni mwa sababu ni ujeuri tu muda ambao wahusika hawana hoja, katika sababu nyingine zinazo fanya watu wapinge ni ujinga yaani kutokujua kama mnavyo fanya nyinyi.

Ili niwe sina hoja ni wewe sasa kukosoa hiki ninacho kiandika na utuandike kilicho sahihi.


Anajieleza vipi ametoka wapi wakati yupo na haja tanguliwa na kutokuwepo yaani wakati. Kusema wapi alipotoka ni udhaifu na kuonyesha yeye si mkamilifu wakati amepwekeka na hiyo sifa.

Yeye amejithibitisha tayari katika kila kitu, hapa ndipo pale tunaangalia sababu zenu za nyinyi kumpinga na tuna washangaa. inakuwaje kwa uwazi ambao Mola ameuweka juu ya uwepo wake nyinyi namuuoni, hapa ndipo pale tunakuja kuhitimisha ya kuwa ni ugonjwa wa akili, ujinga, ulimbukeni, utoto na kutokufikiria mambo katika uhalisia wake.

Kwanza sijashindwa kumthibitisha na hili ni jambo dogo sana, bali tumemthibitisha kila tunapoingia katika hii mijadala.

Kulinganisha ya ufunuo na hadithi za kale huu ni utoto mwingine sababu hivi havifanani kuanzia machimbuko yake na uhalisia. Huku sasa ni kukosa hoja na hili sharti dhaifu sana.

Mola wetu alishatueleza ya kuwa yeye yuko wapi, Allah yuko juu ya Arshi yake amestawi na Arshi ni katika kiumbe kikubwa cha Allah ambacho amekiumba kuzidi viumbe vyote, Arshi iko juu ya mbingu ya saba. Ama ametoka wapi hili swali la uongo sababu haliingii kwake hilo.
Zaidi ya kujitetea sijaona hoja ya kumthibitisha hapo.
 
Back
Top Bottom