Kwa Wanayanga: Nini Kifanyike ili Yanga icheze Fainali ya CAF Champions League msimu ujao

Kwa Wanayanga: Nini Kifanyike ili Yanga icheze Fainali ya CAF Champions League msimu ujao

Hii timu wai maintain tu, na waongeze wachezaji 2 tu, we are ready to go
 
Zalan na wale marumo gallant ndio wameleta fujo zote hizi lets see next season.
 
kuna makosa madogo wanafanya ni kama wana overconfidence but still ni team bora sana!
Yaan wale hawana bahati kabisaa, msimu wa 4 huu wanaishia Robo na nusu, afu kikosi chao ni boraa sanaaa.
 
Yanga inahitaji mawinga wawili wabunifu wanaoweza kudrible na wenye speed, morison na kisinda watemwe moloko abaki ila asiwe kikos cha kwanza.

Winga kama kisinda na moloko ni ma winga wa kizaman sana hawaendan na mpira wa kisasa, wanahitajika mawinga wanaomfata beki wakiwa na mpira kisha wanaingia ndan kufunga au kutoa pasi.

Pia yanga inahitaji kiungo wa kati namba 8 mwenye uwezo wa kukaa na mali kama niyonzima, mchezaji mwenye first touch nzuri sio kama sure boy ambye ni mzur ila first touch yake sio nzuri, kiungo mwepes mwenye uwezo wa kukaba na kumiliki mpira ili wawe wanapishana na aucho.

Alafu namba kumi mwenye uwezo wa kukaba na kushambulia mwenye uwezo wa kupiga pasi za mwisho kiufund na kupiga mashuti kiusahihi.

Yanga inahitaji wachezaji 4 tu kuboresha kikos mawinga wawili ,kiungo wa kati namba 8 na kiungo mshambuliaji namba 10
 
mamerod.wanacheza.mpira.wa.mtaani
Mamelod sijui hata walikosea wapi kwenye Champs league, yaan wanatokaa vizuriii wakifika nusu eti wanatolewa, afu unaweza kuta team hiyo ilikutana wakiwa makundi na aliwachapa nje ndani, lakini ikifika Robo au nusu wanatolewa wao.

Sikuamini Al Ahly atacheza final huu mwaka, khaaah, mpira Una matokeo ya ajabu mnoo.
 
Wampe Nabi mahitaji anayo yataka,wamwachie yy apendekeze wachezaji wa kiwasajili na mwisho viongozi waache ubahili, hela ambayo Yanga kaingiza kwenye michuano hii ina karibia dola 3m,inatosha kufanya usajili wa wachezaji hawa 3-5 wakubwa na nyingine tufanyie mambo mwengine.

Tukifanikiwa kumbakisha Nabi,Mayele na Diara ,tutakuwa hatari sana.
Lazima aondoke mmoja hapo. Hasahasa Mayele sioni akibaki
 
IMG_7574.jpg
 
Tatizo la Yanga miaka yote ni kutokuwa na play makers. Dribblers.

Wafanye usajili wa Dribblers wawili..defender mrefu mmoja au wawili wa kuruka aerial balls na second strickers wawili.

Sidhani kama mayele atabaki msimu ujao.

Yanga michuano yote haijaweza kucheza katikati hata kidogo..hao akina sure boy hawana maajabu ya kushindana championship..kama malumo gallants tuu waliwasumbua vile.

Alafu wachezaji wafundishwe mambinu magumu wayaweze.

Kukaba kienyeji na counter hazikupeleki popote champions league.

Ndio maana waliaibishwa na al hillal ya sudan

Sent from my SM-A310F using JamiiForums mobile app
Mechi ya Al hilal zote 2 yanga ndo walicheza vzr kuliko Al hilal tuwe wakweli .

Ila ukweli una baki pale pale viungo wa yanga kama sure boy sio wa kuwategemea kbsa mfano mudathir ni mzur kukaba tu ila hana ubunifu, na pia sure akikutana na team inayokaba kwa nguvu utamktaa kwasababu kwanza ni mchezaji ambye hana first touch nzuri, anahitaji kupokea mpira akiwa ktk nafas kubwa bila kubugudhiw sas mechi za ushindan lazma apoteze tu mipira.

Kiufupi pale yanga wachezaji wa kati wenye first touch nzuri ni aucho, bangala na aziz ki japo aziz anazingua
 
"Yanga hawajafa KIUME wala hawajafa KISHUJAA.

Vita inapofika MWISHO wanajeshi wote—walioshinda na walioshindwa—hurudi nyumbani wakiwa HAI. Waliokufa ni wale ambao hawakufika mwisho wa mpambano.

Yanga HAWAJAFA kabisa. Wamefika mwisho wa mpambano na sasa wanarudi nyumbani wakiwa HAI." Maundu Mwingizi


Kwanza niipongeze timu ya Yanga Kwa kufika Fainali ya Kombe la shirikisho barani Afrika, hii ni mara ya Kwanza Kwa timu ya Tanzania kufika hiyo hatua kubwa kabisa. Tumekua tukishuhudia timu za kaskazini na walau Kwa ukanda huu wa kusini mwa jangwa la Sahara ni timu za Congo na Afrika kusini pekee ndo hua zinafika hiyo hatua.

Hii sasa italeta hamasa kuelekea msimu ujao. Kikubwa tujipange kuboresha kikosi. Viongozi wafanye usajili kulingana na matakwa ya mwalimu Kwa kuzingatia nafasi zinazopwaya....

Hakika tulikua na msimu Bora Sana, na tumepata mafanikio makubwa Sana lakini tunatakiwa kufanya makubwa zaidi.

Karibu mwananchi mwenzangu tujadili maboresho na mapendekezo ambayo tunapaswa kufanya ili msimu ujao tufike Fainali ya CAF Champions League...
View attachment 2645534View attachment 2645536
Haitatokea tena ndugu
 
Mechi ya Al hilal zote 2 yanga ndo walicheza vzr kuliko Al hilal tuwe wakweli .

Ila ukweli una baki pale pale viungo wa yanga kama sure boy sio wa kuwategemea kbsa mfano mudathir ni mzur kukaba tu ila hana ubunifu, na pia sure akikutana na team inayokaba kwa nguvu utamktaa kwasababu kwanza ni mchezaji ambye hana first touch nzuri, anahitaji kupokea mpira akiwa ktk nafas kubwa bila kubugudhiw sas mechi za ushindan lazma apoteze tu mipira.

Kiufupi pale yanga wachezaji wa kati wenye first touch nzuri ni aucho, bangala na aziz ki japo aziz anazingua
Aziz ki mtoe kabisaa na usimtajee, yule ndo aliharibu mfumo wenu wote janaa, sijui kwann Ali ingia. Yaan anapoteza mipira kizembe anaporwa kiwepesi afu hajui kukaba au kurudisha mpira alio porwa,

Yule labda awe eneo zuri kwa kupiga mshuti bas.
 
Lazima aondoke mmoja hapo. Hasahasa Mayele sioni akibaki
Mpira pesa kaka,kama Yanga wakimpa mzigo na wakaelewana anaweza akabaki, hamna mtu anayecheza mpira kwa kufuata mapenzi.
 
Zalan na wale marumo gallant ndio wameleta fujo zote hizi lets see next season.
Mtibwa, Namungo, KMC, Azam hao wote wamekusumbua na umeshindwa kuchukua Ligi kuu, FA cup, Ngao ya jamii nk.
 
hata wachezaji wa kaskazini(waarabu)wanajua kumzonga refa.refa anajikuta anaweka tuta au faulo au kubadili maamuzi kwasababu ya kuzongwa zongwa tu wachezaji.
Upo sahihi. Waarabu wanajua fitna..tena ambazo tunaona ulaya zikifanyika pia. Na washajua watu weusi wanapanikigi au kutoka mchezoni kwa vitu vidogovidogo kama hivyo.

Sent from my SM-A310F using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom