Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Damushin sunbae-nim,
Nimemaliza kuangalia "Oh My Geum Bi". Bando langu lime-pay off na wala sijutii kuitazama! Machozi yamenitoka kwa wingi.. Nipe nyengine, sunbae!
mimi nimeanza kuangalia temperature of love. ipo vizuri sana na nimevutiwa zaidi na muigizaji mkuu wa kike seo hyun jin yupo vizuri sana ukilinganisha na waigizaji wengine wa kike wa korea ambao wanapewa promo sana na vyombo vya habari.
pia nimevutiwa sana na kim jae wook hyungnim ambaye kwenye kingdom of the wind alicheza uhusika wa chubalso, natamani apewe nafasi ya muigizaji mkuu kwenye drama yoyote ile.temperature of love ipo vizuri sana na mara hii SBS tv drama awards ni balaa
Temperature-of-Love1.jpg
 
hizi drama zenye kunifanya niumize kichwa sana ninapoziangalia utafikiri nafanya mtihani wa hesabati bila ya kuwa na scientific calculator nitaachana nazo kuziangalia kwa sababu ninapomaliza kuzitazama hunifanya nitamani kuzirejea tena ili nipate kuzielewazaidi .Sisi waafrika hatujazoea kuumiza vichwa sana hivyo basi while you were sleeping na black drama huenda nikazipotezea. dama ya black bado kuna mambo yananichanganya hivyo basi chingus nahitaji munisaidie. haya ni baadhi ya mambo niliojifunza kwenye black drama
  1. mwanadada kang ha ram (go ara) muda wote anavaa miwani ambayo alipewa na baba yake ambaye alikuwa ni detective, anavaa miwani kwa sababu ya uwezo wake wa kuona kivuli cha kifo anapomuangalia mtu pindi asipovaa miwani, lakini bahati mbaya hana uwezo wa kutoa msaada wowote ili kuepusha tukio la kifo, ukiangalia wasifu wa kang ha ram na hong joo (bae suzy) wa kwenye while you were sleeping wanafanana kwa sababu wote wana uwezo wa kuona tukio la baadae lakini hawana uwezo wa kulibadilisha tukio hivyo basi wote wanahitaji mtu wa kuwaongoza.ha ram anamtegemea detective han moo gang na hong joo anamtegemea prosecutor jae chan. na wote wawili wamekuwa wakijilaumu kwa kushindwa kuzuia tukio la kifo la baba zao.
  2. mpaka sasa nimeshindwa kufahamu ni kwa sababu ipi inayomfanya kang ha ram awe na uwezo wa kuona kivuli cha kifo, yeye binafsi anaona ni kama laana lakini detective han moo gang anamuona kama amejaaliwa kipaji kutoka kwa Mungu. je inawezekana ha ram ana mahusiano ya karibu na grim reaper?, kwa sababu baadae ha ram atajikuta naye akiwa na mahusiano na black ambaye ni grim reaper.
  3. han moo gang ni detective ambaye ni mzembe sana anapokuwa kazini lakini kumbe anapokuwa kwenye maeneo yake ni mtu mmoja mjanja sana na alikuwa anachunguza kesi iliotokezea miaka ya zamani ambapo kesi hiyo pia ilikuwa inamhusu mpenzi wake Soo wan ambaye ni daktari wa upasuaji katika hospital.Han moo gang kwenye mkono wake alikuwa anavaa bracelet, hapo zamani ha ram alimpa zawadi ya bracelet kama ile mchumba wake ambaye alikuwa anaitwa joon ambaye alikuwa na ndoto ya kuwa detective pindi atakapokuwa mkubwa. kama han moo gang ndiye joon kwa nini amebadilisha jina lake?
  4. oh man soo ni kijana anayefanya kazi kwenye kampuni ya bima na pia anachukiwa sana na kaka yake, pia ana ukaribu sana na ha ram na anamini ha ram ana uwezo wa kupiga ramli na mwisho wa siku anamuomba afanye kazi katika kampuni yake ili amsaidie kujua mambo yatakayowatokezea wateja wao.kwa kumtumia ha ram ambaye ana uwezo wa kuona kifo ataweza kujua ni mtu gani tunapaswa kuingia naye mkataba wa bima na yupi hatupaswi kuingia naye mkataba wa bima,na kampuni ya bima ya royal ndio iliohusika na tukio la moto lilitokezea maeneo ya Moojin miaka 20 iliopita na ndio tukio lililopelekea kifo cha baba yake ha ram.
  5. mwishoni mwa episode ya 1 detective han moo gang alipigwa risasi na muuaji kwa makusudi na yeye alikuwa ni mateka na pale wapigaji risasi walikuwa ni wawili na alipopelekwa hospitali alifariki dunia. baade ameonekana hajafariki lakini amepoteza kumbukumbu zake na kufanya matukio ya ajabu kama vile kutembea bila ya nguo ya kujisitiri sehemu yake ya siri, kujibizana na bosi wake,pia kutokuogopa tena maiti kama ilivyokuwa kawaida yake na pia amekuwa na uwezo mkubwa sana wa kuchunguza matokeo ya uhalifu.
  6. kiukweli detective han moo gang amefariki kwa kupigwa risasi lakini ndani ya mwili wake ameingiliwa na gream reaper number 444 ambaye ni kim tae woo na amekuja kwenye dunia kumtafuta mwenzake ambaye amekimbia, hivyo basi tabia zote anazozionyesha han moo gang si za binadamu wa kawaida ila ni tabia za gream reaper.kwa sababu gream reaper ana uwezo wa kufahamu jinsi gani binadamu alifariki, ana upeo mkubwa sana na ana nguvu na ndio maana kwenye episode ya 3 han moo gang aliwapiga majambazi mpaka wenzake wakashangaa uwezo wake.
    4_(4)_1.JPG
  7. hivyo basi kwenye episode ya kwanza han moo gang ndio yule yule ambaye anafahamiana na ha ram ila episode zinazofuata black hamfahamu ha ram kwa sababu sura ni ya han moo gang ila matendo ni ya gream reaper no 444 . na inawezekana han moo gang alipatwa na ugonjwa wa kusahahu ndio maana ameshindwa kumtambua ha ram ambaye walikuwa ni marafiki tokea utotoni, na pia anashindwa kujibu barua zake kwa sababu amemsahau ha ram lakini bado najiuliza kama amemsahau kang ha ram mbona bracelet aliyopewa hajaitupa na anaithamini?
  8. kuna gream reaper mmoja amevaa nguo za kizamani (hanbok) na kwa jinsi inavyoonekana alikuwepo wakati wa utawala wa joseon na kuna sehemu moja alisikika akisema kumwambia mwenzake ya kwamba alishuhudia kifo cha crown prince sado ambaye alifungwa gerezani na baba yake kwa siku saba bila ya kupewa chakula na prince sado alikuwa ni baba yake mfalme yi san, anashirikiana na gream reaper 444 kwa ajili ya kumtafuta mwenzao aliyekimbia na kujificha kwenye mwili wa binaadamu na ndio maana gream reaper 444 akajiingiza kwenye mwili wa detective han moo gang.
  9. kwa inavyoonekana kisheria gream reaper hapaswi kuwa na mahusiano na mtu ambaye tayari ana mahusiano na mwenzake na kuingilia mahusiano ya watu kwao wao ni makosa, kwenye episode ya 2 mwanzoni tulishuhudia tukio la mauaji la wapenzi wawili wakiwa kwenye gari, ukiangalia macho ya gream reaper aliefanya mauaji yale inaonekana dhahiri alimpenda yule msichana aliekufa na kisheria hapaswi kumpenda kwa sababu tayari ana mchumba wake, hivyo basi yule gream reaper alivunja sheria
    8Wv7Jm.png
    inawezekana gream reaper huyu ndiye anayetafutwa na gream reaper 444 ambaye amejiingiza kwenye kiwiliwili cha detective han moo gang na je inawezekana huyu ndio baba halisi wa ha ram na si yule detective?
  10. mwanzoni mwa episode ya 1 anaonekana black akijitupa kwenye maji na alipofika chini ya maji aliona gari ambayo ndani yake alikuwemo mtu ambaye alikwisha kufa na amefanana naye na akawa anajiuliza inawezekanaje tukafanana,je inawezekana gream reaper 444 alikufa baada ya gari kutumukia kwenye maji?
  11. je inawezekana yule mbwa wa oh man soo ambaye humwita kwa jina la Oh Gip Seo ana uwezo wa kuwaona gream reaper na pia ana uwezo wa kuona kifo kwa sababu tumeona alivyokuwa anasumbuana na black, na pia kwenye tukio la kutaka kujinyonga kwa ha ram yule mbwa alikuwa nje lakini alifahamu ya kwamba kang ha ram anajinyonga.
Khantwe ,aminas ,mbelwaz ,UHURU JR ,EMPTY
Na mimi nasubiria majibu ya haya maswali maana detective Han uwepo wake tu ulikuwa unanichanganya sasa kaja na huyu grim reaper ndo nimechanganyikana kabisaa
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] eti nilikutolea povu mbona unapenda kunisingizia lakini? Nilikuwa naona uvivu kuendelea tena ila nimeona wacha niimalizie tu
sasa nimekuelewa.kumbe ilikuwa ni wivu wa bae suzy kwa minoz. mian hae noona
 
mimi nimeanza kuangalia temperature of love. ipo vizuri sana na nimevutiwa zaidi na muigizaji mkuu wa kike seo hyun jin yupo vizuri sana ukilinganisha na waigizaji wengine wa kike wa korea ambao wanapewa promo sana na vyombo vya habari.
pia nimevutiwa sana na kim jae wook hyungnim ambaye kwenye kingdom of the wind alicheza uhusika wa chubalso, natamani apewe nafasi ya muigizaji mkuu kwenye drama yoyote ile.temperature of love ipo vizuri sana na mara hii SBS tv drama awards ni balaa
Temperature-of-Love1.jpg
Kuna Page Moja Instagram Nimeona Wanaisifia Sana..

Na Hii Nayo Utaiachia Kati....?
 
Na mimi nasubiria majibu ya haya maswali maana detective Han uwepo wake tu ulikuwa unanichanganya sasa kaja na huyu grim reaper ndo nimechanganyikana kabisaa
hahahahaaa balaa na waafrika akili zetu zinapenda mambo mepesi tu (kwa sauti ya trump). gream reaper amejiingiza kwenye mwili wa detective Han moo gang
 
yaaani mpaka leo najiuliza aminas amepatwa na kitu gani mbona nikiingia kwenye account yangu sioni jibu lolote
Nilibanwa Nikashindwa Kuja Kuongeza Povu...

Njiandaa Na Maandalizi Si Unajua Bae Mkubwa Next Week Ndo Anarudi Kwaiyo Niko Busy Kupanga Mipango Nakuweka Sawa Mambo...

ila Kikweli Niko Tyari Kuwa Jino Na Jino Na ........... Naogopa Kumtaja
 
Kuna Page Moja Instagram Nimeona Wanaisifia Sana..

Na Hii Nayo Utaiachia Kati....?
ipo vizuri sana na cha kuvutia uyo mwanadada anajikuta akipendana na kijana ambaye amemzidi umri sasa mama wa kijana hapendi.
 
Nilibanwa Nikashindwa Kuja Kuongeza Povu...

Njiandaa Na Maandalizi Si Unajua Bae Mkubwa Next Week Ndo Anarudi Kwaiyo Niko Busy Kupanga Mipango Nakuweka Sawa Mambo...

ila Kikweli Niko Tyari Kuwa Jino Na Jino Na ........... Naogopa Kumtaja
naomba umtaje leo nitakuunga mkono kwenye vita ya maneno
 
ipo vizuri sana na cha kuvutia uyo mwanadada anajikuta akipendana na kijana ambaye amemzidi umri sasa mama wa kijana hapendi.
Daah Sa Ivi Sitaki Kujaza Aya Mambo Mpaka Leo Hospital Ship Sijandelea Nayo Nimeisitisha,..

Niko Na Black Na Uyo Suzy...Maana Now Niko Tyt Ndomana Naogopa ATA kuanza Drama Mpya
 
sasa nimekuelewa.kumbe ilikuwa ni wivu wa bae suzy kwa minoz. mian hae noona
[emoji23] [emoji23] [emoji23] wivu tena loh ningekuwa na wivu nisingeanza hata kuiangalia. Basi leo nimeota nimemuona bae yupo na zile nywele zake alizokuwa nazo kwenye Boys Over Flowers....akawa anakuja mbele yangu anatabasamu then anapotea. Nilivyoamka nimechukiaje
 
[emoji23] [emoji23] [emoji23] wivu tena loh ningekuwa na wivu nisingeanza hata kuiangalia. Basi leo nimeota nimemuona bae yupo na zile nywele zake alizokuwa nazo kwenye Boys Over Flowers....akawa anakuja mbele yangu anatabasamu then anapotea. Nilivyoamka nimechukiaje
aigooooooo unapaswa umtafute jae chan ili apate kuibadilisha ndoto yako
 
Daah Sa Ivi Sitaki Kujaza Aya Mambo Mpaka Leo Hospital Ship Sijandelea Nayo Nimeisitisha,..

Niko Na Black Na Uyo Suzy...Maana Now Niko Tyt Ndomana Naogopa ATA kuanza Drama Mpya
medical drama hazini vutii sana na ndio maana sijaitafuta hospital ship
 
Back
Top Bottom