doctor stranger ndiyo drama pekee yenye maudhui ya medical ndio niliimaliza episode zote.
Naanza Kuangalia Hii Drama, Japo Nimekuwa Na Tabia Yakutozimalizia Medical Drama Mpka Mwisho Nilofanikiwaga Kuimaliza ni Doctors Ya Kim Rae Won na Park Shin Hye. Natamni Na Hii Nifike Nayo Mbali kama Siyo Mwisho
Hapana Siijuhi Sababu Nidokezee.doctor stranger ndiyo drama pekee yenye maudhui ya medical ndio niliimaliza episode zote.
unajua ni kwa sababu gani?
kang sora
hahahahahaaaaaaaa umenifanya nicheke kama jinga jingaWamecheza Kiserious Sana Umu Ndani Jamni Uwaoni Kucheka Cheka.
Kuna Sehemu Kuna Mtu Alicomment kuwa Yeyote Aliejitolea Kusub Hii Drama Ashapoteza Uhai Maana Si Ugumu Wake.
Yaani Ata Kauli ama Maneno Yanyotumika Umu Ndani Ni Magumu Gumu Na Ukweli Kuwa Ni Tofauti na Drma Nyingi za Medical!
hahahahahaaaaaaaa umenifanya nicheke kama jinga jinga
baadhi ya wakati nalazimika kunotes terminologies ndipo nikamuulize MR google maana yake.
subtitle yake nayo kama hujapita shule zetu za speaks english please utapata tabu sana na unaweza kuichukia hii drama. inanilazimu baadhi ya wakati nami nisome comment za wachangiaji ndipo niiifahamu zaidi stori yake.
nahisi anayetafsiri hii drama ni mwanasheria.
jawabu nimeliweka hapo juu.Hapana Siijuhi Sababu Nidokezee.
Dah!jawabu nimeliweka hapo juu.
kuna project moja nilikuwa naiangalia inaitwa MISAENG (incomplete life) ni nzuri sana sana ila nimeiacha kwa muda vyuma vimeanza kukaza.
humu ndani yumo im siwan, kang sora, kang ha neul, byun yo han n.k
ndio best drama kwa mwaka 2014.
some time inafika wakati najiuliza maswali mbona hii drama kama iannihusu na mimi na wengineo niliyoyapitia na ninayoyapitia kwenye maisha yangu ya kila siku.
ndio nikaikumbuka hii nukuu
maisha yote njia hufunguka pale ambapo utakapoamua kutembea, njia isiyofunguka haiwezi kuwa ni njia.
njia inaweza kuvunguka kwa mtu yeyote yule lakini si kila mtu anaweza kuwa na njia.
hii mitandao wanatufanya sisi watumiaji kama ni matajiri sana wanaamua bila ya sababu kupunguza bundle lakini thamani haishuki.
nimeshazoea free internet kupitia wireless basi kipindi hiki nasumbuka mnoooo.
na kwa hali niliyofikia siwezi tena kuangalia drama zilizotafsiriwa kwa kiswahili.
kwa hali ilivyo acha niendelee kuifuatilia MR SUNSHINE kila week end na hizi nyengine nazihifadhi kwenye mtungi.
Mkuu nashukuru sana kwa kusoma mabandiko yangu,Nadhani umenipita kila kitu.하하하하 하하하하
ahsante sana brother kwa heshima ulionipa inanipasa nizipokee kwa moyo mkunjufu pasina kinyongo..
unajua binadamu hawezi kuwa mkalifu kwa kila jambo ndio maana pakawepo na chain kwa dhumuni kuu la kusaidiana ili kuyakabili maisha kwa urahisi zaidi.
msingi mkuu wa kuyafurahia maisha ni kupenda kila ambacho kinaleta mwangaza kwenye nafsi yako na kwangu mimi kwa miaka hii 5 ukiachana na football kitu pekee kinachonivutia ni kufuatilia korean wave entertainment.
na sababu kubwa hii ndio starehe pekee isiyoniletea athari kwenye kiwiliwili changu.
nitakapovutiwa na kitu chengine cha kuondoa stress zaidi ya korean drama basi nitaachana na series za Asia.
upande wa pili hata wewe upo vizuri baadhi ya maeneo ambayo mimi sina uelewa nayo mkubwa na inafika wakati najiuliza maswali kama wewe
je ninaweza kuwa mfuatiliaji mzuri wa masuala ya dunia, imani, historia kama Da'Vinci ?
unaweza ukawa na dhana ya kwamba nakudharau au kukukejeli lakini ndio ukweli, ninayoyaeleza yana ukweli kutoka ndani ya kiwiliwili changu kilichohai muda huu na kimaarifa.
japokuwa inavyoonekana tuna tofautiana kiimani lakini hainizuiii mimi kusoma maandiko yako yenye maudhui ya dini unayoiamini unayoyaweka kwenye jukwaa la intelijensia na kiukweli nimekuwa nikijifunza mambo mengi sana kupitia kwako.
pia kupitia andiko lako linalomuhusu leonardo davinchi nimejifunza mambo mengi sana yanayomuhusu genius wa kitaliano aliyeishi karne nyingi zilizopita lakini uwezo wake wa kufukiri ulikuwa ni kama mwanadamu wa karne hii ya ARTIFICIAL INTELLIGENCE
maisha yote anayechagua sehemu ya kujifunza hawezi kuwa msomi mahiri katika ulimwenguu huu wa sasa.
nami pia nikushukuru hyung nim /dong saeng / ahjussi / harabuji kwa uwepo wako hapa JF.
hahahahahaaaaaa naomba comment yako uifanyie mabadiliko haraka kabla wenye jinsia yao hawajaamka.Mkuu nashukuru sana kwa kusoma mabandiko yangu,Nadhani umenipita kila kitu.
Mimi ni orabanyi (?)mkuu..
Nimependa tone ya uandishi wako
Hahaaaaaaaaaaaaaaà umeniingiza mtego bro Mimi ni Hyungnim Lee Kang to ndio alivyokua anamwita kaka yake (blidal mask)hahahahahaaaaaa naomba comment yako uifanyie mabadiliko haraka kabla wenye jinsia yao hawajaamka.
orabeoni wanatumia wanawake to indicate brother.
wanaume wanatumia hyungnim to indicate brother.
umenikumbusha episode moja ya return of superman ambapo ilitokezea song il kook alimuuliza mtoto wake wa mwisho kati ya wale mapacha watatu umri wake wa kuzaliwa.
jina lake anaitwa song manse na alipoulizwa akajibu umri wake ni manse
manse = hurray, long live, idumu miaka 10000.
song il kook alicheka kama mwehu
lakini ndio kujifunza kama nilivyokwambia binadamu tunategemeana.
gwenchanah gwenchanahHahaaaaaaaaaaaaaaà umeniingiza mtego bro Mimi ni Hyungnim Lee Kang to ndio alivyokua anamwita kaka yake (blidal mask)
Daaah wee mkorea wa Bububu umeniacha mataa hapogwenchanah gwenchanah
hyungnim / dongsaeng
Apa Nimeikumbuka Waikikigwenchanah gwenchanah
hyungnim / dongsaeng
Naingilia. Apo Anakujibu Kuwa Haina Shida, It's Okay.Daaah wee mkorea wa Bububu umeniacha mataa hapo
Inawezekana Mr. Sunshine Inaelezea Hii Ya Kutawaliwa Na Wajapan Kisha Urusi Na Marekani Wakaja Kuwakomboa, Maana Naona Ndo stori Inayozungumzia Sana Mule.Happy National Liberation Day of Koreakila inapofika tarehe 15 August nchini korea wanasherehekea siku yao ya kupata uhuru kutoka kwa wakoloni wa kijapani.
hii ni sherehe ambayo husherehekewa na wakorea wote pasina kuangalia itikadi zao na sera zao za kiutawala( south na north korea)
ilikuwa ni 15/08/1945 ndipo bendera ya japan iliondolewa nchini korea na kupandishwa bendera ya korea kwa msaada mkubwa wa Marekani na Urusi.
- korea kusini sherehe hizi wamezipa jina la Gwangbokjeol wakimaanisha siku ambayo muangaza wenye nuru umerudi kwa wakorea.
- korea kaskazini sherehe hizi wamezipa jina la Chogukhaebangŭi nal wakimaanisha siku ambayo uhuru umerudi kwenye ardhi ya mababa zetu.
kosa kubwa walilolifanya wakorea ni kuwa walishindwa kuchagua sera halisi za kuongoza taifa lao hivyo basi kila upande uliamua kufuata itikadi wanazoziamini.
unadhani nini kinatokezea kama upande mmoja unafuata sera za kijamaa kutoka kwa urusi na upande mmoja wa wapigania uhuru wanafuata sera za kibepari kutoka kwa marekani.?
ndipo mwaka 1948 pande hizi mbili zikaamua kugawana madaraka.
wote nimewaita madikteta kwa sababu pande zao walishindwa kuziunganisha na kuzifanya nchi moja na hatimaye kusababisha vita iliopoteza zaidi ya watu millioni 5. miaka miwili baadae.
- pro U-S dictator syngman rhee akachaguliwa kuwa rais wa korea kusini.
- pro soviet dictator kim IL sung akachaguliwa kuwa rais wa korea kaskazini.
- mwanadada kim so hyun ameandika maneno yafuatayo kwenye account ya instagram : sitoisahau siku hii.
- mwanadada chae soo bin ameandika maneno yafuatayo: leo tunasherehekea miaka 73 ya uhuru lakini sitosahau sadaka zilizotolewa na watu wenye tabia za kishetani.
- song il kook naye ameandika maneno yafuatayo : nipo mbele ya ukuta wa berlin muda huu, nimekutana na marafiki ambao wamenipa zawadi, nasisi leo tunasherehekea uhuru na natumai siku moja tutakuwa nchi moja.
Jamhuri ya watu wa korea iendelee kudumu kwa amani na mshikamano.