Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

mkuu wacha niongeze maarifa kwanza kwa kuijua vizuri historia ya korea maana itansaidia sana kuelewa mambo mengine pia
 
Yaani nami nahisi hivo. Ukinipa niangalie namaliza season moja yenye 40 episodes in a day. Ila kukariri ndio nshashindwa.
Labda hiyo siku usiinde kula wala kujisaidia labda unaweza maliza episode 26
 
Labda hiyo siku usiinde kula wala kujisaidia labda unaweza maliza episode 26
Nakula Mara moja tu. Mm huwa naweza tazama in a fast forward mode pia. Yaani mfano mtu anaanza kulia kulia basi mm napeleka mbele. Ila naweza anza kutazama saa mbili usiku hadi tano asubuh ndio nikalala hadi Saba then namalizia hadi mbili usiku tena game over.





Ila kwasasa nimestop koz ya majukumu. Viepisode vinne chali usingizi kesho job[emoji3]
 
JUMONG ndo drama yangu ya kwanza kuiona na nilimuelewa sana YOUNG PO naisi ndo aliyenogesha series akisaidiwa na MO-PAI-MO huyu mzee naye alinibamba! nyingine ninayoikubali sana ni ile ya THE WARRIOR BAEK DON SOO
Ni kweli Ju Mong ni hatareee
 
Mkuu kwa sie wananchi wazalendo wa taifa la GOGURYEO kutomuweka THE GREAT KING GWANGAETO umetufanyia uhaini mkubwa sana kiukweli.
Chonde Chonde bwana.

Shikamoo Gwangaeto!

Ilikuwa bahati mbaya kutokumtaja "the great king Gwanggaeto". Nilisahihisha kipindi humu humu jamvini.

Nina karibu "series" zote the "Historical drama" za zamani na mpya yapata 2TB.
 
Me hayo maelezo yako nimerudia Mara NNE ila wapi. Yaani nna tabu

Innocizy, labda kwa kukusaidia soma historia fupi ya Taifa la Korea katika hizo "drama series".

Korea imekuwapo kwa karibu miaka elfu moja. Falme ya kwanza ilijulikana kama GoJoseon ambayo ilianzishwa mwaka 2333 BC na Dangun hatimaye ikaangushwa na Han (China) katika mwaka 108 BC. Baada ya hapo GoJoseon ikagawanyika katika makabila mbalimbali na falme ndogondogo zinazounda Taifa la Manchuria ya sasa na rasi ya Korea. Eneo lote la GoJoseon likatawaliwa na Han ambayo ilianzisha komandi za kijeshi ili kuwazuia watu wa GoJoseon kukaa mbali na utawala wao.

Kwa haraka haraka twende mwaka wa 57 BC, wakati Ufalme wa Silla (aka Shilla) ulipoanzishwa na Bak HyeokGuhSen. Hata hivyo, zama za Falme Tatu (Three Kingdoms) si kweli kwamba ulipata kuanza kabla ya 37 BC bali ni baada ya huo mwaka na mwanzilishi wa Goguryeo, ambaye ni Jumong. Yeye aliweza kuyaunganisha baadhi ya makabila ya GoJoseon yaliyokuwa yametawanyika na kuyachukua tena baada ya kuliondoa Taifa la Han eneo hilo. Goguryeo ilizidiwa nguvu mwaka 18 AD na Baekje iliyoanzishwa na mke Jumong, Soseono na wanawe.

Baadhi ya tamthilia zinazosisimua (bora kuziona) wakati wa "Three Kingdoms" ni kama zifuatazo:
Jumong
The Kingdom of the Wind
Princess Ja Myung Go
Kim Soo Ro
King Geunchogo (aka Geunchogo Wang)
The Legend
King Gwanggaeto the Great
The King's Daughter, Soo Beak Hyang
Ballad of Seo Dong
Queen Seon Duk
Gye Baek
The Great King's Dream (aka The King's Dream)
The Great Hero (aka Yeon Gaesomun)
Sword and Flower
Dae Jo Young
The Emperor of the Sea (aka Hae Shin or Sea God)
 
Hapo ukitoa Kama tano zingine sijaona. Naomba link au Kama unazo uniambie mkuu nije nizichukue.



Nashukuru kwa historia nitaanza fatilia
 
Ilikuwa bahati mbaya kutokumtaja "the great king Gwanggaeto". Nilisahihisha kipindi humu humu jamvini.

Nina karibu "series" zote the "Historical drama" za zamani na mpya yapata 2TB.

Mkuu nitakutafuta aisee nipate hizo series
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…