Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Hivi wadau kuna mtu ambaye drama ya Yi San mwishoni haikumuumiza kiasi cha chozi kulenga?

Wiki iliyopita nimeimaliza inaisha kihuzuni sana hata maji nilishindwa kunywa!!
 
Itafute pia na Movie yake ambayo Storyline yake ndio imetumika kwenye hiyo Drama uliyoitazama.

Movie inaitwa Masquerade ya mwaka 2012.
hii movie imechangia kwa kiasi kikubwa sana niachane na mpango wa kuiendeleza the crowned clown drama.
gwanghae alikuwa ni mfalme aliyepitia maisha ya ovyo sana ya kiutawala.
gwanghae pia alikuwa ni mfalme aliyefanya baadhi ya matukio ya kishujaa yanayopaswa kukumbukwa.
aliondolewa madarakani kwa njia ya mapinduzi yakiongozwa na watu wa magharibi.
ni miongoni mwa wafalme waliopita kwenye tawala za korea wasipewe jina la heshima.
kama ni mtihani gwanghae amepata 5/10
 
Inashangaza sana kwakweli kutompa Gwanghae temple name wakati mfalme aliyerithi utawala baada yake, Injo alipewa temple name pamoja na kwamba aliboronga zaidi ya Gwanghae.

Kama ni kuwanyima heshima hiyo ingetakiwa wanyimwe wote na si kumtosa Gwanghae na kumpa Injo.
 
labda ni kwa sababu aliondolewa madarakani kwa njia ya mapinduzi ndio maana hakupewa heshima.
si unajua tena maisha yote aliyeshinda vita ndiye mwenye haki ya kuandika historia atakavyo, inawezekana watu wa mgaharibi (western faction) walimwenkea ngumu asipewe heshima
 
Dah! Umeiandika kibabe!! Loo! Kweli nimeamini usipokuwa mshapu kwenye kufanya maswali assignment zitakuua maana zinakuja zimepangana.
Ndo kwanza Emperor wang nipo sehemu ya 4.
Sijakaa sawa unanipa hii.
 
Kweli, hata yule mshikaji wao aliyekuwa General.
Kwa taarifa yako.
Yi san anatajwa kama mfalme bora wa Joseon.
1. Yi do ( Sejong the Great)
2. Yi san ( JeongJo)
Hao best Kings wa Joseon.
Yeah wote nimewasoma hadi huyo Sejong ndo aliyegundua lugha na maandishi ya Hangul
Kuna hadi mji umepewa jina Sejong City na wizara karibu zote zimehamishiwa huko.
Walikuwa na mpango wa kuufanya mji mkuu badala ya Seoul
 
Yeah wote nimewasoma hadi huyo Sejong ndo aliyegundua lugha na maandishi ya Hangul
Kuna hadi mji umepewa jina Sejong City na wizara karibu zote zimehamishiwa huko.
Walikuwa na mpango wa kuufanya mji mkuu badala ya Seoul
Cha kushangaza wamelelewa na Wafalme wenye akili nyingi halafu na madikteta:

Sejong tewang, yeye alichukua nchi kutoka kwa Baba yake Taejong, Taejong aliamini kuwa Nchi inapaswa kuongozwa kwa mkono wa chuma, ikiwa kama ngao ya kuepusha migongano ya ndani, na kwa ajili ya ustawi wa taifa. Taejong aliwauwa Ndugu zake wa damu, pia kina Jeong Mong-Ju ( Poeun), Jeong Do-Jeon ( Sambong) n.k

JeongJo: alichukua nchi kutoka kwa Babu yake YeongJo( mwana wa Dong Yi), YeongJo pia aliongoza kwa mkono wa chuma, pia alikuwa ana wajali wananchi wake. na moja ya tukio la kukumbukwa alitoa amri kali na kupewa adhabu ya kifo mtoto wake Crown Prince( Yi sado) kwa kosa la kutakata kufanya mapinduzi.Ingawa jambo hili halipo clear sana, wengine wanadai Yi sado alisingiziwa na wengine wanasema yaweza kuwa kweli.
 
Daemusin : ttok ttok nugu eopso = Knock knock anyone there?
aminas : Knock knock i'm here, knock knock right there.

kuna yoyote aliye tayari kunishikilia (kuwa pamoja nami)
nahitaji kuwa na mtu, nahitaji kuondoa upweke
kila ninapoangazia kila pande za jf,
sioni mtu wote wamekimbia amebakia great conquer
nashindwa kuvumilia, tafadhali rudi (njoo) kwangu
sihitaji tena kuwa mpweke
kiukweli hata sifahamu mjinga wewe umekwenda wapi
idon't care about shit


where are you chingu?
ndio nini kwenda likizo bila ya kunipa taarifa ahjummaaa au nimegeuka maua ya msituni (wild flower)?

nimekuwa lonely kwa takribani wiki tatu lakini ok baada ya miaka mitatu my crown princess lee hi amekuja kuniondolea upweke siku ya leo.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…