Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Daah kweli tunatofautiana, yaani mimi empress Ki ndio ilinifanya nielewe siasa hata za hapa bongo
Great King Sejong
Jeong Do Jeon
JingBirog(The Book Of Correction)
Queen SeonDeok

God Of War( Soldier)

Hizo ni moja ya Drama nzuri za kisiasa.
"Empress Ki" sikumbuki vizuri ilikuwa 2014 mwaka niliyoiona.
 
dear brother,
sifahamu mfumo wako wa kimaisha ukoje ila unaonekana ni mwanadamu ambaye either uko bize sana jambo linalokupelekea ukose muda wa kufungua hata link moja, pengine una tatizo la kusahau au vile vile pengine ni mwingi wa dharau (sifa hizi mbili za mwisho Mungu akuepushe nazo).

umeomba nikutajie drama alizoigiza ha ji won ila kwa wema wangu nimekuwekea link iliokusanya taarifa zake zote, cha ajabu unaniomba tena nikupe taarifa ya drama mpya aliyoshiriki au atakayoshiriki.

maana yake ni kwamba umenidharau na hiyo link niliokuwekea hujaifungua.

gwenchanah gwenchanah.​
drama yake mpya inaitwa chocolate na inatarajia kuanza kuonyeshwa mwishoni mwa mwezi November.
View attachment 1256713

musiendelee kuugeuza wema wangu kuwa ni utumwa, kuna siku nitachoka, nitachukia na baadae nitakimbia humu ndani tofauti na watumwa wale weusi walioendelea kuvumilia mateso yalioongozwa na mafedhuli baada ya kufungwa kwao minyororo jambo lililopelekea washindwe kukimbia.

bado sijachukia ila siku naona kama zinazidi kukaribia.
Kwanza kabisa ni samehe brother kiufupi ninakuaga nipo bussy Sana Wala sikuwa na lengo la kukwaza na sisi wote ni binadamu kukoseana ni sehemu ya Maisha yetu.
 
Screenshot_20191108-171815.png
Hatari sana wee Daemusin, Tayari ushaitupia Joeng do Joen
Hat Off
 
VAGABOND Hii Kitu, Korean Entertainment Ahsante. Stori Tamu Inasisimua Kila Scene Haipiti Bure,
Ina Mtiririko Mzuri Hakuna Nguo Za Ndani Wazi Mule Ndani Wala Mwili Wazi, Hakuna Viungo Vya Wakike Wazi Mule Ndani Na Bado Inakufanya Uhitaji Kuingilia Kila Inapotoka.

Wametengeneza Kitu Kiutamaduni Wao Na Bado Kinavutia.

Tanzania Yangu Tunakosea Wapi!?!
Naikubali sana, iko poa kweli kweli
 
Wee Daemusin mbona Yule Mke mkubwa wa wang Gun, mbona haonekani tangu alipoambiwa aende nje ya Palace kama ikiwa njia pekee ya kumtibu, kutokana kuwa Wild Gisaeng za mika 1000 zilikuwa zishatumwa Sangju kwa mzee Ahjigae( Baba yake Kyeon Hyeon).
Je Queen Huyo alikufa ama ndo uhusika wake ashamaliza, hata dingi yake( Lord Yu) simuoni tena Pale Palace.



Mzee mkubwa Kati ya Goryeo na Joseon, ni Nasaba ( Dynasty) ambayo ilikuwa na Wafalme wazuri na Ipi ilikuwa Powerful?
 
Wee @Daemusin mbona Yule Mke mkubwa wa wang Gun, mbona haonekani tangu alipoambiwa aende nje ya Palace kama ikiwa njia pekee ya kumtibu, kutokana kuwa Wild Gisaeng za mika 1000 zilikuwa zishatumwa Sangju kwa mzee Ahjigae( Baba yake Kyeon Hyeon).
wewe mjinga kutoka chato district hivi utaacha lini tabia ya kuniuliza maswali yako ya kijinga jinga?
badala ya kuniuliza maswali yanayomuhusu mke wangu mtarajiwa cha kushangaza mjinga wewe unaniuliza maswali yanayoomuhusu mke wa sheikh wang guhn,

huyo bwege alikuwa na wake takribani 30 ina maana mjinga huyo alikuwa na nguvu za kiume zenye ujazo wa pipa la maji.
kwa ufupi nimeshasahau kwa asilimia fulani kilichotokezea ndani ya hiyo drama, ila kama nitakuwa nipo sahihi hiyo drama imetuonyesha zaidi maisha ya wake zake wawili kwa asilimia kubwa sana.

  • mke wake mmoja ni yule aliyebahatika kumzalia mtoto wake aliyemkabidhi madaraka baada ya kifo chake.
  • mke mwengine ndiye yule aliyekuwa anampenda sanaaaa kama wema sepetu na ndio maana alimzalia watoto wengi akiwemo wang so, nina wasiwasi mke huyu ndiye aliyemtuma akapumzike nje ya palace kwa sababu ya ugonjwa na stress za kumpoteza mtoto wake wa kwanza. baadae kama nipo sahihi alirudi tena ndipo akaanza zoezi la kufyatua watoto takribani watano.
1573365062755.png


I wish ningelikuwa emperor wang guhn.
jamaa alikuwa hapumziki kufanya harusi kama ukumbi.
 
Me kutumia telegram nimeshindwa kabisa, na mb ni nyingi mno kwa kudownload wengine tunatumia bundles za kawaida, naomba aliye huku DSM , nije aniwekee kwenye device yangu! Plz plz
 
Back
Top Bottom