Thank u alot mamaa nimeanza na Empress Ki.Korean Dramas Tz Fans
Link hiyo hapo Mkuu, ingia upakue drama bure huko kwingine naona mnauziwa [emoji1787][emoji1787][emoji1430]
Sent from my iPhone using JamiiForums
hahaha Unapitia kipindi kama ambacho nilichopotia na mwenzangu tunaitazama WAIKIKI 1, Tulikuwa tunacheka kwa sauti mpaka najiuliza hizi ni miye ndio nacheka hivi!! au nimefungiwa spika, maana hiyo Drama kwa vituko ni bora sana.Jamani hii Marry Me Now karibu itanifanya kichaa na my colleague, kuna wakati mpaka tunajisahau tunacheka kwa sauti SMH 🤦♀️
itafute modern farmer drama......
ila sharti uangalie peke yako, nilibahatika kuiangalia mpaka episode 4, kwa kujali afya yangu niliamua ni bora niachane nayo.
unaweza kucheka mpaka ukapelekwa hospitali ya vichaa bila ya kujifahamu
huyu fala ukiamuangalia tu sura yake basi unacheka.
dah! mpambano umeshakuwa mgumu (sijui nichague project ipi ili niiweke kiporo)............
- my father is strange
- my golden life
- my only one
- five enough
- all about my mom
- mother of mine
Numbisa kuja hapa mara moja, wewe ndiye raisi wa korean family drama.
zote ni project nzuri, ila nahitaji ilio bora zaidi kwa uoni wa jicho lako (huenda umeshaziangalia zote)
Shukrani sana, ila nilihitaji ni- download
Sawambona tupo jirani humu ndani, huoni tunasaidiana kwa kadri ya uwezo wetu tuliojaaliwa.
hiyo kauli yako umenikumbusha tukio la karibuni lililotokezea dhidi yangu.
hahahahaaaaaaa
PATA 500 KWA KUDOWNLOAD APP YA TIGOPESA
Wadau fursa imejitokeza sio ya kukosa kabisa...
kama una tumia laini ya Tigo zama play store download app ya Tigopesa na uifungue weka namba yako watakutumia verification code weka baada ya hapo watakuomba promo code weka 👉 ROBL5582 ili upewe hiyo jero ni lazima uweke hiyo promo code
marry me now (shall we live together)
kilichonivutia na kujifunza
kilichonichukiza:
- mapenzi hayana muda maalum wala ukomo wa umri (the power of love)
- fanya kazi kwa bidii yenye kuambatana na nidhamu ili ujitengezee msingi bora wa maisha, wajapani wanasema mbora wao ni yule anayeanguka mara saba lakini mara ya nane akainuka tena, kwenye maisha hutakiwi kukata tamaa, (kongole kwake jang mi hee ahjumma, inaniwia vigumu kuamini ya kwamba huyu mama amezaliwa miaka 63 iliopita kwa umri wa korea)
- Muombe mungu akujaalie kwenye maisha yako uzungukwe na watu waliojawa upendo, utu dhidi yako kwa sababu hata kama utazungukwa na changamoto ngumu za kimaisha kama ugonjwa, anguko la kiuchumi basi upendo wao usio mithilika dhidi yako, imani yao kwako, matumaini yao dhidi yako yataweza kukuinua tena juu na kukufanya uendelee na safari yako ya kimaisha (endelea kuangalia hiyo drama ndipo utakapogundua nilichomaanisha)
wakorea wanavyo tuchukulia Waafrika........
najua waafrika tuna matatizo yasiohesabika ndani ya bara letu yanayosababishwa zaidi na ukosefu wa elimu ya utambuzi (kujitambua) kuanzia kwa raia wa kawaida kama mimi hadi viongozi wetu wakubwa tuliowapa mamlaka makubwa ya kutulinda na kuzisimamia rasilimali zetu zinazohamishika na zisizohamishika, bahati mbaya elimu hii ya utambuzi haipatikani ndani ya chumba cha darasa kwa sababu wapo waafrika waliobahatika kuwa na elimu kubwa sana ya darasani lakini matendo yao na utu wao ukizidiwa kwa kiwango kikubwa sana na wengineo wakiwemo hao waliokimbia darasani
kupitia drama hii nimeendelea kutofurahishwa na tabia hii ya kuendelea kutuchukulia waafrika wote ni watu dhaifu mno kwa kila jambo (na huu ugonjwa si mara ya kwanza kuushuhudia kupitia vipindi vya wakorea nilivyobahatika kuviangalia), mara nyingi sana wanapoizungumzia Afrika huoainisha kama ni sehemu moja yote (yenye matatizo, yenye watu wasiojielewa, wapenda vita, wasioweza kuishi bila ya kupatiwa msaada, sehemu ambayo ukitembelea lazima usafiri na choo chako na maji ya kujisafishia) jambo ambalo si sahihi kwa mtazamo wangu kwa sababu afrika si muunganiko wa nchi moja na pia hatufanani kiutamaduni, kiuchumi na hata kimatatizo licha ya kwamba tunatokea bara moja hivyo basi si sahihi kutuhukumu sote kama ni species tegemezi isiyo na faida yeyote.........
Wanapoandaa project zao basi ingelipendeza zaidi kama wangelibase zaidi na eneo maalum na si kutuangushia mzigo waafrika wote
kama wanashindwa kufanya hivyo basi watengeneze japo eneo la kubuni pindi wanapotengeza project zao kama walivyofanya descendent of the sun drama (walibuni eneo lisilo rasmi kwenye dunia yetu linaloitwa Urk ambalo tulishuhudia lead actors wakiongozwa na song hye kyo wakienda kujitolea kutoa huduma za kiafya)
Halafu hizi nchi zilizoendelea kama zinaongozwa na nia ya kweli ya kutaka kutusaidia sisi waafrika tusiojielewa (kama wanavyotuchukulia wengi wao) basi zipo njia njema zaidi ya hii ya kujitolea kutoa huduma husika kama za kiafya, elimu au tafiti (voluntary works) kwa muda maalumu
Haya matendo wanayoyafanya hayana utofauti wowote na yale yanayotekelezwa na wazee waliojaalia kipato cha fedha (utamkuta mzee anampa mwanawe kiwango cha fedha taslimu kila baada ya muda, au mwengine anampa credit card) wakati alikuwa na uwezo wa kumpa nyenzo mtoto wake zitakazomuwezesha kujiongoza mwenyewe kupata pato lake la halali ili kuepukana na utegemezi na si kusubiria kila siku suruali ya mzee itanuke.
kwa mfano wanatupa huduma za kiafya kama madawa na hata wataalamu kwa muda maalumu, misaada ya kifedha, wanatuletea walimu wanatufundisha kwa muda maalum, wanatuletea wataalamu kupitia sekta nyenginezo na wao pia kwa muda maalumu n.k
kivyovyote kwa mfumo huu sisi waafrika tutaendelea kuwa wategemezi kwao (Ingelipendeza zaidi kama wangelikuja kuwekeza moja moja huku kupitia sekta zote muhimu wakiongozwa na moyo safi wenye kuambatana na uadilifu wa kutufunza ili kupeukana na utegemezi pamoja na kuheshimu rasilimali zetu zilizopo na si kutuonjesha keki zao kwa muda mfupi then wanakimbia (msaada wa muda mfupi hauwezi kuondoa tatizo sugu)
kwa mfano hawa mabwana kama wanatupenda kweli basi waje japo kutumia ardhi yetu kwa ajili ya film location, tumejaaliwa mito, maziwa, misitu ya kuigiza hata filamu za kivita, Mungu ametupa zawadi ya milima (basi wawatumie celebrities wao kutangaza utalii ili kigwangwala apumzike kulialia twitter, pia tumejaaliwa hoteli na visiwa vilivyojaaliwa mandhari nzuri hata kwa wanandoa wanaohitaji kupumzika (wasiishie kwenda jeju, japan, Bali indonesia, america) bila ya kusahau population ya vijana waliotayari kufanya kazi kwa bidii kwenye mazingira yeyote ilimradi wapate gawio linaloendana na matumizi ya nguvu zao ..........
kwa kuwa serikali zetu ni sikivu basi naamini suala la kodi linaweza kuzungumzika na kupatiwa ufumbuzi wenye kunufaisha pande zote mbili
Kudos to all volunteers who sacrifice themselves and their families for the good of humanity
favorite couple: Yeon Da Yeon + Park Jae Hyung
huenda ni kwa sababu tulikuwa tunalingana nao sana kimaisha kabla ya vugu vugu la mapinduzi na uhuru kufanikiwa, kitendo cha wao kutuacha nyuma baada ya uhuru ndio kunawafanya waamini ya kwamba waafrika wote ni jamii isiyojielewaKijana aliyekata tamaa ya maisha au kutaka kujiweka mbali na dunia anaitaja afrika kama sehemu ya kwenda huku wenzie wakishtuka anaenda pabaya
Mtoto au kijana wa kitajiri akileta ujeuri anatishiwa kutupiwa afrika. Hawa watu tunawapenda ila ni wabaguzi balaa
Acheni Maskhara, Umesema eti China?!!!.....!!!.Hata wao walibaguliwa sana na wazungu mpaka walipoamua kuwa na akili ya kizungu ili kupambana na wazungu
Elimu, siasa uchumi bado ni kituko kwao acheni watubague tuwe na akili, wakati tunapata Uhuru tulikuwa sawa na China je Leo tuko wapi?
Mifumo ya inayoongoza familia inatoka kwenye Sera ya nchi pamoja na kazi za serikali.Acheni Maskhara, Umesema eti China?!!!.....!!!.
kwa taarifa yako Qing Dynasty iliwahi kutawala kiuchumi Duniani, kuanzia GDP na fact zingine nyingi za kiuchumi. na walishuka kiuchumi baada ya madhara ya vita dhidi ya Wajapan na baadaye waingereza.
Halafu hao wachina ambao unasema kuwa wazungu waliwabagua si kwa sababu hawakuwa na akili, laah!! Siku zote Unapaswa kuwa na akili uweze kumtambua mwenye akili. ni wazi kuwa Wazungu walitumia Ubaguzi na matusi as right tool to mask their incompetence.
China ni moja ya sehemu chache za Dunia iliyozalisha majitu yaliyokuwa na uwezo mkubwa wa kufikiri, mfano;-
Master Kong Fu zi ( Confucius), Meng zi ( Mencius), Laozi, Zhuangzi, Xunzi, zhu xi, zhuge liang( Greatest military Advisor katika history ya Dunia) , zhuang zhou n.k maana ni wengi mno. na walikuwa wanaishi vizazi mpaka vizazi. Ni wazi kuwa hawakuwa wanyonge.
Kwahiyo kama sisi tunataka tusonge ni lazima tuanze kubadilika sisi wenyewe ( Wananchi), People are the limbs of the Government, na Serikali inajengwa na watu, Serikali yenyewe ni kama msimamizi.
kwahiyo kabla haujailaumu Serikali itazame kwanza Familia na Jamii yako inazalisha watu wa aina gani? maana hizo tabia walizonazo ndizo zitakazo wajenga hata mpaka wakipata nafasi ya utumishi wa umma ndizo watakazofanya, kama ni njema basi tutakuwa na Serikali endelevu na Nchi yenye matumaini, kama wamejawa na uovu basi tegemea serikali masikini na Nchi isiyokuwa na matumaini na Dira.
Ubora wa Taifa lolote unategemea Ubora wa watu wake, kuanzia ngazi familia mpaka...
View attachment 1419440
hahaha Naam, baada ya Burudani niliyoipata kwenye WAIKIKI, sasa nimeamua kuitafuta WAIKIKI 2.
Karibuni sana tucheke wenyewe kama vile hatujielewi.
Zinasifiwa sana ngoja nizitafute maana waikiki niliwahi ivuta episode moja tu ikanishinda pale story ilipoanzia mtoto aliyetelekezwa maana hii story nshaiona kwa wahindi mwanzo mwisho kisha bongo movie wakaua kabisa kwa kuiiiga vibaya
Kaka Nimechoka kutype.Mifumo ya inayoongoza familia inatoka kwenye Sera ya nchi pamoja na kazi za serikali.
Qing dynasty haikuwahi kutawala dunia kiuchumi labda unisaidie wakati UPI? Tunaposema dunia onyesha ulinganifu pamoja na Nguvu za kisiasa kwan uchumi unaendana na utawala
Ni kweli tamaduni zao Confucius na Mencius ziliwajengea hamu ya kusoma tangu kale. Tujiulize sisi waafrika kusoma tumeanza lini?
Huwezi kuwa na taifa bora nawakati elimu si utamaduni wenu. Fuatilia nchi za afrika zenye mifumo angalau mizur ya elimu hata siasa na uchumi angalau ni safi.
Lkn afrka wajinga ni wengi kuliko walioelimika hivyo tubadike kwanza na ndipo hatutabaguliwa
Hahah Haya mambo ni sehemu ya Historical Drama tunazotazama.Tucheki muvi wakuu
Huu si Uzi WA kufirikishana Bali kurelieve sonona zetu na uchovu