marry me now (
shall we live together)
kilichonivutia na kujifunza
- mapenzi hayana muda maalum wala ukomo wa umri (the power of love)
- fanya kazi kwa bidii yenye kuambatana na nidhamu ili ujitengezee msingi bora wa maisha, wajapani wanasema mbora wao ni yule anayeanguka mara saba lakini mara ya nane akainuka tena, kwenye maisha hutakiwi kukata tamaa, (kongole kwake jang mi hee ahjumma, inaniwia vigumu kuamini ya kwamba huyu mama amezaliwa miaka 63 iliopita kwa umri wa korea)
- Muombe mungu akujaalie kwenye maisha yako uzungukwe na watu waliojawa upendo, utu dhidi yako kwa sababu hata kama utazungukwa na changamoto ngumu za kimaisha kama ugonjwa, anguko la kiuchumi basi upendo wao usio mithilika dhidi yako, imani yao kwako, matumaini yao dhidi yako yataweza kukuinua tena juu na kukufanya uendelee na safari yako ya kimaisha (endelea kuangalia hiyo drama ndipo utakapogundua nilichomaanisha)
kilichonichukiza:
wakorea wanavyo tuchukulia Waafrika........
najua waafrika tuna matatizo yasiohesabika ndani ya bara letu yanayosababishwa zaidi na ukosefu wa elimu ya utambuzi (kujitambua) kuanzia kwa raia wa kawaida kama mimi hadi viongozi wetu wakubwa tuliowapa mamlaka makubwa ya kutulinda na kuzisimamia rasilimali zetu zinazohamishika na zisizohamishika, bahati mbaya elimu hii ya utambuzi haipatikani ndani ya chumba cha darasa kwa sababu wapo waafrika waliobahatika kuwa na elimu kubwa sana ya darasani lakini matendo yao na utu wao ukizidiwa kwa kiwango kikubwa sana na wengineo wakiwemo hao waliokimbia darasani
kupitia drama hii nimeendelea kutofurahishwa na tabia hii ya kuendelea kutuchukulia waafrika wote ni watu dhaifu mno kwa kila jambo (na huu ugonjwa si mara ya kwanza kuushuhudia kupitia vipindi vya wakorea nilivyobahatika kuviangalia), mara nyingi sana wanapoizungumzia Afrika huoainisha kama ni sehemu moja yote (yenye matatizo, yenye watu wasiojielewa, wapenda vita, wasioweza kuishi bila ya kupatiwa msaada, sehemu ambayo ukitembelea lazima usafiri na choo chako na maji ya kujisafishia) jambo ambalo si sahihi kwa mtazamo wangu kwa sababu afrika si muunganiko wa nchi moja na pia hatufanani kiutamaduni, kiuchumi na hata kimatatizo licha ya kwamba tunatokea bara moja hivyo basi si sahihi kutuhukumu sote kama ni species tegemezi isiyo na faida yeyote.........
Wanapoandaa project zao basi ingelipendeza zaidi kama wangelibase zaidi na eneo maalum na si kutuangushia mzigo waafrika wote
kama wanashindwa kufanya hivyo basi watengeneze japo eneo la kubuni pindi wanapotengeza project zao kama walivyofanya
descendent of the sun drama (walibuni eneo lisilo rasmi kwenye dunia yetu linaloitwa Urk ambalo tulishuhudia lead actors wakiongozwa na song hye kyo wakienda kujitolea kutoa huduma za kiafya)
Halafu hizi nchi zilizoendelea kama zinaongozwa na nia ya kweli ya kutaka kutusaidia sisi waafrika tusiojielewa (kama wanavyotuchukulia wengi wao) basi zipo njia njema zaidi ya hii ya kujitolea kutoa huduma husika kama za kiafya, elimu au tafiti (voluntary works) kwa muda maalumu
Haya matendo wanayoyafanya hayana utofauti wowote na yale yanayotekelezwa na wazee waliojaalia kipato cha fedha (utamkuta mzee anampa mwanawe kiwango cha fedha taslimu kila baada ya muda, au mwengine anampa credit card) wakati alikuwa na uwezo wa kumpa nyenzo mtoto wake zitakazomuwezesha kujiongoza mwenyewe kupata pato lake la halali ili kuepukana na utegemezi na si kusubiria kila siku suruali ya mzee itanuke.
kwa mfano wanatupa huduma za kiafya kama madawa na hata wataalamu kwa muda maalumu, misaada ya kifedha, wanatuletea walimu wanatufundisha kwa muda maalum, wanatuletea wataalamu kupitia sekta nyenginezo na wao pia kwa muda maalumu n.k
kivyovyote kwa mfumo huu sisi waafrika tutaendelea kuwa wategemezi kwao (Ingelipendeza zaidi kama wangelikuja kuwekeza moja moja huku kupitia sekta zote muhimu wakiongozwa na moyo safi wenye kuambatana na uadilifu wa kutufunza ili kupeukana na utegemezi pamoja na kuheshimu rasilimali zetu zilizopo na si kutuonjesha keki zao kwa muda mfupi then wanakimbia (msaada wa muda mfupi hauwezi kuondoa tatizo sugu)
kwa mfano hawa mabwana kama wanatupenda kweli basi waje japo kutumia ardhi yetu kwa ajili ya film location, tumejaaliwa mito, maziwa, misitu ya kuigiza hata filamu za kivita, Mungu ametupa zawadi ya milima (basi wawatumie celebrities wao kutangaza utalii ili kigwangwala apumzike kulialia twitter, pia tumejaaliwa hoteli na visiwa vilivyojaaliwa mandhari nzuri hata kwa wanandoa wanaohitaji kupumzika (wasiishie kwenda jeju, japan, Bali indonesia, america) bila ya kusahau population ya vijana waliotayari kufanya kazi kwa bidii kwenye mazingira yeyote ilimradi wapate gawio linaloendana na matumizi ya nguvu zao ..........
kwa kuwa serikali zetu ni sikivu basi naamini suala la kodi linaweza kuzungumzika na kupatiwa ufumbuzi wenye kunufaisha pande zote mbili
Kudos to all volunteers who sacrifice themselves and their families for the good of humanity
favorite couple: Yeon Da Yeon + Park Jae Hyung