Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Jamani naombeni mnisaidie ni app gani nzuri ninayoweza kuwa natazama korean drama,maana nshahangaika bila majibu,hasa hasa naitaka drama ya emperor of the sea na iljimae

Tulia hivyo hivyo dawa ikuingie..[emoji382]
 
Niko Episode ya 17 Hii "SHIN DON" sio mchezo, naona Empress KI anayomuenda Gongmin na Goryeo.
ila Huyu Mfalme Gongmin bado alikuwa mdhaifu kwelikweli.
Nadhani hizi zama za Gongmin ndio za Ambazo Waliishi kina Sambong, Choi Young & Yi Songgye.
Yote kwa Yote Wa-Goryeo walikuwa mashujaa sana kuliko wa-Joseon, huwa nawaza kwa jinsi wa-choseon walivyodhaifu wasingeweza kupata uhuru kutoka kwa Wa-Mongolia.
 
Huyo Queen Noguk alikuwa Smart mpaka raha, alikuwa mjasiri sana na Mshauri na mtu wa kumpa mfalme matumaini na kumtia moyo.
Miye mwenyewe nimempenda bure kwa ujasiri wake, Nadhani kama angeishi miaka mingi nadhani tusingeiona JOSEON( YI dynasty).

Hivi kwani Hamna Drama ya kumuhusu Mfalme JANG SU wa Gogryeo?
 
Hahaha Wachina wasituchanganye, yaani King Gwanggaeto(Dam Doek) awe mchina!!, King Dongmyeong( Jumong)!!, Daemusin( Muyul)!! wasituzingue hao.
Basi hiyo Gogryeo haikuwa ya mchezo, mpaka wanagombania umiliki wa historia yake.

Lakini King Jang Su alikuwa ni mfalme mzuri, ni moja kati ya wafalme bora kabisa wa Gogryeo.
Ndiye mfalme aliyetawala miaka mingi zaidi, Karibu miaka 78 kwenye kiti cha enzi, aliyafaidi matunda ya baba yake King Gwanggaeto the Great.
yeye ndiye aliyeifupisha jina Gogryeo to Goryeo, na alihamisha makao makuu kitoka Gungnae-seong to Pyeongyang-seong.
 

Hio marry me now itabidi niitafute naona inasifiwa sana


Sent from my iPhone using JamiiForums
 
Hakika Daemusin lkn pia wanatufundisha carrier za watu wa kawaida na nmna wanavyointeract
Pia suala la uhalisia na hisia tofauti na kwetu watu wanajibadili sauti, hakuna hisia wala harara ktk matendo ukiacha zilizotengenezwa na wageni kama Siri ya Mtungi,, Fatuma nk
Pia wanatufundisha tamaduni zao ni za namna gani nasi tunaweza ishi hivyo lkn tunaogopa au kudhauriana
Kulala watu wengi nyumba moja kwenye My Father is Strange pia inadhihirisha sio big deal ni uchoyo wetu tu kukaribisha watu
S korea seems people live simple but kama nchi wako mbali kimaendeleo

Suala la posho linaendelea pia yaani ukipitisha umri
wa kukaa nyumban lazma uchangie kama kodi kila mwezi na kama huna kazi wanakudistab mpaka upate

Golden sijaiangalia lkn naitafuta nikimaliza whisper na innocent Defendant

Vipi kuhusu king of amnbition
 
Duh! kweli hao Gogryeo walikuwa Wanaume.
ilikuwa miaka 700 ya kiume.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…