Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Sijui huu uvivu nimeutolea wapi
Duh!

Kuna kamsemo kanasema, "kushindwa jambo sio makosa, bali kuacha kufanya jambo kabisa ni makosa makubwa."

Tukiuleta msemo huo katika tasnia yetu hii;
Kama ni projects, tazama hata mwanzo wake tu na kadri utazamapo unaweza kukutana na mambo mbalimbali yatayokupa hamasa zaidi ya kuendelea kutazama.
 
Guys
Naomba ambaye ameshaiona season 1 ya ''KINGDOM'' ambayo imeshatoka anipe summary kabla sijaanza iangalia
Nisijekutana na mauzauza
Utakutana na 'mazombi' ya hapa na pale!

Kama wewe ni mpenzi wa filamu za namna hiyo (horror), basi na hiyo utapata kuipenda.

KINGDOM inamuelezea Mwana Mfalme wa Joseon aitwae Lee Chang ambaye katika harakati za kiuchunguzi kufahamu undani wa ugonjwa uliomkumba Mfalme wa kipindi kile (baba yake) anasafiri kuelekea mbali kidogo na mji ili kutafuta ufumbuzi juu ya suala hilo.

Lee Chang anafika katika eneo moja la kitabibu akiwa na mlinzi wake binafsi ama bodyguard na kubaini kuzuka kwa janga kubwa na la kushangaza la wafu kurejea katika maisha na kuwaua wale walio hai, janga ambalo tayari limekwisha leta athari kubwa katika eneo hilo. Huko anakutana na mfanyakazi mmoja wa kitabibu, mtu pekee aliyenusurika katika kituo hicho cha kitabibu, mwanadada unaweza muita Seo-Bi.

Ni jukumu la Lee Chang pamoja na ushirika wa watu wake wa karibu kupambana dhidi ya kuenea kwa janga hilo kubwa na la kutisha katika eneo hilo na taifa la Joseon kwa ujumla.

Nakutakia utazamaji mwema!
 
Me swez nliacha mwanzon baada ya kuona lile li vampire uwiiiih
 
Inabide nifanye hivyo mkuu
 
Una weekend nzuri mno,hwarang ipo vizuri
Ile scene anayo mpa soda ya coca imenipa demu mtaani kwangu
[emoji3][emoji3][emoji3][emoji3][emoji3]
 
View attachment 1510809
Nani ame check It’s okay not to be okay ep 9 jana?
Daamn hii drama ni [emoji91][emoji91]
Kim soohyun hii drama anaitendea haki kwa kweli
Yaaan Yuko vizuri,alililia kwa hisia utasema kweli kumbe igizo tu,hadi chozi lilinitoka.
yuko njema ndo maana anaongoza kwa kulipwa vizuri
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…