Currently watching.
1. Through the darkness drama:
kumbu kumbu zangu ikiwa zipo sahihi kuanzia episode 6 muandishi ameamua kuturudisha kwenye mkasa wa ukweli wa kihalifu uliotokezea nchini korea mnamo mwaka 2003/04, kuna muhuni anaitwa yoo young chul(nafikiri bado yupo gerezani),
huyu fala alihusika na mauaji ya wanawake takribani 20. Alikuwa akiwalenga zaidi wanawake wanaotokea kwenye familia za kitajiri na alitumia nyundo kama ni silaha yake kubwa ya kutekeleza ushenzi wake.
huyo bwana alipoulizwa kwa nini anafanya mauaji hayo alijibu
Women shouldn't be sluts, and the rich should know what they've done."
mwishoni mwa mwaka 2021, mtandao wa netflix walirelease special documentary inayozungumzia mkasa mzima wa mauaji ya huyu bwana na wameipa jina la
The Raincoat Killer: Chasing a Predator in Korea.
2. King of tears, taejo Lee bang won
hii drama ilisimama kwa takribani wiki tatu
, hawa mabwana wanaozalisha hii drama walifanya dhambi isiosameheka ya kusababisha kupotea kwa uhai wa farasi waliomtumia kushoot tukio la yi seong gye kuanguka na farasi akiwa mawindoni. Ili kutengeneza uhalisia wa tukio waliamua kutumia farasi wa ukweli, wakaamua kumfunga kamba za miguu, katika kumuangusha farasi akaanguka vibaya na hatimaye baada ya siku chache farasi akafariki.
Hapo ndipo mgogoro wenye kuambatana na matamko ulipozuka ndani ya korea.
Mwanamke ni kama majani ya chai huwezi kuona nguvu yake mpaka uyachanganye na maji ya moto.
utakapoiangalia hii drama ndipo utakapofahamu nilichomaanisha.
- Yi seong gye alizungukwa na mwanamke mwenye ushawishi
- Yi bang won naye akaongozwa na mwanamke jasiri.
What next: ni vita ya kutoana roho Kati ya baba na mwana.