Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

kumbe si wa nchi hii na unaonekana unazo nyingi sana
 
Hahaha nimekumbuka slave hunter ni kweli itakuwa ndio swaga zake za uigizaji tumvumilie tu huyu ni Jang Hyuk, lakini hata mimi huwa namfananisha sana na Kim Nam-gil ambaye yuko kwenye bad guy...
hahahahahaaaaa hata mimi wakati naangalia shine or go crazy nilikuwa nachukia ile style yake ya kucheka na kujifanya kama ni bwege, ila jamaa ni mkali sana kwa martial arts naweza kusema kwa waigizaji wote wa korea yeye ni bora kwangu mimi.kwa sasa hivi amepata offer ya kuigiza drama inayoitwa voice ambapo anacheza kama ni detective (afande)
 
Hii inayoitwa shine or go crazy mimi mbona hata siielewi...nimejaribu mara kadhaa kuiangalia moyo umegoma kabisa
 
Msaada kwa wanaojua series za kikorea kali zaid nikimaanisha nzuri zaid ila na pendelea zziwe za mjini zisizo za action au history most na prefer za romance , fantasy, melody and comedy au medical drama pia napendelea drama za mijini sio kijijini naomba mnitajie majina kwa wanaozifahamu .
 
prime minister and I.
 
Be strong geum soon
 
Korean celebrities ambao wanatarajia kutumikia shughuli za kijeshi
(military activities) 2017


Kwa yeyote Yule ambaye ni mpenzi wa Korean entertainment naamini kitendo cha korean celebrities kwenda kutumikia shughuli za kijeshi (military activities) ni jambo ambalo humuacha na huzuni sana kwa sababu atashindwa kumuona celebrity anayempenda kwa takribani miaka miwili (2). Kama ni mwanamme na umezaliwa 1997 kwa sasa utakuwa unatimiza miaka 20 ambao ndio umri ambao unapaswa kujiandikisha kutumikia jeshi hadi miaka 38 kwa sheria za korea kusini.

Celebrities wanapaswa kutumikia military activities kabla hajavuka miaka 30 ya kuzaliwa na baada ya kujiandikisha unapaswa kutumikia mazoezi kwa takribani wiki 4 katika kambi ya kijeshi na pia kutumikia miezi 21 katika kambi ya jeshi iliyopo eneo lolote,kama ni marine service utatumikia miezi 23 na kama ni air force ni miezi 24.

Hata hivyo wapo baadhi ya waigizaji ambao baada ya kurudi kutumikia military activities walirudi kwa mafanikio makubwa sana,kwa mfano Song Joong Ki baada ya kumaliza miaka 2 ya kutumikia jeshi alirudi kwa mafanikio makubwa baada ya project yake ya descendent of the sun kuwa ni drama bora kwa mwaka 2016.

Miongoni mwa celebrities ambao wametangaza kutumikia shughuli za kijeshi ni pamoja na :-

Big bang T.O.P:


Kama ulipata kuangalia IRIS 1 (2009) drama basi utakuwa unamkumbuka huyu jamaa,alicheza kama ni X killer (muuaji) anayetumikishwa na MR BLACK na BAEK SAN (iris) ,licha ya kuwa ni muigizaji ila kazi yake kubwa ni uimbaji ambapo ni miongoni mwa member wanaounda group la muziki linalojulikana kama ni BIG BANG, amezaliwa November/ 4/ 1987.

Siku ya tarehe 9/2/2017 ndio alijiandikisha kwa ajili ya kutumikia jeshi na anatarajiwa kutumikia wiki zake 4 za mazoezi katika kambi ya Nonsan Army Training Center.

Siku ya tarehe 8/2/2017 katika account yake ya instagram alipost picha ya chupa ya mvinyo (wine) ambayo alipokea kutoka kwa rafiki yake ambaye ni LEE BYUNG HYUN ambapo aliandika

“kutoka kwa kaka yangu mpendwa ambaye pia ni rafiki yangu”

Chupa hiyo ya wine ilikuwa na ujumbe ambao umeandikwa na Lee Byung Hyun

tafadhali naomba urudi ukiwa na afya njema na natumai muda ambao utautumia huko hautojisikia kama umeupoteza na natumai utakapo rudi tutapata muda wa kunywa pamoja

Chupa hiyo ya wine ya kifaransa aina ya Chateau Petrus 1987 gharama yake ni won million 5 hadi 6 won million kwa chupa ($4370 hadi $ 5240) ambayo ni sawa na wastani wa Tzs 10 million hadi Tzs 12 million.

Wawili hao walikutana mwaka 2009 ambapo kwa pamoja walishiriki kwenye IRIS 1 drama ambapo LEE BYUNG HYUN ambaye pia ndiye mmiliki wa BH entertainment aliigiza kama ni KIM HYUN JUN (TK1) agent wa NSS.

JI CHANG WOOK

Amezaliwa july5 1987, ni actor na pia ni muimbaji ila mpaka sasa hajatangaza tarehe rasmi ya kujiunga na military activities, kazi yake ya mwisho itakuwa ni crime action movies inayoitwa Fabricated City.baadhi ya nyimbo zake zimetumika kama ni original sound track (ost) katika drama alizoshiriki kama vile EMPRESS KI, WARRIOR BAEK DONG SOO, K2. Amesema ya kwamba
kujiunga na jeshi nikiwa na miaka 30 itakuwa ni maisha tofauti, nina hamu ila nahofia

SEO IN GUK

Amezaliwa Oct 23 1987, ni actor na pia ni muimbaji,mara yangu ya kwanza nilimuona kwenye historical drama ya KING FACE ambayo aliigiza kama ni prince Gwanghae ambaye alikuwa ni mtoto wa mfalme Seonjo,Gwanghae ni mmoja ya crown prince waliorithi ufalme kwa shida sana naamini kama umeangalia hii drama ,pamoja na JING BIROK: THE MEMORY OF IMJIN WAR, ADMIRAL YI SOO SHIN na nyenginezo utakubaliana na mimi kwa sababu kwanza alipewa cheo cha crown prince wakati wa vita kubwa sana dhidi ya japan ( imjin war vilivyodumu kwa miaka 7 ) Seo In Guk amesema ya kwamba

Nategemea kujiunga na jeshi pale ambapo nitapokea barua,nategemea kukutana na watu wapya na maisha mapya na anategemea atakua bado Na mwonekano mzuri atakapo maliza kutumikia military activities”

JOO WON

Amezaliwa Sep 20 1987, kazi yake ya mwisho ni historical inayojulikana kama ni MY SASSY GIRL, alifaulu mtihani wa kutumikia Seol Police Metropolitan Agency ila ameamua kujiunga na jeshi ambapo kwa sasa anasubiri tarehe ya kujiandikisha jeshini.miongoni mwa drama alizoigiza ni pamoja na BRIDAL MASK, YONG PAL,GOOD DOCTOR, LEVEL 7.

LEE MIN HO


Amezaliwa jun 22 1987, ni actor na pia ni muimbaji, project yake ya mwisho inasemekana kuwa ni LEGEND OF THE BLUE SEA, Minoz ambaye mwaka uliopita pia alicheza movie ya THE BOUNTY HUNTERS alifaulu katika physical exam yake,na ameamua kutumikia katika huduma za kijamii kuliko kujiunga na jeshi.

JANG GEUN SUK

Amezaliwa aug4 1987 ni actor na pia ni muimbaji, mwenyewe anajiita Asia’s prince, mpaka sasa hajathibitisha kama atakwenda kutumikia shughuli za kijeshi ila amesema

“wala sijashitushwa na kujiunga na military activities kwani ni jukumu la kila mkorea mwanamme

Miongoni mwa drama alizoigiza ni pamoja na LOVE RAIN ambayo nyimbo yake ya love rain ilitimika kama ni ost, HONG GIL DONG, JACKPOT (daebak), YOU ARE BEAUTIFUL.

KIM SOO HYUN


Amezaliwa feb16 1988, ni actor ambaye ameigiza drama kama THE PRODUCER, MY LOVE FROM ANOTHER STAR, THE MOON THAT EMBRACE THE SUN, GIANT (young seongmo), ila mpaka sasa hajaweka tarehe ambayo atajiandikisha kutumikia jeshi, amesema

atatumikia military activities baada ya kumalizia project ya movie yake mpya ya REAL premier

YOO AH IN


Amezaliwa oct6 1986 ni miongoni mwa waigizaji wanaofanya vizuri nchini korea,ameshiriki drama kama vile JANG OK JUNG, FASHION KING, SIX FLYNG DRAGON, anategemea kutumikia na huduma za kijamii kuliko jeshi kwa sababu aliumia bega lake la kushoto.


Korean celebrities ambao wanatarajia kurudi uraiani baada ya kutumikia jeshi

KIM HYUN JOONG


ni actor na pia ni muimbaji ambaye alijiunga na jeshi tokea May12 2015 ambapo alikuwa ni border patrol na anatarajiwa kurudi mwezi huu wa February,ila kurudi kwake kunaweza kufufua upya kwenye vyombo vya habari lile sakata pamoja na aliyekuwa mpenzi wake ambalo bado lipo kwenye vyombo vya sheria.miongoni mwa drama alizoigiza ni pamoja na BOYS OVER FLOWER, PLAYFULL KISS.

PARK YOO CHUN


Ni actor na pia ni muimbaji na anatarajiwa kurudi August 2017 ambapo alikuwa akifanya kazi za kijamii katika maeneo ya Gangnam,mwaka uliopita alishutumiwa kwa kosa la sexual assault. miongoni mwa drama alizoigiza ni pamoja na 3 DAYS,I MISS YOU, THE GIRL WHO SEES SMELL.

CHOI SI WON

Ni actor na pia ni muimbaji ambaye ni member wa band inayoitwa Super Junior ambaye imekusanya vijana wenye vipaji vya kuimba kama vile Super Junior Kyu Hyun, Super Junior Yesung anatarajiwa kurudi mwezi August ambapo alikuwa akitumikia jeshi la police,miongoni mwa drama alizoigiza ni pamoja na ATHENA, POSEIDON, SHE IS PRETTY.
Licha ya kuwa anatokea katika familia ya kitajiri Choi siwon na member wenziwe wa super junior ni miongoni mwa bendi zinazotengeneza pesa nyingi sana kupitia kazi zao za muziki.

LEE SEUNG GI


Miongoni mwa best actor nchini korea,

Miongoni mwa best ballad singer, kpop singer niliopata kuwashuhudia katika maisha yangu

Miongoni mwa best singer niliopata kuwashuhudia linapokuja suala la kuimba live

Je wajua lee seung gi ni mwanafunzi wa mwanamama LEE SUN HEE gwiji wa muziki nchini korea.

Alijiunga na jeshi February mwaka 2016 na anatarajiwa kurudi October 2017.

Miongoni mwa drama alizoigiza ni pamoja GU FAMILY BOOK.MY GIRLFRIEND IS GUMIHO, SHINING INHERITANCE, YOU ARE ALL SURROUNDED.

NB:
Laiti kama sheria hii ingelikuwepo Tanzania basi ningelijirudisha umri kila siku,
hahahahahaaaaaa kishindo cha JKT na JKU sikiwezi na utawala wenyewe ndio huu mwaka wa pili mshahara haujapanda, mara unaamka asubuhi kambini hata mkate hamuna.na pembeni yako unamkuta celebrity DIAMOND PLATNUMZ amekata kipara munabaki kutazamana tu.

nongdam - ee - ehyo = (natania tu) = im just kidding
Dangyunhee jangnanigi = kweli natania = Of course I’m just kidding.
 
Aigooo aigoooo JF nasi tuna kijiwe chetu cha kikorea.
Hahahah wakorea wa JF tukiongozwa na gwiji Damushinmuhyool

Asante sana mkuu kwa uchambuzi huu. Ama hakika huwa naumia sana nikisikia waigizaji niwapendao wanaenda kulitumikia jeshi.
Mwanzoni nilidhani ni wanaenda kwa hiyari kumbe ni sheria,safi sana.

Nitammiss sana Lee Min Ho na Kim Soo Hyun.

Vipi mkuu Bidam nasikia baada ya kulitumikia jeshi aliachana na kazi ya uigizaji na kuwa mjeshi kabisa,ni kweli?
 
kumbe si wa nchi hii na unaonekana unazo nyingi sana
[emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji23] Napenda sana miziki ya kikorea,ipo emotional sana.
Sasa kwa mtu emotional kama mimi you can imagine vile nawakubali.

Sasa usikute ktk series kuna scene ya majonzi halafu na OST ikawa ya majonzi...nitalia sana.
I love Koreans kwakweli.
 
kwanza nakushukuru ila nahisi umenipa heshima kubwa sana ila sina budi kupokea zawadi yako,
ila nimejaribu kuangalia katika soompi fans thread ya kim nam gil nimeona bado anafanya kazi yake ya uigizaji ila tokea arudi kutumikia jeshi 2013 ameigiza drama moja tu inayoitwa DONT LOOK BACK:THE LEGEND OF ORPHEUS (Shark) pamoja na mwanadada SON YE- JIN ambaye naweza kusema ndiye mkali wa comedy kwa wanawake kama umeangalia personal taste drama na movie ya ART OF SEDUCTION aliyocheza pamoja na Song Il Kook utakubaliana na mimi.
pia tokea arudi jeshini amecheza movies nyingi sana. unajua ile drama ya BAD GUY ilipaswa kuwa na episode 20 ila episode 3 zilipunguzwa kwa ajili ya kumfanya kim nam gil awahi kwenda kutumikia jeshi mwaka 2010


 
ni yupi muimbaji wako bora nchini korea
 
Mianhada (pole),watu sasa hivi wanachanga pesa kwa ajili ya kutumia baadae ila mimi nataka nizihifadhi ili nipate kwenda kuhudhuria harusi ya Lee Min Ho na Bae Suzy siku itakayotangazwa tu nitakwenda japo kwa Bombardier haidhuru igome njiani
 
Damushinmuhyool heshima kwako.
Huu uchambuzi umesimama yani umenianzishia wikiendi vizuri sana kunywa maji hapo kwa bill yangu.
Naona mahandy wengi mwaka huu ni wao, sasa Lee min hoo ana udhuru gani mpaka anatumikia jeshi kwa shughuli za kijamii? Namuona mayai yeye na mwenzie Jang keun suk...lol
Tutawamiss lakini soon tutawaona kama ilivyokuwa kwa Song Joong ki. Nimekuona unavyomkubali Lee Seung gi nikushukuru sana kwa kunitambulisha kipaji chake cha uimbaji...ongeza maji mengine Nifah atakuja na Kimbap utafunie.
 
Mianhada (pole),watu sasa hivi wanachanga pesa kwa ajili ya kutumia baadae ila mimi nataka nizihifadhi ili nipate kwenda kuhudhuria harusi ya Lee Min Ho na Bae Suzy siku itakayotangazwa tu nitakwenda japo kwa Bombardier haidhuru igome njiani
Hahahaha hiyo siku ikifika najitolea kukununulia Hanbok.
 
Bad guy sikupenda mwisho wake kabisaaa, hasa hukumu ya yule mama na Kim Nam gil alivyoishia. Ilitaka kuniudhi kama Iris 1
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…