Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

List ya kibabe hii. Nakubaliana na wewe kwenye kigongo cha Jumong, kisiki cha Chuno, Emperor of the sea na Dong-Yi hizi ni moja ya kazi bora za kikorea kwa upande wa hitorical.

Vipi umeshacheki Emprrss Ki? Land of the Wind?. Six flying Dragons? Haziingii kwenye list yako kama honourable mentions?

tumblr_inline_o4fmwuYoE81qefvus_640.jpg

Yi Bag Won( Taejong)
Six_Flying_Dragons_(육룡이_나르샤).jpg

(SIX FLYING DRAGON POSTERS)

Kaka zote hapo tayari,
Hapo kwenye Six flying dragon inaingia kwenye 20 bora yangu, Mwaka 2015 Channel ya SBS walijitahidi sana kwenye hii kazi nadhani humu ndani kuna Martial arts za hali ya juu mno. Ila kabla yake ilikuwepo kazi inaitwa Jeong Do Jeon hii iliandaliwa na KBS, drama hii ilikuwa ikielezea zaidi maisha ya Sambong( Jeong do Jeon) na jinsi ambavyo aliiangusha Goryeo iliyokuwa imeoza na Kuianzisha Joseon. Ukiniuliza kati ya Six flying dragon ambayo ilifokasi na maisha ya Taejong( Lee Bang won) na hii Jeong do Jeon ya Sambong, nakwenda na Jeong do Jeon. Ingawa kazi zote ni nzuri mno.

MV5BZTlkZjliNTAtMTI2Yy00OGRkLTk2MWItZDdkMjY3MmRiMTc0XkEyXkFqcGdeQXVyNjI4NDY5ODM@._V1_.jpg


Hapo ilikuwa battle of Legend Generals; General Choi Young( wa kulia) ambaye anahesabika kama Shujaa wa Goryeo, akipambana na Kijana wake General Yi Songgye( Taejo of Joseon)ambaye ni shujaa wa Joseon na msaliti wa Goryeo.
Hawa wote mpaka Leo wanahesabika Mashujaa wa Korea.
Lee min Ho aliwahi kucheza uhusika wa General Choi kwenye Drama ya Faith.
ABx6Xf.jpg


Sambong kwenye Jeong do Jeon drama. 2014 KBS1
 
Habari, Leo nimekuja na list ya historical drama 10 ambazo zilinivutia zaidi kwa kuwa na story nzuri.

1. Dong Yi: Jewel in the Crown
Hii tamthilia haijawahi kunichosha kuanzia sehemu ya kwanza mpaka mwisho kwa jinsi ambavyo uhusika unavovaliwa na waigizaji lakini pia mpangilio wa visa na mikasa ndani ya tamthilia hii. Credit kwa mzee Lee Byung-Hoon, ambaye ndiye muongozaji wa kazi hii akisaidiwa na Kim Sang-Hyub · Kim Yi-Young ambaye ndiye mwandishi. Kazi ilirushwa na MBC
mwaka: 2010

2. Dae Jang Geum: Jewel in the Palace
Hii tamthilia ilitwaa tuzo nyingi sana, pia inatajwa kuwa ndio tamthilia iliyotangaza utamaduni wa korea duniani kote, pia ilichochea ongezeko la utalii, sababu ilitangaza vivutio vya utalii. Hii tamthilia kwangu mimi naipa vyeo vyote. Mzee wetu Lee Byung Hoon(mtayarishaji) akiwa na msaidizi wake Kim young( mwandishi) ndio walikuletea hii kazi kupitia MBC
Mwaka: 2003

3. Prince Of Legend: Jumong
Kazi hii niliipenda tu, miaja ya 2008 nilipokuwa naifuatilia kupitia ITV Tanzania ingawa. Ratiba yake ilikuwa J.tatu mpaka J.tano kuanzia saa 5 usiku enzi hizo ikifika saa 4 au 3 na nusu tayari mtu ushaambiwa kasome au kalale kesho uwahi shule. So Jumamosi ndio muda mzuri wa kuirudia.
Umewakumbuka wale wahuni 3( Mari, Hypobo na Oi) ? Pamoja na mkubwa wao Jumong? Ebuana ile combination ilikuwa si mchezo. Seossoneo na watu wa kwao huko Keru na Pyiru ilikuwa inavutia zaidi. Ingawa ilikuja kupungua kidogo baada ya mwamba kuwa mfalme maana huyu Gook il son ndiye alikuwa anainogesha zaidi, maana ukishakuwa kiongozi wa taifa huishi tena kisela bali kwa utaratibu maalum. Hii kazi nimeirudia maranyingi mno bilA kuichoka.
Imetayarishwa na Lee Joo Hwan akisaidiwa na Kim Keum Hong.
Hii kazi ilitwaa tuzo nyingi mno, na haki zake za kurushwa na vituo vingine iliuzwa sehemu nyingi duniani, na ilipendwa zaidi Nchini Iran(90% Audience) walivutiwa zaidi na kazi hii kuliko South Korea (40% Audience) ndio walikongwa nyoyo nayo.
Kupitia umaarufu wa kazi hii ulipelekea sintofahamu kati ya Serikali ya China na S.korea kuhusu historia ya Gogryeo. Si unajua wachina walikuwa wanadai ni Gogryeo ilikuwa yao?. Drama hii ilikuwa na Episode 60 lakini kulingana na umaarufu wake MBC walizirefusha mpaka kuwa 81. Ilirushwa na MBC
Mwaka: 2006

4. The Great Queen Seon Deok
Hii ilikuwa kazi ya pili kunipeleka Korea. Nimeirudia mara nyingi mno. Washiriki wa humu ndani walifanya kazi njema. Hii drama inakupa kila kitu, story nzuri, Comedy, action, naweza kusema most complete historical drama. Humu ndani utajifunza mengi ikiwamo fitina katika siasa na mengine mengi. Na kumbuka Daek man kule jangwani, hata aliporudi Seorobelo alimuweza sana mwana mama Mishil aliyekuwa ameshindikana. Unamkumbuka Jukban na Goddo wake? Mtaalam Gukson Munno na Bidam wake. Hii kazi ilifanyavema sana sana. Mtayarishaji ni Park Hong Kyun akisaidiwa na Kim Keum Hong( alihusika kuandaa pia Prince of Legend) ilirushwa na MBC
Mwaka 2009
Kumbuka Queen Seon Deok, Jumong, Dong Yi zote zilichezewa kwenye Setting moja.

5. Emperor Wang Gun
Kazi hii ya kibabe ilinifurahisha kwa kuwa na historia nzuri sana, naweza kusema kazi hii ilifanya niyajue majimbo mengi ya Goryeo hutojuta kuitazama kila kitu kilikuwa very correct. Humu ndani kuna Acumen Military Advisors nadhani nikitoa Gwanggaeto, The Great Conqueror kwakuwa na watu wenye akili za vita hii Emperor Wang Gun ndio inafuata. Mzanzibari unakumbuka Sutra hata moja ya kibudhism?! Aliokufundisha mzee wako Gung ye?. Kifupi hii kazi ni nzuri mno na ni kazi dume niwana maana ilainafaa uwe mvumilivu ziko Episode 200 hapa. KBS1 ndio waliirusha. Iliandaliwa na Kim Jong Sun, mwandishi alikuwa Lee Hwan Kyung.
Mwaka : 2000

6. Haeshin, Sea God, Emperor of the Sea

Achana na ukatili wa Lee do hyeong, penzi la Lady Jung hwa dhiya Jam bogo na Yeom Jang. Kipindi kile naitazama bado nilishangazwa sana kwani hawa jamaa wanamng'ang'ania huyu mdada?. Miaka michache baadae ndio nilikujakuwaelewa. Nakumbuka( kama sikosei) ilikuwa Bandari ya Yangzhou mida ya jioni kabisa, Yeom Jang alimfuata Lady Jung hwa na kumwambia najua moyoni mwako yupo Jang bogo lakini mie naomba hata huo mwili wako. Hapa nilijifunza kuwa kumbe kweye maisha haya mtu aliyenamoyo wa mtu ndiye wa thamani zaidi. Lee do hyeong alikuwa akimuona huyo mwnamke kama chanzo cha udhaifu wa Yeom Jang. Kama sikosei hawa wote( Jang Bogo na Yeom Jang) hawakuweza kuishi nae mwanadada huyo. Adventure za baharini zilinivutia zaidi pia, Jang Bogo kuwa Gladiator baada ya kuuzwa utumwani. Kifupi kazii hii tamu na sijawahi kuitazama Episode ya mwisho na sina mpango huo. Mbali na yote hii ndo drama ambayo ulikuwa unamu- admire adui. Story ya drama hii inamuunganiko flani na Emperor wang gun drama, maana Gung ye ambaye ni ambaye alikuwa ni Prince wa Shilla, mama yake alikuwa binti wa Jang Bogo. Kazi hii ilitayarishwa na Il-soo Kang, akisaidiwa na Kang Byung Taek. Ilirushwa kupitia KBS2
M
waka 2004

7. Sang Do, Joseon Merchant
Utajifunza mambo mengi kuhusu biashara, kuna mambo umejifunza shuleni kuhusu Ujasiliamali lakini huku ndani utaona watu wakifanya kwa vitendo, ni kazi nzuri kweli kweli. Ilitayarishwa na mzee wetu Lee Byung Hoon, ilirushwa MBC
Mwaka 2001

8. Hur Jun, The Legendary Doctor
Inastory nzuri sana kama Jewel in the Palace, ilinivutia kwa kila kitu. Mtayarishaji ni yule yule Gwiji Lee Byung Hoon, kupitia MBC
Mwaka 1999

9. Chuno, The Slave hunter

Mara ya kwanza nilimuona Jang Hyuk ndani ya hii kazi, hutojuta kuitazama. Iliandaliwa na Kwang Jung Hwan, kupitia KBS
mwaka 2010

10. God of War, Military Official, Soldier
Hii ni kazi ya kibabe yenye story nzuri sana, utaifurahia sana. Alocheza uhusika mkuu alishapoteza maisha. Drama inamuelezea Mtumwa ambaye alipata Bahati na kuwa kiongozi Mkuu wa Jeshi na kuwa conrol serikalini( Overlord). Scene ya malavidavi kati ya mtoto wa Choe ilikuwa nzuri pia. Hii drama ni kama mwendelezo wa Dude la Kiumeni The Age of Warriors. Ilitayarishwa na Lee Hwan Kyun, ikarushwa na MBC
Mwaka 2012

Nakupa hii ya chini kama bonus

11. Shin Don

Hii drama pia inastory nzuri sana, inafanana baadhi ya Visa na Empress Ki, hii drama ni Prio story ya Jeong Do Jeon, Six flying Dragon na The Great Seer.
Drama hii ya Shin Don ilirushwa na MBC
mwaka 2004.


UNAWEZA KUTAJA ZAKO 10 ZENYE STORY NZURI ZAIDIView attachment 2609356
Posta ya drama iitwayo SangDo

[emoji91][emoji91]

Adamas ina season 2!???
 
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]unakosa uhondo
Kati ya hizo nimeangalia prison playbook na Weightlifting Fairy tu. Ni vile hazijafocus sana kwenye hiyo michezo na mimi sikufocus kabisa huko [emoji1787][emoji1787] hapo yenye unafuu ni ipi
 
Zote zimefocus kwenye michezo,kuna michezo mingine kuiona mpaka kwenye olimpic ila wakorea wanaicheza ndo nimeionea kwao pia. Zipotezee tu karibu kwenye realities 😂😂😂
Kati ya hizo nimeangalia prison playbook na Weightlifting Fairy tu. Ni vile hazijafocus sana kwenye hiyo michezo na mimi sikufocus kabisa huko [emoji1787][emoji1787] hapo yenye unafuu ni ipi
 
Zote zimefocus kwenye michezo,kuna michezo mingine kuiona mpaka kwenye olimpic ila wakorea wanaicheza ndo nimeionea kwao pia. Zipotezee tu karibu kwenye realities [emoji23][emoji23][emoji23]
Kwenye realities nako hamnipati [emoji1787][emoji1787][emoji1787] labda drama zinichoshe
 
Zote zimefocus kwenye michezo,kuna michezo mingine kuiona mpaka kwenye olimpic ila wakorea wanaicheza ndo nimeionea kwao pia. Zipotezee tu karibu kwenye realities [emoji23][emoji23][emoji23]

Tuendelee kumuhamasisha na realities jaman ataelewa tu


Nimeshusha jinny’s kwa nkiri, ina rangi nzuri japo dakika moja tu nimetizama

Nimependa hata intro ya masikhara, najikaza nimalize kuishusha ndo niitazame nshahisi itanikosesha usingizi[emoji23]
 
Habari, Leo nimekuja na list ya historical drama 10 ambazo zilinivutia zaidi kwa kuwa na story nzuri.

1. Dong Yi: Jewel in the Crown
Hii tamthilia haijawahi kunichosha kuanzia sehemu ya kwanza mpaka mwisho kwa jinsi ambavyo uhusika unavovaliwa na waigizaji lakini pia mpangilio wa visa na mikasa ndani ya tamthilia hii. Credit kwa mzee Lee Byung-Hoon, ambaye ndiye muongozaji wa kazi hii akisaidiwa na Kim Sang-Hyub · Kim Yi-Young ambaye ndiye mwandishi. Kazi ilirushwa na MBC
mwaka: 2010

2. Dae Jang Geum: Jewel in the Palace
Hii tamthilia ilitwaa tuzo nyingi sana, pia inatajwa kuwa ndio tamthilia iliyotangaza utamaduni wa korea duniani kote, pia ilichochea ongezeko la utalii, sababu ilitangaza vivutio vya utalii. Hii tamthilia kwangu mimi naipa vyeo vyote. Mzee wetu Lee Byung Hoon(mtayarishaji) akiwa na msaidizi wake Kim young( mwandishi) ndio walikuletea hii kazi kupitia MBC
Mwaka: 2003

3. Prince Of Legend: Jumong
Kazi hii niliipenda tu, miaja ya 2008 nilipokuwa naifuatilia kupitia ITV Tanzania ingawa. Ratiba yake ilikuwa J.tatu mpaka J.tano kuanzia saa 5 usiku enzi hizo ikifika saa 4 au 3 na nusu tayari mtu ushaambiwa kasome au kalale kesho uwahi shule. So Jumamosi ndio muda mzuri wa kuirudia.
Umewakumbuka wale wahuni 3( Mari, Hypobo na Oi) ? Pamoja na mkubwa wao Jumong? Ebuana ile combination ilikuwa si mchezo. Seossoneo na watu wa kwao huko Keru na Pyiru ilikuwa inavutia zaidi. Ingawa ilikuja kupungua kidogo baada ya mwamba kuwa mfalme maana huyu Gook il son ndiye alikuwa anainogesha zaidi, maana ukishakuwa kiongozi wa taifa huishi tena kisela bali kwa utaratibu maalum. Hii kazi nimeirudia maranyingi mno bilA kuichoka.
Imetayarishwa na Lee Joo Hwan akisaidiwa na Kim Keum Hong.
Hii kazi ilitwaa tuzo nyingi mno, na haki zake za kurushwa na vituo vingine iliuzwa sehemu nyingi duniani, na ilipendwa zaidi Nchini Iran(90% Audience) walivutiwa zaidi na kazi hii kuliko South Korea (40% Audience) ndio walikongwa nyoyo nayo.
Kupitia umaarufu wa kazi hii ulipelekea sintofahamu kati ya Serikali ya China na S.korea kuhusu historia ya Gogryeo. Si unajua wachina walikuwa wanadai ni Gogryeo ilikuwa yao?. Drama hii ilikuwa na Episode 60 lakini kulingana na umaarufu wake MBC walizirefusha mpaka kuwa 81. Ilirushwa na MBC
Mwaka: 2006

4. The Great Queen Seon Deok
Hii ilikuwa kazi ya pili kunipeleka Korea. Nimeirudia mara nyingi mno. Washiriki wa humu ndani walifanya kazi njema. Hii drama inakupa kila kitu, story nzuri, Comedy, action, naweza kusema most complete historical drama. Humu ndani utajifunza mengi ikiwamo fitina katika siasa na mengine mengi. Na kumbuka Daek man kule jangwani, hata aliporudi Seorobelo alimuweza sana mwana mama Mishil aliyekuwa ameshindikana. Unamkumbuka Jukban na Goddo wake? Mtaalam Gukson Munno na Bidam wake. Hii kazi ilifanyavema sana sana. Mtayarishaji ni Park Hong Kyun akisaidiwa na Kim Keum Hong( alihusika kuandaa pia Prince of Legend) ilirushwa na MBC
Mwaka 2009
Kumbuka Queen Seon Deok, Jumong, Dong Yi zote zilichezewa kwenye Setting moja.

5. Emperor Wang Gun
Kazi hii ya kibabe ilinifurahisha kwa kuwa na historia nzuri sana, naweza kusema kazi hii ilifanya niyajue majimbo mengi ya Goryeo hutojuta kuitazama kila kitu kilikuwa very correct. Humu ndani kuna Acumen Military Advisors nadhani nikitoa Gwanggaeto, The Great Conqueror kwakuwa na watu wenye akili za vita hii Emperor Wang Gun ndio inafuata. Mzanzibari unakumbuka Sutra hata moja ya kibudhism?! Aliokufundisha mzee wako Gung ye?. Kifupi hii kazi ni nzuri mno na ni kazi dume niwana maana ilainafaa uwe mvumilivu ziko Episode 200 hapa. KBS1 ndio waliirusha. Iliandaliwa na Kim Jong Sun, mwandishi alikuwa Lee Hwan Kyung.
Mwaka : 2000

6. Haeshin, Sea God, Emperor of the Sea

Achana na ukatili wa Lee do hyeong, penzi la Lady Jung hwa dhiya Jam bogo na Yeom Jang. Kipindi kile naitazama bado nilishangazwa sana kwani hawa jamaa wanamng'ang'ania huyu mdada?. Miaka michache baadae ndio nilikujakuwaelewa. Nakumbuka( kama sikosei) ilikuwa Bandari ya Yangzhou mida ya jioni kabisa, Yeom Jang alimfuata Lady Jung hwa na kumwambia najua moyoni mwako yupo Jang bogo lakini mie naomba hata huo mwili wako. Hapa nilijifunza kuwa kumbe kweye maisha haya mtu aliyenamoyo wa mtu ndiye wa thamani zaidi. Lee do hyeong alikuwa akimuona huyo mwnamke kama chanzo cha udhaifu wa Yeom Jang. Kama sikosei hawa wote( Jang Bogo na Yeom Jang) hawakuweza kuishi nae mwanadada huyo. Adventure za baharini zilinivutia zaidi pia, Jang Bogo kuwa Gladiator baada ya kuuzwa utumwani. Kifupi kazii hii tamu na sijawahi kuitazama Episode ya mwisho na sina mpango huo. Mbali na yote hii ndo drama ambayo ulikuwa unamu- admire adui. Story ya drama hii inamuunganiko flani na Emperor wang gun drama, maana Gung ye ambaye ni ambaye alikuwa ni Prince wa Shilla, mama yake alikuwa binti wa Jang Bogo. Kazi hii ilitayarishwa na Il-soo Kang, akisaidiwa na Kang Byung Taek. Ilirushwa kupitia KBS2
M
waka 2004

7. Sang Do, Joseon Merchant
Utajifunza mambo mengi kuhusu biashara, kuna mambo umejifunza shuleni kuhusu Ujasiliamali lakini huku ndani utaona watu wakifanya kwa vitendo, ni kazi nzuri kweli kweli. Ilitayarishwa na mzee wetu Lee Byung Hoon, ilirushwa MBC
Mwaka 2001

8. Hur Jun, The Legendary Doctor
Inastory nzuri sana kama Jewel in the Palace, ilinivutia kwa kila kitu. Mtayarishaji ni yule yule Gwiji Lee Byung Hoon, kupitia MBC
Mwaka 1999

9. Chuno, The Slave hunter

Mara ya kwanza nilimuona Jang Hyuk ndani ya hii kazi, hutojuta kuitazama. Iliandaliwa na Kwang Jung Hwan, kupitia KBS
mwaka 2010

10. God of War, Military Official, Soldier
Hii ni kazi ya kibabe yenye story nzuri sana, utaifurahia sana. Alocheza uhusika mkuu alishapoteza maisha. Drama inamuelezea Mtumwa ambaye alipata Bahati na kuwa kiongozi Mkuu wa Jeshi na kuwa conrol serikalini( Overlord). Scene ya malavidavi kati ya mtoto wa Choe ilikuwa nzuri pia. Hii drama ni kama mwendelezo wa Dude la Kiumeni The Age of Warriors. Ilitayarishwa na Lee Hwan Kyun, ikarushwa na MBC
Mwaka 2012

Nakupa hii ya chini kama bonus

11. Shin Don

Hii drama pia inastory nzuri sana, inafanana baadhi ya Visa na Empress Ki, hii drama ni Prio story ya Jeong Do Jeon, Six flying Dragon na The Great Seer.
Drama hii ya Shin Don ilirushwa na MBC
mwaka 2004.


UNAWEZA KUTAJA ZAKO 10 ZENYE STORY NZURI ZAIDIView attachment 2609356
Posta ya drama iitwayo SangDo
Ukiachana na hiyo ya bonus, hizo zote ulizotaja hapo juu nimebahatika kuziangalia, zote ni nzuri na sikujutua bando lango livha ya kuwa zina episode 50-60. Nyingine iliyostahili kukaa hapo ni HWAJUNG.

Ngoja niifuatilie hiyo bonus drama.
 
Soon atakuja tu😂😂😂

Nilijaribu kuangalia episode moja kutest kama nzuri nikajikuta mzima mzima naangalia zote na kusubiria zinazofatia,uzuri ijumaa tunamaliza ila nimenasa kwenye ongoing drama the secret romance guesthouse nzuri hii
Tuendelee kumuhamasisha na realities jaman ataelewa tu


Nimeshusha jinny’s kwa nkiri, ina rangi nzuri japo dakika moja tu nimetizama

Nimependa hata intro ya masikhara, najikaza nimalize kuishusha ndo niitazame nshahisi itanikosesha usingizi[emoji23]
 
Basi mtizame hata sugar dady wang nam goo min kwenye stove league akiwa na park eun bin (attorney woo).
Nilihisi unamzungumzia Namkoong min nikasema ngoja nijiridhishe gugo. Ila wewe kumbe katoto sana yaani huyu kwako ni sugar daddy [emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Nitajaribu nikipata muda ambao hauna kazi [emoji16]
 
Soon atakuja tu[emoji23][emoji23][emoji23]

Nilijaribu kuangalia episode moja kutest kama nzuri nikajikuta mzima mzima naangalia zote na kusubiria zinazofatia,uzuri ijumaa tunamaliza ila nimenasa kwenye ongoing drama the secret romance guesthouse nzuri hii
Hiyo Jinny's kitchen ina episode ngapi? Naweza kuangalia kwa sababu ya Tae
 
Nimeangalia K-drama nyingi za historical zikihusisha
himaya za (Goguryeo,Silla,Baekje,Goryeo,Joseon-hapa ndo za kumwaga-early Joseon, middle Joseon and late Joseon during Japan invansion, pia za Joseon-during independence fighting).

images.png


Kitu ambacho kinashangaza hawa wakorea jinsi wanavyo-depict historia yao kwenye maigizo zinaonesha himaya zao zilikua na nguvu sana na wababe sana. Drama nyingi za kihistoria toka Korea zikiachiwa mara nyingi wachina wanalalama wakisema historical kdramas baadhi zinakengeuka na ku-edit baadhi ya matukio halisi ya kihistoria tofauti na jinsi yalivyotokea hapo zamani.

Miongoni mwa himaya za mashariki ya kati na mashariki ya mbali basi;himaya zilizokuwepo ndani ya Korea wakati huo ( Goguryeo, Silla, Baekje, Balhae,Goryeo na Joseon) kwenye historia inaonekana zilikua himaya dhaifu kwa sababu :

1. Mgawanyiko ulikua mkubwa katika utawala. Wakorea ni watu wanaopenda kuwa katika makundi makundi ya ukabila, koo na kikanda hali iliyopelekea kukosekana kwa umoja miongoni mwao hivyo kuwa dhaifu na kupelekea kupigwa kirahisi na maadui zao.

✓Mfano China alitumia mbinu ya kuungana na Silla akampiga Goguryeo
na Baekje na kwa mfuatano na kuzi-conquer hapo ikaundwa Goryeo (Unification of the three kingdoms).

✓Joseon kulikua na mpasuko mkubwa ilikua kila baada ya muda wanapindua wafalme wao na kuweka wengine madarakani mvutano ukihusisha factions zenye mrengo tofauti kama (Sarim,Seo-in,Dong-in,So-ron,No-ron).

tsksgorgeous-politicale027720pko_cn07737400-45-41.jpg


✓Hali hii imeendelea hadi karne ya 20 na 21 baada ya uhuru nchi imejigawa kuwa Korea ya kaskazini na kusini. Tangu zamani wenyewe ni wazee kuungana, kusalitiana, kupigana kisha kutengana.

2. Himaya za zamani za Korea zilipigwa na zikatawaliwa na karibia kila himaya mbabe wa enzi hizo.

✓Kwanza walisumbuliwa na himaya za China ya Wakati huo zikiwemo (Han, Ming,Liao/Khitan,Yuan,Tang na Qing,Jin).

Hizi himaya zilipigana vita kwa vipindi tofauti tofauti na himaya za Korea na baadhi zikafanikiwa kuwatawala wakorea na kupelekea wafalme wa korea kuongoza nchi kama vibaraka/viongozi kivuli hivyo kukosa maamuzi ya mwisho kama watawala.

✓Katika nyakati hizi watawaliwa walitumia lugha ya kichina katika kuandika, wakaletewa dini ya buddhism, na mfumo wa kuongoza falme zao ulifanania sana na mfumo uliokuwepo China.

✓Hapa drama nyingi zimeonesha hili zikiwemo Emperor of the sea na Chuno/Slave hunters.

images (23).jpeg


✓Korea ilitawaliwa na Japan 1910-1945. Hili lilitokea juzi tu hapo dunia ikiwa imepiga hatua kubwa ya maendeleo katika nyanja za teknolojia na viwanda.
✓Japan alikua ameendelea sana kipindi hicho. Kulinganisha Japan na korea ilikua kama mbingu na ardhi.
✓Kilichowaokoa kutoka katika huu utawala ni pale Japan aliposhindwa katika vita kuu ya pili dunia hivyo Korea wakapata uhuru wao 1945.

Drama zilizoonesha kwa uzuri maisha halisi yalivyokua Joseon chini ya utawala dhalimu wa Wajapan ni pamoja na The Land (Toji), Mr Sunshine na Pachinko.
zikionesha (mateso, manyanyaso, umaskini,mauaji ya wazalendo, mapambano ya kudai uhuru, wanawake wakisafirishwa kama watumwa)

images (21).jpeg
images (13).jpeg
images (1).jpeg


✓Wakorea pia walipigwa na Wamongolia (himaya ya Yuan) . Mongol (Yuan) chini ya mtaalamu Genghis Khan mnamo karne ya 13-14 ilikua himaya yenye nguvu sana Asia na ilipenda vita. Yaani huyu mpuuzi Genghis Khan alikua mbabe sana kila akiamka asubuhi yeye anawaza kutanua tu mipaka ya falme yake na alifanikiwa kuitanua Mongol kwa kiasi kikubwa wakati wa utawala wake kwa kuzipiga himaya nyingi na kuzitawala.

IMG_20230505_022652.jpg


✓Mongolia wakati huo ilikua ya moto iliitawala China, ikaitawala Korea, ilipigana vita na kuzi-conquer himaya kama Ottoman,India,Serbia,Poland, Bulgaria, Croatia, Hungary na Japan na ilishinda katika vita walizopigana na kutanua mipaka yake kuifanya Mongolia kuwa himaya yenye nguvu sana mshariki ya kati na mashariki ya mbali kwa wakati huo.

IMG_20230505_022541.jpg


✓Nikiwaangalia Wamongolia sasa hivi walivyo masikini nikalinganisha na ubabe waliokua nao zamani nashindwa kuelewa imekuaje wamepooza hivi!!!!

IMG_20230505_022225.jpg


✓Yuan dynasty (Mongol) chini ya mtoto wa 3 wa Genghis Khan aitwae Ögedei Khan iliingia vitani na himaya ya Goryeo na kujaribu kuitawala kwa vipindi tofauti katika karne ya 13 ikifanya uvamizi mara kwa mara takribani mara tisa (9) na baadae ilishinda vita na hivyo Goryeo ikatawaliwa na Mongolia (Yuan dynasty).

IMG_20230505_022259.jpg


✓Utawala na Vita ya Mongol (Yuan) dhidi ya Goryeo imeoneshwa kwenye drama ya Empress Ki.

IMG_20230505_014008.jpg


✓Himaya za Korea kwa vipindi tofauti zimeingia vitani dhidi ya Han,Qing, Tang, Ming,Japan, Mongol,Jurchens ,Khitans nk kwa vipindi tofauti tofauti.

✓Kitu kinachoshangaza kwenye Drama za wakorea tunazoangalia zinaonesha Korea lilikua dude kubwa ikiwa na watu-watu kweli wababe wa vita na wajuzi wa elimu ya siasa na sayansi ya ulimwengu waliopikwa kutokea Sungkyunkwan.

IMG_20230505_015225.jpg


✓Historical figures walioshiba wamepambwa wakiwemo miamba kama Queen Seondeok,Lady/Empress Ki,mwanasayansi Jang Yeong-sil, Daemusin Muhyul, Jumong, General Yi Seong-Gye (King Taejo), Warrior Yi Bang-Ji, Yi-San (King Jeongjo), King Gwanggaeto, King Geunchogo,Yi Do (Sejong the great), General Choi young, General Kim Yushin, General Gye-Baek, Kim Suro, Bidam,Great scholar Jeong Do-Jeon (Sambong). Jang Bogo, King Yeongjo, Shin Sa im dang nk

images (27).jpeg

images (25).jpeg


✓Drama zinaonesha himaya za korea zilikua zimeendelea kimapigano na hivyo kupelekea kushinda vita nyingi, Pia zinaonesha korea ilikua imestaaribika na ni jamii bora kimavazi na vyakula, pia inaonesha kielimu ilipiga hatua kiasi ya Sungkyunkwan kutoa scholars wengi waliochonga mfumo wa uongozi wa vizazi na vizazi katika Joseon na baadae Korea ya Sasa.

jeong-do-jeon-1b159f74-42e5-4fa7-b3e3-d52e9aae6ad-resize-750.jpeg


∆Je, hawa wataalamu hawatufungi kamba kweli? na kuikuza historia ya nchi yao tofauti na uhalisia ulivyo? Sababu historia inaonesha yeye(Korea) ndiye aliekua kibonde wa wote akisumbuliwa na majirani wa karibu na wa mbali.

images (26).jpeg

Hii imekaaje?
Gwanggaeto the Great
 
Nilihisi unamzungumzia Namkoong min nikasema ngoja nijiridhishe gugo. Ila wewe kumbe katoto sana yaani huyu kwako ni sugar daddy [emoji1787][emoji1787][emoji1787]. Nitajaribu nikipata muda ambao hauna kazi [emoji16]

Katoto wapi ni shangazi hapa[emoji1787]
Sema vile napenda hivo vi marioo vya korea inabid huyo awe sugardady tu
 
Back
Top Bottom