Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Kwa wapenzi wa Korean Dramas, hii ni thread yako!

Six Flying Dragon ~ Namkubal Sana Master SABONG
Sword Dance~ Yung Gae So Mun, na King Bojang
Dae Mury Army ~ Ya King Jumong

Ktka Korea Historical Drama Nlowah Kuangalia Hzo Ndyo Bora Kwangu!!
 
Mkuu kwa sie wananchi wazalendo wa taifa la GOGURYEO kutomuweka THE GREAT KING GWANGAETO umetufanyia uhaini mkubwa sana kiukweli.
Chonde Chonde bwana.
Ni wafalme wawili tu katika historia ya Korea waliopewa Posthumous tiltle ya Great King,
1. The Great King Gwangaeto.
2. The Great King Sejong.
"Today, King Gwanggaeto the Great is one of two rulers of Korea who were given the title 'Great' after their name (the other one being King Sejong the Great of Joseon, who created the Hangul)."

Usifanye hivyo mkuu bwana, mtu alipiga Mongolia,Japan, China,hadi Urusi alifika na akaiweka chini yake bwana huyu ni great, Tang na Silla kuungana kumpiga kwasababu mmoja mmoja hamna aliyeweza.

Shikamoo Gwangaeto!
Katika historia yote ya Korea huyo ndo mtu ambaye alikuwa anatisha, ni mfalme aliyeogopeka sana
 
Kwangu miye Lee san(Jeong Jo) ndiye mfalme wangu bora wa Joseon 2 anashika Sejong the Great 3 Yoeng Jo 4 SukJong 5TAE JO. INGAWA MIYE KWETU NI GUGNANGSOENG(GOGRYEO)
 
Imagine unaifuatilia Empress Ki at the same time unaifuatilia King Gwanggaetto the Great.nilikuwa nakerwa na yule mfalme bwege alikuwa anaendeshwa kibwege anajiliza hovyo hii tabia yake ilifanya nikajikumbushie King Gwanggaetto jinsi mfalme Dam doek(Gwanggaetto) alikuwa anaongoza kibabe.
 
Umewahi kusikia ile wasemayo Shika hapa wacha hapa, sasa imenikuta mara baada ya kuimaliza Yi san(Wind of the Palace) sasa nafuatilia Jewel in the Palace, Emperor of the Sea na Joseon Gunman. kwenye Joseon Gunman niko epi. ya 3 nimefurahishwa nayo pia kuna muhuni Anashabaha usipime muhuni huyu alikuwa Grand duke kwenye ile Kim Soo ro pia nilimuona kwenye Faith alikuwa adui vilevile. Emperor of the Sea nilikuwa mvivu kuitazama tangu siku nyingi na nilikuwa naichukulia poa ndo kwanza niko sehemu ya 2, Ila hao Ma-Pirate Wanamatusi!! wanabalaa hao jamani, halafu mbona kama Jumong ndiye Jambazi halafu Dae Jo young ndiye stelingi . Jewel in the Palace nipo epi.5 ngoja nikaone vizuri haka kadogo katakuwa na miujiza gani mpaka kaitwe Jewel. Ni tamthilia inayoonekana kuwa Kitovu cha tamthilia zingine kubwa maana hii kitu imesheheni mafundi niliowacheki kwenye baadhi ya tamthilia kama. Dong yi, Yi san , Legend of the Prince Jumong,Dae Jo Young, King Gwanggaetto the Great Conqueror .n.k kingine hii Jewel of the Palace, Dong yi na Yi san nahis zitakuwa zimetayarishwa na mtu mmoja kama sikosei.
 
Nahitaji soft copy ya series kali za kikorea n.k zaidi ya 100 (ziwe zimetafsiriwa kiswahili)
Kwa makubaliano ya kibiashara njoo PM tufanye biashara.
Nipo Dar

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Screenshot_2019-01-03-21-02-55.png
nani anakumbuka huu moto? Hii ni moja ya tamthilia niliyoitazama mara nyingi inaitwa Bridal Mask ila sijui kama ilikuwa true story ama vipi. Ila humo ndani kuna balaa asikwambie mtu. Ina episode 28 tu.
Acheche
 
View attachment 1005329nani anakumbuka huu moto? Hii ni moja ya tamthilia niliyoitazama mara nyingi inaitwa Bridal Mask ila sijui kama ilikuwa true story ama vipi. Ila humo ndani kuna balaa asikwambie mtu. Ina episode 28 tu.
Acheche
Nzuri kweli hii nilikua kila nikianza inaniboa natafuta nyingine siku nilokosa drama, nikaianza kufika ep ya ngapi Yani hata kula Nala na pc lol

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Major Broadcasting Stations Making Changes After Popularity Of Cable Dramas
kama nawaona TBC za korea dawa zimeanza kuwaingia kwenye mishipa ya ufahamu, walibweteka sana na hatimaye wakawapa mwanya cable tv wawageuzie kibao cha ubora wa project.

kwa mujibu wa stori zilizotoka siku tatu zilizopita ni kwamba mashirika ya SBS na MBC wameamua kubadilisha mfumo wao wa uonyeshaji wa drama ili waweze kuendana na kasi ya cable tv drama..

SBS wameamua drama mpya inayoitwa “The Fiery Priest" ratiba yake iwe ni siku ya ijumaa na jumamosi, hii itakuwa ni mara ya kwanza kwa kituo cha SBS kuonyesha drama siku ya ijumaa ambapo kwa miaka 6 walikuwa wanaonyesha show the law of jungle ambayo itahamishiwa siku ya jumapili.uongozi wa SBS unaamini ya kwamba kuonyesha drama siku ya ijumaa na jumamosii ni maamuzi bora kwa sababu project zote mbili zilizofanya vizuri kupitia cable tv zimeonyeshwa siku hiyo (goblin, sky castle).

MBC nao wameamua kurudisha tena ubora wao kwa kutafuta watu wenye vipaji, kwa kuthibitisha hilo wameamua kufanya kazi na director Ahn Pan Suk ambaye project yake ya some thing in the rain (pretty noona who buys me food) ilifanya vizuri sana kupitia JTBC mnamo mwaka 2018, MBC pia wameamua kuwapa offer waliokuwa waigizaji wakuu wa something in the rain ambao ni jung hae in na son ye jin kushiriki kwenye project mpya lakini bado hawajathibisha ushiriki wao.

pia MBC wameamua kuja na project yenye utofauti wa kimaudhui ya romantic comedy na kuamua kuja na project nyengine itakayowakutanisha waigizaji wazoefu kama chae sira, kim sang joong, yoo dong geun itakayoangazia matukio ya nyakati za ukoloni wa japani nchini korea.

Si hilo tu pia MBC wameamua kupunguza drama za mwisho wa wiki kwa dhumuni la kuhakikisha wanajiandaa vilivyo kupambana na cable drama.
hmmmmmmmm!!!!!!!!!!!!!
muhudumu niongezee chupa za soju na bakuli tano za kimchi, jajjangmyeon pamoja na ramen nipate kushuhudia huu mpambano kati ya televisheni za wananchi dhidi ya televisheni za sekta binafsi.

nimesikia stori eti tajiri huzidiwa na serikali kimkakati na utoaji wa huduma, ndio maana shule za serikali ni bora kuliko shule za sekta binafsi zilizokosa hata vikalio vya wanafunzi
huku kwetu tukiangalia drama hatukai na mabisi (pop corn)

hivi huku kwetu ukiiwekea ngumu TBC unakutana na suprise gani vileeeeeeeee..................................................;'[-;;';[p-[[';[[==''[]=--&^9*($#@
1548578087013.png
 
Emperor of the sea kwangu mimi moja kati ya bonge la muvi yny stori nzuri vle vle ina mafunzo mengi
 
Imagine unaifuatilia Empress Ki at the same time unaifuatilia King Gwanggaetto the Great.nilikuwa nakerwa na yule mfalme bwege alikuwa anaendeshwa kibwege anajiliza hovyo hii tabia yake ilifanya nikajikumbushie King Gwanggaetto jinsi mfalme Dam doek(Gwanggaetto) alikuwa anaongoza kibabe.
Yule king anaboa sana. Vey weak. Ukitazama Ja Myung Go (ambayo inaelezea story ya Prince Hodong wa Goguryeo ambaye kwenye Land/Kingdom of the Wind inaisha akiwa bado mdogo) utamuona King Deamushin (Muhyul) alivyo mbabe.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Haswa hyo Emperor of the sea wameboa kinyama jinsi walivyo imaliza
But ukisoma synopsis yake kule Dramacool, wanakuambia ni 50 episode drama. Ila wameweka 51 na hiyo ya 51 ndo inaudhi sana. Ukikomea ya 50, mambo shwari.
Jang Bogo ana mtoto, business inaenda na king yupo kijana kabisa
 
Back
Top Bottom