Kwa yaliotokea Jana usiku wa mabingwa haraka Mwakinyo aandaliwe pambano

Allafrica.

Allafrica
Mkuu nimesoma hiyo article yote sijaona sehemu wamesema kuwa mwakinyo ni bondia namba 1 africa kwenye uzito wake, labda unisadie wewe kama umeona, lakini pia hiyo website haipo special kwa ajili ya boxing ispokuwa inatoa habari zote mchanganyiko, na wanaelezea namna ambavyo boxing inaweza kuwa fursa Tanzania kwa kutumia mfano wa mwakinyo, mwongozo please
 
Mnyonge mnyongeni lakini haki yake mpeni. Mwakinyo anastahili heshima aliyoitafuta mwenyewe nje ya nchi. Kaenda nje bila watu kujua zaidi ya watu wachache walio karibu naye, watu tumeshtuka baada ya kuanza kupata taarifa mitandaoni kuwa kuna mtanzania kapiga mtu huko Uingereza kabeba mkanda. Ndio tukaanza kumfuatilia mtandaoni na kujua jamaa kuwa hata vifaa vya mazoezi vya kisasa hakuwa navyo zaidi ya matairi yaani ilikuwa "from zero to hero" Sasa hawa wakina Kiduku na wengineo waache kukurupuka badala ya kupoteza muda sijui wanaomba mapambano na Mwakinyo na wao si waende wakawatandike wazungu huko warudi na mikanda dunia itawatambua kama inavyomtambua sasa Mwakinyo badala ya kung'ang'ania kila siku ooh namtaka Mwakinyo namtaka Mwakinyo. Kuna wazungu kibao wapo huko wanataka mabondia wa kuwapiga ili waongeze rekodi zao na kupanda ngazi. Sasa hao ndio wazuri badala ya hao wazungu kuweka rekodi wakina Twaha Kiduku wao ndio waende wakapindue meza kama Mwakinyo watengeneze rekodi zao kama Mwakinyo iwapo kweli wana uwezo huo. Vinginevyo kelele zao zitabaki blah blah na kupotezeana muda tu wakati jasiri muonyesha njia Mwakinyo kashawaonyesha njia ya kupita ili waweze kufanikiwa.

Kwenye kupromoti ngumi kati ya Azam na Mwakinyo kiukweli wote Mwakinyo na Azam wanastahili pongezi sana na ndio wamefanya wengi wetu tuanze kupenda tena ngumi mchezo uliokuwa umekufa kabisa. Kwa sababu kabla ya Mwakinyo kushinda nje ya nchi hata hao Azam walikuwa hawana ujasiri wa kudhamini ngumi na zaidi wangepoteza fedha zao. Kwani kila mdau wa michezo anajua ujanja ujanja ulio kuwa unaendelea kwenye mchezo wa ndondi kiasi ulikuwa unaonekana mchezo wa kitapeli tapeli na upangaji wa matokeo. Jiulizeni ilikuwaje kila bondia aliyekuwa anaenda nje alikuwa anapigwa tena raundi za mwanzo kabisa na hata wakirudi walikuwa hawasikitiki na kila siku walikuwa wanapishana uwanja wa ndege kwenda nje kupigwa..
 
Twaha akirudiana na Dulla atafanya nini eti [emoji1529][emoji1529][emoji1529]?
 
Yani mwakinyo apigane na watu wa ndondo mwakinyo levo zingine
 
Uyo bondia wa ndondo baada ya wiki atamtafuta chiz mwenzake wapigane utasikia nilitafunwa na Mbuzi Mara sho sho watu kulazimisha mwakinyo apambane na Hao watu wao wa morogoro ni kutaka wapate Jina kwa mgongo wa mtu
 
UnaZi
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…