Pre GE2025 Kwahiyo Serikali na Polisi Maandamano yanafaa yakifanywa na CCM na Chawa, wakifanya wanaopinga serikali ni Uvunjifu wa Sheria?

Pre GE2025 Kwahiyo Serikali na Polisi Maandamano yanafaa yakifanywa na CCM na Chawa, wakifanya wanaopinga serikali ni Uvunjifu wa Sheria?

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)

Cute Wife

JF-Expert Member
Joined
Nov 17, 2023
Posts
1,906
Reaction score
5,000
Wakuu,

Tukio linaondelea wakati huu ni ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi kwa Mwaka 2024 na Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Polisi Tanzania.

Kwenye maadhimisho haya wameonesha pia na kikosi cha FFU ambacho kinatumika kutuliza ghasia kukiwa na vurugu.

Cha kushangaza ni kuwa wamefanya igizo la kuonesha jinsi FFU wanavyotawanya watu wakisema kwamba kuandamna na uvunjifu wa sheria!

Hivi polisi wanajua kweli kama maandamano ni haki ya kikatiba? Kwa maigizo haya inaonesha maagizo wanayopewa ni kuwa maandamano ni kinyume na sheria na wanaofanya maandamano haya wanatuakiwa kupigwa ili wasiandamane.

Tena wameitwa waletwa fujo.

Mnataka wananchi watumie njia gani kama wanaona hawasikilizwi wanapofikisha kero zao. Na maanadamano haya huwa yanakuwa ya amani lakini bado mnawanyima haki wananchi.

Nani huwa anatoa ushauri huko juu, mbona mnafanya maamuzi ya ajabu hivi?

Mpo serious kweli ninyi? Kadri siku zinavyoenda mnazidi kuminya haki za wananchi, hawa wananchi mnaowaona mafala siku wakichoka hakuna polisi ataweza kutuliza chochote!

Rudi kwenye mstari tafadhali, kama mnapita humu kweli muache kuwa 'vyura viziwi', bomu mnalotengeza mtashindwa kulitegua.

Na tunajua hii ni msg sent kwa CHADEM, lakini mkumbuke hii nchi si ya CHADEMA pekee au ya CCM pekee, ni ya wananchi wa tanzania ambao wana kila haki ya kuandamana na kuiwajibisha serikali yao ikiwa wanaona hakuna uwajibikaji.

Lakini pia maandamano siyo siyo kwaajili ya chawa au CCM pekee wakitaka kusifia utendani wa mama, na wenye kero zao wakitaka kuandamana wakatakiwa kulindwa.

Serikali na Vyombo vya Ulinzi MNATUANGUSHA!


Embu angalieni hili igizo, na wakapitisha wakaona linafaa kabisa!​
 
Wakuu,

Tukio linaondelea wakati huu ni ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Maafisa Waandamizi wa Jeshi la Polisi kwa Mwaka 2024 na Maadhimisho ya Miaka 60 ya Jeshi la Polisi Tanzania.

Kwenye maadhimisho haya wameonesha pia na kikosi cha FFU ambacho kinatumika kutuliza ghasia kukiwa na vurugu.

Cha kushangaza ni kuwa wamefanya igizo la kuonesha jinsi FFU wanavyotawanya watu wakisema kwamba kuandamna na uvunjifu wa sheria!

Hivi polisi wanajua kweli kama maandamano ni haki ya kikatiba? Kwa maigizo haya inaonesha maagizo wanayopewa ni kuwa maandamano ni kinyume na sheria na wanaofanya maandamano haya wanatuakiwa kupigwa ili wasiandamane.

Tena wameitwa waletwa fujo.

Mnataka wananchi watumie njia gani kama wanaona hawasikilizwi wanapofikisha kero zao. Na maanadamano haya huwa yanakuwa ya amani lakini bado mnawanyima haki wananchi.

Nani huwa anatoa ushauri huko juu, mbona mnafanya maamuzi ya ajabu hivi?

Mpo serious kweli ninyi? Kadri siku zinavyoenda mnazidi kuminya haki za wananchi, hawa wananchi mnaowaona mafala siku wakichoka hakuna polisi ataweza kutuliza chochote!

Rudi kwenye mstari tafadhali, kama mnapita humu kweli muache kuwa 'vyura viziwi', bomu mnalotengeza mtashindwa kulitegua.

Na tunajua hii ni msg sent kwa CHADEM, lakini mkumbuke hii nchi si ya CHADEMA pekee au ya CCM pekee, ni ya wananchi wa tanzania ambao wana kila haki ya kuandamana na kuiwajibisha serikali yao ikiwa wanaona hakuna uwajibikaji.

Serikali na Vyombo vya Ulinzi MNATUANGUSHA!

Mkuu, tatizo la Tanzania na serikali yake ya CCM, Ukomunist na Ujamaa bado upo kwenye damu yao. Bado kuna Uchinachina, Ukoreakorea, Ucubacuba na Urusiarusia kwenye sytem yetu. And CCM like that way.
 
Askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia (FFU) wakionesha namna wanavyokabiliana na ghasia za maandamano ya wananchi.

FFU wamefanya hayo katika kilele cha maadhimisho ya miaka 60 ya Jeshi la Polisi nchini Tanzania.

 
Swali fikirishi hivi nguvu ya umma huwa ni nini hasa maana mimi ni mshamba wa haya mambo
 
Swali fikirishi hivi nguvu ya umma huwa ni nini hasa maana mimi ni mshamba wa haya mambo
Ni hivi karibuni tu, nguvu ya umma ilitumika nchini Bangladesh kumsambaratisha mama Sheikh, ambaye naye alijiona kuwa ni kisiki.
Hakuna kiongozi yeyote duniani anayeweza kushindana na nguvu ya umma iliyo dhamiria kumng'oa.
 
Kumbe ndiyo hiyo inaitwa people's power?, haa kumbe nisawa na watu wenye hasira wamejichukulia sheria mkononi, badala ya kichwani
Pamoja na kukutambua sasa kuwa kumbe ni chizi, lakini ngoja nikusaidie.
Kibaka anaye kutishia kuondoa uhai wako unamfanyaje kabla hajakumaliza? Ondoa uchizi kwanza kichwani kabla hujajibu.
 
Pamoja na kukutambua sasa kuwa kumbe ni chizi, lakini ngoja nikusaidie.
Kibaka anaye kutishia kuondoa uhai wako unamfanyaje kabla hajakumaliza? Ondoa uchizi kwanza kichwani kabla hujajibu.
Nikipewa dhamana tu kweli huwa naahirisha kufikiri kizalendo, a.k.a kujizima data,
 
Nikipewa dhamana tu kweli huwa naahirisha kufikiri kizalendo, a.k.a kujizima data,
Ndio uchizi wenyewe huo. Watu wa aina yako wapo wengi tu. Bahati nzuri ni kuwa hamuwezi kuzuia mabadiliko yanayotafutwa na wazalendo wa nchi hii.
 
Ndio uchizi wenyewe huo. Watu wa aina yako wapo wengi tu. Bahati nzuri ni kuwa hamuwezi kuzuia mabadiliko yanayotafutwa na wazalendo wa nchi hii.
Tena nina tabia ya unyumbu wa kisiasa, unyumbu wa kisiasa ni tabia ya wanao pewa dhamana kuahirisha kufikiri kwa nafsi kwasababu ya kujipendekeza ama kulitumikia kundi fulani kwa masilahi binafsi na uoga kwa viongozi wao bila utii,(unafiki)
 
Tena nina tabia ya unyumbu wa kisiasa, unyumbu wa kisiasa ni tabia ya wanao pewa dhamana kuahirisha kufikiri kwa nafsi kwasababu ya kujipendekeza ama kulitumikia kundi fulani kwa masilahi binafsi na uoga kwa viongozi wao bila utii,(unafiki)
Sina sababu hata kidogo ya kuendelea nawe humu JF. Kuna ya muhimu zaidi ya kupotezea muda kuliko uhayawani wa mtu fulani.
 
Back
Top Bottom