Kwako Lissu; Kwenye public speeches na Live interviews kunahitaji Sanaa ya kuusema ukweli na kuepuka UKALI wakati usio sahihi ili kushawishi watu

..andiko lako linawatia moyo wanaofanya dhuluma na ukatili hapa nchini.

..tumia kalamu na kipaji chako vizuri kwa kutetea HAKI.

Kwa namna ipi?

Mimi kumwambia Lisu abadili Mbinu ili apate uungwaji mkono na watu wengi zaidi. Watu wamuelewe nawezaje kuunga Mkono dhulma?

Mbinu anayotumia Lisu hawezi kushinda kama hatapata ushawishi kutoka kwa Watu wengi
 
Mwambieni Lissu asifikiri hizi akili anazozisoma mitandaoni za akina Tindo Proved Lord denning kalama et al ndo akili za wapiga kura walioko ground!!

Siasa sio mahali pa amri kama jeshini au kazini!! Siasa zina dynamics zake na tamaduni zake!! Mwambieni huko ground watu wanapewa redio sasa inabidi ajiulize lugha gani ataitumia wamuelewe!! Ujuaji sio mzuri aliwasema sana wenzie naona anaanza kukwama mapema sanaaa

Kula kitu hichooo
 

Attachments

  • IMG_2206.jpeg
    1.1 MB · Views: 1
Si mlisema hivyo hivyo kuwa hashindi Uenyekiti Chadema kwa kuwa watu wa motandao sio wapiga kura! Vipi kiko wapi?
 
1. Hii ya Balile jana si kwamba alikuwa haelewi bali alikuwa anamvuta Tundu Lissu katika uelekeo aliokuwa anautaka yeye, uelekeo wa uchawa wa mama a.k.a Chura Kiziwi lakini alishindwa kwa kuwa alikuwa mbele ya mtu ambaye ufahamu na uelewa wake ktk issues mbalimbali ni wa juu na wa mbali miles nyingi kuliko Balile na anaowatumikia...

2. All in all, kupitia mkutano ule jana kati ya CHADEMA na Jukwaa la Wahariri - TEF, mimi binafsi nimegundua jambo moja kuwa, wahariri na waandishi wa habari wengi ni mbumbumbu wa issues nyingi. Mfano wengi waliohudhuria jana hata hawaijui katiba ya JMT ya 1977 ukimwondoa Balile tu ambaye naye alikuwa anafurukuta na kujikanyaga kanyaga tu mbele ya Tundu Lissu na ndiyo maana akawa anauliza "nonsense questions..."

3. Waandishi wa habari na wahariri wa dizaini hii ambao wao wanachojua kufanya ni kuripoti matukio na kutafuta umbea mitaani na kuutangaza kwenye online tvs na vijigazeti vyao, waandishi wa dizaini hii wasiotumia muda wao kujisomea ili kujua mambo ya nchi yao na wajibu na haki zao, si rahisi kivile wakaelewa movement ya No Reforms, No Election...

4. Na wakati mwingine ili waelewe, unahitaji kutumia mitulinga ikiwemo kuwaambia hadharani waache "nonsense" na kufuga ujinga ktk vichwa vyao na badala yake wajifunze kuukubali ukweli unaowakodolea macho kwenye nyuso zao...

5. Tundu Lissu naturally anakubalika na kamwe hamhitaji mtu kama Balile ili kumfanya akubalike...
 
Si mlisema hivyo hivyo kuwa hashindi Uenyekiti Chadema kwa kuwa watu wa motandao sio wapiga kura! Vipi kiko wapi?
Sasa utafananisha mkutano mkuu wa chadema uliokua na wajumbe 900 na asilimia kubwa wanywa visungura waliokua wakipiga hovyo kelele (ambao ni ninyi) na bado mkashinda sijui kwa kura 13 ndo inawapa bichwa kuwa mtaiweza nchi nzima kweli?? Kwahyo zile kura ndo zinamfanya Lissu Tumbo lizidi kujaa namna ile? Hivi mna akili kweli nyie?
 
Dah! Angalau leo umeongea pwenti! Nashauri kama Lissu alishawishi kundi la tatu, basi arudi shule ajifunze kuhusu "Public Speaking". Itamsaidia sana kuwapata watu wa kundi la tatu.
 
Safi, endeleeni na sifa zenu za kijinga. Mtu anashauri jambo muhimu kabisa mnaleta ujinga.
Katoa ushauri mzuri naukubali, ila alichofanya Balile ni nonsense. Rudi kasikilize ile clip, alikuja na matokeo mfukoni ya kulazimisha Tume ya Uchaguzi ni huru. Kila akieleweshwa anakuja ana hamisha magoli tu
 
Narudia, ni suala la muda tu kabla mshamba flani hajatema au kutemeshwa bungo!!


Mtoa mada wasioosema watu basi andiko hili litasimama kukusemea.
 
Aiseeh!
Kwamba Mimi niitetee dhulma?

Mimi nimemshauri Lisu namna ya kufika huko anakotaka kufika. Hiyo ni juu yake kuelewa kwa namna yako au Kwa namna atakayoona yeye
Wakati wa kubembelezana na kutongozana umekwisha. CCM wamekuwa wanafiki kwa muda mrefu na kete yao kubwa ni umaskini wa wananchi kwa kutoa zawadi ndogo ndogo na kuendesha propaganda za vitisho na vita.

Wananchi pia wanaelekea kukinaishwa na unafiki wa CCM lakini bado hawajapata mwongozo sahihi wa kuiadhibu. Katiba na sheria zipo lakini zinakiukwa kwa makusudi kwa visingizio mbalimbali.

Hivyo kuendelea kuchekeana na CCM ni kupoteza muda bure! Wakati wa kuambiana na kujibizana na CCM kwa maneno makavu ni sasa vinginevyo maisha ya wananchi yataendelea kupotea kwa kisingizio cha kulinda amani!
 
vibaka na matapeli wa siasa huwa hawanaga utulivu wakiulizwa kitu wasichokua na majibu nacho kulingana na marking scheme za majibu walioyojiandaa nayo
 

Ni sahihi lakini wanachama na Mashabiki wa CCM ni MUHIMU pia kwa Tundu Lisu
Na ndipo hoja yangu ilipo
 
Naunga mkono hoja
P
 
Yaani umfundishe hayo mh.Tundu Lissu akuelewe ?!!

Familia yao nzima inajulikana kwa kuwa na "mbango".....

Kila aliyefanya kazi na mh.Tundu Lissu atakwambia huyo bwana ni "much know"...mbishi ,mkaidi ,alitakalo yeye ndilo huliamini kuwa ni bora kuliko ya wengine.....kifupi ana "jeshi la wafuasi wenye mapungufu hayo kama alivyo yeye na humu ndani wapo akina Lord Denning ,Erthrocytes et al...".
 
Kiongozi, kuhusu kitu unachokiita ukali katika kuongea, inaonekana huelewi maana yake, au huelewi study za mawasiliano commutation skills.
Katika an art of public speaking.

Kwa mwanasiasa, Mwalimu, CEO aliyeiva hawezi kuongea mwanzo mwisho kwa same tone.

Lazima kuwe na tone variety,namna nyingine ukikosa hiyo hadhira inakuwa tired , inapoteza hamu ya kumsikiliza mhusika.

Kwahiyo katika art of public speaking Kuna
1.Rising ,
2.Falling tone

Moja inaonesha msistizo, Moja inaonesha kuweka kituo baina ya hoja Moja na nyingine .

Ndio maana unaona hakuna nyakati Nyerere, Nelson Mandela, Mugabe Robert, Julius Malema,Late Christopher Mtikila, Samora Moses Marchel wamekuwa na pitch and Intonation yenye same rhyme all the time.

Nakuomba sana pitia speech za hao hasa JULIUS MALEMA, uanaharakati ni attitude na msimamo,kuliko namna ya kuongea.

All in all andiko lako lipo vizuri, ila nipo kinyume kabisa na concern yako eti Lissu anaongea kwa ukali na kiharakati.

Nakuomba check na watu waliosoma Linguistic hasa katika sarufi matamshi Phonology utaelewa mtindo wa kuongea wa Lissu sio bahati mbaya, ni professional public speaking, kajifunza na ana practice.

πŸ™πŸ™πŸ™
 

Mkuu Mimi nimesoma Phonology nilichokiandika nakielewa

Hata hivyo pia umeeleza sahihi Kabisa
 
πŸŒ€οΈπŸ™‹β€β™‚οΈβœοΈπŸŽ―πŸ‘πŸ‘ŒπŸ‘πŸ‘ŠπŸ€πŸ™πŸ’ 🎁 πŸ†’
 
πŸŒ€οΈπŸ™‹β€β™‚οΈβœοΈπŸŽ―πŸ‘πŸ‘ŒπŸ‘πŸ‘ŠπŸ€πŸ™ πŸ’πŸŽπŸ†’πŸ”Š
 
Mimi naona huo UKALI ndio unaomfanya aaminike zaidi na watu wengi. UKALI wake unaonesha SERIOUSNESS. UKALI wake unaonesha hanunuliki. Nashauri aendelee kuwa MKALI hivyo hivyo kwa sababu siku akiwa MPOLE atazushiwa kuwa kala hela za Abduli kama Chaupole Mbowe. Yaani ikiwezekana ang'oe 'bandama' ili hata kucheka asiwe anacheka kabisa. Ni mwendo wa sura ya kaziπŸ˜„
 
Kwa namna ipi?

Mimi kumwambia Lisu abadili Mbinu ili apate uungwaji mkono na watu wengi zaidi. Watu wamuelewe nawezaje kuunga Mkono dhulma?

Mbinu anayotumia Lisu hawezi kushinda kama hatapata ushawishi kutoka kwa Watu wengi
Wewe umejuaje kwamba hapati uungwaji mkono na watu wengi zaidi?. Una takwimu?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…