Kwako Ridhiwani Kikwete Waziri wa Vijana, Ajira na wenye Ulemavu

Kwako Ridhiwani Kikwete Waziri wa Vijana, Ajira na wenye Ulemavu

NAFIKIRE

JF-Expert Member
Joined
Sep 5, 2014
Posts
660
Reaction score
456
Kwanza nianze kukupongeza Mheshimiwa waziri kwa kazi kubwa na nzuri unayoifanya kwenye wizara unayoiongoza..Hongera sana

Mheshimiwa waziri niende moja kwa moja kwenye dukuduku langu lilonisukuma kupandisha hili wazo langu hapa kwenye jukwaa letu pendwa la JF.


Mheshimiwa waziri ninajua fika moja ya jukumu mama la wizara yako ni kuwatafutia vijana ajira na mazingira bora ya kazi.

Mheshimiwa waziri nimefikiria niakona moja ya njia ya kuongeza fursa za kazi ndani ya serikali ni kupunguza umri wa kustaafu kwa hiyari utoke kwenye miaka 55 mpaka miaka 45..Mimi ninaamini wewe ukishirikiana na viongozi wengine ndani ya serikali na viongozi wakuu mnaweza mkalichata jambo hili mkaona faida zake na hasara zake kama zipo na hatimaye mkapeleka mswada bungeni kwa majadiliano zaidi.

Faida ya kunguza umri wa kustaafu kwa "HIYARI" kwa mtazamo wangu mimi ni nyingi sana.Moja ya haraka ya kupunguza umri wa kustaafu kwa hiari ni ongezeko la nafasi za ajira ndani ya serikali kwa kiwango kikubwa na vijana wengi wanaotamani kuajiriwa na serikali watapata ajira serikalini.

Faida ya pili ninayoiona kwa haraka watu watakaostaafu kwa hiari wataingiza fedha zao mtaani kwa kuanzisha biashara mbalimbali ambazo zitatoa ajira kwa vijana na watu wengine na hivyo kufanya mzunguko wa fedha kwenye jamii kuwa mkubwa.

Pia kuingia kwa vijana wengi ndani ya serikali kwa kiwango kikubwa wenye uzoefu mbalimbali kutaongeza ufanisi wa kazi kwa kiasi kikubwa.

Nawasilisha
 
Mstaafu ni drain kwa uchumu financially speaking kwa sababu value ya production yake inapungua lakini matumizi na consumption kwenye upande wa huduma zinaongezeka.

Ndio maana nchi za ulaya zinapandisha umri wa kustaafu, wewe unataka upunguze???

Solution ni kuongeza ajira kwenye sekta binafsi. Kodi zipunguzwe haswa za makampuni ili watu waanzishe biashara na kuziformalize bila kuhofia serikali itakula fungu kubwa la faida yao (30%).

Washushe corporate tax to 10% kisha waondoe kodi kwa mapato mengineyo (allowances) kama extraduty, overtime, transport and housing allowance zisikatwe kodi kama wanavyofanya serikalini (very unfair to private sector employees). Pia SDL ifutwe maana ni kama financial penalty ya kuajiri watu wengi hivyo hudiscourage waajiri.

Wakipunguza kodi watu watabaki na faida kubwa, rushwa itapungua kwenda TRA, pia watu watapasa hamasa ya kuajiri watu formally kama kodi za kipuuzi kama SDL zitaondolewa
 
Unamshukuru kwa kipi, waziri wa ajira. Vijana na walemavu.

Kuna ajira zipi kwa hao vijana?
 
Mstaafu ni drain kwa uchumu financially speaking kwa sababu value ya production yake inapungua lakini matumizi na consumption kwenye upande wa huduma zinaongezeka.

Ndio maana nchi za ulaya zinapandisha umri wa kustaafu, wewe unataka upunguze???

Solution ni kuongeza ajira kwenye sekta binafsi. Kodi zipunguzwe haswa za makampuni ili watu waanzishe biashara na kuziformalize bila kuhofia serikali itakula fungu kubwa la faida yao (30%).

Washushe corporate tax to 10% kisha waondoe kodi kwa mapato mengineyo (allowances) kama extraduty, overtime, transport and housing allowance zisikatwe kodi kama wanavyofanya serikalini (very unfair to private sector employees). Pia SDL ifutwe maana ni kama financial penalty ya kuajiri watu wengi hivyo hudiscourage waajiri.

Wakipunguza kodi watu watabaki na faida kubwa, rushwa itapungua kwenda TRA, pia watu watapasa hamasa ya kuajiri watu formally kama kodi za kipuuzi kama SDL zitaondolewa
wakifanya hivo nchi itazidi kuomba,me naona waongeze ukusanyaji wa mapato.
 
Hii naiunga mkono moja kwa moja.

Wanao baki kazini mda mrefu mara nyingi hujilimbikiza mali tu.

Watoke ili watoto wao waingie tuendeleze kazi. na wao wafanye biashara.
 
Back
Top Bottom