Kwangu mimi hiyo ndiyo hotuba ya maana kuliko zote zilizopata kuhutubiwa na Hayati mzee Nyerere


Nyerere alikuwa msemaji mzuri sana na aliujua ukweli. Ingawa enzi za utawala wake kuna wakati alikuwa akipindisha baadhi ya mambo KIMKAKATI ili kufanikisha malengo yake - (kwa nia nzuri).

Aliyoyasema kwenye hotuba hii ni mema sana ingawa ni ya wazi (obvious) kabisa kwa mwenye uelewa makini. Na aliyaona akiwa “nje ya system” akishuhudia jinsi utawala wa Mwinyi ulivyokuwa ukifanya “vurugu” zake.

TATIZO hakuwa na nia ya kung’oa mzizi wa yote aliyokuwa akikemea. Kuacha mfumo ulioisimika CCM kama chama dola na Rais/mwenyekiti mwenye madaraka yote (absolute power) ndio janga au msiba mkuu unaoitesa Tanzania hadi leo. Wanaingia madarakani watu aina tofauti tofauti waliojaa tamaa, uroho, ukabila, udini, ukatili, n.k.

Kwa nguvu ya CCM na dola wanayokuwa nayo, hakuna wa kuwadhibiti wala kuwarekebisha viongozi. Wananchi hawana sauti wala namna ya kudhibiti uongozi kupitia chaguzi huru wala bunge wala mabaraza ya uwakilishi. Wamebakia kuomba huruma na hisani ya serikali/Rais.

Hotuba za Nyerere zote zimebakia kuwa nice words but ineffectual (bla bla). Nobody can apply them to a good national cause. Viongozi wanatumia vipande vyake kupigia propaganda za ukandamizaji.
 
Nyerere ni kweli alisomesha watu bure lakini uchumi ulimshinda kutokana na sera zake za kijamaa. Ukitaka kuleta visingizio vya nchi yetu changa, vita baridi, sijui ukame sivikubali. Kuna nchi za Asia zimepata uhuru baada ya sisi wameendelea. Ukame upo sehemu nyingi tuu lakini serikali zinapanga. Kabla ya vita na Uganda uchumi ulikuwaje? Maana vita na Uganda kila siku inatumika kama kisingizio cha kushindwa Nyerere kushindwa uchumi. Unafikiri ujamaa uliishia tuu vijijini? Kasome kitabu chake utaelewa Ujamaa alioufanya Nyerere hapa maana naona huna experience nao.
 
Kwa nini Nyerere hakubadilika wakati China inabadilika na kufanya economic reforms? Mfano wa sera mbovu za Ujamaa wake alizofanya aliona wakati wa Cultural revolution ya China. Akaukomalia Ujamaa wake mpaka mwisho. Kama angetaka welfare state unayoifagilia wewe angewaiga hata Sweden kuliko kung'ang'ania Ujamaa wake.
 
Hakuna ujamaa wa Nyerere kuna socialism inayobadilika kulingana na wakati, mahitaji na nyenzo ulizonazo, Kubadilika kwa China kumekwenda hatua kwa hatua..., Ujamaa na Kujitegemea ungefanyika sasa hivi kungekuwa hakuna mashamba ya kijiji ya watu kulima na Jembe la Mkono bali multi industrial automated farms ambazo zina tija (wakati ule zilikuwa hazipo sasa hizi technology ipo) Kwahio multi industries (commanding heights of the economy) kama ilivyo China bado zitakuwa mali za UMMA ingawa na private sectors zinafanya kazi sambamba...

Sweden pamoja na welfare state (ambayo mimi siifagilii) inafanya nchi kama sweden kuwa na kodi kubwa sana sababu hizo pesa lazima zitoke sehemu ambayo ndio hio kuwaminya baadhi ili kuwapatia wengine..., ninachofagilia mimi sio kugawana mkate wa wengine wakishatafuta bali kupeana fursa ya kutafuta mkate huo....

To Each According to his Need..., From each According to his Ability (Though I believe Each should be given opportunity to earn his keep)
 
Nyerere ni kweli alisomesha watu bure lakini uchumi ulimshinda kutokana na sera zake za kijamaa.
Sasa hivi Uchumi tulioweza upo wapi na maendeleo gani ? Ukizingatia sasa hivi tuna idadi kubwa ya rasilimali watu na madini tunayachimba kila leo, na kufungua milango ya kuuza kila kinachouzwa.., Uchumi umefikia wapi kwenye household level ? Watu hawana disposable income pamoja na vitu kuwepo buying power hakuna
Ukitaka kuleta visingizio vya nchi yetu changa, vita baridi, sijui ukame sivikubali.
Alivyochukua nchi alikuwa na wataalamu wangapi na specialists wangapi ? Vita baridi sio story ilikuwepo na ulikuwa ukienda ndivyo sivyo unamalizwa uliza kuhusu kina Sankara
Kuna nchi za Asia zimepata uhuru baada ya sisi wameendelea.
wameendelea baada ya muda gani, na katika scenarios zipi ? wameendelea sababu ya kutokuwa Wajamaa au kuna some extra issue in play
Hivi wewe unajua ukame uliotokea miaka ya 70 na 80 kupelekea njaa na watu kula ugali wa yanga ? Hard times zipo dunia nzima kwa nyakati tofauti iwe America, Germany au UK zote zimepitia hard times nyakati tofauti na ilichukua muda kuondoka pale walipo Hata Marekani katika their Economic Boom in 60's baada ya stock market Crash watu walikuwa katika ufukara wa kutupwa (the unstability of capitalism boom and bust) au inflation and hyper inflation ya UK, leo mpo vizuri kesho uchumi unachokua a Nose Dive.... (Cycles of Boom and Bust)
 
Kwa nini mzee aliyejaa hekima na busara alikomalia sera za ujamaa na zilizoharibu uchumi na kuacha nchi masikini?
Sera ilikuwa nzuri, hii Sera lengo kuu ni nchi iwe ndo mmiliki kamili wa raslimali na mzalishaji ,kwa [emoji817]. nchi inazalisha bidhaa tosherezi ndani ya nchi,na ziada zinauzwa nje, kwa maana hiyo hii Sera hulifanya taifa kuwa na nguvu kiuchumi ,kwa sbb ya kuteka soko la ndani ,na nje,like China,they produce products for themselves & they sell surplus product to foreigner country!! Sera ilikuwa nzuri Sana lkn wahuni wakaivuruga!! Kama ingeenda vyema tusingekuwa hapa tulipo,kwani China wanaishi malaika!? Waliwezaje !!??
 
Na hao Mabepari huko nchi zao zipo katika hatari ya watu kuandamana siku yoyote na kupinga kwamba tunanyonywa au kodi ya matajiri iongezwe ili sisi masikini tupewe...., au Kampuni yako kubwa sana ina monopoly tuivunje (Google, Microsoft, Amazon, Rockoffeller n.k.) Au Corporations kubwa kuhonga Policy Makers au mpaka hata Rais ili kupitisha sera zao thus kuibia wananchi (ENRON) Bila kusahau Profit at all Costs zinazoharibu Mazingira kila kukicha (In short mwananchi hata nafasi ni howmuch money to be made)

Na bila kunyonya na marginalization of poor countries hizo developed countries zisingekuwa hapo zilipo (huku sisi ndio soko, raw materials na dumping ground ya kila kitu)
 
Kwanini Tanzania haijawa ya tatu kiuchumi duniani kama ilikuwa sera nzuri?
Tumeachana na hizo Sera tumefungulia milango ambayo ilikuwa imefungwa na kuuza nchi left right and centre (Je hali ya Mwananchi imebadilika to the better )?

Bila kumbuka kuna Rasilimali ambayo China walikuwa nayo wakati wote na Nyerere alikuwa hana na sasa Hivi imeongezeka (Rasilimali Watu)..., Na hayo yote machache yalifanyika na kuwapa watu elimu (sio sasa hata mikopo hakuna) kwa kutokuchimba nchi yetu kila kona na kuuza madini kila sehemu (mapato yameongezeka)

In Short kinchoendelea sasa sio sustainable
 
Ukitaka kujua kwa nini Nyerere na Ujamaa wake uliharibu uchumi na kuacha watu masikini msikilize huyu mchumi

Nyerere aliacha madaraka lini na tokea aondoke kwanini tumeshindwa kufikia hapo unapopataka?

Anawezakuwa na mapungufu yake lakini anabaki kuwa miongoni mwa viongozi bora kabisa.

Kuna mambo tumeshindwa kuyatekeleza na tunabaki kumrushia lawama Nyerere.
 
State inamiliki vitu gani?
 
Uchumi wa Pakistan kwa siku za hivi karibuni umekua ukikua kwa Kasi lakini unfortunately ukuaji wake umekua ni kwa corporations,campanies na few Richie's,So the govt ilijikuta inatafuta ku punguza hiyo growth ambayo sio inclusive..

Point ni nini,ni kwamba tutafute model yetu badala ya kuiga models za wengine.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…