Kwani Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) haiwezi kuwa na accounts za malengo kwa wanafunzi wa darasa la kwanza?

Kwani Bodi ya Mikopo ya Elimu ya Juu (HESLB) haiwezi kuwa na accounts za malengo kwa wanafunzi wa darasa la kwanza?

Itakuwa ni idea nzuri sana ila changamoto tuliyo nayo Tz ni usjmamizi uoneshao uaminifu na uwazi.

Mzee aliyeajiriwa miaka 30 iliyopita Leo hii anastaafu hadi anakufwa kama sio kufariki KIINUA MGONGO CHAKE KUKIPATA NI SHIDA he vipi au itakuwaje kwa mtoto ambaye amewekezewa fedha hizo toka kwa wazazi wake?

Once uzalendo,uwazi na uaminifu ukiwa dhahiri naamini hakuna litakalokuwa gumu.

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
 
Hii sio biashara mkuu, hapa unaweka pesa kwa ajili ya mtoto wako. Kama mwanafunzi atasoma mpaka kidato cha sita inakuwa hivi;

8,000 x 12 x 13 = 1,248,000

Mtoto wako anapewa mkopo huku tayari akiwa na collateral ya 1,248,000 kwenye account ya HESLB
Idea yako Ni nzuri, lakini unajua gharama za chuo za mwaka mmoja kwa mwanachuo mmoja?

Pili vipi concept ya "Time Value of Money"?? Yaan uweke 8,000/- leo Kisha baada ya miaka 13 uje upewe 8,000/- hiyo hiyo ni haki kweli?
 
Itakuwa ni idea nzuri sana ila changamoto tuliyo nayo Tz ni usjmamizi uoneshao uaminifu na uwazi.

Mzee aliyeajiriwa miaka 30 iliyopita Leo hii anastaafu hadi anakufwa kama sio kufariki KIINUA MGONGO CHAKE KUKIPATA NI SHIDA he vipi au itakuwaje kwa mtoto ambaye amewekezewa fedha hizo toka kwa wazazi wake?

Once uzalendo,uwazi na uaminifu ukiwa dhahiri naamini hakuna litakalokuwa gumu.

Sent from my TECNO KB7j using JamiiForums mobile app
Tatizo la waafrika tunapenda sana wizi na mambo yetu hayapo wazi kabisa
 
Habari zenu waungwana wa humu jamiiforums

Kwanini Bodi ya mikopo ya elimu ya juu (HESLB) isianzishe campaign ya kuhamasisha wazazi kuanza kuwalipia watoto wao pesa kidogokidogo katika accounts maalum ya bodi wangali wakiwa bado wanasoma elimu ya msingi (Darasa la Kwanza)?

Jenga picha mtoto anasoma darasa la kwanza kwa miaka saba (7) kisha baada ya kuhitimu anajiunga na kidato cha kwanza mpaka cha nne kwa miaka minne (4) ambacho kwa sehemu kubwa hapa Tanzania ndicho kiwango cha elimu ambacho wanafunzi anaruhusiwa kujiunga na chuo cha ufundi kama amekosa fursa ya kuendelea na Advanced Level.

MATHEMATICAL BREAK DOWN
==========
Idadi ya miezi ndani ya mwaka: 12

Idadi ya miaka atakayosoma mwanafunzi kabla ya kujiunga na elimu ya juu/ufundi: 11

Kiwango cha chini cha uchangiaji kwa kila mwezi: 8,000/=

Makusanyo ya mwaka mzima kwa mwanafunzi mmoja - 12 x 8,000 = 96,000

Makusanyo ya miaka 11 kwa mwanafunzi mmoja - 12 x 11 x 8,000 = 1,056,000

Kutokana na takwimu niliyoipata humu humu jamiiforums: "Wanafunzi 947,221 wa darasa la saba kutoka shule 17,051 za Tanzania bara, wanatarajia kufanya mtihani wa kumaliza elimu ya msingi kesho Jumatano na keshokutwa Alhamisi Septemba 12, 2019"

Just assume kwamba wanafunzi walioanza la kwanza ndio haohao waliomaliza darasa la saba na hakuna aliyekufa wala kuacha shule na idadi kamili ni 947,221.

Makadirio ya makusanyo ya mwezi kwa wanafunzi wote wa darasa la kwanza - 8,000 x 947,221 = 7,577,768,000

Makadirio ya makusanyo ya mwaka mzima kwa wanafunzi wote wa darasa la kwanza - 8,000 x 12 x 947,221 = 90,933,216,000

Kwa makusanyo kama haya kwa mwezi kwa wanafunzi wote takribani shilingi 90,933,216,000 bodi ya mikopo wanaweza kuwekeza hii pesa katika fixed deposits kwenye banks za kibiashara pamoja na kununua "government securities" na kupata returns kubwa na za maana tu kila baada ya miezi sita au mwaka.

Kama familia ina wanafunzi wawili mmoja akifa pesa zinahamia kwenye account ya mdogo/kaka yake.

Ndugu zangu, mimi sio mtaalam sana wa hesabu na uchumi lakini bila shaka idea yangu mtakuwa mmeielewa. Ninawakaribisha kwa michango zaidi pamoja na kukosolewa (Constructive Criticism)

USISAHAU: ENDELEA KUWA MZALENDO IPENDE TANZANIA. USICHAFUE TASWIRA NJEMA YA TAIFA LAKO. USTAWI WA NCHI YETU UNAANZA NA WEWE. TIMIZA WAJIBU WAKO IPASAVYO.
Nafikiri taasisi za kibenki zina jukumu la moja kwa moja na zinashughulika na hili, pia mifuko ya hifadhi ya jamii yaweza chukua hii hao ndio watu sahihi wenye uzoefu ktk masuala ya akiba ya kifedha...

Bodi ya mikopo yenyewe ibaki kama regulatory authority tu kwa vyombo vyote na taasisi zinazoshughulika na mikopo/akiba kwaajili ya elimu ya juu sio eti yenyewe nayo ifungue account.

Ili kuleta ufanisi, ni kutanua wigo wa huduma za mikopo na akiba kwaajili ya elimu ya juu zifanywe na taasisi nyingi na si kuiongezea taasisi moja majukumu...
 
Nafikiri taasisi za kibenki zina jukumu la moja kwa moja na zinashughulika na hili
Mkuu, siwezi kuingia JF kuishauri taasisi binafsi kwa maana hazina shukrani hata kidogo. Bora kushauriana na serikali yangu ambayo ninajua mwisho wa siku faida inakuwa kwa watanzania wote...
 
mifuko ya hifadhi ya jamii yaweza chukua hii hao ndio watu sahihi wenye uzoefu ktk masuala ya akiba ya kifedha...
Mkuu, hiyo mifuko ya hifadhi ya jamii watu wanawapigia kelel kila siku kwamba wanaonewa juu za pesa zao.

Sasa sijui ni kweli au wanawasingizia tu.
 
Bodi ya mikopo yenyewe ibaki kama regulatory authority tu kwa vyombo vyote na taasisi zinazoshughulika na mikopo/akiba kwaajili ya elimu ya juu sio eti yenyewe nayo ifungue account.
Kama NSSF na PSSSF wameweza kuwa mifuko ya kijamii kwanini HESLB isiweze kuwa mfuko wa kijamii ilhali inaihudumia jamii ya wanafunzi na sio wafanyakazi?...
 
Mkuu, siwezi kuingia JF kuishauri taasisi binafsi kwa maana hazina shukrani hata kidogo. Bora kushauriana na serikali yangu ambayo ninajua mwisho wa siku faida inakuwa kwa watanzania wote...
Nafikiri wapaswa fahamu mchango wa sekta binafsi ktk maendeleo ni mkubwa mnoo na hiyo serikali inatambua ushirikiano wa PPP ( Public and Private Partnership).

Taasisi binafsi zina shukrani kwa jamii, labda kama ni taasisi uchwara, ktk utendaji wake mathalani kampuni kitaalamu na kisheria zinapaswa kujitoa kwa jamii (corporate social Responsibility) sehemu ya faida yao wanairudisha kwa jamii achilia mbali kodi yao wanayochangia kwa serikali ambayo huleta maendeleo uyatakayo.

Uzoefu unaonyesha, huduma inayotolewa na serkali peke yake bila ushirikiano na sekta binafsi ina changamoto kubwaaa mifano ipo lukuki.
 
Mkuu, hiyo mifuko ya hifadhi ya jamii watu wanawapigia kelel kila siku kwamba wanaonewa juu za pesa zao.

Sasa sijui ni kweli au wanawasingizia tu.
Malalamiko yapo kila sehemu kwenye hizi taasisi haswa za serikali hata bodi ya mikopo inalalamikiwa mnooo.

Sasa je tunafanyaje?
 
Kama NSSF na PSSSF wameweza kuwa mifuko ya kijamii kwanini HESLB isiweze kuwa mfuko wa kijamii ilhali inaihudumia jamii ya wanafunzi na sio wafanyakazi?...
Kila chombo kinaundwa na sheria na kina majukumu yake mahususi. NSSF na PSSF wao wameweza sababu ni majukumu yao ya kimsingi ndani ya wigo wao, tena kuna mafao kwa wanufaika yanayogusa elimu.


HESLB wao sio jukumu lao, ni bodi ya mikopo yaani wao wanatoa tu funds kwaajili ya wanufaika kwa vigezo vyao, labda utaratibu ubadilishwe kuwezesha wazo lako.
 
Back
Top Bottom