Kwani kuna Cheo chochote kile Mtangazaji Babie Kabae anakitaka ndani ya Serikali ya Rais Samia?

Kwani kuna Cheo chochote kile Mtangazaji Babie Kabae anakitaka ndani ya Serikali ya Rais Samia?

Ila we jamaa ni noma
Na ndiyo tofauti yangu ya GENTAMYCINE na Wengine hapa. Yaani hakuna Silaha kubwa niliyonayo na ninayojivunia kama ya Kujiamini Kitaarifa na Kimaarifa ya kujua Mambo / Masuala mengi ya Kimtambuka. Ukiona napigwa mno Mawe hapa jua HATERS wangu wameshindwa kuvaa Viatu vyangu japo wanapambana nami kila Kukicha.
 
Hehe hapo kwenye bange mie chifu Nyabange nikafurahi tu hiiiii
Tokea nimjue miaka ya kuanzia 1997 hasa nilipokuwa nikila sana Hela zake katika Kipindi chake alichokuwa akikiendesha East Africa Radio alikoanzia ambako alikuwa akiuliza Swali ( hasa ya General Knowledge tu ) na ukishinda unajishindia Hela na Zawadi ya CD ya Nyimbo nilijua alikuwa akiivuta mno tu Bangi / Bange na bahati nzuri hata Wafanyakazi wake wengi wa hiyo Media walikuwa wakilijua hilo na wala halikuwa jambo geni Kwao. Na kati ya Wasikilizaji wake Wakubwa ambao ndiyo tulikuwa tukishinda sana Hela zake katika Kipindi chake hicho nilikuwa ni Mimi GENTAMYCINE, Tija Juma ( TJ ) na Roga Roga.
 
Kweli kabisa, sijui huwa hawajiandai, ila pia general knowledge yao iko chini na hawako updated sana na masuala current. Wakati mwingine wanaulizana maswali wanakosa majibu, na tunategemea wao wenye kipindi ndio wawe na majibu, ukijumlisha na uchawa kipindi kinapoa kabisa. Yule binti unamuona kabisa anaota ateuliwe kila kukicha
Na labda tu nimwambie Kijakazi Yunus ( Kijah ) kuwa atahangaika sana Kujipendekeza kwa Marais wa Tanzania na Wenyeviti CCM Taifa ili ateuliwe nao lakini hiyo bahati hatoipata kamwe kwakuwa ameshashtukiwa kuwa ni Ndumilakuwili ( Mchana CCM na Usiku ni Upinzani ) na hata kama labda kuna Kauteuzi kokote alikapata huko nyuma ndani ya CCM au Serikali ajue ilikuwa ni Ajali / Bahati mbaya tu.
 
Tunachangamoto ya kuwa na mifumo inayotupeleka pabaya kama nchi, tumekuwa na vyombo vya habari vya kichawa na waandishi wasio na weledi hivyo kupelekea kulisha jamii taarifa ambazo ni matango pori. Hii sio afya kabisa hata wanaofaidika kwa sasa kuna muda itakuja kuwa hatari kwao kwani nchi inajenga watu wasio na mwelekeo wowote bali wanafuata matukio tu.
Heko mno Mkuu na nasikitika sana kuona hii Post yako Watu hawajailaiki kwani umetema Madini Tukuka ya Ukweli pia.
 
Back
Top Bottom