Kwani mahari gharama gani?

Kwani mahari gharama gani?

ngombe.jpg
 
Sie kwetu mahari ni hiari ya mzazi. Ila kama mama hakutolewa mahari ndio mwisho wa channel ya mahari so binti atakayeolewa wa uzazi wa huyo mama mahari haitapokelewa na hio familia bali kwa mama mwenye kiporo kwa familia yake.

Mahari huwa ni ngombe jike ambaye hajawahi kuzaa na kondoo jike. Basi.

Utaratibu mwingine ni makubaliano
-Kutoa taarifa au kutangaza kuwa umeona ua kwenye nyumba husika ni kasherehe ka mbege na nyama
- kutambulishwa ndugu. Kapombe kengine inaweza kutenganishwa pia. Wamama. Wababa. Wajomba. Mashangazi. Makaka. Wadada. Kila.moja sherehe yake
- kuna kutangaza au kuomba harusi kasherehe kengine. Hapa pia unaweza kutoa zawadi kwa mama baba mashangazi bibi na kaka za bi mlengwa. Huwa ni panga kanga vitenge mablanketi na kondoo.
- kwa kawaida wazazi na wazee hawahudhurii harusi so inabidi kuwaachia chakula ambacho huwa ni mguu wa ngombe vinywaji na ndizi.
Kama nilivyosema yote haya yanategemeana na familia. Wengi huamua kuishi tu. Ila binti ukifanyiwa hayo familia yako unakotoka wanawapeni baraka sana si unajua tena unawalisha karibia mara 5. Na mumeo akienda kusalimu anaheshimiwa kuliko rais.
Sio jambo rahisi kakini.

Wengi hutoa tu zawadi. Mahari na sherehe moja basi.
Mimi babu mzaa mama alikataa mahari kwa baba so na baba alikataa mahari yangu so. Na mie ni hivyohivyo. Ila mambo mengine yako palepale.
 
Hii kitu inaumiza we acha tu. Wanapiga hesabu ya msosi sahani sh. 20,000. Bia minimum 3 * 100, maji kilimanjaro, juice..dah!! Acha kabisa..! Ukitoka hapo hata sherehe huiwezi tena...na ukianza maisha ya ndoa mifuko imetoboka kabisa.

Halafu baada ya muda unasikia mke wako anachepuka aisee!!
 
ukiona mwenzio ananyolewa za kwako tia maji let me wait after some 5 years na mimi nitanyolewa vipi:A S wink::A S wink::A S wink:
 
Tunakomoana

huu ndio utaratibu wetu. wewe si umeuliza mahari kwetu zikoje? ndo ziko hivi. tena hapo sijakupa mashariti'

1.lazima ng'ombe mmoja awe ana mtoto yaani tayari ana maziwa ili wakifika tu waanze kukamua na kunywa maziwa.

2.lazima ng'ombe wanne wawe makisai ili wakifika tu ukweni wawe na makisai za kulimia.

3.ng'ombe wanajichagulia wenyewe upande wa mke. wewe kazi yako ni kuwaonyesha zizi tu. alafu wanatabia ya kuchagua majike tu yaliyo karibia kupandwa lakini hayajawahi kuzaa ili kwa mfano yakiwa 30 baada ya mwaka majike yote yanazaa na idadi inaongezeka mara dufu.

4.kama ng'ombe huna ila umewanunua mnadani bado watawatathimini ubora wao na wanaweza kuwakataa baadhi kawa hawajaridhika nao. inabidi ukanunue tena

5.na mbuzi wa mjomba lazima,mashangazi nao kuna chao, bibi na babu nao kama kawaida.

karibu usukumani.

huu ni utaratibu tu wala hatumkomoi mtu.
 
Usiombe uoe uchagani au umasaini...utajuta kuzaliwa

Kwa gharama ya maisha haya ya sasa hivi ukioa mchaga wa mjini jiandae kutokwa na kitita kama cha milioni 3 kwenda juu...

milioni tatu mbona haifikishi hata ng'ombe 10? hiyo iko poa tu. ukiibadili na kwenda kununua ng'ombe utakuja na ng'ombe wasiozidi 8 kawa umewanunulia vijijini na kama ni town utakuja na ng'ombe wanne tu.
 
mie najua mtu alielipiwa mahari Tshs 1,000/= tu. Hiyo ilikuwa ng'ombe wanne na mbuzi tatu za wajomba. Hapo mbuzi ya mama ilipelekwa physically na mablanket na vitenge vitatu. Sio kila familia haijastaarabika kaka

duuh. kwingine kote ila siyo usukumani.

huu ni utani.
 
Kwa mzazi ambae anategemea kuwa huyo mkwewe ataendelea kuwa kama mwanae; na kuwajibika kuja na mafurushi ya vyakula wakati anamtembelea. Na hata kusaidia matibabu ama elimu za ndugu na majukumu ya kiafrika. Sidhani kama atadai mahari ya hela nyingi. Roho ya kimaskini tu hiyo, kijana wa watu anakaa nyumba ya kupanga halafu udai mahari milioni mbili?
kwetu usukumani ukiwa umeoa kitamaduni unawajibika moja kwa moja kutatua tatizo ukweni kama utahitajika na hapo ndipo utaojulikana kama wewe ni mkwilima magumashi ama wa ukweli.

swala la ukubwa wa mahali haliangalii kama utakuwa unahitajika kusaidia ama la.

mahali usukumani ni prestige kwa muoaji na muolewaji.

kwa sababu wanaokuoa(wazazi) wakitoa mahali kubwa wanajisikia fahari na familia inapata kuheshimiwa.

pia wazazi wa msichana wanajisikia fahari kama mtoto wao anatolewa mahali ya ng'ombe wengi.
 
huu ndio utaratibu wetu. wewe si umeuliza mahari kwetu zikoje? ndo ziko hivi. tena hapo sijakupa mashariti'

1.lazima ng'ombe mmoja awe ana mtoto yaani tayari ana maziwa ili wakifika tu waanze kukamua na kunywa maziwa.

2.lazima ng'ombe wanne wawe makisai ili wakifika tu ukweni wawe na makisai za kulimia.

3.ng'ombe wanajichagulia wenyewe upande wa mke. wewe kazi yako ni kuwaonyesha zizi tu. alafu wanatabia ya kuchagua majike tu yaliyo karibia kupandwa lakini hayajawahi kuzaa ili kwa mfano yakiwa 30 baada ya mwaka majike yote yanazaa na idadi inaongezeka mara dufu.

4.kama ng'ombe huna ila umewanunua mnadani bado watawatathimini ubora wao na wanaweza kuwakataa baadhi kawa hawajaridhika nao. inabidi ukanunue tena

5.na mbuzi wa mjomba lazima,mashangazi nao kuna chao, bibi na babu nao kama kawaida.

karibu usukumani.

huu ni utaratibu tu wala hatumkomoi mtu.

Mkuu sisi si wafugaji,je watu ambao si kabila lenu inakwaje?utaratibu haubadiliki?
 
Mkuu sisi si wafugaji,je watu ambao si kabila lenu inakwaje?utaratibu haubadiliki?

hapo inategemea sana na mambo yafuatayo.

1.uelewa wa hao wazazi.

2.uelewa wa msichana.

MNAWEZA KUKUBALIANA IDADI YA NG'OMBE MATHALANI 20 ALAFU UKIWA HUNA ZA KUTEMBEA(REAL CATTLE) BASI MNAWEKA KWENYE THAMANI YA PESA.

UKIAMBIWA NG'OMBE MMOJA WA MAHALI ANA THAMANI YA 300,000. MAANA YAKE NI 300,000X20=6,000,000.

KAMA NI 200,000 MAANA YAKE NI 200,000X20=4,000,000.

hapo taratibu zilizobaki pia bado. kwa maana ya bibi,babu,shangazi na mjomba.

ALAFU KWETU UKIWA BADO HUJATOA MAHALI ILA UMECHUMBIA NIKIJA MIMI NIKATOA MAHALI KUKUSHINDA WEWE BASI NAOA MIMI NA WEWE UNAPIGWA CHINI.

LA SIVYO URUDI HARAKA KABLA JAMAA HAJATOA NA WEWE UPANDISHE MAHALI.

MFANO KAMA MLIKUBALINA NG'OMBE 18, MIMI NIKAJA KESHO YAKE NIKAAHIDI KUTOA 22 HAPO NISHAKUPOKA MCHUMBA. KAMA UNAMTAKA INABIDI URUDI HARAKA SANA UAHIDI ZAIDI YA 22MFANO 25.JAMAA AKIONA ANAMHITAJI SANA HUYO BINTI ANAWEZA KURUDI TENA AKAWEKA 30.

TE TE TE TE TE TE HAPO MPAKA JASHO LITAKUTOKA.

UNLESS UMPATE ANAYEPELEKA MAMBO KISASA KUWA MAPENZI NI MLIOKUBALIANA.
 
hapo inategemea sana na mambo yafuatayo.

1.uelewa wa hao wazazi.

2.uelewa wa msichana.

MNAWEZA KUKUBALIANA IDADI YA NG'OMBE MATHALANI 20 ALAFU UKIWA HUNA ZA KUTEMBEA(REAL CATTLE) BASI MNAWEKA KWENYE THAMANI YA PESA.

UKIAMBIWA NG'OMBE MMOJA WA MAHALI ANA THAMANI YA 300,000. MAANA YAKE NI 300,000X20=6,000,000.

KAMA NI 200,000 MAANA YAKE NI 200,000X20=4,000,000.

hapo taratibu zilizobaki pia bado. kwa maana ya bibi,babu,shangazi na mjomba.

ALAFU KWETU UKIWA BADO HUJATOA MAHALI ILA UMECHUMBIA NIKIJA MIMI NIKATOA MAHALI KUKUSHINDA WEWE BASI NAOA MIMI NA WEWE UNAPIGWA CHINI.

LA SIVYO URUDI HARAKA KABLA JAMAA HAJATOA NA WEWE UPANDISHE MAHALI.

MFANO KAMA MLIKUBALINA NG'OMBE 18, MIMI NIKAJA KESHO YAKE NIKAAHIDI KUTOA 22 HAPO NISHAKUPOKA MCHUMBA. KAMA UNAMTAKA INABIDI URUDI HARAKA SANA UAHIDI ZAIDI YA 22MFANO 25.JAMAA AKIONA ANAMHITAJI SANA HUYO BINTI ANAWEZA KURUDI TENA AKAWEKA 30.

TE TE TE TE TE TE HAPO MPAKA JASHO LITAKUTOKA.

UNLESS UMPATE ANAYEPELEKA MAMBO KISASA KUWA MAPENZI NI MLIOKUBALIANA.

Kwa mtindo huu usukumani hatuoi
 
Kwa mtindo huu usukumani hatuoi

sisi ndio utaratibu wetu na tushauzoea wala hautupi tabu.

kama huna kabisa mahari inabidi umtafte demu umsaundishe akubali kutoroshwa.

ukimtorosha ni kosa.

wanachofanya kuna kitu utatoa lakini siyo mahali tena kinaitwa MCHENYA/NCHENYA (FAINI)

faini huwa ni ng'ombe wawili tu.

HAPO WAKIFIKA HAKUNA CHA MJADALA NI LAZIMA UTOE NG'OMBE WAWILI NA WAKIJA WANAKUJA KWA MKWALA USIO WAKAWAIDA NA KAMA WEWE HUJUI UNAWEZA KUMTELEKEZA MKE KWA KUOGOPA.

ukishatoa faini hiyo si kwamba umemuoa huyo mwamke.

kinachotokea kwa kawaida unatakiwa ukae chini na wazazi mpnge mahali ya mke wako ili uweze kupata haki zote.

usipolipa mahali wao wanasema GUKWA.

kuna hasara hizi.

watoto wote utakaoza na mwanamke si wa kwako bali ni wa upande wa mwanamke mpaka utakapomlipia mahali mama yao.

THIS IS WHAT YOU CAN AFFORD VINGINEVYO HUWEZI KWELI KUPATA MKE USUKUMANI
 
Tuambizane basi posa/mahari huwa ni kiasi gasi kwa kabila yenu?maana suala la kuoa huwa huwezi kukwepa utaratibu wa kikabila.

Mnapokea viumbe wanaohema wangapi kama mbuzi, kuku, ng'ombe, kondoo?
Kabila langu dume la ng'ombe mmoja (hata awe mdogo), ndama mmoja,kondoo wawili.

Inavyoonekana wasukuma na wamasai wana dau kubwa,sijui kama wahaya, wangoni, wasambaa, warangi, wambulu,wameru,wanyamwezi,waluguru, wazaramo, wachaga, wapare,wazanaki, wamakonde etc.

Naomba kujua kabila lenu mahari ni kiasi gani,je hao wanaotaka ng'ombe wengi msichana wao akikutana na kijana wa kizaramo(mfano),hiyo rules za mahari hawabadilishi?

hawa wote hawana tofauti kuanzia mila desturi ,lugha . wote tupo sawa.

na kimsingi wanyamwezi ni wasukuma. sema jina la wasukuma ndio lilipita ama kuwa maarufu zaidi.

likafatiwa la mnyamwezi.

kuna majina mengine huezi kuyasikia kwingine zaidi ya wasukuma wanaojua.

KUNA WATU WANAITWA
1.WASUKUMA(WATU WA KASIKAZINI)
2.WADAKAMA(WATU WA KUSINI=WANYAMWEZI)
3.WANANG'WELI(WATU WA MAGHARIBI)
4.WANAKIYA(WATU WA MASHARIKI)


HAWA WOTE COLLECTIVELY NI WASUKUMA.
 
Kwetu sisi ni NG'OMBE wasiopungua watano na hapo umehurumiwa ila ss kuna vitu vingine pembeni Ng'ombe mmoja wa kuchiza siku ya harusi huyu hahesabiki ktk wale watano, utapeleka unga gunia moja, blanket ya baba na sufuria ya mama.
 
...........

kuna majina mengine huezi kuyasikia kwingine zaidi ya wasukuma wanaojua.

KUNA WATU WANAITWA
1.WASUKUMA(WATU WA KASIKAZINI)
2.WADAKAMA(WATU WA KUSINI=WANYAMWEZI)
3.WANANG'WELI(WATU WA MAGHARIBI)
4.WANAKIYA(WATU WA MASHARIKI)


HAWA WOTE COLLECTIVELY NI WASUKUMA.

huwa natamani sana kusikia elimu kama hizi huwa ni kwa nadra sana, asante ndugu yangu
 
inategemea na familia kuna wengine hawafwati mambo ya wazee.....unanunua blanket la mama/baba na zwadi kidogo mnapokea baraka za kwenda kuanza maisha.....kuna jirani yangu kijana wake ameleta mchumba toka kenya mahari jumla 10m mama alimwaga chozi ukizingatia baba alishatangulia mbele za haki kuna makabila mengine mahari kukomoana kama vile unamuuza
 
Back
Top Bottom