Kwani mngegomea, mngepungukiwa na nini?

Kwani mngegomea, mngepungukiwa na nini?

Duh!

Yaani baada ya miaka 14 hapa JF na mabandiko zaidi ya 80K, ni mada yangu moja tu ndo umeikubali?

Ina maana huwa naandika pumba nyingi sana? [emoji1787][emoji1787]

Anywho, utani pembeni, hili suala nimeanza kulizungumzia kwa muda mrefu sana.

Bahati mbaya wahusika wenyewe ni watu wenye vichwa vigumu sana.

Waache tu waendelee kujipotezea muda, la, watakuwa ni wamendea ruzuku na si watu wa kusimamia kanuni.
Viongozi wa Upinzani sio kwamba Wana vichwa vigumu hapana,Ni ubinfsi ndio unafanya waonekane Wana vichwa vigumu
 
Sawa.

Wafanye wanavyotaka basi.

Mimi kamwe sitojihangaisha na kupiga kura chini ya haya mazingira. Kamwe daima!

Nyie anzeni kujipanga kwa ajili ya 2025 [emoji1787][emoji1787].
Bila Tume huru au katiba mpya uchaguzi wa mwaka huu ndio ulikuwa wa mwisho mie kupiga kura.
 
Haondoki huyu. Katiba inakwenda badilishwa. Kisingizio ni ili amalizie miradi yake.
Walishasema..... ‘atake asitake’!

Yeye anaweza kujifanya kukataa ila mwisho wa siku by early 2024 atakubali baada ya ‘kuombwa sana’ na wazee na viongozi wa dini. Kagame style!
 
Sawa.

Wafanye wanavyotaka basi.

Mimi kamwe sitojihangaisha na kupiga kura chini ya haya mazingira. Kamwe daima!

Nyie anzeni kujipanga kwa ajili ya 2025 🤣🤣.
Kwa bahati mbaya mimi sio mwanachama wa chama chochote na wala sina mpango wa siasa nilishaona upuuzi tokea zamani.
 
Wapinzani Kuna wakati tunakwamishwa na viongozi wetu,dalili zote toka uchaguzi wa Serikali za Mitaa zilikuwa zinaonyesha bila katiba mpya bila tume huru ya uchaguzi Basi hakuna uchaguzi huru na wa haki ungefanyika.Sasa Kwanini viongozi walijitoa uchaguzi serikali za Mitaa lkn uchaguzi mkuu hawakujitoa?Viongozi wetu Ni wabinafsi.
Siyo uchaguzi wa serikali za mitaa tu.

Kama ulikuwepo 2010 na 2015, wapinzani hawa hawa waliyakataa matokeo.

Hawakuwa na imani na tume.

Lakini cha kustaajabisha, huwa wanayakataa matokeo na kusema kuwa tume si huru, lakini muda wa uchaguzi ukifika wanashiriki tena.

Na wanashiriki chini ya mazingira yale yale.

Kama huamini, subiri uone 2025 watafanya nini.

Mimi natabiri kuwa watashiriki tena na itakuwa kwenye mazingira haya haya yaliyopo sasa hivi.

Halafu matokeo yakishatangazwa, watasema hawayatambui.

Tuombeane uzima tu ili tuwepo hiyo 2025 ili tuweze kukumbushana.
 
Kwa bahati mbaya mimi sio mwanachama wa chama chochote na wala sina mpango wa siasa nilishaona upuuzi tokea zamani.
Good for you!

Kuendelea kushiriki chaguzi za maigizo ni uwendawazimu.
 
Wamekosa kila kitu iwe bara au visiwani.sasa wale wa visiwani hawajawai kupata uwakilishi toka walivyosusa wenzao wakala na mwaka huu wameshiriki na wamekosa kila kitu.
 
Swali kwa wapinzani.

Kwani mngegomea kushiriki haya maigizo ya uchaguzi wa 2020, mngepungukiwa na nini?

Na hivi mlivyoshiriki, mme-gain nini?

Mimi msimamo wangu uko wazi. Unajulikana.

Hakuna kushiriki chaguzi za maigizo ambazo mtu hauhitaji hata uwe genius kujua matokeo yake yatakuwaje.

Kushiriki chaguzi za hivyo, chaguzi za kutimiza wajibu tu, ni umajinuni.

Baadhi yenu mmetaja chaguzi za serikali za mitaa mwaka jana ambapo wapinzani walizisusia.

Kwanza, chaguzi za serikali za mitaa si sawa na uchaguzi mkuu.

Pili, migomo ya kushiriki chaguzi za maigizo ni lazima iwe endelevu.

Kama mwaka jana mligoma na CCM wakajipa ushindi wote, mwaka huu mmeshiriki na mmeambulia nini zaidi ya kipigo cha mbwa?

Zigomeeni hizo chaguzi. Wekeni mashinikizo mpaka zipatikane taasisi zilizo huru za kusimamia na kuendesha chaguzi.

La sivyo, mtaendelea kutegemea hisani ya CCM kupata ushindi.

Na siku mkikutana na jitu lenye roho mbaya, hata hizo nafasi chache mnazoshindaga, mtanyimwa.

Na jinsi mlivyo na vichwa vigumu, si ajabu mkaanza ule upuuzi wenu wa twende na Shangazi 2025.

Bure kabisa.
Asiekubali kushindwa sio mshindani! Kubalini mmepigwa kipigo kitakatifu, msijifariji bure! Laana ya kumkimbatia lowasa kisa vihela na kumuacha Slaa aliyeijenga chadema ikaonekana!
 
Ta
Wamekosa kila kitu iwe bara au visiwani.sasa wale wa visiwani hawajawai kupata uwakilishi toka walivyosusa wenzao wakala na mwaka huu wameshiriki na wamekosa kila kitu.
Tatizo huko visiwani wanataka sultan arudi, ccm hatuwezi kukubali toka tulivyofanya mapinduzi matukufu!
 
Makamanda ni Wajinga sana hawaelewi wanachotaka kabisa hawana long term plan zaidi ya kukurupuka sasa acha wavune walichopanda, walio soma soma watafute kazi za kufanya
 
Ndugu yangu Nyani kugoma sio suluhisho kabisaaaa maana wakina Sipunda na shibuda watashiriki ikiwezekana watapewa na wabunge 10 kila mmoja ili kuonyesha demokrasia ipo kama ilivyokua zanzibar

Nakubaliana na wewe pia kuendelea kushiriki chaguzi kwenye mazingira haya nayo ni sawa na sifuri maana ccm wana means zote za kupora kura

Tunahitaji njia bora zaidi ya kususia.........watasusia cdm labda act tu halafu vyama mamluki 20 vitashiriki, mwisho wa siku chama kitakosa hata uwezo wa kujiendesha au kifutwe kabisa kama ambavyo kimefanyiwa kwenye uchaguzi huu

NGUVU YA UMMA NDIO SULUHISHO PEKEE......AMINI NAKWAMBIA
 
Ndugu yangu Nyani kugoma sio suluhisho kabisaaaa maana wakina Sipunda na shibuda watashiriki ikiwezekana watapewa na wabunge 10 kila mmoja ili kuonyesha demokrasia ipo kama ilivyokua zanzibar

Nakubaliana na wewe pia kuendelea kushiriki chaguzi kwenye mazingira haya nayo ni sawa na sifuri maana ccm wana means zote za kupora kura

Tunahitaji njia bora zaidi ya kususia.........watasusia cdm labda act tu halafu vyama mamluki 20 vitashiriki, mwisho wa siku chama kitakosa hata uwezo wa kujiendesha au kifutwe kabisa kama ambavyo kimefanyiwa kwenye uchaguzi huu

NGUVU YA UMMA NDIO SULUHISHO PEKEE......AMINI NAKWAMBIA
Sawa.

Mimi sijasema kugoma ndo suluhisho pekee au mwarobaini.

Kugoma ni sehemu tu ya harakati. Ni sehemu ya mapambano.

Na ukigoma leo haina maana kesho utapata unachokitaka.

Licha ya hivyo, acha waendelee kushiriki tuone kama watapata chochote kilicho cha maana....

Maana mimi Ngabu ni kilaza tu niliyeishia kidato cha nne. Sina nilijualo.
 
U

Umma upi? je Wa Ccm sio Umma? Maana mashabiki na wanachama wa Ccm ndio wengi zaidi ya vyama pinzani je wa Ccm wakiandamana (nguvu ya Umma) kuunga mkono serikali 😁 au Neno nguvu ya umma ni mali tu ya upinzani?
Kwa muktadha wako huu unadhani watu kama akina Gadafi na wenzake walioondolewa kwa nguvu ya umma unajua walikua na wafuasi kiasi gani?

Umewahi kujiuliza hivi wale uliojua unawaona wanamshangilia lissu kwenye mikutano yake wakiamua kiandamana itakuaje?
 
Siyo uchaguzi wa serikali za mitaa tu.

Kama ulikuwepo 2010 na 2015, wapinzani hawa hawa waliyakataa matokeo.

Hawakuwa na imani na tume.

Lakini cha kustaajabisha, huwa wanayakataa matokeo na kusema kuwa tume si huru, lakini muda wa uchaguzi ukifika wanashiriki tena.

Na wanashiriki chini ya mazingira yale yale.

Kama huamini, subiri uone 2025 watafanya nini.

Mimi natabiri kuwa watashiriki tena na itakuwa kwenye mazingira haya haya yaliyopo sasa hivi.

Halafu matokeo yakishatangazwa, watasema hawayatambui.

Tuombeane uzima tu ili tuwepo hiyo 2025 ili tuweze kukumbushana.
Nilikuwa Mjinga mwaka huu kushiriki uchaguzi lakini stakuwa Mjinga Tena kushiriki uchaguzi mwingine wowote Kama Mazingira ya uchaguzi Ni hayahaya
 
Nilikuwa Mjinga mwaka huu kushiriki uchaguzi lakini stakuwa Mjinga Tena kushiriki uchaguzi mwingine wowote Kama Mazingira ya uchaguzi Ni hayahaya
2015 na 2010 hukushiriki?

Na ulikuwa hujui kuwa mwenyekiti wa CCM ndo huunda tume ya uchaguzi?
 
Nyani ngabu toka huko USA njoo njoo uishi na sisi hapa Miaka 5(Wala vumbi) ndio tutaelewana

Ukisemea kwa huko hatukuelewi unapiga kelele tu[emoji2][emoji3577]
 
Ushauri wako wa kwenye keyboard ni tofauti kabisa na hali halisi. Hata huyu diktekta uchwara alikuwa ame-set mambo ili wapinzani wagomee.

Alishaandaa na wapinzani bandia ili washiriki kwenye uchaguzi wa bandia na wapewe viti vichache. Hali ilikuja badilika pale alipokuja Lissu na kubadilisha upepo hivyo ikabidi technics zibadilike.

Kuhusu upinzani umepata nini kwa kushiriki uchaguzi well mimi nadhani watanzania wote na Magufuli mwenyewe wamejua hali halisi ya wananchi wanaionaje serikali ya Magufuli. Nadhani hata Magufuli mwenyewe ameshangaa jinsi alivyokataliwa pamoja na kudhani anapendwa sana.

Kwa kifupi hisia za wananchi zimejionyesha hadharani. Hii inaweza kutumia kama foundation ya kudai tume huru japo kwa namna navyowajua watanzania walivyo waoga kuwa-convince waingie barabarani ni ngumu mno.
Kuna watu huwa mnaandika vitu ili mradi umeandika tu
 
Back
Top Bottom