Kwanini Africa ukifikisha 35, 45, 55, tunasema ni mzee?

Kwanini Africa ukifikisha 35, 45, 55, tunasema ni mzee?

Sio Africa pekee, hata ulaya, marekani na kwingineko iko hivyo.

Nafasi ya mtu katika jamii ndio husababisha awekwe kwenye kundi flani.

Kuna aina flani ya nafasi zinataka watu wenye umri mdogo. Hivyo ukifikisha tu miaka 30 unaitwa mzee kwa sababu huko ni kwa watu wenye umri mdogo. Mfano kwenye mpira, ukifikisha 30 wewe tayari ni mzee. Christiano ronaldo, messi na wengine wanaitwa wazee kwa sababu ya nature ya mpira.

Pili, kwenye mafanikio ya kiuchumi, hapa mara nyingi watu hupata ukwasi wa maana wakiwa wazee, mostly above 55 years walau ndio unaanza. Ndio maana Elon musk, Mo dewji waanaitwa vijana sababu wamepata fedha mapema zaidi kabla ya umri uliozoeleka wa watu wengi kupata mafanikio ya kiuchumi. Search orodha ya mabilionea duniani halafu angalia umri wao, majority wako 70+. Kumbuka msemo wa life starts at 40, miaka arobaini ndio unaanza kujitafuta sasa then unakuwa na interval ya miaka 15 hapo mbele ya kustabilize. Ukiwa bilionea chini ya hapo wewe utaitwa kijana tu.

Pia, kwenye siasa. Normally umri wa kushika nyadhifa za juu zaidi za kiuongozi kisiasa zinakuwa miaka 50+. Ndio maana Obama kuwa rais akiwa na 48 alionekana kijana. Vipi kama angetaka kucheza mpira kwa umri huo, je bado angeitwa kijana? Mwana FA amekuwa naibu waziri akiwa na 40+. Huyu anaitwa waziri kijana kwa sababu umri wake kisiasa bado ni mdogo. Lakini vipi kama mwanaFA akirudi kwenye bongo flava, utakuwa na guts za kumwita kijana bado?
Mkuu umeelezea vizuri sana.
 
Obama alianza uraisi akiwa 48 yrs na tulimuuita kijana.

Elon Musk ana 53, tajiri mkubwa namba moja duniani, tunamuuita kijana
Mark Zuckerberg ana 39, tajiri mkubwa tunamuita kijana

Kwanini Africa ukifikisha 35, 45, 55, tunasema ni mzee?

Nataka, kutoa somo moja Leo. Chanzo kingine cha Africa kuwa maskini ni kudharau watu wenye mkubwa.

Ni kawaida, mwanadamu anapifikisha 50 yrs, huwa anakuwa.

Kwenye ukomavu na utimamu wa akili. Chini ya hapo ni kubahatisha.

Viongozi wengi kwenye mashirika, makampuni, nchi huwa kwenye huo umri kuanzia 50-70 yrs.

Huwezi kupata maendeleo kwa kujaza uongozi kwenye kampuni, shirika, nchi watu wenye umri chini ya hamsini. Huo ni utani. Hutapata maendeleo.

Nchi zilizoendelea wanalijua hilo ndiyo maana labour tegemezi ni hiyo miaka.

Chini ya hapo mtu anakuwa Hana experience ya Mambo mengi hence makampuni mengi hayakuwi au kufilisika kabisa

Binadamu mwenye miaka kuanzia 50-70, anakuwa na uwezo mkubwa sana wa ki akili

Hata chunguza, wagunduzi wengi zamani walifanya ugunduzi wakiwa ni hiyo miaka.

Ni wachache walifanya maajabu chini ya hiyo miaka. Tukijaza watoto kwenye maendeleo ya jamii yetu ni hatari mno. Hatuwezi
Kusonga, mbele kama jamii

Old is Gold
Kweli kabisa Mtu ana miaka 50 hapa Tanzania wanasema ni mzee, hata kidogo! Uzee ni miaka 76 na kuendelea.

1. 0-17 Mtoto
2. 18-50 Kijana
3. 51-75 Mtu mzima
4. 76> Mzee
Naelewa Africa watu wanawaona wenye miaka 50 kuwa wazee kwasababu ya age profile ya Africa ambapo watoto na vijana chini ya 35 ni wengi kuliko makundi mengine.
 
Sasa wewe kjana ana miaka 16 anaanza kupiga kamunyweso ka smart gin mixer na gongo, mo energy anashushia na ugoro . Bado pia pia zake kageuza ekzosi ya ist muda wote zinatoa Moshi wa bange, sigara na gozo, utegemee mpaka afike 20 atakua bado kjana. Saivi vijana wanaonekana wazee sababu ya mtindo mbovu wa maisha. Kjana unakuta kavimba mashavu na pia yamelegea sababu ya pombe Kali. Midomo imeunguzwa na sigara.
Wacha niishie hapa tu
 
Kwa mfano Finland old age sio 70 tena , sababu watu wenye miaka 70 wako ngangari haswa. Uzee unatokana na maisha mabovu.
 
Sifa kubwa ya uzee ni kitambi.Ukiwa na kitambi hata kama una 25 utaitwa mzee.Hao waliotajwa hapo kina Obama hawakuwa/hawana na vitambi
 
Obama alianza uraisi akiwa 48 yrs na tulimuuita kijana.

Elon Musk ana 53, tajiri mkubwa namba moja duniani, tunamuuita kijana
Mark Zuckerberg ana 39, tajiri mkubwa tunamuita kijana

Kwanini Africa ukifikisha 35, 45, 55, tunasema ni mzee?

Nataka, kutoa somo moja Leo. Chanzo kingine cha Africa kuwa maskini ni kudharau watu wenye mkubwa.

Ni kawaida, mwanadamu anapifikisha 50 yrs, huwa anakuwa.

Kwenye ukomavu na utimamu wa akili. Chini ya hapo ni kubahatisha.

Viongozi wengi kwenye mashirika, makampuni, nchi huwa kwenye huo umri kuanzia 50-70 yrs.

Huwezi kupata maendeleo kwa kujaza uongozi kwenye kampuni, shirika, nchi watu wenye umri chini ya hamsini. Huo ni utani. Hutapata maendeleo.

Nchi zilizoendelea wanalijua hilo ndiyo maana labour tegemezi ni hiyo miaka.

Chini ya hapo mtu anakuwa Hana experience ya Mambo mengi hence makampuni mengi hayakuwi au kufilisika kabisa

Binadamu mwenye miaka kuanzia 50-70, anakuwa na uwezo mkubwa sana wa ki akili

Hata chunguza, wagunduzi wengi zamani walifanya ugunduzi wakiwa ni hiyo miaka.

Ni wachache walifanya maajabu chini ya hiyo miaka. Tukijaza watoto kwenye maendeleo ya jamii yetu ni hatari mno. Hatuwezi
Kusonga, mbele kama jamii

Old is Gold
Uzee na ujana mara nyingine ni kitu relative ambacho kinaendana na life expectancy pamoja na demographics za nchi.

Katika nchi ambayo life expectancy ni miaka 50, na asilimia 90 ya watu wake wako chini ya miaka 40, ukiwa na miaka 40 wewe ni mzee.

Katika nchi ambayo life expectancy ni miaka 90, na 40% ya wananchi wake wana miaka chini ya 40, kuwa na miaka 40 si mzee.

Huko Afrika watu wanaonekana wazee mapema kwa sababu life expectancy ni ndogo halafu population zina watoto wengi.

Ukiwa wewe mtu mmoja una miaka 45 katika kundi la wengine watoto watoto 99 wenye miaka chini ya 18, utaitwa mzee tu.

Ukiwa wewe mmoja mwenye miaka 45 umekaa kundi la watu wengine 99 waliozidi miaka 70, utaitwa kijana tu.
 
Inategemea ujue kuna watu wanamiaka 20 Ila wanonekana Kama wana 40 yrs

Ukija katika Hoja yako kuwa watu wenye umri mkubwa wana akili zilizokomaa labda ulaya na sio Tanzania
 
What does it matter ni life Expectancy ya nchi husika au sehemu husika,, kwa Tanzania kuitwa mzee katika hiyo age ni kitu cha kawaida kabisa,, kwa sababu ukiangalia life Expectancy ya Tanzania ni below 70 kwa asilimia kubwa.

And the rest ni kwamba watoto na vijana wenye age below 40 ni wengi ukilinganisha na kundi lingine.
 
Mtoto ndio anaweza kumuita au kumuona mtu mwenye miaka 35/45/55 mzee.
Hata mimi nilipokuwa mdogo baba yangu wakati ana 40s nilkuwa namuona mzee.
[emoji3581][emoji3581][emoji3581]
 
Back
Top Bottom