Kwanini app za mikopo ya mtandaoni zinatumia picha za wanawake warembo kutangaza biashara zao?

Kwanini app za mikopo ya mtandaoni zinatumia picha za wanawake warembo kutangaza biashara zao?

Hawa jamaa ni kausha damu kweli kweli, nilikopa nikarudisha kwa wakati zaidi ya mara tano sikupandishiwa kiwango zaidi ya wao kuwa na riba kubwa...nikaona ngoja na mimi niwatese nikakopa karibu aplication nne na zote sikulipa ....kilichotokea wakaanza kuwasumbua watu wangu wa jirani.. aisee niliwapandia hewani nikawaambia siwalipi kwa demage mlionifanyia ....wanajua kusumbua aiseee nilichofanya nikablock incoming unknown call zote na msg at the end waliacha kunisumbua zaidi ya kutuma msg za kunipa offer kwamba wameniongezea kiwango cha kukopa nilipe deni nipate double hahaha nabaki nacheka tu wanajua me mjinga labda nitalipa🤣🤣🤣
Kwa wateja aina yako ku-survive lazima wawe kausha damu. Watanzania wengi si waaminifu wanakopa halafu wanaingia mitini halafu vijana wanalalamika hatuna mitaji. Mitaji ni mikopo ambayo mkikopa hamtaki kulipa.
 
Kuna njia mbalimbali zimeanza kutumika kwa sasa wameanzia ngazi ya elimu. Juzi April 1 walizindua shindano rasmi kwa baadhi ya vyuo vyenye kozi za kifedha kwa kushirikiana na Tanzania Institute of bankers (TIOB) shindano linatomtaka mwanafunzi awe na uelewa kuhusiana na athari za mikopo hiyo nadhani litaisha july 7 mwaka huu kwa baadhi ya wanavyuo walio hapa watakua wananielewa.

Mbali na hiyo Benki Kuu ya Tanzania (BOT) imezindua rasmi mtaala wa wakufunzi wa elimu ya fedha nje ya mfumo rasmi ambapo wananchi watapata elimu ya matumizi sahihi ya fedha ikiwemo akiba ili kuepuka mikopo umiza na kausha damu.

Wizara ya Fedha kupitia Benki Kuu ya Tanzania kwa sasa wanashirikiana vyema na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania, Makampuni ya simu na Polisi ili kuona namna ambayo wanaweza kulitatua suala hili la udhalilishaji linalofanywa na watoa huduma za fedha kupitia mitandao ya simu

Pia Wizara ya Fedha kupitia Benki Kuu ya Tanzania hivi karibuni itaendesha kampeni kupitia vyombo vya habari na njia mbali mbali za kutoa elimu kwa umma ili kujenga uelewa kwa wananchi na watoa huduma ndogo za fedha kuhusu masuala muhimu ya kuzingatia katika utoaji na upatikanaji wa huduma ndogo za fedha nchini
 
Kwa wateja aina yako ku-survive lazima wawe kausha damu. Watanzania wengi si waaminifu wanakopa halafu wanaingia mitini halafu vijana wanalalamika hatuna mitaji. Mitaji ni mikopo ambayo mkikopa hamtaki kulipa.
Bado kuna utata;

Wanajua huwezi kutegemea uaminifu wa mkopaji kurejesha mikopo,

Sasa kwanini wasifanye kama zile kampuni za kukopesha simu, usipolipa simu inajigomea

Mimi nakubaliana na waliosema huu ni mradi wa kutakatisha pesa
 
Kwa wateja aina yako ku-survive lazima wawe kausha damu. Watanzania wengi si waaminifu wanakopa halafu wanaingia mitini halafu vijana wanalalamika hatuna mitaji. Mitaji ni mikopo ambayo mkikopa hamtaki kulipa.
Nilikuwa mlipaji mzuri tena kwa wakati..kilichotokea ni kwamba zaidi ya mara tano hawaniongezei kiwango na niliwalalamikia wakadai wanalifanyia kazi but hakukuwa na chochote
 
Uzuri wa makampuni hayo na wateja wake mnaendana....si unaona? Lazima wawe na riba kubwa maanake wateja wenyewe ndio nyinyi.
Ukikopa branch, mpaka wakupe laki, wanakua wameshakula laki mbili zako kwa riba.
Kwa maana hiyo, wakikufikishia laki tano, kanunue bia unywe, huku ukisubiri simu za matusi na kudhalilishwa kupitia phone book yako.
 
Ukikopa branch, mpaka wakupe laki, wanakua wameshakula laki mbili zako kwa riba.
Kwa maana hiyo, wakikufikishia laki tano, kanunue bia unywe, huku ukisubiri simu za matusi na kudhalilishwa kupitia phone book yako.
Nadhani branch watakuwa wamenisamehe 150k yao maana kwa riba zile tumelipana juu kwa juu
 
B.O.T wako kwenye mchakato wa kuyamaliza haya... Kuna wakati nawaza watu kama hawa walipewaje leseni za biashara pasipo BOT kusoma mikataba yao iliyosheheni vigezo na masharti
Wengi hawana leseni.
 
Usipolipa hawana countermeasures zozote?

wanakuacha tu?
Ukiwa hujui Sheri wanakomaa na wewe.
Wao wanatumia askari kwa posho kiasi, ila mkisimama mahakamani hawana vibari, na unawashinda.
Nilifanya research kwa kampuni moja inaitwa TARA 2019. Sikuwalipa mpaka leo bado wanatuma sms za vitisho. Wakipiga nawaambia wanipeleke mahakamani wanasonya😁
 
Hivi mwanamke mrembo ni lazima awe na matako makubwa?

Binafsi sikubaliani eti urembo wa mwanamke upo katika matako makubwa
Hahahah !
Ni kweli wengine si warembo na hawana matako makubwa,
hizo picha walizoweka ni urembo na matako vimehusika muheshimiwa ila

hata kuongeza tako kwa mwanamke ni urembo .

Nje ya yote,nielekeze rafiki nikakope nisafishe macho kwa hao wakopaji huenda nikawakuta hao warembo ila kama watakuwa na uzuri nitafurahi zaidi.😅
 
Back
Top Bottom