Kwanini baadhi ya vitabu vimetolewa katika biblia?

Kwanini baadhi ya vitabu vimetolewa katika biblia?

jf user

JF-Expert Member
Joined
Aug 22, 2018
Posts
777
Reaction score
623
Biblia ni kitabu kinachojumuisha vitabu mbalimbali vilivyoandikwa na watu mbalimbali katika nyakati tofauti na sehemu tofauti.

Biblia ni mkusanyiko wa hivi vitabu ambavyo viliandikwa na waandishi mbalimbali kisha vikapangwa katika mtiririko unaofaa kuanzia miaka ya mwanzo kabisa hadi ya mwisho (Mwanzo hadi ufunuo).

Kitabu cha kwanza kwenye biblia ni Mwanzo ambacho kinaelezea uumbaji wa hii dunia, binadamu wa kwanza na habari za awali kabisa za dunia na ulimwengu. Kitabu cha mwisho ni Ufunuo Kilichoandikwa na Yohane Mbatizaji.

Hivi vitabu viliandikwa katika lugha ya kiebrania eneo la mashariki ya kati na sehemu za kaskazini mwa Africa (Misri, Ethiopia, Libya n.k) kwa sababu ndipo MUNGU alipopachagua ili neno na habari zake zisambae sehemu nyingine za ulimwengu.

Biblia imeanza kutumika rasmi baada ya kuondoka kwa Yesu Kristo ila maandiko yalikua yamehifadhiwa hata kabla ya Kristo kuja duniani.

Shida yangu ni hii
1/Kwanini vitabu kadhaa vitolewe kwenye biblia kwa misingi ya mawazo ya watu? Kama maandiko yanaonya kuongeza au kupunguza neno la MUNGU kwanini binadamu wanatoa hivyo vitabu?

2/Kitabu cha Enoch kimeondolewa, vitabu vya deuteron kanoni vinatumiwa na Roman Catholic ila Protestant na makanisa mengine hayavitumii! Injili ya Thomas, Bikira Maria, Injili ya Yuda, Injili ya Barnabas, Injili ya Eva na vitabu vingine vingi?

Ni kwanini hivi vitabu vitolewe wahusika hawakuona wanakwenda kinyume na maandiko ya MUNGU?
 
Biblia ni kitabu kinachojumuisha vitabu mbalimbali vilivyoandikwa na watu mbalimbali katika nyakati tofauti na sehemu tofauti.
Biblia ni mkusanyiko wa hivi vitabu ambavyo viliandikwa na waandishi mbalimbali ksha vikapangwa katika mtiririko unaofaa kuanzia miaka ya mwanzo kabisa hadi ya mwisho (Mwanzo hadi ufunuo).

Kitabu cha kwanza kwenye biblia ni Mwanzo ambacho kinaelezea uumbaji wa hii dunia, binadamu wa kwanza na habari za awali kabisa za dunia na ulimwengu. Kitabu cha mwisho ni Ufunuo Kilichoandikwa na Yohane Mbatizaji.

Hivi vitabu viliandikwa katika lugha ya kiebrania eneo la mashariki ya kati na sehemu za kaskazini mwa Africa (Misri, Ethiopia, Libya n.k) kwa sababu ndipo MUNGU alipopachagua ili neno na habari zake zisambae sehemu nyingine za ulimwengu.
Biblia imeanza kutumika rasmi baada ya kuondoka kwa Yes Kristo ila maandiko yalikua yamehifadhiwa hata kabla ya Kristo kuja duniani.


Shida yangu ni hii
1/Kwanini vitabu kadhaa vitolewe kwenye biblia kwa misingi ya mawazo ya watu? Kama maandiko yanaonya kuongeza au kupunguza neno la MUNGU kwanini binadamu wanatoa hivyo vitabu?
2/Kitabu cha Enoch kimeondolewa, vitabu vya deuteron kanoni vinaumiwa na Roman Catholic ila Protestant na makanisa mengine hayavitumii! Injili ya Thomas, Bikira Maria, Injili ya Yuda, Injili ya Barnabas, Injili ya Eva na vitabu vingine vingi?
Ni kwaninihivi vitabu vitolewe wahusika hawakuona wanakwenda kinyume na maandiko ya MUNGU?
Kuficha ukweli
 
Biblia ni kitabu kinachojumuisha vitabu mbalimbali vilivyoandikwa na watu mbalimbali katika nyakati tofauti na sehemu tofauti.
Biblia ni mkusanyiko wa hivi vitabu ambavyo viliandikwa na waandishi mbalimbali ksha vikapangwa katika mtiririko unaofaa kuanzia miaka ya mwanzo kabisa hadi ya mwisho (Mwanzo hadi ufunuo).

Kitabu cha kwanza kwenye biblia ni Mwanzo ambacho kinaelezea uumbaji wa hii dunia, binadamu wa kwanza na habari za awali kabisa za dunia na ulimwengu. Kitabu cha mwisho ni Ufunuo Kilichoandikwa na Yohane Mbatizaji.

Hivi vitabu viliandikwa katika lugha ya kiebrania eneo la mashariki ya kati na sehemu za kaskazini mwa Africa (Misri, Ethiopia, Libya n.k) kwa sababu ndipo MUNGU alipopachagua ili neno na habari zake zisambae sehemu nyingine za ulimwengu.
Biblia imeanza kutumika rasmi baada ya kuondoka kwa Yes Kristo ila maandiko yalikua yamehifadhiwa hata kabla ya Kristo kuja duniani.


Shida yangu ni hii
1/Kwanini vitabu kadhaa vitolewe kwenye biblia kwa misingi ya mawazo ya watu? Kama maandiko yanaonya kuongeza au kupunguza neno la MUNGU kwanini binadamu wanatoa hivyo vitabu?
2/Kitabu cha Enoch kimeondolewa, vitabu vya deuteron kanoni vinaumiwa na Roman Catholic ila Protestant na makanisa mengine hayavitumii! Injili ya Thomas, Bikira Maria, Injili ya Yuda, Injili ya Barnabas, Injili ya Eva na vitabu vingine vingi?
Ni kwaninihivi vitabu vitolewe wahusika hawakuona wanakwenda kinyume na maandiko ya MUNGU?
Niliwahi kugusia kidogo kuhusu hili swala la kwanini baadhi ya vitabu viliachwa na kama kuna siri tunafichwa embu pitia humu uone maoni ya wadau utapata mawili matatu

Siri iliyofichwa kuhusu BIBLIA - JamiiForums
 
Niliwahi kugusia kidogo kuhusu hili swala la kwanini baadhi ya vitabu viliachwa na kama kuna siri tunafichwa embu pitia humu uone maoni ya wadau utapata mawili matatu

Siri iliyofichwa kuhusu BIBLIA - JamiiForums
Sawa mkuu kinachonikera ni jinsi watu na mashirika mbalimbali yanavyozidi kutumia lugha yao kwenye kuandika biblia khaaa ni kero sana kwani wanapoteza original content ya bible.
Kwa mfano kwenye huo uzi utaona kila toleo la biblia lugha inatofautiana.
 
Kikubwa mkuu Mambo ya biblia na madhehebu hayakusaidii kitu wewe pambana kumtafuta mungu kama kweli yupo
Hujajibu swali na wala hukumusaidia muuliza swali.sisi wakrito tumeaminishwa biblia ndio muongzo wetu tumeaminishwa biblia ni takatifu pia tukaambiwa walio andika biblia hayakua mawazo yao ni ya mungu sasa kwa nini vipunguzwa?
 
Shida ya wa tanzani wengi ni watu wa ndio tu.ukihoji kuhusu biblia au kuruhan wanasema unamkosea mungu eti wewe saligi tu.kwan kuhoji ni kosa?na kama kuna vitu vilitolewa ktk biblia kwa nini vilitolewa?kama ndivyo ni mambo mangapi yalipotishwa?
 
1. Kuficha maarifa.
Vitabu vingi vilitolewa/havikuwekwa kwenyr biblia kwa lengo la kuwafanya watu walio wengi kuwa wafuasi wa watu wengine kwa kuwa kama vyote vingewekwa bayana, kweli ingejulikana na kila mtu, kwa hiyo asingejuwepo yeyite ambaye angefunga safari ya kwenda kanisani kumsikiliza mchungaji. Mtu kama mtume paulo alikuwa msomi, nasikia alikuwa mwanafunzi wa aristotle (naomba kurekebishwa kama nimekosea hapa). Mtume paulo aliandika vitu vingi sana kinaga ubaga kiasi cha watu kuhofia kuwa watu hawatakuwa ni wenye kutii mamlaka kama maandiko yake yote yatawekwa wazi.

2. Kulinda heshima ya baadhi ya watu wa Mungu
Kuna rafiki yangu mmoja anasoma theolojia aliniambia kuwa kuna vitabu ambavyo havipo kwenye biblia vinaeleza mabaya/mapunhufu ya mitume/wafalme/manabii ambayo kama yakiwa wazi watu watapunguza imani yao kwa watu hao na Mungu. Kwa mfano, wote tunajua kuwa daudi alikuwa mzinzi, lakini kuna vitabu vinaenda mbali zaidi na kusema kuwa aliwahi kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja. Pia injili ya tomaso kama sikosei, inaeleza kuwa yesu wakati akiwa mdogo aliwahi mpiga mtoto wa jirani hadi kumuua. Pia injili ya mke wa yesu (maria magdalene) inaonyesha ni jinsi gani yesu alioa na kupata watoto na kanisa aliachiwa maria magdalene na sio perto kama tujuavyo sasa.
Kwa hiyo mambo kama haya kama yangekuwa wazi kabisa sidhani kama kuna mtu angekuwa anasumbuka na dini

3. Kulinda maslahi binafsi.
Wale walioandaa hii biblia ni wanadamu na walikuwa na malengo yao fulani fulani mbali na hili la kuweka wazi uwepo wa nguvu ya mungu kati yetu. Kwa hiyo kuna namna ambayo huenda walitumia kuondoa baadhi ya vitu ili kulinda maslahi yao.

N.B. Sina utaalam/ujuzi/maarifa/elimu kuhusu mambo ya dini wala biblia.
 
1. Kuficha maarifa.
Vitabu vingi vilitolewa/havikuwekwa kwenyr biblia kwa lengo la kuwafanya watu walio wengi kuwa wafuasi wa watu wengine kwa kuwa kama vyote vingewekwa bayana, kweli ingejulikana na kila mtu, kwa hiyo asingejuwepo yeyite ambaye angefunga safari ya kwenda kanisani kumsikiliza mchungaji. Mtu kama mtume paulo alikuwa msomi, nasikia alikuwa mwanafunzi wa aristotle (naomba kurekebishwa kama nimekosea hapa). Mtume paulo aliandika vitu vingi sana kinaga ubaga kiasi cha watu kuhofia kuwa watu hawatakuwa ni wenye kutii mamlaka kama maandiko yake yote yatawekwa wazi.

2. Kulinda heshima ya baadhi ya watu wa Mungu
Kuna rafiki yangu mmoja anasoma theolojia aliniambia kuwa kuna vitabu ambavyo havipo kwenye biblia vinaeleza mabaya/mapunhufu ya mitume/wafalme/manabii ambayo kama yakiwa wazi watu watapunguza imani yao kwa watu hao na Mungu. Kwa mfano, wote tunajua kuwa daudi alikuwa mzinzi, lakini kuna vitabu vinaenda mbali zaidi na kusema kuwa aliwahi kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja. Pia injili ya tomaso kama sikosei, inaeleza kuwa yesu wakati akiwa mdogo aliwahi mpiga mtoto wa jirani hadi kumuua. Pia injili ya mke wa yesu (maria magdalene) inaonyesha ni jinsi gani yesu alioa na kupata watoto na kanisa aliachiwa maria magdalene na sio perto kama tujuavyo sasa.
Kwa hiyo mambo kama haya kama yangekuwa wazi kabisa sidhani kama kuna mtu angekuwa anasumbuka na dini

3. Kulinda maslahi binafsi.
Wale walioandaa hii biblia ni wanadamu na walikuwa na malengo yao fulani fulani mbali na hili la kuweka wazi uwepo wa nguvu ya mungu kati yetu. Kwa hiyo kuna namna ambayo huenda walitumia kuondoa baadhi ya vitu ili kulinda maslahi yao.

N.B. Sina utaalam/ujuzi/maarifa/elimu kuhusu mambo ya dini wala biblia.
Inabidi utafute hayo maarifa ili uje utuelezee ukweli kwani kweli humuweka mtu huru. Nakushauri mtafute MUNGU kisha umshirikishe haya mambo nae atakuonyesha kweli kama Yeremia 33:3 inavyosema kuhusu mambo yaliyofichika.
 
Ambacho nimeona mimi ni kuwa wengi wanaobishana kuhusu Biblia kuwa na vitabu pungufu, ni watu ambao sio watu wa kusoma na kutafakari Neno la Mungu na cha zaid ni agenda zao flani flani ambazo either hazipo kwenye Biblia sasa ndo wanazitafutia uhalali kupitia maandiko mengine mengine.
Ninachoweza kukisema mimi ni kwamba Biblia hii tunayosoma pamoja na kutokuwepo kwa baadhi ya vitabu kama mnavyosema ila ina ukamilifu mwingi sana na inatosha sana kumpa mtu uelewa kuhusu huyu Mungu tunaye mwabudu.. Wasomaji wa Biblia wanalijua hili
 
Ambacho nimeona mimi ni kuwa wengi wanaobishana kuhusu Biblia kuwa na vitabu pungufu, ni watu ambao sio watu wa kusoma na kutafakari Neno la Mungu na cha zaid ni agenda zao flani flani ambazo either hazipo kwenye Biblia sasa ndo wanazitafutia uhalali kupitia maandiko mengine mengine.
Ninachoweza kukisema mimi ni kwamba Biblia hii tunayosoma pamoja na kutokuwepo kwa baadhi ya vitabu kama mnavyosema ila ina ukamilifu mwingi sana na inatosha sana kumpa mtu uelewa kuhusu huyu Mungu tunaye mwabudu.. Wasomaji wa Biblia wanalijua hili
MUNGU kaonya lisipunguzwe neno lolote kwenye maandiko yake kwa hiyo waliotoa hivyo vitabu tayari wamefanya makosa makubwa sana.
Mimi siungi mkono hoja yako kwa sababu ni kinyume na maandiko matakatifu ya MUNGU.
 
Ambacho nimeona mimi ni kuwa wengi wanaobishana kuhusu Biblia kuwa na vitabu pungufu, ni watu ambao sio watu wa kusoma na kutafakari Neno la Mungu na cha zaid ni agenda zao flani flani ambazo either hazipo kwenye Biblia sasa ndo wanazitafutia uhalali kupitia maandiko mengine mengine.
Ninachoweza kukisema mimi ni kwamba Biblia hii tunayosoma pamoja na kutokuwepo kwa baadhi ya vitabu kama mnavyosema ila ina ukamilifu mwingi sana na inatosha sana kumpa mtu uelewa kuhusu huyu Mungu tunaye mwabudu.. Wasomaji wa Biblia wanalijua hili
Ukisoma theolojia utakuja kufuta hiki ulichoandika.
 
Inabidi utafute hayo maarifa ili uje utuelezee ukweli kwani kweli humuweka mtu huru. Nakushauri mtafute MUNGU kisha umshirikishe haya mambo nae atakuonyesha kweli kama Yeremia 33:3 inavyosema kuhusu mambo yaliyofichika.
Katika mambo haya nishafikiaga maamuzi zamani sana. Sitetereki, sidanganyiki maana namiini niaminicho nimefunuliwa na Mungu aliyeiweka dunia katika uwepo wake.
 
Katika mambo haya nishafikiaga maamuzi zamani sana. Sitetereki, sidanganyiki maana namiini niaminicho nimefunuliwa na Mungu aliyeiweka dunia katika uwepo wake.
Aisee kama wewe ni mwanatheolojia ningetegemea uwe msaada kwetu.
 
Aisee kama wewe ni mwanatheolojia ningetegemea uwe msaada kwetu.
Sijasoma theolojia ile darasani kama taaluma, ila nina watu wa karibu wanaonizunguka ambao wamepita/wanapita hiko. Na kwa **** nami pia nimekuwa mdadisi sana katika haya mambo nilikuwa nahoji baadhi ya vitu vya msingi nilivyokuwa navitilia shaka, hivyo imenisababisha nikajua vitu baadhi ambavyo vinasababisha nisimame mahala nilipo ambapo naamini ni mahala sahihi.

Ila naweza kuwahakikishia watu kuwa, ukisahau kuhusu dini, ukasahau kuhusu vitabu vya dini, ukasahau maoni ya sayansi kumhusu Mungu. Na ukaanza kumfiria Mungu ukiwa umevitoa hivyo nilivyovitaja hapo juu, huenda ukawa umeanza safari itakayokupa mwangaza angalau na utakua huru kiimani. Labda kama lengo lako ni kuchunguza biblia tu
 
MUNGU kaonya lisipunguzwe neno lolote kwenye maandiko yake kwa hiyo waliotoa hivyo vitabu tayari wamefanya makosa makubwa sana.
Mimi siungi mkono hoja yako kwa sababu ni kinyume na maandiko matakatifu ya MUNGU.
Neno kama neno sina hakika limepunguzwaje nikimaanisha content ya vitabu vilivyoko kama iko sawa basi si tabu, ndo maana unaeza kuta wakat mwingine wametenga Agano jipya na Agano la kale , au kuna vitabu vina Zaburi tu, kuna vingine viko ni Mathayo mtakatifu basi, sas binafsi sidhani kama neno litakuwa limepunguzwa hapo kama kilichoandikwa hapo kwenye Zaburi separate kinaendana na kile cha kwenye Zaburi ya kwenye mkusanyiko wote kwa ujumla
 
Neno kama neno sina hakika limepunguzwaje nikimaanisha content ya vitabu vilivyoko kama iko sawa basi si tabu, ndo maana unaeza kuta wakat mwingine wametenga Agano jipya na Agano la kale , au kuna vitabu vina Zaburi tu, kuna vingine viko ni Mathayo mtakatifu basi, sas binafsi sidhani kama neno litakuwa limepunguzwa hapo kama kilichoandikwa hapo kwenye Zaburi separate kinaendana na kile cha kwenye Zaburi ya kwenye mkusanyiko wote kwa ujumla
Hakuna neno lililopunguzwa wakati kitabu kizima au vitabu vimetolewa kabisa?
Alaa wacha utani kabisa na neno la MUNGU
 
Ukisoma theolojia utakuja kufuta hiki ulichoandika.
Ni kweli Mkuu sina uelewa kabisa kuhusu theolojia lakini atleast nmeshawahi kusoma Biblia kwa kiwango flani nikaona ina utoshelevu mwingi sana. Na nafikir tafsiri ambayo unaipata unaposoma neno kwa msaada wa Roho wa Mungu ndo kitu hasa kinacho takikana mbali na uchambuz wa historia kuhusu hilo neno japo inaweza ikakupa uelewa mwingi pia zaidi
 
Back
Top Bottom