Kwanini baadhi ya vitabu vimetolewa katika biblia?

Kwanini baadhi ya vitabu vimetolewa katika biblia?

Biblia ni kitabu kinachojumuisha vitabu mbalimbali vilivyoandikwa na watu mbalimbali katika nyakati tofauti na sehemu tofauti.
Biblia ni mkusanyiko wa hivi vitabu ambavyo viliandikwa na waandishi mbalimbali ksha vikapangwa katika mtiririko unaofaa kuanzia miaka ya mwanzo kabisa hadi ya mwisho (Mwanzo hadi ufunuo).

Kitabu cha kwanza kwenye biblia ni Mwanzo ambacho kinaelezea uumbaji wa hii dunia, binadamu wa kwanza na habari za awali kabisa za dunia na ulimwengu. Kitabu cha mwisho ni Ufunuo Kilichoandikwa na Yohane Mbatizaji.

Hivi vitabu viliandikwa katika lugha ya kiebrania eneo la mashariki ya kati na sehemu za kaskazini mwa Africa (Misri, Ethiopia, Libya n.k) kwa sababu ndipo MUNGU alipopachagua ili neno na habari zake zisambae sehemu nyingine za ulimwengu.
Biblia imeanza kutumika rasmi baada ya kuondoka kwa Yes Kristo ila maandiko yalikua yamehifadhiwa hata kabla ya Kristo kuja duniani.


Shida yangu ni hii
1/Kwanini vitabu kadhaa vitolewe kwenye biblia kwa misingi ya mawazo ya watu? Kama maandiko yanaonya kuongeza au kupunguza neno la MUNGU kwanini binadamu wanatoa hivyo vitabu?
2/Kitabu cha Enoch kimeondolewa, vitabu vya deuteron kanoni vinaumiwa na Roman Catholic ila Protestant na makanisa mengine hayavitumii! Injili ya Thomas, Bikira Maria, Injili ya Yuda, Injili ya Barnabas, Injili ya Eva na vitabu vingine vingi?
Ni kwaninihivi vitabu vitolewe wahusika hawakuona wanakwenda kinyume na maandiko ya MUNGU?
We si ukajisomee kwani umelazimishwa
 
Ni kweli Mkuu sina uelewa kabisa kuhusu theolojia lakini atleast nmeshawahi kusoma Biblia kwa kiwango flani nikaona ina utoshelevu mwingi sana. Na nafikir tafsiri ambayo unaipata unaposoma neno kwa msaada wa Roho wa Mungu ndo kitu hasa kinacho takikana mbali na uchambuz wa historia kuhusu hilo neno japo inaweza ikakupa uelewa mwingi pia zaidi
Una hoja nzuri hapa, nikuelewa mkuu. Hongera.
 
Hakuna neno lililopunguzwa wakati kitabu kizima au vitabu vimetolewa kabisa?
Alaa wacha utani kabisa na neno la MUNGU
Hujanielewa Mkuu, nasema kwamba Sioni kama kupunguza idadi ni shida as long as hawajapunguza kile kilichoandikwa ndani ya hivyo vitabu. Nikasema ndo maana kuna mahali unaeza ukakuta vitabu vya methali na Zaburi vimetengwa peke yake sas Kwa tafsiri yangu siwezi sema wameongeza wala kupunguza neno hapo kama kilichoandikwa hapo kinaendana na kile kilichoandikwa kwenye Biblia yenye vitabu vyote
 
Hujanielewa Mkuu, nasema kwamba Sioni kama kupunguza idadi ni shida as long as hawajapunguza kile kilichoandikwa ndani ya hivyo vitabu. Nikasema ndo maana kuna mahali unaeza ukakuta vitabu vya methali na Zaburi vimetengwa peke yake sas Kwa tafsiri yangu siwezi sema wameongeza wala kupunguza neno hapo kama kilichoandikwa hapo kinaendana na kile kilichoandikwa kwenye Biblia yenye vitabu vyote
Mimi najua ili neno lake litimie lazima vyote vilivyoandikwa viwepo kisi miss hata kimoja kama unavyosema wewe.
 
Tafuta kitabu kinaitwa "How To Read The Bible: A Guide To Scripture Then and Now".

Cha James L. Kugel.

Kimefundisha mengi sana kuhusu Biblia kutoka huyu mtaalam aliyefundisha somo la kusoma Biblia mpaka Harvard.
 
Tafuta kitabu kinaitwa "How To Read The Bible: A Guide To Scripture Then and Now".

Cha James L. Kugel.

Kimefundisha mengi sana kuhusu Biblia kutoka huyu mtaalam aliyefundisha somo la kusoma Biblia mpaka Harvard.
Wewe mkuu kama huna Imani na uwepo wa MUNGU utaelewaje yaliyosemwa huko?
 
Paulo Alikuwa Mwanafunzi wa Aristole??? LOL...fanya utafiti kabla ya kuandika..
1. Kuficha maarifa.
Vitabu vingi vilitolewa/havikuwekwa kwenyr biblia kwa lengo la kuwafanya watu walio wengi kuwa wafuasi wa watu wengine kwa kuwa kama vyote vingewekwa bayana, kweli ingejulikana na kila mtu, kwa hiyo asingejuwepo yeyite ambaye angefunga safari ya kwenda kanisani kumsikiliza mchungaji. Mtu kama mtume paulo alikuwa msomi, nasikia alikuwa mwanafunzi wa aristotle (naomba kurekebishwa kama nimekosea hapa). Mtume paulo aliandika vitu vingi sana kinaga ubaga kiasi cha watu kuhofia kuwa watu hawatakuwa ni wenye kutii mamlaka kama maandiko yake yote yatawekwa wazi.

2. Kulinda heshima ya baadhi ya watu wa Mungu
Kuna rafiki yangu mmoja anasoma theolojia aliniambia kuwa kuna vitabu ambavyo havipo kwenye biblia vinaeleza mabaya/mapunhufu ya mitume/wafalme/manabii ambayo kama yakiwa wazi watu watapunguza imani yao kwa watu hao na Mungu. Kwa mfano, wote tunajua kuwa daudi alikuwa mzinzi, lakini kuna vitabu vinaenda mbali zaidi na kusema kuwa aliwahi kujihusisha na mapenzi ya jinsia moja. Pia injili ya tomaso kama sikosei, inaeleza kuwa yesu wakati akiwa mdogo aliwahi mpiga mtoto wa jirani hadi kumuua. Pia injili ya mke wa yesu (maria magdalene) inaonyesha ni jinsi gani yesu alioa na kupata watoto na kanisa aliachiwa maria magdalene na sio perto kama tujuavyo sasa.
Kwa hiyo mambo kama haya kama yangekuwa wazi kabisa sidhani kama kuna mtu angekuwa anasumbuka na dini

3. Kulinda maslahi binafsi.
Wale walioandaa hii biblia ni wanadamu na walikuwa na malengo yao fulani fulani mbali na hili la kuweka wazi uwepo wa nguvu ya mungu kati yetu. Kwa hiyo kuna namna ambayo huenda walitumia kuondoa baadhi ya vitu ili kulinda maslahi yao.

N.B. Sina utaalam/ujuzi/maarifa/elimu kuhusu mambo ya dini wala biblia.
 
Ukitaka kujua chanzo cha biblia kuwa tofauti soma thesis za Martin Luther aliekuwa kasisi wa kanisa la Roman Catholic na pia tafuta history ya uandishi wa biblia kuanzia miaka ya 1500~1600..Mtu kuiongelea injili ya Eva ni jambo la kuchekesha.
 
Sawa mkuu kinachonikera ni jinsi watu na mashirika mbalimbali yanavyozidi kutumia lugha yao kwenye kuandika biblia khaaa ni kero sana kwani wanapoteza original content ya bible.
Kwa mfano kwenye huo uzi utaona kila toleo la biblia lugha inatofautiana.
ulishawahi kuiona original manuscript ya hiyo biblia iliyoandikwa na hao akina marko,musa etc
ukiipata naomba nipatie
 
Kwani ni lini vilikuwemo kwenye bibilia? Wewe ulipo zaliwa bibilia uliyoikuta si ndiyo hii hii au inamabadiliko? Mambo mengine ya kusikia yanachosha akili
 
Ili kupata jibu la swali lako, lazima ujiulize je ni kipi kilianza kati imani au vitabu, yaani ilianza imani na baadaye watu wakaandika hayo mafundisho na kuwa vitabu au vitabu ndio vilianzisha imani?

Waprotestant wana imani yao inaitwa imani ya mitume, na ili kuwa protestant lazima ukili hiyo iman yao ya mitume. Sasa mafundisho yoyote yanayoenda kinyume na imani hai, hayo mafundisho ni ubatili.

Sasa kama vitabu ndio vilianzisha imani je ni vitabu vipi hivyo ambavyo vilianzisha hiyo imani na vimeolozeswa wapi ili sasa kujua kama kuna vitabu fulani vimeondolewa na kupelekea kukosa mafundisho fulani, maana kama kuna vitabu vimekosekana lazima kutakiwa na mapungufu katika imani hiyo iliyo ainishwa katika vitabu hivyo. Mfano kanisa la RC wao wanamisa ya kuombea wafu na ili kusupport hili jambo wanavitabu vyao wanavyotumia kama mwongozo, kwa hiyo mtu akihoji mnapata wapi hayo mafundisho basi anaonyeshwa hayo mafundisho kwenye vitabu vyao. Protestant hawana mafundisho ya kuombea wafu sababu wao hawana vitabu vyenye mafundisho hayo.

Kama imani ndio ilianza na baadaye yale mafundisho yakawekwa katika vitabu, maanayake ni kwamba imani na mafundisho yaliyo katika kitabu lazima yaendane kinyume na hapo yote yanakuwa ni ubatili.

Sasa kwa issue nibble, kilichoanza ni imani ndio ikapelekea vitabu vyenye mafundisho yake, utasema umejiaje, ni kwamba kabla musa kuwapo hakukuwa na torati na kabla ya Yesu kuwapo hapakuwa na injiri, kwa hiyo imani ndio ilizaa vitabu vyenye mafundisho yake

Sasa kuna hoja kwamba mbona bibilia hiyo hiyo imetaja baadhi ya vitabu lakini hivyo vitabu havipo hivyo kwa msingi huo kuna vitu baadhi ya wakristo wanaficha. mfano ndugu zetu Islam wao wanasema injiri ya Barbara, Henoc, pia Qur'an maana Islam kwa mujibu wa mafundisho yao ni kuwa mtume wao ni ndio nabii wa mwisho.

Kama nilivyosema kuwa bible ni mafundosho yalitokana na imani na kupolekea kuandikwa kwa hiko kitabu na sio bible ndio ilizaa imani ya ukristo, hivyo basi vitabu vyote vinavyopingana na imani ya ukristo ni ubatili na havifai kwa mafundisho ya ukristo, hata kama hicho kitabu kina jina linalo fanana na jina la kitabu kikichotajwa katika bible na kutokuwa compiled katika bible ya sasa.

Sasa kwanini kuna baadhi ya vitabu vimetajwa katika bible lakini havijawa compiled katika bible ya sasa.kitendo cha bible kutaja baadhi ya vitabu, kwanza ni uthibitisho kwamba enzi hizo kulikuwa na waandishi wengi walikuwa wanaandika maandiko ya mafundisho mbalimbali including vitabu vya bible.
Na ukisoma hiyo bible inasema kuna waandishi walikuwa wanafanya upotoshaji katika maandiko yao, hivyo swala la kupotosha kupitia maandiko halijaanza leo wala jana. Na huu upotoshaji ndio sababu mojawapo ya baadhi ya vitabu kuwachwa maana vinapingana na msingi wa imani ya ukristo, mfano Qur'an inasema Yesu hakusulubiwa wala hakufa, wakati msingi wa imani ya ukristo unajengwa katika kusulubiwa na kufariki msalabani kwa Yesu wa Nazareth kwa hiyo ilo fundisho la quaran ni ubatili kwa mkristo, lakini ujiulize tuseme kweli kuna vitabu vipo vina mafundisho kama imani ya Kristo inavyosema je ni rahisi kuvi compile na kuwa kitabu kimoja hataka vipo labda elfu moja, hapana na ndio maana vipo hivyo lakini vineeleza kwa upana wake imani ya ukristo.

Nimalizie kwa kusema tu imani ya kikristo ipo wazi haina cha kuficha nai kwamba vitabu vingine vinakosa sifa au vigezo ya kutumia kama mafundisho kuhusu ukristo.
 
Na ndio maana papa francis ameagiza hii biblia ifutwe kipendekezwe kitabu kingine
 
Back
Top Bottom