Kwanini baadhi ya watu wenye dini zao hufikiri kila mtu anapaswa kuendana nao?

Kwanini baadhi ya watu wenye dini zao hufikiri kila mtu anapaswa kuendana nao?

Yoda

JF-Expert Member
Joined
Jul 22, 2018
Posts
48,475
Reaction score
70,102
Waumini wengi wa zinazoitwa dini mbili kubwa za Tanzania kuna mambo kadhaa inabidi mbadilike kuendana na mabadiliko ya wakati.

1. Kusalimia kila mtu "salameleko"
Sijawahi kuelewa sababu za baadhi ya watu kumsalimia kila mtu anayeongea naye kwa hii salamu ya kidini ya salamaleko ukizingatia sio watu wote unaokutana nao ni wa hiyo dini yako.

2. Kujenga hoja kwa kurejea vitabu vya dini.
Unaweza kuwa unajadiliana na mtu au watu masuala mbalimbali ya maisha ambayo ni ya ki-secular kabisa mara unasikia anasema "hata vitabu vya vitakatifu dini vinatuambia blah blah...." Sikubaliani kabisa kujenga hoja za msingi kwa kurejea vitabu vya kidini tena kimoja au viwili tu hasa inapokuwa ni suala au jambo linalohusu mkusanyiko wa watu wenye dini au imani tofauti.

3. Tabia ya kufanya mahubiri kwenye vyombo vya usafiri vya umma
Hii tabia ndugu zetu Wakristo inabidi ifike mwisho sasa au mamlaka zifanye udhibiti wake. Sio sahihi hata kidogo kugeuza vyombo vya usafiri uwanja wa mahubiri, mtu anaposafiri safari ndefu kwanza mtu anachoka hivyo anahitaji utulivu. Pia kwenye hicho chombo kuna watu wa imani tofauti hivyo inakuwa usumbufu mkubwa kwao pia
 
Katika hoja zako 3 iko hivi,

1. Asalaam Aleykum siyo salam ya kidini ni salam ya watu wa middle East, Yesu pia alikuwa akisalimia hivi pia ambapo tafsiri yake kwa kiswahili ni Amani iwe juu yako, na wewe unaitikia na kwako pia, je kuna shida hapo? Shida ni lugha tu huelewi, ni kama Wakristo wanashindana salamu ya bwana asifiwe na tumsifu Yesu kristu ipi sahihi? Huwezi kuona hawa wote ni vichaa? Kuna tofauti gani hapo katika hizo mbili?

2. Hizo refference siyo lazima uzikubali unaweza kuzikataa au kuzikubali kwa sababu vyote ni vitabu vimeandikwa na binadamu havijaandikwa na Mungu.

3. Nakubaliana na wewe mia kwa mia kwenye hoja namba 3.
 
Mimi mtu akinisalimia salamaleko huwa namjibu salama. Sipendi mashindano na watu....
Mimi mtu akinisalimia salamaleko huwa namjibu salama. Sipendi mashindano na watu....
Mind you hizi dini mbili zinqwamiliki wake ambao ni ndio wenye final say. Ingawa islams wanajitahidi kuruhusu ionekane inamilikiwa na Mungu. Ila misikiti yote mikubwa hujengwa na hao wamiliki. Utawaona siku walihitajika kuonekana or ikitokea sababu maalum.

So, sio busara kujibizana na hawa wafuata upepo wadogo. At least ujadili na wale owners. Mfano,pope, raisi wa fungamano la walutheri, Duniani rais wa wasabato nk. Au waandamizi wa Kiarabu.
 
Hiyo inatokea kwa sababu watu wa dini huamini na kutambua kwamba kila mwanadamu ana fursa ya kuokolewa.

Kwa hiyo ukifikishiwa ujumbe wa amani na uponyaji usiweke kibri. Pokea kwa unyenyekevu.

Kama wasingekuwa wanafanya hivyo, nyie haohao mngewatungia nyuzi za kuwasimanga kwamba ni wachoyo au pengine hawana uhakika na kile wanachoamini, kwa vile wamejifungia wao wenyewe.

Ati kama wangeamini kweli katika wokovu na uwepo wa ufalme wa Mungu, wangetushirikisha na sie vilevile.

Ama kweli hekima ni upumbavu kwa Myunani; kwake wema ni uovu na uovu ni wema.
 
Hiyo inatokea kwa sababu watu wa dini huamini na kutambua kwamba kila mwanadamu ana fursa ya kuokolewa.

Kwa hiyo ukifikishiwa ujumbe wa amani na uponyaji usiweke kibri. Pokea kwa unyenyekevu.

Kama wasingekuwa wanafanya hivyo, nyie haohao mngewatungia nyuzi za kuwasimanga kwamba ni wachoyo au pengine hawana uhakika na kile wanachoamini, kwa vile wamejifungia wao wenyewe.

Ati kama wangeamini kweli katika wokovu na uwepo wa ufalme wa Mungu, wangetushirikisha na sie vilevile.

Ama kweli hekima ni upumbavu kwa Myunani; kwake wema ni uovu na uovu ni wema.
Ziko sehemu maalum zimetengwa kufanyia hayo mambo ya kidini.
 
Dini HUSAIDIA katika kuweka maadili sawa kama vile tu katiba/sheria ya nchi ilivyo, tofauti ni kwamba dini hutumia guilt (hatia) kuweka watu katika maadili wakati sheria ya nchi hushurutisha.
 
Katika hoja zako 3 iko hivi,

1. Asalaam Aleykum siyo salam ya kidini ni salam ya watu wa middle East, Yesu pia alikuwa akisalimia hivi pia ambapo tafsiri yake kwa kiswahili ni Amani iwe juu yako, na wewe unaitikia na kwako pia, je kuna shida hapo? Shida ni lugha tu huelewi, ni kama Wakristo wanashindana salamu ya bwana asifiwe na tumsifu Yesu kristu ipi sahihi? Huwezi kuona hawa wote ni vichaa? Kuna tofauti gani hapo katika hizo mbili?

2. Hizo refference siyo lazima uzikubali unaweza kuzikataa au kuzikubali kwa sababu vyote ni vitabu vimeandikwa na binadamu havijaandikwa na Mungu.

3. Nakubaliana na wewe mia kwa mia kwenye hoja namba 3.
Hoja namba tatu: Wengi siyo wala wahubiri bali ni wasaka sadaka tu. Wanajifanya kuhubiri halafu wanasema mtoe sadaka. Hili wenye mabasi wanaweza kulikomesha mara moja kwa sababu ni bughudha kwa abiria.
 
Waumini wengi wa zinazoitwa dini mbili kubwa za Tanzania kuna mambo kadhaa inabidi mbadilike kuendana na mabadiliko ya wakati.

1. Kusalimia kila mtu "salameleko"
Sijawahi kuelewa sababu za baadhi ya watu kumsalimia kila mtu anayeongea naye kwa hii salamu ya kidini ya salamaleko ukizingatia sio watu wote unaokutana nao ni wa hiyo dini yako.

2. Kujenga hoja kwa kurejea vitabu vya dini.
Unaweza kuwa unajadiliana na mtu au watu masuala mbalimbali ya maisha ambayo ni ya ki-secular kabisa mara unasikia anasema "hata vitabu vya vitakatifu dini vinatuambia blah blah...." Sikubaliani kabisa kujenga hoja za msingi kwa kurejea vitabu vya kidini tena kimoja au viwili tu hasa inapokuwa ni suala au jambo linalohusu mkusanyiko wa watu wenye dini au imani tofauti.

3. Tabia ya kufanya mahubiri kwenye vyombo vya usafiri vya umma
Hii tabia ndugu zetu Wakristo inabidi ifike mwisho sasa au mamlaka zifanye udhibiti wake. Sio sahihi hata kidogo kugeuza vyombo vya usafiri uwanja wa mahubiri, mtu anaposafiri safari ndefu kwanza mtu anachoka hivyo anahitaji utulivu. Pia kwenye hicho chombo kuna watu wa imani tofauti hivyo inakuwa usumbufu mkubwa kwao pia
Ila mtu akinukuu akina Aristotle,Mwalimu Nyerere unapenda ? Hekima ipo kwenye vitabu vitakatifu.acha upoyoyo.pia Salamu kama haikuhusu/huijui itika unavyojua. Kwenye vituo vya mabasi kukiwa na miziki ya Koffi,Matangazo ya Dawa, Biashara hakuna shida! Ila akihubiriwa Muumba wa vyote,ni shida! Umekamatwa na ibilisi wewe,yakupasa toba.mfano injili ni habari njema,unakasilikia vipi habari njema?
 
Asalaam Aleykum ndio salamu aliyokuwa anatumia Yesu kwa Kiebrania kwa kiswahili amani iwe nanyi.

Dini zote mbili za Ibrahim hakuna kipya labda zije dini za kijapan au Krishna sijui Buddha ndio labda kuna jipya.

Islamic ni sehemu ya version ya Ukristo.
Kwa kiswahili inanoga sana "amani iwe nanyi" 🤝
 
Back
Top Bottom