Kwanini CCM imejitenga na msiba wa Profesa Sarungi??

Fatma huwa hatukani hovyo huwa anatoa hoja kukosoa jambo ambalo kweli linastahili kukosolewa ila huwa hana muda wa kutukana serikali hata siku moja
Sijaona Maria akitukana serikali zaidi ya kuongoza mijadala,Je Mtoto Ndio afanye kazi ya baba yake ipuuzwe? Tena mtoto aliezidi miaka 18 na ana familia yake?
 
Kwani wakienda itasaidia nini?

Kwamba wakienda marehemu atafutiwa dhambi zake zote?

R.I.P Prof. Philemon Sarungi
 
Katiba ya nchi inamlazimisha kuenda kwenye kila msiba mbona mkuu unakua too personal Raisi ana uhuru wa kuamua nani ampende nani asipende ondoa hapa chuki na ubaguzi wako
 
Kwani Samia ni lazima ajihusishe na kila msiba?

Mbona kama mnataka kumpa umuhimu ambao hana?

Una hakika familia ya Sarungi inataka rais Samia ajihusishe na msiba wao?
 
Kama Serikali.imejitenga ni makosa makubwa sanaaa....SSH uone aibu jamani mtoto kuwa tofauti na baba au familia ni kawaida .....ndio demokrasia hiyoo.....pesa sio zako ni za umma ....toa pesa wakamzile mkongwe Sarungi mengine utajua wewe na Maria wako
 
Reactions: G4N
Yule alikua Raisi wa zamani analindwa na katiba acha kunchanganya mambo.
Waziri mstaafu je? Kwa taarifa yako anapokea pesa za serikali na anatunzwa na serikali mpaka anakufa waziri mstaafu.
 
Kwa hiyo unataka kusema huyu Professor ambae mwanae anshinda mitandaoni kumktukana Rais usiku mchana unaona ulikuwa ni sahihi? SSH nae ni binadamu pia ,hata ungekuwa ni wewe matusi ya mariah sarungi hayavumiliki
Uraisi ni taasisi,kama hataki kutukanwa aachie ngazi arudi Kizimkazi aone kama kuna mtu atamfuatilia
 
Pesa sio za Umma ni za SSH wanavyosema machawa wake na chama chake na wengu wa Watanzania wanakubaliana nap.

Ndio maana naendelea kusema vizazi vyenye umri wa kupiga kura kuiondoa CCM madarakani bado havijazaliwa.
 
Itakuwa jambo la kushangaza sana SSH akaususa huu msiba tena kwenye kipindi hiki cha mfungo kwa sababu tu ya Maria Sarungi.
 
Reactions: G4N
Waziri mstaafu je? Kwa taarifa yako anapokea pesa za serikali na anatunzwa na serikali mpaka anakufa waziri mstaafu.
Ni waziri mkuu mstaafu sio kila waziri kwamba analindwa na katiba kaisome vzri tu.
 
Reactions: G4N
Nadhani ubaguzi unaupika wewe

Over the past 6 months tumefiwa na former ministers zaidi ya sita….

Au kwasababu Huyu prof mwanaye ni chagandumuz basi apewe ufalme mkuu?
 
Huo mtifuano kwenye comments nimeupenda uko live kabisa. Poleni na msiba wafiwa
 
Juzi tu mkwewe kafiwa na baba yake akwenda kutoa pole nyumbani kwao alikuwa na majukumu Tanga.

Watu hawawezi wacha ratiba zao kisa muwaone kwenye misiba.

Kwanza yupo hata Dar kwenyewe au yupo kaskazini huko.
 
Toa upumbavu wako kama una uchungu kamlilie au kama Kuna mtu anatukana Wazazi wako nenda kashiriki shida zao uwasaidie.
 
Unaijua Ccm vizuri?
Unawajua walimu vizuri?
Unawajua polisi vizuri?

Hoja yako ni nzuri sana ila ukishawajua vizuri niliowataja hapo juu kwasasa siyo rahisi Samia kutoshinda au kushindishwa. Taifa hili kwasasa hata mtu yeyote kutoka nchi yeyote awe mbovu au mzuri akifanikiwa kupitia Ccm na akateuliwa na wakaelewana vizuri na Kikwete jua huyo ndiyo rais wako. Maana wasimamizi wa uchaguzi ni walimu na walinda kura ni polisi wetu nadhani unazijua njaa za hao watu. Wakipewa laki tu mzee watavunja watu miguu kama hawana akili na walimu watabeba kura feki utadhani wanalipwa mamilioni baada ya hapo wanaanza kupambana na kausha damu.
 
Watanzania wanadai katiba mpya ya kumpunguzia madaraka rais.

Halafu hapo hapo wanamuongezea rais madaraka ambayo hata hana kikatiba.

Madaraka ya kuifanya misiba iwe na maana.

Watu wanapanga rais aende kwenye msiba wakati hata hawajaui kama wenye msiba wanataka rais aende.

Safari yetu ndefu sana.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…