Kwanini familia za nchi zilizoendelea hazina wasaidizi wa kazi za nyumbani (house girls)?

Unafikiri kwa taratibu za uajiri za hao wasaidizi wa ndani kwa ulaya zingewekwa hapa kwetu naona kabisa hakuna ambaye angeajiri hao wasaidizi labda matajiri...
 
Nna ndugu yangu aliendaga huko majuu yee hanaga mfanya kazi akarudi TZ na ujuzi wa kupika msosi wa wiki nzima alafu unapaki kwenye vicontena vdogovdogo then unagandisha mkitaka kula mnakitoa kimoja kama ni cha maharage na kingine cha nyama then kazi ni kusonga tuu ugali ama kupika wali.
Sasa Cha ajabu ndugu wa mume wakienda pale wanalalamika etii kaka Yao analishwa vipolo[emoji2]wakati mwanamke ni mtu busy sana Hana mda wa kupika l.


Isitoshe familia zetu watu weusi kazi za nyumban zote ni zamama usishangae mkarudi kazin wote Satatu usiku baba akanyosha miguu seblen mama ukaanza kuhangaika na majiko mawilimawili kama upo na mlemavu umo ndani.
 
Unafikiri kwa taratibu za uajiri za hao wasaidizi wa ndani kwa ulaya zingewekwa hapa kwetu naona kabisa hakuna ambaye angeajiri hao wasaidizi labda matajiri...

Kwahiyo serikali inashiriki housegirls kunyonywa
 
Nchi zilizoendelea Matajiri Wana maids hata watano. Ila Hawa wanaishi kwenye vijumba vyao häwana nafasi, Wanaishi Maisha madogo sana yasio na furaha wanateseka mno
 
Hizo familia zilizoendelea hawatumii mkaa kupika Wala masufuria dhaifu ya aluminum yanayopoteza mvuke.

Pia hawafui nguo kwa mikono, Wala hawaendi umbali mrefu kutafuta maji.
Umemaliza kila kitu.
Hawaamki Saa kumi kuteka maji, Wala SAA Kumi na Moja kuandaa Watoto shule
 
Hakuna haja ya housegirl. Kujiendekeza tu. Wakuta kina mama tena wa nyumbani wanarusha miili yao barabarani huku nyumbani hata kuosha vyombo issue. Hata hizo nguo za mazoezi wanafuliwa! Bongo uvivu ubwanyenye ukatili utumwa na uonezi.
Kama wote mnapiga job ni kujipanga tu. Kuna nurseries wakiwa wadogo. Mpokezane. Kila kitu kiwe 50 50. Iwe usafi mapishi kufua kuhudumia mtoto/watoto nk Mambo ya husband/wives kwenda bar hovyo hovyo yaachwe.
Yawezekana. Na bado naamini weekend kuna muda wa kutosha kula bata bar au na familia…
 
Hapo hujaweka gharama ya kumlisha na kumvisha.
Au ndo wale mnawafanya mahousegirl watumwa?
Kwa mtu mwenye utu gharama ya chakula huwa haiongezeki sana anapoongezeka mtu mmoja kwenye familia na mara nyingi (hasa nyumban kwetu) housegirl anakula chakula tunachokula familia nzima.
 
Nchi zilizoendelea MTU anayeweza kumlipa housegirl ni wale mafogo aka matajir wakubwa. Kule HYo ni Kazi rasmi Kabsa na unalipa pesa za kutosha. Sio Kama huku uyaya unalipa 50000 na Bado unamsimamanga
 
Mwanangu nipasie huyo housegirl,,Ili niokoe ndoa yako. Niko sirias
 
Hujakua bado ukikua utaelewa
 
Hizo familia zilizoendelea hawatumii mkaa kupika Wala masufuria dhaifu ya aluminum yanayopoteza mvuke.

Pia hawafui nguo kwa mikono, Wala hawaendi umbali mrefu kutafuta maji.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…