Kwanini flyover Ubungo haimalizi tatizo la foleni?

Kwanini flyover Ubungo haimalizi tatizo la foleni?

Naipongeza Serikali yetu kwa juhudi kubwa za kutuletea maendeleo ikiwemo kuboresha miundombinu yetu. Leo daraja la juu pia limefunguliwa kwa magari yanayotokea mwenge kuelekea Riverside lakini kinachonishangaza ni kwanini foleni bado ni kubwa sana kwa magari yanayotokea Kimara?

Huenda hawajamaliza upanuzi wa barabara ila ni wazi kwa ramani hii wameamua tu kupunguza tatizo la foleni badala ya kulimaliza pamoja na kutumia billions za kutosha.

Nachojiuliza walishindwa vp kuongezea bilioni zingine wakajenga kitu cha kuishi miaka yote kitakachomaliza tatizo? Na hii hali inajirudia pale mbezi mwisho licha ya mapesa mengi yanayotumika ila hakuna dalili za kumaliza tatizo la foleni sana sana ni kama foleni ya Ubungo wanaihamishia Mbezi Mwisho.

Tuna watu wanaofikiri sawasawa? Hawatembei nchi nyingine? Wakitembea huko hawajifunzi wenzetu wanafanyaje?
Ring road ingesolve
 
Foleni haitaondoka mkuu. Itahamia kwenye hizo juction nyingine. Kumbuka barabara ya Morogoro imejengwa mara 5 ndani ya miaka 25 na mara zote inajengwa kuondoa foleni lakini foleni haiondoki. Planners wetu wajifikirie upya. Wanapoplan mradi mkubwa kama huu wafikiri miaka 50 au 100 ijayo siyo 5
Kweli mkuu sijui kwanini plan zao hazioni mbali aisee
 
Naipongeza Serikali yetu kwa juhudi kubwa za kutuletea maendeleo ikiwemo kuboresha miundombinu yetu. Leo daraja la juu pia limefunguliwa kwa magari yanayotokea mwenge kuelekea Riverside lakini kinachonishangaza ni kwanini foleni bado ni kubwa sana kwa magari yanayotokea Kimara?

Huenda hawajamaliza upanuzi wa barabara ila ni wazi kwa ramani hii wameamua tu kupunguza tatizo la foleni badala ya kulimaliza pamoja na kutumia billions za kutosha.

Nachojiuliza walishindwa vp kuongezea bilioni zingine wakajenga kitu cha kuishi miaka yote kitakachomaliza tatizo? Na hii hali inajirudia pale mbezi mwisho licha ya mapesa mengi yanayotumika ila hakuna dalili za kumaliza tatizo la foleni sana sana ni kama foleni ya Ubungo wanaihamishia Mbezi Mwisho.

Tuna watu wanaofikiri sawasawa? Hawatembei nchi nyingine? Wakitembea huko hawajifunzi wenzetu wanafanyaje?
Watanzania tuna haraka sana.

Dozi ya dawa ni siku saba.. wewe siku ya pili..ushaanzahizi dawa hakuna kitu... Kwann tusivumilie mpaka muda utimie!?

Hakuna njia nyingine ya kufanya katikati ya jiji (kuanzia ubungo mpaka posta.. maana itakuwa ghali sana kutekeleza..kwa maana ya fidia..

Kinachofanyika ni kuboresha barabara za ndani, Morogoro connect, Kutoka Mabibo mpaka, Kijitonyama, sinza c Kijitonyama, barabara za ITV kuelekea mikocheni.. Barabara za makumbusho nk.. zote hizo ni kuease traffic kutoka barabara kuu.

Huku nje ya mji wanapanua na super highways.. kama hii ya Morogoro.. itasaidia pia kudiscourage watu kuingia mjini na kuwekeza zaidi nje ya miji kama mbezi, kibamba, luguruni, Kiluvya na Kibaha.. kesho itapunguza foleni.

Ila kwa sasa tuwe na subira Tungoje ujenzi uishe ndio tuhukumu.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Watanzania tuna haraka sana.

Dozi ya dawa ni siku saba.. wewe siku ya pili..ushaanzahizi dawa hakuna kitu... Kwann tusivumilie mpaka muda utimie!?

Hakuna njia nyingine ya kufanya katikati ya jiji (kuanzia ubungo mpaka posta.. maana itakuwa ghali sana kutekeleza..kwa maana ya fidia..

Kinachofanyika ni kuboresha barabara za ndani, Morogoro connect, Kutoka Mabibo mpaka, Kijitonyama, sinza c Kijitonyama, barabara za ITV kuelekea mikocheni.. Barabara za makumbusho nk.. zote hizo ni kuease traffic kutoka barabara kuu.

Huku nje ya mji wanapanua na super highways.. kama hii ya Morogoro.. itasaidia pia kudiscourage watu kuingia mjini na kuwekeza zaidi nje ya miji kama mbezi, kibamba, liguruni, Kiluvya na Kibaha.. kesho itapunguza foleni.

Ila kwa sasa tuwe na subira Tungoje ujenzi uishe ndio tuhukumu.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
I tip my head! for what is stated above!
 
Tatizo ni kutokuwepo kwa alternative routes ambazo zinge-diverte traffic kwenye barabara hizo na ndio maana kumekuwa na bottle neck effect mara tu unapoyavuka madaraja hayo.
 
Naipongeza Serikali yetu kwa juhudi kubwa za kutuletea maendeleo ikiwemo kuboresha miundombinu yetu. Leo daraja la juu pia limefunguliwa kwa magari yanayotokea mwenge kuelekea Riverside lakini kinachonishangaza ni kwanini foleni bado ni kubwa sana kwa magari yanayotokea Kimara?

Huenda hawajamaliza upanuzi wa barabara ila ni wazi kwa ramani hii wameamua tu kupunguza tatizo la foleni badala ya kulimaliza pamoja na kutumia billions za kutosha.

Nachojiuliza walishindwa vp kuongezea bilioni zingine wakajenga kitu cha kuishi miaka yote kitakachomaliza tatizo? Na hii hali inajirudia pale mbezi mwisho licha ya mapesa mengi yanayotumika ila hakuna dalili za kumaliza tatizo la foleni sana sana ni kama foleni ya Ubungo wanaihamishia Mbezi Mwisho.

Tuna watu wanaofikiri sawasawa? Hawatembei nchi nyingine? Wakitembea huko hawajifunzi wenzetu wanafanyaje?
Mkuu unataka kusema akili za wataalam wetu ni kama urefu pua zao?
 
Flyover zawapi mkuu Mimi naona madaraja ya mfugale pale ubungo na tazara!

Watanzania sijui ni ushamba au kutokusafiri yaani akili zote zimetekwa na wasanii wa ccm
 
Flyover zawapi mkuu Mimi naona madaraja ya mfugale pale ubungo na tazara!

Watanzania sijui ni ushamba au kutokusafiri yaani akili zote zimetekwa na wasanii wa ccm
Flyover ni daraja linalovusha magari juu ya barabara nyingine hasa katika makutano ya njia kuu!

Sasa complexity ya structure inategemea eneo, uwezo wa kifedha(kugharamia ujenzi) na mahitaji ya watumiaji wake!

Ukweli hizi tulizonazo ni "Flyover" kabisa.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Shughuli za kiuchumi zihamishwe Kwani sasa, maeneo kama Bagamoyo, Chalinze na Mkuranga, wawekezaji wakajenge ili watu wasilundikane mjini Dar.
 
Daraja limejemeuengwa kupunguza foleni juction ya ubungo na mpaka sasa foleni imepungua ukilinganisha na wakati kuna taa japokua ujenzi haujakamlika kama foleni imehamia kwingine ila suala lingine ila ubungo foleni imepungua
 
Mfugale na Baba yake wameharibu Tazara , Ubungu , Jangwani na Mfumo mzima wa mabsi ya mwendo wa kasi.
Wanajenga kupata sifa zaidi kuliko kufikiria foleni.
Ni ushamba fulani hivi
 
Hamna flyover pale lile ni daraja
Flyover yoyote huwa ni daraja!

1601523161657.png
 
Back
Top Bottom