Kwanini hawa rafiki zangu wanaumia sana mioyo yao

Kwanini hawa rafiki zangu wanaumia sana mioyo yao

Wakuu nipo Daressalam yapata mwezi sasa, nilitoka mkoani kuja huku kufukuzia fursa mbalimbali na kuongeza exposure.

Ukizingatia mimi sio mtu wa kuishi sehemu moja kwa muda mrefu, kule mkoani kuna ishu zangu ambazo huwa nafanya na zinaniingizia pesa ya kuendesha maisha yangu.

Toka nimekuja huku daressalam sijaweza kufanikiwa kwa lolote, naona watu wengi huku wanaishi kinafiki Sana, kuna rafiki yangu nimejiegesha kwake kwa muda yaani mimi ni kulala tu.. mambo mengine yote namaliza mwenyewe.

Sasa kinachoniacha hoi ni kuhusu hawa rafiki zangu wa dar😀😀 nikinunua kitu kizuri mfano kiatu au simu unaona kabisa wanaumia.

Bajeti yangu toka nimefika hapa huwa nanunua ile chupa kubwa ya maji lita 13 ...napo pia naona wanaumia nahisi walitegemea niteseke😀😀😀😀..
Mkiishi masikini-kunuka wote sehemu moja hayo ndiyo matokeo yake.
 
Back
Top Bottom