Kwanini Hospitali ya St. Benedict, Ndanda, Mtwara huuliza wateja dini zao?

Kwanini Hospitali ya St. Benedict, Ndanda, Mtwara huuliza wateja dini zao?

Joined
Nov 23, 2018
Posts
94
Reaction score
202
Salaam wanajamvi!

Sitaki kuwapotezea muda kwa kuwa nami sipendi kupoteza muda wangu, najielekeza moja kwa moja kwenye mada lengwa karibuni.

Jana nilienda hospitali ya Rufaa ya Mt. Benedikto (St. Benedict, Ndanda, Mtwara) kwa ajili ya matibabu. Nakiri hii ni katika hospitali bora kabisa kwa huku Kusini mwa Tanzania.

Hata hivyo, katika mchakato wa Usajili nilipata ukakasi baada ya kuulizwa dini yangu. Ilinichukua sekunde takribani 20 kutafakari na kujibu swali kwakuwa sikuona haja na hoja ya msingi kwa mteja kuulizwa swali hilo.

Niliamua kumuhoji mhudumu wa mapokezi kuhusu umuhimu wa kuwatambua wateja kwa dini zao, alijibu kuwa yeye hafahamu chochote kuhusu mantiki ya hilo bali anachofahamu hilo ni hitaji la lazima la usajili na mfumo wa usajili hauendelei kama kitarukwa kipengele cha dini.

Kwakuwa jamii Forums ni chaka la magwiji, majagina na maguru naomba kwa yeyote mwenye ujuzi anijuze iwapo ipo hoja na haja ya Mamlaka ya Hospitali hii ya Wakatoliki kuuliza dini za wateja.

Naomba kuwasilisha.
20230424_123234.jpg
 
Au hii hospital imeanzishwa na wale magaidi wa Cabo Delgado wa Mozambique nini?
Tunajua pembeni ya Mtwara kuna kundi la kigaidi ambalo linawakata watu vichwa na ili usalimike wanakuuliza maswali kutoka kwenye kitabu kitakatifu cha Quran, ukishindwa kujibu wanajua wewe sio muislam wanakukata kichwa
 
Au hii hospital imeanzishwa na wale magaidi wa Cabo Delgado wa Mozambique nini?
Tunajua pembeni ya Mtwara kuna kundi la kigaidi ambalo linawakata watu vichwa na ili usalimike wanakuuliza maswali kutoka kwenye kitabu kitakatifu cha Quran, ukishindwa kujibu wanajua wewe sio muislam wanakukata kichwa
Kwa hiyo unataka kusema kile kifanywacho na Magaidi wa Cabo Delgado kuwahoji watu dini zao ni sawa na wafanyacho Wabenediktini wa Ndanda.
 
Au hii hospital imeanzishwa na wale magaidi wa Cabo Delgado wa Mozambique nini?
Tunajua pembeni ya Mtwara kuna kundi la kigaidi ambalo linawakata watu vichwa na ili usalimike wanakuuliza maswali kutoka kwenye kitabu kitakatifu cha Quran, ukishindwa kujibu wanajua wewe sio muislam wanakukata kichwa
Pumbavu unafikiri kwa kutumia kinyeo chako

Ndanda ukifika hakuna mtu atakayekuambia kuwa umefika kwenye ngome ya wakristo

Hospital ni ya kikristo (japo serikali ina mkono)

Kuna chuo Cha manesi Cha kikristo hata ukiwa muislamu lazima uende kanisani

Kuna chuo Cha masister na ma brother
 
Salaam wanajamvi!

Sitaki kuwapotezea muda kwa kuwa nami sipendi kupoteza muda wangu, najielekeza moja kwa moja kwenye mada lengwa karibuni.

Jana nilienda hospitali ya Rufaa ya Mt. Benedikto (St. Benedict, Ndanda, Mtwara) kwa ajili ya matibabu. Nakiri hii ni katika hospitali bora kabisa kwa huku Kusini mwa Tanzania.

Hata hivyo, katika mchakato wa Usajili nilipata ukakasi baada ya kuulizwa dini yangu. Ilinichukua sekunde takribani 20 kutafakari na kujibu swali kwakuwa sikuona haja na hoja ya msingi kwa mteja kuulizwa swali hilo.

Niliamua kumuhoji mhudumu wa mapokezi kuhusu umuhimu wa kuwatambua wateja kwa dini zao, alijibu kuwa yeye hafahamu chochote kuhusu mantiki ya hilo bali anachofahamu hilo ni hitaji la lazima la usajili na mfumo wa usajili hauendelei kama kitarukwa kipengele cha dini.

Kwakuwa jamii Forums ni chaka la magwiji, majagina na maguru naomba kwa yeyote mwenye ujuzi anijuze iwapo ipo hoja na haja ya Mamlaka ya Hospitali hii ya Wakatoliki kuuliza dini za wateja.

Naomba kuwasilisha.View attachment 3251613
Je huduma uliyo pata ilikuwa ya haki na sahihi au la ...kama ni ya haki na sahihi basi jua hakuna shida siku nyingine taja dini tofauti huone kama huduma itapungua au kuongezwa
 
Hizo ni kama demographic informations hazina ishu na hamna mahala wanaweza peleka ila nizaweza kuwasaidia kufanya forecasting planning na hata quantification hazina maana ya udini kama ambavyo umetafsiri
Sijatafsiri udini mkuu. Nashukuru kwa jibu lako. Je waonaje sensa ya nchi ikahusisha dini ili kusaidia kila mwenye lengo la kukusanya taarifa za kidemografia kwakuwa imeonekana hilo ni jambo muhimu.
 
Salaam wanajamvi!

Sitaki kuwapotezea muda kwa kuwa nami sipendi kupoteza muda wangu, najielekeza moja kwa moja kwenye mada lengwa karibuni.

Jana nilienda hospitali ya Rufaa ya Mt. Benedikto (St. Benedict, Ndanda, Mtwara) kwa ajili ya matibabu. Nakiri hii ni katika hospitali bora kabisa kwa huku Kusini mwa Tanzania.

Hata hivyo, katika mchakato wa Usajili nilipata ukakasi baada ya kuulizwa dini yangu. Ilinichukua sekunde takribani 20 kutafakari na kujibu swali kwakuwa sikuona haja na hoja ya msingi kwa mteja kuulizwa swali hilo.

Niliamua kumuhoji mhudumu wa mapokezi kuhusu umuhimu wa kuwatambua wateja kwa dini zao, alijibu kuwa yeye hafahamu chochote kuhusu mantiki ya hilo bali anachofahamu hilo ni hitaji la lazima la usajili na mfumo wa usajili hauendelei kama kitarukwa kipengele cha dini.

Kwakuwa jamii Forums ni chaka la magwiji, majagina na maguru naomba kwa yeyote mwenye ujuzi anijuze iwapo ipo hoja na haja ya Mamlaka ya Hospitali hii ya Wakatoliki kuuliza dini za wateja.

Naomba kuwasilisha.View attachment 3251613
Mmmmh mbona simpo hii, hata hosp za serikali ilikuw inapaswa kuwa hivi. Kama ambavyo huwa unaweza ulizwa jinsia hata din pia ni sawa, au kama umri na vingine ni sawa. Haya yote yapo katika kuchukua tu takwimu na historia ya ugonjwa husika.
 
Back
Top Bottom