Maalim Raphael
Member
- Nov 23, 2018
- 94
- 202
Salaam wanajamvi!
Sitaki kuwapotezea muda kwa kuwa nami sipendi kupoteza muda wangu, najielekeza moja kwa moja kwenye mada lengwa karibuni.
Jana nilienda hospitali ya Rufaa ya Mt. Benedikto (St. Benedict, Ndanda, Mtwara) kwa ajili ya matibabu. Nakiri hii ni katika hospitali bora kabisa kwa huku Kusini mwa Tanzania.
Hata hivyo, katika mchakato wa Usajili nilipata ukakasi baada ya kuulizwa dini yangu. Ilinichukua sekunde takribani 20 kutafakari na kujibu swali kwakuwa sikuona haja na hoja ya msingi kwa mteja kuulizwa swali hilo.
Niliamua kumuhoji mhudumu wa mapokezi kuhusu umuhimu wa kuwatambua wateja kwa dini zao, alijibu kuwa yeye hafahamu chochote kuhusu mantiki ya hilo bali anachofahamu hilo ni hitaji la lazima la usajili na mfumo wa usajili hauendelei kama kitarukwa kipengele cha dini.
Kwakuwa jamii Forums ni chaka la magwiji, majagina na maguru naomba kwa yeyote mwenye ujuzi anijuze iwapo ipo hoja na haja ya Mamlaka ya Hospitali hii ya Wakatoliki kuuliza dini za wateja.
Naomba kuwasilisha.
Sitaki kuwapotezea muda kwa kuwa nami sipendi kupoteza muda wangu, najielekeza moja kwa moja kwenye mada lengwa karibuni.
Jana nilienda hospitali ya Rufaa ya Mt. Benedikto (St. Benedict, Ndanda, Mtwara) kwa ajili ya matibabu. Nakiri hii ni katika hospitali bora kabisa kwa huku Kusini mwa Tanzania.
Hata hivyo, katika mchakato wa Usajili nilipata ukakasi baada ya kuulizwa dini yangu. Ilinichukua sekunde takribani 20 kutafakari na kujibu swali kwakuwa sikuona haja na hoja ya msingi kwa mteja kuulizwa swali hilo.
Niliamua kumuhoji mhudumu wa mapokezi kuhusu umuhimu wa kuwatambua wateja kwa dini zao, alijibu kuwa yeye hafahamu chochote kuhusu mantiki ya hilo bali anachofahamu hilo ni hitaji la lazima la usajili na mfumo wa usajili hauendelei kama kitarukwa kipengele cha dini.
Kwakuwa jamii Forums ni chaka la magwiji, majagina na maguru naomba kwa yeyote mwenye ujuzi anijuze iwapo ipo hoja na haja ya Mamlaka ya Hospitali hii ya Wakatoliki kuuliza dini za wateja.
Naomba kuwasilisha.